Nimetapeliwa jamani

Babuyao

JF-Expert Member
Jun 6, 2009
1,741
272
Wanabodi, habari zenu.
Leo asubuhi nimeenda zangu city centre kwa shughuli. Nilikuwa na kiasi fulani cha hela ya kigeni mfukoni. Nikaamua kwenda kwenye moja ya maduka ya kubadiili pesa mtaa wa samora. Katika kusimama na kuangalia vibao vya exchange rates kwenye maduka hayo jamaa mmoja akanikaribia na kunambia kuna duka jirani ambalo wanabadili kw bei nzuri zaidi. Akapendekeza nimfuate anioneshe. Ilikuwa ni jirani sana, jengo refu la gorofa.

Kufika pale tukakutana na" mwenye duka" kwenye ngazi. Jamaa angu akamweleza shida yangu. Mwenye duka akaniuliza kiasi cha hela ninachotaka kubadilisha. Nikamweleza. Akasema tumsubiri. Akapanda juu akarudi na hela ya kitanzania kaifunga vema. Akanipa. Nikahesabu, nikaridhika. Tukaagana. Nikiwa njiani nikapata kishawishi cha kuangalia hizo pesa. Nilishangaa kukuta nimebakiwa na elfu 50 tena zikiwa zimekunjwa na kufungwa kwenye mpira kama nilivokuwa nimekabidhiwa.

Sikuamini macho yangu. Kwa kuwa nilikuwa nimefika mbali nilishindwa kuwarudia wale watu. Nipo hapa nauguza maumivu ya kutapeliwa kimazingaombwe. Sielewi nifanye nini! Jihadharini sana na matapeli jamani.
 
Pole sana..sasa mkuu nawe unapandishwa ngazi na kukabidhiana pesa ngazini kweli? Mbona maduka yapo wazi tu hapo City Centre na vibao vimewekwa vya bei za kubadilishia pesa? Basi ungeenda hata benki mkuu.
 
Karibu Dsm ndugu yangu. Huenda excess uliyokuwa unafukuzia haifikii hata elfu 10 .. Pole sanaaa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hao jamaa wapo,nna ndo kazi zao,kama umemmaki sura unaweza wapata kwani daily wapo mitaa hiyo.pole sana Mkuu
 
Pole sana hao wapo siku nyingi na sijui kwanini hawakamatwi, maana wamewaliza watu kibao!
 
Unbelievable! hii lazima umetunga tu, no way, absolutely impossible.
Yaani leo, Machi 2013, uibiwe kiZOMBIE namna hiyo? no way.
Kama ni kweli basi AMKA!.
 
Pole sana ndugu yangu. Wakati mwingine ni vigumu kuhisi mtu fulani anaweza kukutapeli.
 
Pole sana..sasa mkuu nawe unapandishwa ngazi na kukabidhiana pesa ngazini kweli? Mbona maduka yapo wazi tu hapo City Centre na vibao vimewekwa vya bei za kubadilishia pesa? Basi ungeenda hata benki mkuu.

Ni kishawishi tu cha kupata hela nzuri ndicho kimeniponza mkuu
 
Karibu Dsm ndugu yangu. Huenda excess uliyokuwa unafukuzia haifikii hata elfu 10 .. Pole sanaaa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Hapana mkuuu, nilipewa mkononi laki 2 na elfu 22. Nikanywewa zote na kubakiwa na elfu 50 tu.
 
Wanabodi, habari zenu.
Leo asubuhi nimeenda zangu city centre kwa shughuli. Nilikuwa na kiasi fulani cha hela ya kigeni mfukoni. Nikaamua kwenda kwenye moja ya maduka ya kubadiili pesa mtaa wa samora. Katika kusimama na kuangalia vibao vya exchange rates kwenye maduka hayo jamaa mmoja akanikaribia na kunambia kuna duka jirani ambalo wanabadili kw bei nzuri zaidi. Akapendekeza nimfuate anioneshe. Ilikuwa ni jirani sana, jengo refu la gorofa.

Kufika pale tukakutana na" mwenye duka" kwenye ngazi. Jamaa angu akamweleza shida yangu. Mwenye duka akaniuliza kiasi cha hela ninachotaka kubadilisha. Nikamweleza. Akasema tumsubiri. Akapanda juu akarudi na hela ya kitanzania kaifunga vema. Akanipa. Nikahesabu, nikaridhika. Tukaagana. Nikiwa njiani nikapata kishawishi cha kuangalia hizo pesa. Nilishangaa kukuta nimebakiwa na elfu 50 tena zikiwa zimekunjwa na kufungwa kwenye mpira kama nilivokuwa nimekabidhiwa.

Sikuamini macho yangu. Kwa kuwa nilikuwa nimefika mbali nilishindwa kuwarudia wale watu. Nipo hapa nauguza maumivu ya kutapeliwa kimazingaombwe. Sielewi nifanye nini! Jihadharini sana na matapeli jamani.
Umetapeliwa kimazingaombwe au Kikondoo? Wewe mtu anakuja anakuzoa kama gunia?
 
Hao jamaa wapo,nna ndo kazi zao,kama umemmaki sura unaweza wapata kwani daily wapo mitaa hiyo.pole sana Mkuu

Nikirudi nitawakumbuka : mmoja ni mfupi mweusi anavaa suti nyeusi na mwenzake maji ya kunde. Dar inatisha.
 
Unbelievable! hii lazima umetunga tu, no way, absolutely impossible.
Yaani leo, Machi 2013, uibiwe kiZOMBIE namna hiyo? no way.
Kama ni kweli basi AMKA!.
Mkuu, niamini. Imenitokea leo asubuhi.
 
Hawa jamaa kuna siku nimegombana nao sana, huwaa wala hawaogopi. Mi nawajua sana maana wamemfuatilia mume wangu mara nyingi sana. Mara ya kwanza ilibaki kidogo waondoke na millioni kumi.
 
Hapana mkuuu, nilipewa mkononi laki 2 na elfu 22. Nikanywewa zote na kubakiwa na elfu 50 tu.

hakuna mazingaombwe wala nini. walikuchezea fix paleplae lakini hukuona tu. Huku ni kuibiwa kizembe kabisa. Anyway sio kama nafurahia ila lazima ukweli usemwe.
 
Babuyao, pole sana!! Lakini wakati mwingine ni mipango ya kukuandaa kupata pesa nyingi zaidi!! kwa hiyo usisikitike sana. We chukulia tu kuwa hiyo pesa umeichange kwa exchange rate ya chini sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom