Babuyao, pole sana!! Lakini wakati mwingine ni mipango ya kukuandaa kupata pesa nyingi zaidi!! kwa hiyo usisikitike sana. We chukulia tu kuwa hiyo pesa umeichange kwa exchange rate ya chini sana.
Wanabodi, habari zenu.
Leo asubuhi nimeenda zangu city centre kwa shughuli. Nilikuwa na kiasi fulani cha hela ya kigeni mfukoni. Nikaamua kwenda kwenye moja ya maduka ya kubadiili pesa mtaa wa samora. Katika kusimama na kuangalia vibao vya exchange rates kwenye maduka hayo jamaa mmoja akanikaribia na kunambia kuna duka jirani ambalo wanabadili kw bei nzuri zaidi. Akapendekeza nimfuate anioneshe. Ilikuwa ni jirani sana, jengo refu la gorofa.
Kufika pale tukakutana na" mwenye duka" kwenye ngazi. Jamaa angu akamweleza shida yangu. Mwenye duka akaniuliza kiasi cha hela ninachotaka kubadilisha. Nikamweleza. Akasema tumsubiri. Akapanda juu akarudi na hela ya kitanzania kaifunga vema. Akanipa. Nikahesabu, nikaridhika. Tukaagana. Nikiwa njiani nikapata kishawishi cha kuangalia hizo pesa. Nilishangaa kukuta nimebakiwa na elfu 50 tena zikiwa zimekunjwa na kufungwa kwenye mpira kama nilivokuwa nimekabidhiwa.
Sikuamini macho yangu. Kwa kuwa nilikuwa nimefika mbali nilishindwa kuwarudia wale watu. Nipo hapa nauguza maumivu ya kutapeliwa kimazingaombwe. Sielewi nifanye nini! Jihadharini sana na matapeli jamani.
Asamte kwa ushauri. Ukweli pes hiyo wala sijaitumia kwani inanipa kichefuchefu.
Babuyao, pole sana!! Lakini wakati mwingine ni mipango ya kukuandaa kupata pesa nyingi zaidi!! kwa hiyo usisikitike sana. We chukulia tu kuwa hiyo pesa umeichange kwa exchange rate ya chini sana.
Mkuu pole sana ndiyo Dunia ilivyo.Ujumbe wako ni somo kwa wengine,ingawa kuna watu wanafikiri haiwezi kuwatokea.
Narudia tena. Mi nikuwa makini sana, na nilihesabu lwa mkono na macho yangu mwenyewe. Lakini baada ya hapo kilichotokea namwachia Mungu. Yeye ndo atashugulika nao ndo mana sikutaka hata kurudi kupambana nao. Mungu atawalipa kadiri ya matendo yao. By the way jengo alimo huyo tapeli ndipo ime pia ofisi ya dr. Lamwai na makampuni mengine. Hizi taarifa nilizisoma kwenye lango la kupandia ngazi. Maandishi yako ukutani kabisa.
Mambo ya mazingaombwe yapo kama hayajakutokea wewe shukuru Mungu. Afadhali huyo ametapeliwa pesa ndogo. Mimi nilitapeliwa Dollar 2,100 nikajikuta nina 270,000 tu.
Ndugu yangu amini usiamini hao watu wapo, hata mimi nilishawahi kukutana nao, wakaniambia kuwa kuna mtu ana change kwa bei nzuri, nikawajibu asante nikaishia zangu. Sasa wewe unayesema unbelievable subiri mpaka yakukute ndio uta believe. Hata hivyo jamaa ametoa tahadhari tu kwa vile yamempata yeye yasije yakampata mwingine.
Nilivyomwelewa jamaa hakubisha au haamini kama hao watu wana exist. Yeye haamini kama kuna mtu anaweza kutapeliwa kimbulula namna hii miaka hii, kwani huo utapeli ni siku nyingi sana...
jamani sio kikondoo kwani sote tupo kwa ajili ya faida na si vinginevyo, hiyo ni bahati mbaya kwani nikatika utafutaji2.
Hao watu nahisi wanatumia kiini macho, ni kama wale ambao walikuwa Mlimani City, anajidai nataka kwenda mahali sasa sipajui naomba unipeleke nina madini naenda kuuza, upuuzi mtupu, ukiwasikiliza tu umekwisha. Na hao ni hivyo hivyo ukiwapa muda wa kuongea nao tu tayari.