Nimeamua kuwa Atheist

Nimeamua kuwa Atheist

Hakuna anaewafuata kanisani au misikitini kuwataka uthibitisho wa uwepo wa Mungu , unajua kwanini?
Kwa sababu nyie sio waumini wa hizo nyumba za ibada kama ambavyo hakuna muislamu anaenda kanisani kubishana kuhusu Yesu ni Mungu au si Mungu au mkristo anaenda msikitini kubishana kuhusu utume wa Muhammad.
 
Kwa sababu nyie sio waumini wa hizo nyumba za ibada kama ambavyo hakuna muislamu anaenda kanisani kubishana kuhusu Yesu ni Mungu au si Mungu au mkristo anaenda msikitini kubishana kuhusu utume wa Muhammad.
Upo sahihi wala hauwezi kuta mimi naeleza au kupinga chochote kwenye jukwaa la dini humu jf.
 
Kama ni imani tu wala hakuna uthibitisho, hivyo basi hakuna sababu ya kutaka na mimi niamini, kuamini ni haki yako wala hakuna anaekunyima kufanya hivyo .
Na hakuna anayekulazimisha kuamini mkuu.
 
Upo sahihi wala hauwezi kuta mimi naeleza au kupinga chochote kwenye jukwaa la dini humu jf.
Wewe kupinga popote wala sio kosa kabisa, kama ilivyo kwamba mtu kueleza imani yake popote sio kosa.
 
Hakuna anae nilazimisha ili ukisema yupo ni haki yangu kutaka uthibitisho , wala ukishindwa kufanya hivyo hakuna tatizo .
Kwamba mie nikisema Mungu yupo inakuwa haki yako kunidai mie uthibitisho?
 
Wewe kupinga popote wala sio kosa kabisa, kama ilivyo kwamba mtu kueleza imani yake popote sio kosa.
Naelewa misingi ya imani ni ndani ya box la imani tu na sio fikra huru , hivyo siwezi pinga chochote kanisani wala msikitini au kwenye majukwaa ya dini ambayo yamefungamanishwa na misingi ya kiimani tu
 
Kwamba mie nikisema Mungu yupo inakuwa haki yako kunidai mie uthibitisho?
Angekuwepo na mimi na wewe tunajua hilo , wala kusingekua na haja ya wewe kuniambia kuwa yupo .

Hivyo kama unajua yupo ni haki yangu kukuhoji uwepo wake , ila sio lazima wewe uthibitishe huenda umeropoka tu
 
Huo ndiyo ukweli mkuu. Kila mtu anazaliwa bila kujua mambo ya dini au Miungu.
Ila mazingira utakayokulia ndiyo yataamua unakuwa muislam au mkristo, budha nk
Upo sahihi kabisa
 
Kwanza kabisa, kisichopo hakithibitishiki kwamba hakipo.

Narudia tena, kisichopo, hakithibitishiki kuwa hakipo.

Kwa sanabu hakipo, na kama hakipo, hakithibitishiki kiwa hakipo, uthibitisho unaendana na kilichopo.

Tunaweza kujenga hoja kama za proof by contradiction kuonesha contradiction zinazoonesha kitu fulani hakiwezibkuwapo. Katika hii dhana ya Mungu (mjuzi wa yite, mwenye uwezo wote na uoendo wote) hayupo, nimeelezea sana Epicurean Paradox mpaka michoro nineiweka hapa. Googke Epicurean Paradox, soma, ielewe, kama una swali kuhusiana an Epicurean Oaradox lilete hapa.

Zaidi.

Mzigo wa uthibitisho unamuangukia yule anayesema kitu kipo.

Ndiyo maana Polisi wakija nyumbani kwako, wakisema una madawa ya kulevya, wao wanaosema una madawa ya kulevya wanatakiwa wafanye msako mpaka wayapate, wathibitishe yapo.

Hawakwambii wewe unayesema huna madawa ya kulevya uthibitishe huna madawa ya kulevya.

In principle, we cannot prove a negative, but we can show contradictions that shows the impossibikity of a negative.

Swali la kuuliza hapa, ni kuwauliza wanaosema Mungu yupo, wathibitishe Mungu yupo.

Unasema Mungu yupo?

Kama unasema hivyo, thibitisha Mungu yupo.
Mungu yupo, ndiye Muumba wa kila kitu mwenye uwezo usiyowezwa na alivyoviumba, mwenye ujuzi wa kila kitu alichokiumba ni yeye ndiye mwenye kuendesha mambo ya kiulimwengu na walimwengu.
 
Imani zote ni imani tu hazina uthibitisho wa imani ya kweli wala ya uwongo , hiyo ya kusema imani yako ndio sahihi na inapaswa kufuatwa ni ego za kimani na kampeni zake tu
Tafsiri ya imani ni kuamini,kuamini maana yake ni kua na hope au matarajio,

Kifupi ni kwamba Imani ni jambo ambalo linaaminika ila haliwezi kuthibitishwa physically,ndio maana ikaitwa imani,maana yake kuamini,

So,binafsi hua sioni mantiki ya watu kubishana kwenye issue ya "Imani" issue ya kuamini jambo.
 
Mungu yupo, ndiye Muumba wa kila kitu mwenye uwezo usiyowezwa na alivyoviumba, mwenye ujuzi wa kila kitu alichokiumba ni yeye ndiye mwenye kuendesha mambo ya kiulimwengu na walimwengu.
Hii ni kauli ya imani.

Imani si uthibitisho. Unaweza kuamini hata uongo.

Unaweza kuamini wewe ndiye huyo Mungu.

Lakini je, kuamini kuwa wewe ndiye huyo Mungu, kunakufanya wewe uwe huyo Mungu?

Thibitisha huyo Mungu yupo.

Usiweke kauli ya imani tu.
 
Tafsiri ya imani ni kuamini,kuamini maana yake ni kua na hope au matarajio,

Kifupi ni kwamba Imani ni jambo ambalo linaaminika ila haliwezi kuthibitishwa physically,ndio maana ikaitwa imani,maana yake kuamini,

So,binafsi hua sioni mantiki ya watu kubishana kwenye issue ya "Imani" issue ya kuamini jambo.
Sio kubishana mkuu, sema watu wanaoamini wanaona kama ni kubishana kwa sababu wao wana amini imani zao ndio ukweli wa mambo , sasa ukitaka kuhoji wewe ulie nnje ya imani ya huo ukweli upo vipi ndipoo jambo likaonekana kama unawabishia .

Africa mtu akikuhubiria mambo ya Mungu ukimwambia wewe hauamini Mungu anapandisha ukichaa kabisa ,nafikiri wewe unajua na unaweza linganisha bwashee
 
Sio kubishana mkuu, sema watu wanaoamini wanaona kama ni kubishana kwa sababu wao wana amini imani zao ndio ukweli wa mambo , sasa ukitaka kuhoji wewe ulie nnje ya imani ya huo ukweli upo vipi ndipoo jambo likaonekana kama unawabishia .

Africa mtu akikuhubiria mambo ya Mungu ukimwambia wewe hauamini Mungu anapandisha ukichaa kabisa ,nafikiri wewe unajua na unaweza linganisha bwashee
Labda nitake kujua tu,

Lengo la mtu aliye nje ya dini kuhoji issue ya uwepo wa Mungu au dini,hua wanahoji kwa lengo gani hasa?

Na majibu watakayoyapata ambayo yapo kwenye matarajio yao,hua wamejiandaa kubadili uamuzi wao au ni kuuliza tu?
 
Hii ni kauli ya imani.

Imani si uthibitisho. Unaweza kuamini hata uongo.

Unaweza kuamini wewe ndiye huyo Mungu.

Lakini je, kuamini kuwa wewe ndiye huyo Mungu, kunakufanya wewe uwe huyo Mungu?

Thibitisha huyo Mungu yupo.

Usiweke kauli ya imani tu.
Mungu anataka kuaminiwa kwa imani tu, hajataka athibitishwe kwa logic na akanushwe kwa falacy, kwani ufahamu wetu upo kinyume na uhalisia wake. Sisi ufahamu wetu unataka uwe kwenye mipaka ya wakati na mahali, wakati Mungu yupo kinyume na hicho.
 
Back
Top Bottom