Nimekumbuka zamani

Nimekumbuka zamani

Habari za siku nyingi wanajukwaa….

Leo nimekaa nimejiwazia nikajikuta tu naona watoto wa sikuizi hawaenjoy kama ambavyo sisi zamani tulikuwa tunaenjoy,. Watoto wa saizi hawajui hata raha za kwenda likizo kwa bibi

Kwanza niseme tu kuwa bibi yetu kama wajukuu kabarikiwa nao ,. Mpaka sasa nadhani tunaweza kuwa hata tuko 50 na wengine ambao hatuwajui wanaweza kuwa hata 60 tumefika,. Imagine watoto 13 naa wote wana watoto sio chini ya wanne😄😄 ( ila hiii sio lengo la uzi ) ila mtaelewa kwanini nimesema hivi.

Kipindi kile ilikuwa likizo zote za sikukuu yaani December na ile likizo ya pasaka bibi yangu alikuwa anasisitiza wajukuu wotee tuende kumwona,. Yaani tulikuwa tunakuwa wengii kwa bibi ( kila kona unayopita ina mtu😅😅😅) ,. Na kwa vile tulikuwa wengi uharibifu kila siku kuanzia kwenye vyombo watu wanavunja,. mafundi TV sasa ndio kabisa mpaka bibi alikuwa anafungia ndani Tv zake zote hakuna kuangalia mpaka tuondoke,.

Sasa hapo ndio ile mikakati ilikuwa inaanza,. Ikikaribia likizo simu zinaanza kipigwa basi kila watu tunapangiana vitu vya kubeba,. Mie na dada angu tulikuwa tunabeba zetu TV ,. Binamu zetu wengine wa mwanza walikuwa wanabeba deki,. Wa arusha walikuwa wanabeba CD ( baasi hapo kila mtu ataagiza movie anazozitaka wao kazi yao kuzifatuta zilizotafsiriwa wanakuja na CDs Kibao ),. Wengine wa Dar ilikuwa kazi yao kubeba snacks ,.Wengine mipira midoli yaani Ili mradi tu kila mtu awe na chakubeba ….. Yaani ilikuwa tukifika kwa bibi ni kuangalia tu movie kuanzia asubuhi hadi usiku maana ilikua marufuku mtu kutoka nje ya geti😁😁😁

Usiku sasa kila watu wakishaingia chumbani kwao ni muda wa mastori hadi mida mibovu asubuhi hata hakunaa anayekumbuka alilala saa ngapi,. Kila watu wanasimulia stori za nyumbani shuleni yaani ilikuwa raha kipindi kile….

Bibi kwanza alikuwa ananunua sahani nyingi na vikombe vya plastiki kila mtu anamwandika jina kwenye sahani yake ( maana hataki kero mda wa kula zilikuwaga kelele sio za nchi hii watu wanachagua sahani maara vikombe mwisho wa siku kuvunja ),. Baaasi nguo zetu zote zilikuwa zinaandikwa majina ili akija mtu wa kufua kila mtu kambani anaenda kuanua nguo zilizoandikwa jina lake,. Ila bibi😂😂😂

Bibi alikuwa anatuambia yaani babu yenu wakati anajenga hii nyumba aliweka vyumba vikubwa kwajili yenu,. Yaani dream yake ilikuwa muwe mnakuja mnajaa kama hivi mnacheza mnampigia kelele,. Lakini kwa bahati mbaya alifariki bila kumwona mjuu wake hata mmoja ,. Yaani wote tumezaliwa akiwa kashakufa🥹🥹🥹

Kipindi kile ilikuwa hata kama likizo imekukuta mgonjwa utang’a ng’ania usafiri tu hivyo hivyo maana utajisi unyonge wenzio wote wako kwa bibi,.
Sema ndio hivyo sasa watu wenyewe wotee saizi washakuwa watu wazima ,. Wakuoa wameoa na wakuolewa wameshaolewa wengine toka waliendaga nje kusoma haawajarudi wenginee ndio hivyo yaani kwenda kwa bibi sikuizi laabda litokee tukio na hata mkienda hamui wengi na hata hao wachache kila mtu yuko busy na mambo yake yaani nyumba imepoozaaa😔😔 sio kama zamani…
Nimeanza kusoma kwa shauku kweli, lakini nilipofika pale "eti kwa bibi tukawa tunavunja TV......" mudi wote wa kusoma ukaisha! Zamani tunayoijua sie sio hiyo!!!
 
Habari za siku nyingi wanajukwaa….

Leo nimekaa nimejiwazia nikajikuta tu naona watoto wa sikuizi hawaenjoy kama ambavyo sisi zamani tulikuwa tunaenjoy,. Watoto wa saizi hawajui hata raha za kwenda likizo kwa bibi

Kwanza niseme tu kuwa bibi yetu kama wajukuu kabarikiwa nao ,. Mpaka sasa nadhani tunaweza kuwa hata tuko 50 na wengine ambao hatuwajui wanaweza kuwa hata 60 tumefika,. Imagine watoto 13 naa wote wana watoto sio chini ya wanne😄😄 ( ila hiii sio lengo la uzi ) ila mtaelewa kwanini nimesema hivi.

Kipindi kile ilikuwa likizo zote za sikukuu yaani December na ile likizo ya pasaka bibi yangu alikuwa anasisitiza wajukuu wotee tuende kumwona,. Yaani tulikuwa tunakuwa wengii kwa bibi ( kila kona unayopita ina mtu😅😅😅) ,. Na kwa vile tulikuwa wengi uharibifu kila siku kuanzia kwenye vyombo watu wanavunja,. mafundi TV sasa ndio kabisa mpaka bibi alikuwa anafungia ndani Tv zake zote hakuna kuangalia mpaka tuondoke,.

Sasa hapo ndio ile mikakati ilikuwa inaanza,. Ikikaribia likizo simu zinaanza kipigwa basi kila watu tunapangiana vitu vya kubeba,. Mie na dada angu tulikuwa tunabeba zetu TV ,. Binamu zetu wengine wa mwanza walikuwa wanabeba deki,. Wa arusha walikuwa wanabeba CD ( baasi hapo kila mtu ataagiza movie anazozitaka wao kazi yao kuzifatuta zilizotafsiriwa wanakuja na CDs Kibao ),. Wengine wa Dar ilikuwa kazi yao kubeba snacks ,.Wengine mipira midoli yaani Ili mradi tu kila mtu awe na chakubeba ….. Yaani ilikuwa tukifika kwa bibi ni kuangalia tu movie kuanzia asubuhi hadi usiku maana ilikua marufuku mtu kutoka nje ya geti😁😁😁

Usiku sasa kila watu wakishaingia chumbani kwao ni muda wa mastori hadi mida mibovu asubuhi hata hakunaa anayekumbuka alilala saa ngapi,. Kila watu wanasimulia stori za nyumbani shuleni yaani ilikuwa raha kipindi kile….

Bibi kwanza alikuwa ananunua sahani nyingi na vikombe vya plastiki kila mtu anamwandika jina kwenye sahani yake ( maana hataki kero mda wa kula zilikuwaga kelele sio za nchi hii watu wanachagua sahani maara vikombe mwisho wa siku kuvunja ),. Baaasi nguo zetu zote zilikuwa zinaandikwa majina ili akija mtu wa kufua kila mtu kambani anaenda kuanua nguo zilizoandikwa jina lake,. Ila bibi😂😂😂

Bibi alikuwa anatuambia yaani babu yenu wakati anajenga hii nyumba aliweka vyumba vikubwa kwajili yenu,. Yaani dream yake ilikuwa muwe mnakuja mnajaa kama hivi mnacheza mnampigia kelele,. Lakini kwa bahati mbaya alifariki bila kumwona mjuu wake hata mmoja ,. Yaani wote tumezaliwa akiwa kashakufa🥹🥹🥹

Kipindi kile ilikuwa hata kama likizo imekukuta mgonjwa utang’a ng’ania usafiri tu hivyo hivyo maana utajisi unyonge wenzio wote wako kwa bibi,.
Sema ndio hivyo sasa watu wenyewe wotee saizi washakuwa watu wazima ,. Wakuoa wameoa na wakuolewa wameshaolewa wengine toka waliendaga nje kusoma haawajarudi wenginee ndio hivyo yaani kwenda kwa bibi sikuizi laabda litokee tukio na hata mkienda hamui wengi na hata hao wachache kila mtu yuko busy na mambo yake yaani nyumba imepoozaaa😔😔 sio kama zamani…
Wewe hujafaidi kitu asee kama Kwa bibi yenu kulikuwa na geti na Tv huko sio vijijini ni mjini huko.


Raha ya kufaidi mwe huru sio kufungiwa kwenye geti. Hizo movie hata kwenu unaweza kuzitafta ukapata tu.



Sisi tulikuwa tunaenda Kwa bibi kijijini Tena miaka hiyo hata CD hazikuwepo

Kwanza wajukuu maximum ni 25 Hivi
Kwa bibi kulikuwa ng'ombe wengi zaidi ya 100!!

Babu alikuwa mkarimu mno na bibi pia.....tukifika tu tunachinja wenyewe mbuzi kubwa la kuchoma tu yaani linaishia juujuu tu kwenye shikome😂

Muda huo Kuna nyama za kubanika zimeshakauka mpaka basi zinaitwa ng'homele kisukuma ni mwendo wa kukata na kuloweka kwenye maji ya chumvi Kisha unakula...

Maziwa sio ya kuuliza ni muda wowote tu unajipimia ....basi wajomba kesho yake mnaenda nao kuchunga pamoja na kuwinda huko mnakutana Watoto shazi mnawinda sungura,digidigi na ndege kama kware ama kanga kama ni masika pamoja na kuchoma uyoga mnakula!!!(Hivi vitu vyote mjini huwezi pata hata ukiwa milionea)


Mkirudi kutoka machungani kulikuwa na bwawa mnaenda kuogelea weee acha tu hapa sio wanawake au wanaume mnaoga mtakavyo maana tulikuwa wadogo wakubwa ndo walikuwa hawaogi...


Mkirudi mtakula mpaka mnakula Tena. Siku ya sikukuu tulikuwa tunaenda kununulia juice cola zile zinaweka kwenye chupa za soda tulikuwa tuna nunua shilingi5 Hadi kumi!!

Michezo ilikuwa mingi sana kuumizwa ilikuwa sehemu ya michezo pia.

Kuna siku hamuendi kuwinda ni Tour ya kusaka matunda pori na kumletea bibi na Babu imagine tulikuwa tunaanza saa3 Hadi saa8 ndo tunarudi na mizigo ya matunda tumechoka mbaya😹😹

Sisi video kipindi chetu huwezi kuikuta Kijiji kiza hata Kwa diwani huikuti wewe ulichoelezea ni miaka ya 2007 hapa tu Kuna CD/DVD!!

Ukweli na miss sana enzi hizo Kuna mto maji tulikuwa tuna yaziba Kisha tunakamata samaki na vidagaa mkimaliza ni kuchoma hapohapo pilipili tulizia huko kula acha kabisa

Kuna matunda mizizi Yale uking'oa linakuwa kama muhoga ila Lina maji tupu matunda Yale hata nyani wanayapenda sana..

Ni vingi vya kuelezea hii ni miaka ya 1995-2002 Hivi acha kabisa
Screenshot_20250329-142451_1.jpg
 
Wewe hujafaidi kitu asee kama Kwa bibi yenu kulikuwa na geti na Tv huko sio vijijini ni mjini huko.


Raha ya kufaidi mwe huru sio kufungiwa kwenye geti. Hizo movie hata kwenu unaweza kuzitafta ukapata tu.



Sisi tulikuwa tunaenda Kwa bibi kijijini Tena miaka hiyo hata CD hazikuwepo

Kwanza wajukuu maximum ni 25 Hivi
Kwa bibi kulikuwa ng'ombe wengi zaidi ya 100!!

Babu alikuwa mkarimu mno na bibi pia.....tukifika tu tunachinja wenyewe mbuzi kubwa la kuchoma tu yaani linaishia juujuu tu kwenye shikome😂

Muda huo Kuna nyama za kubanika zimeshakauka mpaka basi zinaitwa ng'homele kisukuma ni mwendo wa kukata na kuloweka kwenye maji ya chumvi Kisha unakula...

Maziwa sio ya kuuliza ni muda wowote tu unajipimia ....basi wajomba kesho yake mnaenda nao kuchunga pamoja na kuwinda huko mnakutana Watoto shazi mnawinda sungura,digidigi na ndege kama kware ama kanga kama ni masika pamoja na kuchoma uyoga mnakula!!!(Hivi vitu vyote mjini huwezi pata hata ukiwa milionea)


Mkirudi kutoka machungani kulikuwa na bwawa mnaenda kuogelea weee acha tu hapa sio wanawake au wanaume mnaoga mtakavyo maana tulikuwa wadogo wakubwa ndo walikuwa hawaogi...


Mkirudi mtakula mpaka mnakula Tena. Siku ya sikukuu tulikuwa tunaenda kununulia juice cola zile zinaweka kwenye chupa za soda tulikuwa tuna nunua shilingi5 Hadi kumi!!

Michezo ilikuwa mingi sana kuumizwa ilikuwa sehemu ya michezo pia.

Kuna siku hamuendi kuwinda ni Tour ya kusaka matunda pori na kumletea bibi na Babu imagine tulikuwa tunaanza saa3 Hadi saa8 ndo tunarudi na mizigo ya matunda tumechoka mbaya😹😹

Sisi video kipindi chetu huwezi kuikuta Kijiji kiza hata Kwa diwani huikuti wewe ulichoelezea ni miaka ya 2007 hapa tu Kuna CD/DVD!!

Ukweli na miss sana enzi hizo Kuna mto maji tulikuwa tuna yaziba Kisha tunakamata samaki na vidagaa mkimaliza ni kuchoma hapohapo pilipili tulizia huko kula acha kabisa

Kuna matunda mizizi Yale uking'oa linakuwa kama muhoga ila Lina maji tupu matunda Yale hata nyani wanayapenda sana..

Ni vingi vya kuelezea hii ni miaka ya 1995-2002 Hivi acha kabisa
View attachment 3286837
Umesimulia hadi nimejikuta natabasamu pekeyangu,. Ila maisha haya raha sana aisee ukiwa kwa wazee
 
Nyie mlikuwa wa kishua
Sisi ukienda kwa bibi mtachota maji mtoni mtachanja kuni
Mtaenda shamba
Kukamua ng'ombe na kusafisha zizi
Michezo yetu ilikuwa rede,kombolela n.k
Mambo ya cd hatukuwa nayo ni mwendo wa VHS zile mnaangalia kwaya za kkkt Mkichoka mnaweka za kinaijeria au Neriaaa
Sisi tulikuwa wadogo sana tatizo, Tusingeweza vyote hivyo😃😄
 
Sisi kwetu likizo ilikua kama camp ya mateso ni mwendo kwenda shamba hapo kulima, kuchimba mashimo ya kupanda migomba, kutifua & kupalilia pia kusomba majani hapo mpaka likizo iishe ushakua mweusi mweusi hivi
Eti ushakuwa mweusi mweusi hivi,.
Ila we jamaa😂😂
 
Nyie mlikuwa wajukuu wa kishua. Mambo ya CD na snacks.

Sisi michezo yetu ilikuwa kombolela, na kuiba kamba za bibi tunafunga bembea zile za kwenye mti . Halafu kuna kwenda kuogelea mtoni huko na kula vimatunda pori.
Nimeshtuka aliposema zamani Kisha akataja vitu vya kisasa imagine tv,deki,CD hadi snack itakuwa mi nimeishi zama za mawe maana kwa bibi ilikuwa Raha unaenda nae shambani we unalima kidogo kidogo ukila mihogo
Ukirudi unasifiwa unajua kulima
 
Awali ya yote zamani ina zama nyingi...

Leejay, hii zamani yenu inaonekana kama ni zamani ya Jakaya Kikwete hivi yenye kupigiana hadi simu ninyi wajukuu, maana nikikumbuka zamani ya simu za TTCL si kaya nyingi zilikuwa na huduma ya zile simu, na hata zikiwepo basi wazazi walikuwa wakizifungia kwenye kiboksi cha mbao chenye kikufuli au ile sehemu ya kuzungusha namba inawekwa lock...

Sisi wengine zamani zetu tulikuwa ni kwenda mtoni au mabwawani huko kuogelea na kuvua visamaki (hii tulikuwa tunapigwa marufuku sana sababu ya matukio ya kufa maji), kwenda porini kutafuta kuni, kwenda porini kuchunga mbuzi na ng'ombe lakini ukiwa mtoto lazima awepo mtu mzima sababu ya matukio ya kunyonya damu (tulikuwa tunaamini kuna nyonya damu 😅)...
Hivi Hawa nyonya damu ni kina nani??, ni watu au wadudu ?? Maana tulikuwa tunatishiwa sana hadi mtu unaogopa kutoka njee😆😂😂,.

Simu zilikuwa za wazazi mkuu,. Labda anapiga uncle anawapa binamu na mzee atanipa Mimi au labda dada angu tunaongea nao hivyo . Ni miaka ya 2014 kurudi huko nyuma ndiyo nilikuwa shule ya msingi enzi hizo
 
Nimeshtuka aliposema zamani Kisha akataja vitu vya kisasa imagine tv,deki,CD hadi snack itakuwa mi nimeishi zama za mawe maana kwa bibi ilikuwa Raha unaenda nae shambani we unalima kidogo kidogo ukila mihogo
Ukirudi unasifiwa unajua kulima
Eti zama za mawe😂😂😂,.
Maneno Huwa mnayatoaga wapi ?? ..

Ila sijui kwanini ukiwa unaishi kwa bibi Kuna Ile feeling ya comfortability hadi raha
 
Mie na dada angu tulikuwa tunabeba zetu TV ,. Binamu zetu wengine wa mwanza walikuwa wanabeba deki,. Wa arusha walikuwa wanabeba CD ( baasi hapo kila mtu ataagiza movie anazozitaka wao kazi yao kuzifatuta zilizotafsiriwa wanakuja na CDs Kibao ),. Wengine wa Dar ilikuwa kazi yao kubeba snacks ,.Wengine mipira midoli yaani Ili mradi tu kila mtu awe na chakubeba …
Mkuu una miaka mingapi? Maana haya mazingira ni ya juzi hapo enzi za kikwete na unasema ulikuwa bado mtoto.
 
Hivi Hawa nyonya damu ni kina nani??, ni watu au wadudu ?? Maana tulikuwa tunatishiwa sana hadi mtu unaogopa kutoka njee😆😂😂,.

Wakubwa walikuwa wanasema ni watu...

Simu zilikuwa za wazazi mkuu,. Labda anapiga uncle anawapa binamu na mzee atanipa Mimi au labda dada angu tunaongea nao hivyo . Ni miaka ya 2014 kurudi huko nyuma ndiyo nilikuwa shule ya msingi enzi hizo

Kama ni 2014 kwenda nyuma basi ndio maana sijaona ni zamani ya ambayo mimi naiona zamani...
 
Back
Top Bottom