Nimeamua kuwa Atheist

Nimeamua kuwa Atheist

Sasa wanachosahau ni kwamba imani sio kwa masuala ya dini na Mungu tu, sasa mtu anaposema hataki imani kabisa hunishangaza.
kwa muktadha huo unaosema wewe nadhani ni mambo ya misamiati tu,
 
Hatuwezi kuelewana mkuu na si mara moja kuzungumzia issue ya uthibitisho, shida ni kwamba wewe unachukulia kuwa uthibitisho ndio hufanya kitu kuwepo yani kwamba mimi leo nikiuwa halafu mahakamani ukakosekana uthibitisho basi inafanya kuwa mie sijauwa na kwamba umekosekana uthibitisho wa kunitia hatiayani.

Jielimishe mkuu kuhusu uthibitisho.
Wewe ndio unapaswa kujielimisha kuhusu uthibitisho.

Mpaka useme Mungu yupo, ina maana tayari unajua na una uthibitisho wa uwepo wake.

Sasa mkiambiwa mthibitishe Mungu yupo, hamuwezi. Ila mnakataa kwamba hayupo.

Kama unakataa Mungu hayupo na umeshindwa kuthibitisha Mungu yupo, Unataka nini zaidi?
 
Kwanza kabisa, kisichopo hakithibitishiki kwamba hakipo.

Narudia tena, kisichopo, hakithibitishiki kuwa hakipo.

Kwa sanabu hakipo, na kama hakipo, hakithibitishiki kuwa hakipo, uthibitisho unaendana na kilichopo.

Tunaweza kujenga hoja kama za proof by contradiction kuonesha contradiction zinazoonesha kitu fulani hakiwezi kuwapo. Katika hii dhana ya Mungu (mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote) hayupo, nimeelezea sana Epicurean Paradox mpaka michoro nimeiweka hapa. Google Epicurean Paradox, soma, ielewe, kama una swali kuhusiana an Epicurean Paradox lilete hapa.

Zaidi.

Mzigo wa uthibitisho unamuangukia yule anayesema kitu kipo.

Ndiyo maana Polisi wakija nyumbani kwako, wakisema una madawa ya kulevya, wao wanaosema una madawa ya kulevya wanatakiwa wafanye msako mpaka wayapate, wathibitishe yapo.

Hawakwambii wewe unayesema huna madawa ya kulevya uthibitishe huna madawa ya kulevya.

In principle, we cannot prove a negative, but we can show contradictions that shows the impossibility of a negative.

Swali la kuuliza hapa, ni kuwauliza wanaosema Mungu yupo, wathibitishe Mungu yupo.

Unasema Mungu yupo?

Kama unasema hivyo, thibitisha Mungu yupo.
Ni nani alikutofautisha kati ya wanyama kama mbwa, mbuzi, ng'ombe na wengineo wasiojua kuchati Wala kutumia sim kama wewe unavochati hadi Kwa kiingereza,

Na hii oxygen unayoivuta inatoka wapi na imeundwa na nani na kwanini iwe tuu hapa duniani na sio kwenye sayari NYINGINE.

Haya maghorofa marefu yanayojengwa na ndege/plane zinazopaa walotengeneza hizo akili walizipata wapi au walipewa na nani
 
Aisee
Wewe nati mlegezo loose Nut , naona umewasha moto halafu umekaa huku unaburudika na ng'weng'we zinavyokabana makoo

1770825973147.png
 
Ni nani alikutofautisha kati ya wanyama kama mbwa, mbuzi, ng'ombe na wengineo wasiojua kuchati Wala kutumia sim kama wewe unavochati hadi Kwa kiingereza,

Na hii oxygen unayoivuta inatoka wapi na imeundwa na nani na kwanini iwe tuu hapa duniani na sio kwenye sayari NYINGINE.

Haya maghorofa marefu yanayojengwa na ndege/plane zinazopaa walotengeneza hizo akili walizipata wapi au walipewa na nani
Unavyouliza "ni nani..." unajuaje "ni nani..." ndiyo swali husika?

Oxygen inakuwa formed katika photosynthesis. Hujasoma photosynthesis? Na kabla ya hapo chain ya atomic synthesis kwenye supernovae inatengeneza oxygen.Kuna sayari nyingine zina oxygen, Mercury ina oxygen, kuna exoplanets kama HD 209458b ina Oxygen.

Ukiuliza waliojenga maghorofa akili wamepewa na nani unajuaje nani ndiyo swali sahihi?

Hayo maswali yako yote, hata nikisema sijui jibu la hata swali moja, hayathibitishi Mungu yupo.

Maswali yanathibitisha wewe hujui sayansi ya msingi ndiyo maana unaona haja ya Mungu kuwepo.
 
Mungu ambaye anataka kuaminiwa hana tofauti na Demu anayetafuta attention ya kuaminiwa.
mkuu,natoka nje ya mada kidogo

unahisi dini na imani kuhusu Mungu ilikuwa na mchango wowote chanya kwenye maisha yako kabla ya kuacha kuamini katika hayo yote
 
Endelea kusubiri uthibitisho, mimi naendelea kumwamini Mungu.

Nyie endeleeni kusubiri uthibitisho

Kila mtu aendelee na imani yake
 
Kwani mara ngapi mnasema hamtaki imani mnataka kujua?

Sasa kama nipo sawa kwanini bado mnataka uthibitisho wa imani? Hao wanasema wanaweza kwa sababu nyie mnasema hakuna Mungu kwa sababu hakuna uthibitisho, mnatumie kutokuwepo huo uthibitisho wa imani kuhitimisha madai yenu kuwa ndio hakuna Mungu.

Atheists humu hawana hoja nyengine kujadili kuhusu Mungu zaidi ya kudai uthibitisho.
Sasa unajili vipi kitu ambacho hakipo?
 
Unavyouliza "ni nani..." unajuaje "ni nani..." ndiyo swali husika?

Oxygen inakuwa formed katika photosynthesis. Hujasoma photosynthesis? Na kabla ya hapo chain ya atomic synthesis kwenye supernovae inatengeneza oxygen.Kuna sayari nyingine zina oxygen, Mercury ina oxygen, kuna exoplanets kama HD 209458b ina Oxygen.

Ukiuliza waliojenga maghorofa akili wamepewa na nani unajuaje nani ndiyo swali sahihi?

Hayo maswali yako yote, hata nikisema sijui jibu la hata swali moja, hayathibitishi Mungu yupo.

Maswali yanathibitisha wewe hujui sayansi ya msingi ndiyo maana unaona haja ya Mungu kuwepo.
Hiyo photosynthesis inayotokana na mimea au jua ni nani alibuni hio mimea au alifanya Hilo jua

Na hizo chain za atomic kwanini zitengeneze oxygen sio carbon dioxide yani nani alizidizaini zitengeneze oxygen

Na hiyo sayansi yote na mpangilio wote kwanini usiwepo kwenye jua au bahari au sayari kama mercury au jupita

Kwanza hiyo sayansi mpaka ikawa sayanzi ilidizainiwa na nani au kivip
 
Endelea kusubiri uthibitisho, mimi naendelea kumwamini Mungu.

Nyie endeleeni kusubiri uthibitisho

Kila mtu aendelee na imani yake
Hawa atheists hawasubiri uthibitisho ndio maana wameshafanya hitimisho kwa kudai hakuna Mungu, ndio maana hata Agnostics wanawashangaa wamewezaje kujua tena kwa uhakika kuwa hakuna huyo Mungu hadi kutoa madai ya kwamba huyo Mungu.
 
Wewe ndio unapaswa kujielimisha kuhusu uthibitisho.

Mpaka useme Mungu yupo, ina maana tayari unajua na una uthibitisho wa uwepo wake.

Sasa mkiambiwa mthibitishe Mungu yupo, hamuwezi. Ila mnakataa kwamba hayupo.

Kama unakataa Mungu hayupo na umeshindwa kuthibitisha Mungu yupo, Unataka nini zaidi?
Ndio maana nimesema kwa uelewa wako wewe huo ina maana hata mie nikiuwa mtu halafu mahakamani ukakosekana uthibitisho wa kunitia hatiani kwa hiyo kesi ya mauwaji maana yake kwako wewe ni kwamba sijauwa kwa kuwa hakuna uthibitisho badala ya kuwa umekosekana tu uthibitisho wa kunitia hatiani.
 
Nitakuwa mwema hadi kwa Bacteria na virus. Hata nikiumwa sitaki matibabu wala kumeza dawa kwasababu zitaua hawa viumbe ambao nao wana haki ya kuishi.
😂😂😂Mkuu usiwe serious sana usije ukajinyonga.

Ukiachana na kina bacteria 🦠 na virus kuna viumbe hai wengine kama vile nafaka karanga mpunga ngano mahindi maharage miwa etc...(zile ni mbegu ujue na zinaishi ukipanda zikaota zinakua zimeingia ktk phase nyingine ya maisha,

Pia matunda mboga mboga nk.
Sasa unaposema unawaonea huruma inamaana wewe ukatishe maisha yako ili hivyo viumbe viishi... Inabidi uvionee huruma na vyakula vya aina yoyote.

We amini nature tu na uelewe kua katika nature kuna kuishi kwa kutegemeana kikubwa tu nature i-balance (balance of nature (food web &food chain) nature haijali nani kaliwa au nani ana umuhimu sana hapa duniani yenyewe inahakikisha kulaneni kadri muwezavyo ila kusiwe na extinction ya species yoyote.
 
Hiyo photosynthesis inayotokana na mimea au jua ni nani alibuni hio mimea au alifanya Hilo jua

Na hizo chain za atomic kwanini zitengeneze oxygen sio carbon dioxide yani nani alizidizaini zitengeneze oxygen

Na hiyo sayansi yote na mpangilio wote kwanini usiwepo kwenye jua au bahari au sayari kama mercury au jupita

Kwanza hiyo sayansi mpaka ikawa sayanzi ilidizainiwa na nani au kivip
Kwamba unataka kusema kuwa nani aliileta ile BIG BANG kabla haijabanguka,😂😂😂 na kuzi-form hizi sayari katika huu ulimwengu.
Kiranga
 
Haikuwa na mchango wowote.

Sanasana ilinipotezea muda kumtegemea Mungu ambaye hayupo.
i don't think so,na imani kwamba the way unawatreat watu uko nje kwenye real life achana na hii life ya JF

80% imetoka katika dini na hofu ya Mungu,pengine utapinga hili kuonesha members hapa how intelligent you are.

pengine sijasoma sana kama wewe na sijui vitu vingi kama wewe lakini i keep learn kila siku.

lakini maisha ya watanzania kwa asilimia kubwa yanafanana

dini zina michango mikubwa sana kwenye malezi yetu pengine you're not ready for this Gumzo.
 
Back
Top Bottom