Nimepata ajali, niombeeni wana JF

Nimepata ajali, niombeeni wana JF

Pole aiceee, mwenyezi Mungu akujaalie wepesi upone na chombo chako kiludi njiani ili uzidi kulisaka tonge
 
Ulikuepo tukio linatokea!??
Ukiwa unaitafakari ajali lazima ulinganishe Mazingira, ndio maana Mungu ametupa utashi WA utambuzi kuendana na Mazingira na uzoefu! Usitake kutoa Pole bila kutoa mawazo kuzuia lisitokee tena
 
Nashukuru sana Ndugu zangu kwa pole zenu, Mungu atanilipa ila swali langu lipo kwenye Bima hapo duuh
 
Nashukuru sana Ndugu zangu kwa pole zenu, Mungu atanilipa ila swali langu lipo kwenye Bima hapo duuh
1. Report kwenye bima yako kuhusu hiyo ajali hakikisha ni ndani ya saa 48
2. Pata documents za polisi PF,90 PF 91, PF 115 hii haina haraka
3. Wasilisha hizo nyaraka ukiwa na
.nakala ya leseni
.nakala ya kadi
.mkataba wa bima
.nakala ya risiti ya bima nk
Huko bima utapewa form ya madai(claim form) hii hakikisha unapata msaaada wa kujaza maana ina maswali ya mtego
 
Habari JF,

Leo mida ya saa kumi na Moja Kamili, nikiwa na Bajaj yangu kazini, natoka mji Mwema kwenda ferry Kigamboni.

Nikiwa katika low speed ukizingatia hali ya hewa nikiwa upande wangu, ghafla niliona altezza White imeovertake Iko mbele yangu.

Aisee, nilijitahidi kukwepa lakini alikuwa speed sana, baadaye kakimbia sijui hata rangi ya gari, Nina maumivu kichwani na mguuni.

Bajaj yangu Ina Bima kubwa
Askari wamepima na kuchora
Taratibu zingine zipoje nirudi kazini

View attachment 2558751View attachment 2558752View attachment 2558754
Pole sana member mwenzetu. Tushukuru kwamba wewe mwenyewe hukupata majanga zaidi ya yaliyokifika chombo chako cha kazi.
 
Hamna dereva bajaj au bodaboda mwenye akili timamu, tezza ingekumaliza lofa wewe, bahati yako.
Usione Wanaongea hapa Kwa unyonge, kwenye anga zao ni noma sana, Hawajali, hawana tahadhari ni Majanga!! Na Sasa Bajaji zina mwendo ukiamua kuwapita ukae mbele Yao pia hufanya Mashindano, ukikaa nyuma Yao ghafla akiona mteja husimama ghafla na kukuletea ajali, Kwa kweli Hawa watu wanahitaji elimu ya Matumizi Bora ya barabara
 
Pole sana mzee, ndio mambo ya barabarani, ajali nyingine unasababishiwa tu.

Madereva wengi wa altezza,subaru na gari jamii hizo, barabarani huwa na wenge,kila sehwmu wao ni mbio na kuovertake tu.
 
Pole sana,anza traffic police kwanza, wakishaweka kila kitu kwenye maandishi jinsi ajali ilivyotokea,then nenda kwa watu wa bima ulipokatia bima yako...
 
1. Report kwenye bima yako kuhusu hiyo ajali hakikisha ni ndani ya saa 48
2. Pata documents za polisi PF,90 PF 91, PF 115 hii haina haraka
3. Wasilisha hizo nyaraka ukiwa na
.nakala ya leseni
.nakala ya kadi
.mkataba wa bima
.nakala ya risiti ya bima nk
Huko bima utapewa form ya madai(claim form) hii hakikisha unapata msaaada wa kujaza maana ina maswali ya mtego
Uliyoeleza ni practical advice nzuri sana. Hivyo ndivyo inavyotupasa wana-JF wote kufanya kulibakiza Jukwaa hili kuwa la Great Thinkers. Naamini kabisa hapa Jukwaani hakuna utaalamu ambao hakuna member hata mmoja anayeufahamu. Hivyo, tuutumie ujuzi huo kwa manufaa yetu sote.
Zidumu fikra zako member uliyetoa mawaidha hayo mazuri.
 
Pole sana. Upande uliopigwa inaonyesha kweli ulikuwa unakwepa. Hivi hamna kamera zinazoweza kusaidia kumpata mhusika? Mji ungewekewa kamera.
China ina kamera zaidi ya milioni 500

London inaongoza duniani kwa kuwa na kamera nyingi kwa idadi ya watu.

Marekani pia ina kamera nyingi

Nchi zote hizo kuna matukio hutokea na watu hawajakamatwa hadi leo

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Watu hukimbia ajali sababu Watanzania hasa Boda boda na Bajaj hawana ustaarabu, wao hukimbilia mfanyia fujo, kuharibu mali.
Njia pekee ni mtu kukimbia au kama una bastola unakubali kufa na wachache kabla polisi hawajafika

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom