Wanajamvini naomba msaada wenu kuna siku nilikuwa nachokonoa meno na stepple ikawa kipande cha stepple pin likavunjika nikaimeza imenikwama kooni napata maimivu makali sana nifanyeje ni wiki ya pili sasa maumivu yananitesa nombeeni msaada ndugu
Pole sana jaribu kunywa maji halafu unafanya kama unasukutua kwa kuinua kichwa juu kidogo na kusukutua sehemu ya koo. Pia kuwahi hospitali ni muhimu sana kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Wiki mbili ingekuwa imekukwama hiyo homa yake usingeingia JF.Itakuwa ni kidonda tu ama memory of pain that was registered in the brain.Kwa uhakika zaidi onana na ENT.Usirudie tena eeh
mkuu umemeza steppler? dah! hii inaitwa ofisi tumboni. wahi hospitali kabla hiyo stepler haijafanya zile shuhuli zake za kutoboa na kuunganisha huko stomach world
Uko kijiji gani wewe? Yaani wiki mbili bado hujaenda hospitali tuuu! Utapata inflammation ambayo itakuja kuziba koo kabisa ushindwe kumeza chochote na matokeo yake ni kufa. Hivyo wahi hospitali haraka ili waone ni jinsi gani ya kukusaidia! Siku nyingine usirudie kutumia pin, maana wachina wamewaletea tooth pick wewe unatumiaje pin?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.