Nimekumbuka zamani

Nimekumbuka zamani

I miss those golden moments, kwa sasa watu wamekuwa wabinafsi kupitiliza, sio ajabu hata ndugu mnaokaa mkoa mmoja kutotembeleana, watoto wa ndugu hawafahamiani,
Teknolojia imeleta maisha ya ajabu sana, ule ukaribu wa zamani haupo tena.ni kawaida ukienda kusalimia kwa ndugu kuulizwa unarudi kwako lini?
Zamani ilikuwa ni burudani sana kukutana pamoja ndugu, watoto na wajukuu hasa mwisho wa mwaka maana ndo kipindi ambacho watu wengi walikuwa na nafasi hiyo.Babu na bibi wanafurahia kuona matunda ya watoto wao( kucheza na kuwa na wajukuu zao) .Haya yote yamebaki historia kwa jamii nyingi.
Asante sana mleta mada umenikumbusha mbali sana.Kwa sasa tunaishi nyakati za hivyo sana
 
I miss those golden moments, kwa sasa watu wamekuwa wabinafsi kupitiliza, sio ajabu hata ndugu mnaokaa mkoa mmoja kutotembeleana, watoto wa ndugu hawafahamiani,
Teknolojia imeleta maisha ya ajabu sana, ule ukaribu wa zamani haupo tena.ni kawaida ukienda kusalimia kwa ndugu kuulizwa unarudi kwako lini?
Zamani ilikuwa ni burudani sana kukutana pamoja ndugu, watoto na wajukuu hasa mwisho wa mwaka maana ndo kipindi ambacho watu wengi walikuwa na nafasi hiyo.Babu na bibi wanafurahia kuona matunda ya watoto wao( kucheza na kuwa na wajukuu zao) .Haya yote yamebaki historia kwa jamii nyingi.
Asante sana mleta mada umenikumbusha mbali sana.Kwa sasa tunaishi nyakati za hivyo sana
Of course yes,. Teknolojia imeleta mambo ya ajabu sana,.. Ndugu hatutembeleani kama zamani
 
Ulipotaja mambo ya Simu na TV, CD ndipo nilipogundua kuwa, rafiki yangu hauna uzamani wa mbali sana na Dunia ya sasa.
Maana wa Zamani ya nyuma yako, hakukua na Simu hizi za kila mtu yake, bali simu za uma, na nyumba yenye kuvutiwa Simu hiyo nyumba ni mboga saba.
Zamani hiyo hakukua na TV mambo ya Tv yalianza mwishoni miska ya 80 miaka ya 90 ikanza kuenea Ungo wa wavu, ukiona nyumba ina Ungo ni mboga saba sanasana ungo unaona nyumba masaki huko, na 90 hiyohiyo ndipo mambo ya Simu za mkononi yakanza.
 
Ulipotaja mambo ya Simu na TV, CD ndipo nilipogundua kuwa, rafiki yangu hauna uzamani wa mbali sana na Dunia ya sasa.
Maana wa Zamani ya nyuma yako, hakukua na Simu hizi za kila mtu yake, bali simu za uma, na nyumba yenye kuvutiwa Simu hiyo nyumba ni mboga saba.
Zamani hiyo hakukua na TV mambo ya Tv yalianza mwishoni miska ya 80 miaka ya 90 ikanza kuenea Ungo wa wavu, ukiona nyumba ina Ungo ni mboga saba sanasana ungo unaona nyumba masaki huko, na 90 hiyohiyo ndipo mambo ya Simu za mkononi yakanza.
Huko zamani sana mkuu aisee,. Mie nazungumzia miaka kuanzia 2014 kurudi nyuma huko ndio nilikuwa shule ya msingi
 
Yaanii,. Sikuizi watoto hata hawana utaratibu kwa kwenda kusalimia kwa bibi
Mbona wanaenda! Wa kwangu kwa vile uoande wangu nilishawapoteza wazazi wote basi wamebaki wanaenda upande wa mama yao! Ni hivyo hivyo ulivyosimulia na wa kwangu wakienda kwa bibi yao!
 
Mkuu we ni wa mwaka gani kama mlikuwa mnatumia CD kucheki movie,ungekuwa wa zamani kidogo mngetumia VHS(yale mamikanda makubwa kama ka biblia)
 
Sema sijui hawa wazee hela walikuwa wanatoaga wapi?,. Maana kwenye suala la kula kuanzia asubuhi mpaka usiku na wanalisha wajuu na wanafamilia kibao aisee walijitahidi
Usishangae ilikuwaje. Nyuma ya pazia ni kwamba nyie mnapokuwa mpo huko mjini au Shuleni(bweni) huku wazee walikuwa ni kilimo kwa kwenda mbele. Likizo zenu Pasaka au June (nusu mwaka) baadhi ya mazao yanakuwa yamekomaa ile ya Desemba mavuno yote yanakuwa yameshatoka mashambani inabaki ni kuuza au kula huku wakisubiri tena mzunguko mwingine wa mazao uanze. Lakini siku hizi wazee eti wanaenda kijiweni nao kubishanIa Simba na Yanga- WAZEE WA KUWEKA MZIGO
 
Habari za siku nyingi wanajukwaa….

Leo nimekaa nimejiwazia nikajikuta tu naona watoto wa sikuizi hawaenjoy kama ambavyo sisi zamani tulikuwa tunaenjoy,. Watoto wa saizi hawajui hata raha za kwenda likizo kwa bibi

Kwanza niseme tu kuwa bibi yetu kama wajukuu kabarikiwa nao ,. Mpaka sasa nadhani tunaweza kuwa hata tuko 50 na wengine ambao hatuwajui wanaweza kuwa hata 60 tumefika,. Imagine watoto 13 naa wote wana watoto sio chini ya wanne😄😄 ( ila hiii sio lengo la uzi ) ila mtaelewa kwanini nimesema hivi.

Kipindi kile ilikuwa likizo zote za sikukuu yaani December na ile likizo ya pasaka bibi yangu alikuwa anasisitiza wajukuu wotee tuende kumwona,. Yaani tulikuwa tunakuwa wengii kwa bibi ( kila kona unayopita ina mtu😅😅😅) ,. Na kwa vile tulikuwa wengi uharibifu kila siku kuanzia kwenye vyombo watu wanavunja,. mafundi TV sasa ndio kabisa mpaka bibi alikuwa anafungia ndani Tv zake zote hakuna kuangalia mpaka tuondoke,.

Sasa hapo ndio ile mikakati ilikuwa inaanza,. Ikikaribia likizo simu zinaanza kipigwa basi kila watu tunapangiana vitu vya kubeba,. Mie na dada angu tulikuwa tunabeba zetu TV ,. Binamu zetu wengine wa mwanza walikuwa wanabeba deki,. Wa arusha walikuwa wanabeba CD ( baasi hapo kila mtu ataagiza movie anazozitaka wao kazi yao kuzifatuta zilizotafsiriwa wanakuja na CDs Kibao ),. Wengine wa Dar ilikuwa kazi yao kubeba snacks ,.Wengine mipira midoli yaani Ili mradi tu kila mtu awe na chakubeba ….. Yaani ilikuwa tukifika kwa bibi ni kuangalia tu movie kuanzia asubuhi hadi usiku maana ilikua marufuku mtu kutoka nje ya geti😁😁😁

Usiku sasa kila watu wakishaingia chumbani kwao ni muda wa mastori hadi mida mibovu asubuhi hata hakunaa anayekumbuka alilala saa ngapi,. Kila watu wanasimulia stori za nyumbani shuleni yaani ilikuwa raha kipindi kile….

Bibi kwanza alikuwa ananunua sahani nyingi na vikombe vya plastiki kila mtu anamwandika jina kwenye sahani yake ( maana hataki kero mda wa kula zilikuwaga kelele sio za nchi hii watu wanachagua sahani maara vikombe mwisho wa siku kuvunja ),. Baaasi nguo zetu zote zilikuwa zinaandikwa majina ili akija mtu wa kufua kila mtu kambani anaenda kuanua nguo zilizoandikwa jina lake,. Ila bibi😂😂😂

Bibi alikuwa anatuambia yaani babu yenu wakati anajenga hii nyumba aliweka vyumba vikubwa kwajili yenu,. Yaani dream yake ilikuwa muwe mnakuja mnajaa kama hivi mnacheza mnampigia kelele,. Lakini kwa bahati mbaya alifariki bila kumwona mjuu wake hata mmoja ,. Yaani wote tumezaliwa akiwa kashakufa🥹🥹🥹

Kipindi kile ilikuwa hata kama likizo imekukuta mgonjwa utang’a ng’ania usafiri tu hivyo hivyo maana utajisi unyonge wenzio wote wako kwa bibi,.
Sema ndio hivyo sasa watu wenyewe wotee saizi washakuwa watu wazima ,. Wakuoa wameoa na wakuolewa wameshaolewa wengine toka waliendaga nje kusoma haawajarudi wenginee ndio hivyo yaani kwenda kwa bibi sikuizi laabda litokee tukio na hata mkienda hamui wengi na hata hao wachache kila mtu yuko busy na mambo yake yaani nyumba imepoozaaa😔😔 sio kama zamani…
Wananiita updated generation
 
Back
Top Bottom