Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

mnazidi kunipasua kichwa
mbona nlishaamua kutokumweleza ila hawa WAKENYA nawajua vizuri tabia zao siku wakijua tu kuwa nina mchumba na tena anasali kanisa wanalosali sjui itakuwaje......dear usimpe dhamana changudoa atakufunga nawajua vizuri

Tatizo lako hukubali ushauri unang'ang'ania Wakenya mata roho inakusuta.We unajifanya mgumu tu bila sababu wapewa ushauri unasema wa kupasua kichwa. Usinge kuja kuomba ushauri. Kama IPO IPO tu. Au kama kuna kitu hujakieleza unahofia.
 
Mtu asikudanganye wewe eti ukweli utakuweka huru, wanaume wana inferiority complex, ukimwambia tu atakuwa anajidharau kuwa hakuridhishi, maana katika hao mamia umekutana nao kuna mitulinga tofauti ya haja, we vunga.

Je jamaa yake akipata taarifa kwa watu wengine itakuwa vipi? Kuna hao anaowakwepa Kanisani.
Reaction ya mtu ipo ndani ya nafasi yake. Wangapi wanaambiwa waache wake zao walikuwa machangu lakini bado wapo nao?
 
Mi nakushauri kuwa rudi kwenye kanisa lako la zamani kawaface hao wadada Wakenya waambie ukweli kuwa hayo mambo uliyoyafanya yalikuwa ni ya kupita tu kwa sababu ulikuwa na hali ngumu, lakini kwa sasa umeokoka na umeacha hayo mambo na Ya kale yamepita kwani wewe ni kiumbe kipya sasa.
hawa wakenya nahisi bado wanajiuza ila kisasa na sio kimtaani
ukiwafaham machangudoa na tabia zao hutakaa uwaamini hata chembe na hawa wadada lazma watakuwa na nongwa juu yangu kwa kuwa nina kazi na nna mchumba na tuna uelekeo
 
baada ya matatizo yote ya utotoni kwa sasa nimekuwa mpole sana
nilikuwa kiongozi wa vijana kanisani ila nlilazimika kuhama baada ya MKENYA MDADA flani kuanza kuhudhuria huduma ya hapa kanisani.
BF alinishangaa kwani nahama kanisa ninaloheshimika kwa namna nlivyowaongoza vijana na mchungaji aliingilia akinitaka nisihame....mwishowe nikahama kilazima mkaanza kusali kikanisa kidogo njee ya mji....nayaona maisha yangu yoote yamejaa uongo nateseka sana

we dada una hakika umetubu hiyo dhambi kwa roho na kweli na ukaamini Mungu amekusamehe? Nauliza hivyo kwa sababu maelezo yako yanaonyesha kuwa dhambi yako inakutangulia. Kama ulishaungama na una hakika hata ukitishiwa kiPRADO hutarudi kwenye uchagudoa basi amini umesamehewa. Ukiamini umesamehewa unakuwa na amani moyoni. Hata ukikumbuka dhambi yako inakuwa kama unavyokumbuka chakula ulichokula jana kwa hiyo husononeki wala kuogopa sijui nani atajua. Ukiwa na amani na wewe mwenyewe huwezi kukosa amani kwa wengine. Tatizo unajiona ulifanya dhambi kubwa mno kama umeua dunia. Unajiona mchafu sana kiasi kwamba hata utubu vipi huwezi kusamehewa (ni vizuri kujiona mchafu sana na ni vizuri kuamini hakuna uchafu unaoshindikana kuoshwa pale unapoamua kujirudi.

Kwa hiyo nachoweza kukuambia ni kuwa ujisamehe, utafute amani yako kwanza - kuwa mkweli kwa Mungu wako na kama umetubu amini kusamehewa na ujifunze kufurahia msamaha badala ya kuangalia angalia nyuma. Au unataka uone ishara gani ndo uamini kama umekuwa mpya? Halafu hao rafiki zako unatarajia wafichue siri kwani wao hawajipendi? Kama kweli na wao wamemrudia Mungu hawawezi kamwe kusema huo upuuzi labda utuambie mnaenda kwenye hayo makanisa kutafuta wanaume. Hapo lazima muoneane wivu.

Na kama uhusiano wako na Mungu ni mzuri na Mungu ameweza kukuinua umtumike na ukaweza kuongoza vijana vizuri, huoni kama hiyo hofu yako inakurudisha nyuma kiroho? Ona sasa umeacha huduma umekimbilia sijui nje ya mji wapi ili shoga zako wasikusemee. Hapo huwakimbii shoga zako. Unakimbia kivuli chako. Hata ukienda wapi kitakufata tu mpaka upatane nacho. Ila kama unakosa amani saaaaana kumficha huyo mchumbako basi we mwambie. Kwanini ukose amani? funguka, kitakachofuata ni matokeo tu - kuachwa au kuolewa.
 
Siku utakapoona umeshindwa kukaa na huyo mpenzi wako, basi msimulie mkasa mzima.
 
in case u promise me to marry ur brother ntamwambia otherwise not!!!!!
usindanganye nijiue usiku huu

Sasa mbona tumekushauri unajitia oooh mtu wa diniii mtu wa dini utakuwa weeeeweeeeeee (in masanja's voice
 
my dea kwanza pole hayo ni maisha ,pili tambua ushasamehewa na moyo wako mungu ameona ,mwisho nikutie moyo kuwa ,kuna wanawake wengi tu wamekuwa na mahusiano zaidi ya wanaume 10 na wote hao wamefanya nao ngono ila kutokana na matatizo ambayo tunakutana nayo unajikuta unaacha na unaanzisha na mwingine,huyo hana tofauti na ww,sema tu ww ulikuwa unauza kwa pesa tena kwa masaa ulikuwa hudumu na mtu lkn mwisho wa siku tumeolewa,sasa usiogope,mradi umepima huna ukimwi,basi uko salama,na kuhusu mchumba wako ww ndie unamjua je ukimwambia ukweli atareact kiasi gani,bora usimwambie,tambua na hao pia wadada wa kenya nao wapo hapo kanisani kutubu zambi zao hivyo basi lbd kama yupo hapo kukufatilia ww na si mungu,lkn waweza wafata na kuongea nao kuwa pamoja na ukahaba niliofanya lkn mungu kaniokoa na mume nmepata soon naolewa na nishatubu,na uzuri mchumba wangu anajua hivyo kanipenda na tumepima,mwisho wakkaribishe ktk sherehe,uone kama watasema neno lolote kwa mtu
thanks alot
kama umekaa na wadad wa KENYA wanajifanya ni wa ulaya ulaya so hawakawii kumwomba shemeji yao awasaidie kutafuta waume wa kuwaoa na kwenye hayo mazungumzoo lazma wataeleza sana kuhusu kujiuza tulikokuwa tukifanya nairobi then hapo BF wangu ataujua ukweli wangu lazma ataniacha.

mfano:just wiki mbili zilizopita tulichelewa tukarudi usiku njiani akiendesha gari akawa anawaona machangudoa akaanza kufokea usukani yaan roho iliniuma sana
 
sikuwahi kufanya kinyume na maumbile
pia kuna wadada wakenya wako hapa AR wanaweza kuvujisha hii siri ikawa msala zaidi sjui hata nianzie wapi..

Sikia sister, ,maisha ni mafupi sana kuhishi kwa hofu na kukimbia kukwepa watu, taarifa kama hiyo kwa mara ya kwanza huwa inaleta shock sana kwa wanaume, bt time inavyoenda ukijumuisha na upendo kama upo mambo yata tulia tu.

Wew ndo wamjua vema mwenza wako tafuta njia sahihi ya kumwambia, ila usije mshirikisha yeyote wakati unamweleza haya muwe walili tena home.
 
Kheri asikie kutoka kwako kuliko kusikia kutoka kwa watu wengine,utakuwa huru sana ukifunguka kwake na kumwambia ukweli usifiche uhalisia wako utakuwa unajidanganya ww na kumdanganya huyo mwenza wako.Kama anakupenda atakupenda pamoja na kasoro zako.Tegemea vilevile kasoro yako hio inaweza kutumiwa kama fimbo ya kukuchapia mkikwaruzana..All in all natumai jamaa atakuwa muelewa.Kila la kheri
 
Maisha mtihani. Kufa na tai shingoni bibie.

Kiherehere chako cha kujikosha utajakosa bara na pwani....trust me.

Always let bygone be bygone.

Nimemaliza.
 
Kheri asikie kutoka kwako kuliko kusikia kutoka kwa watu wengine,utakuwa huru sana ukifunguka kwake na kumwambia ukweli usifiche uhalisia wako utakuwa unajidanganya ww na kumdanganya huyo mwenza wako.Kama anakupenda atakupenda pamoja na kasoro zako.Tegemea vilevile kasoro yako hio inaweza kutumiwa kama fimbo ya kukuchapia mkikwaruzana..All in all natumai jamaa atakuwa muelewa.Kila la kheri

Naheshimu sana michango yako humu MMU. Ila ningetaka kuelewa kama unatujua wanaume vizuri.....atasema kujikosha ila je una habari atadharaulika kwa maisha yake yote awapo ndoani?

Na hapo ni endapo jamaa ataamua kumuoa tu.
 
Binadamu haeleweke unaweza kumwambia basi ikatokea lolote kwenye maisha yenu akachukulia tukio ulilomweleza lina apply sasa. Kabla ya kumweleza je ni mtu wa gubu na anachukuliaje vitu pale anapogundua au kujua kitu kidogo
 
Fikiria zaidi theni jiongeza kidogo bidada, ukiendekeza huo moyo wako utamkosa huyo jamaa yako, watamfaidi wengine shauri yako, tumeona mengi ndo maana tunakushauri umezee!!
mbona nlishaamua kumezea ila wakenya najua wataniharibia
ukiwa unawajua vizuri machangudoa hata siku mmoja usiwaamini
 
Remember! You only answer to God, yeye ndiye mlishi wetu. Kama umeomba msamaha kwa Mungu utakuwa huru na utakuwa huru tu, hata akija kujua. Kwahiyo carry on.....

which is which...carry on kwa kusema ukweli au niache nature to take its own course in case akijajua???
 
Naheshimu sana michango yako humu MMU. Ila ningetaka kuelewa kama unatujua wanaume vizuri.....atasema kujikosha ila je una habari atadharaulika kwa maisha yake yote awapo ndoani?

Na hapo ni endapo jamaa ataamua kumuoa tu.

Hapo kuna possibility mbili aidha jamaa awe muelewa au amdharau.Kumbuka hakufanya hivyo kwa kupenda kwasababu wapo wanaobadili wanaume kila kukicha kimaslahi tu hao nao wana tofauti gani na malaya/machangudoa au kwasababu wao hawasimami barabarani??walau yeye alifanya kwa dhiki.Tofauti ni kubwa sana kati ya anayefanya kitu kwasababu hana choice au anayefanya kitu kwa kupenda kwake.Aombe sana mungu huyo bwana awe muelewa but hio ni risk anayotakiwa aichukue.Unafikiri jamaa akiyajua hayo angali wapo ndoani na mfano washazaa itakuwaje?kutafuta kuumiza nyoyo zisizokuwa na makosa kwasababu na watoto watahusika.Amwambie sasa angali hawajaingia ndoani ili jamaa aamue kunyoa au kusuka.Heshima kama ipo ipo tu....Hakuna kitu kama perfect person kila mtu ana madudu yake...let the past stay in the past we live in the present and thats all that matters
 
Hili neno KUUNGAMA hili!dunia yenyewe hii imevaa nepi waungwana wachache mishenzi mingi hata kuamini kuwa kweli umestaafu ikitokea mmepishana kauli kidogo oohooh anaanza kukusimanga mpaka utajuta let bygone be bygone confession ni jambo zuri ila kwa mioyo ya makaratasi ya uzao huu piga bunda sister kuwa kauzu kuliko dagaa mtapikie hiyo khabari kesho utatuletea mrejesho jinsi morani alivyo pandisha mori wakati umemaliza kumuelezea hadith hiyo tamu.
 
Kahadithi km ka Shigongo vile
usome Form III mpaka umalize Chuo ndani ya miaka 3 Mama akaachiwa (Elimu Kenya ni kiboko)
ujiuze usomeshe na kulisha wadogo zako kila siku miaka 3 na kuwasomesha wote boarding (du Kenya biashara hii inalipa)
hakuna haja ya biashara ingine
Bora huyo Mmasaai asieleweshwe
wewe mdiye wa ajabu
miaka mitatu YES
FORM FOUR MMOJA then chuo miwili au wewe kwako chuo lazma Universuty na lazma mtu asome ADVANCE LEVEL????

yes ni miaka mitatuna tena mama alinikuta sjamaliza
 
Back
Top Bottom