Nimeamua kuwa Atheist

Nimeamua kuwa Atheist

Ndio maana nimesema kwa uelewa wako wewe huo ina maana hata mie nikiuwa mtu halafu mahakamani ukakosekana uthibitisho wa kunitia hatiani kwa hiyo kesi ya mauwaji maana yake kwako wewe ni kwamba sijauwa kwa kuwa hakuna uthibitisho badala ya kuwa umekosekana tu uthibitisho wa kunitia hatiani.
Habari za mahakama na Mungu hazina uhusiano.

Wewe unakataa kwamba Mungu hayupo, halafu kuthibitisha Mungu yupo huwezi.

Sasa unataka nini?

Una simama wapi?
 
Nimefanya tafiti yakinifu nimekuja kugundua Mungu hayupo. Ni story tu za kutupa matumaini hewa.

Nimeamua kuwa Atheist. Nitaupa muda nao ukizingua namrudia Yesu.

Dhulma, uonevu, usaliti na ukatili umetamalaki sana.

Bora kuamini nature na kuwa mwema kwa viumbe hai hata visivyonekana.

Ni maamuz yangu binafsi.
Ni sawa maana ni uhuru wako
 
Wewe guluguja usiye ubongo wala uti wa mgongo hujui hata herufi za Kiswahili huna cha kuniambia nitumie logic wapi na wapi nisitumie.

Huyo Mungu wako wa hadithi huwezi kuthibitisha yupo, ndiyo maana unakuja na mazingaombwe ya "tumia logic kwenye vitu vingine na si kwenye masuala ya Mungu".

Unajua mtu akitumia logic kwenye masuala ya Mungu, atagundua huyo Mungu hayupo.

Ndiyo maana unabwabwaja hapa lakini huwezi kuthibitisha Mungu yupo.

Thibitisha Mungu yupo.
Athibitishe ili iweje?

Sisi tunaamini Mungu yupo, wewe unaumia nini kwa sisi kuamini hivi?

Kama wewe huamini basi Ishi maisha yako, sisi tayari tumemuona Mungu kwenye maisha yetu siyo lazima na wewe umuone au utake kila muda tukuthibitishie ili iweje? Kama wewe umeshindwa kumthibitisha basi endelea na maisha yako.

Ni ngumu kubadili kitu kinachoaminiwa na kukubaliwa na zaidi ya watu asilimia 98 duniani.

Waache watu waendelee na imani zao na wewe endelea na imani yako.

Kila mtu atazikwa kivyake hivyo amini unachoamini bila kusumbua wengine
 
Wewe guluguja usiye ubongo wala uti wa mgongo hujui hata herufi za Kiswahili huna cha kuniambia nitumie logic wapi na wapi nisitumie.

Huyo Mungu wako wa hadithi huwezi kuthibitisha yupo, ndiyo maana unakuja na mazingaombwe ya "tumia logic kwenye vitu vingine na si kwenye masuala ya Mungu".

Unajua mtu akitumia logic kwenye masuala ya Mungu, atagundua huyo Mungu hayupo.

Ndiyo maana unabwabwaja hapa lakini huwezi kuthibitisha Mungu yupo.

Thibitisha Mungu yupo.
Upumbavu wako ni uthibitisho tosha wa uwepo wa Mungu.
Nyinyi ndiyo mliyotajwa makafiri, kama msingekuwepo tungeitilia shaka maneno ya Mungu, lakini nyinyi mnadhihirisha ukafiri wenu na kufanya maneno ya Mungu kuwa kweli.
Na hiyo misemo yako ni kama mtu aliye-left group.
 
Mbona kama umetupa taulo mkuu 😁
Unajua ukiwa unajadiliana kistaarabu inapendeza zaidi kuliko kuleteana maneno ya kipumbavu.
Hoja za kuleta kusema kuna duara la pembe nne, halipo.
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
Upumbavu wako ni uthibitisho tosha wa uwepo wa Mungu.
Nyinyi ndiyo mliyotajwa makafiri, kama msingekuwepo tungeitilia shaka maneno ya Mungu, lakini nyinyi mnadhihirisha ukafiri wenu na kufanya maneno ya Mungu kuwa kweli.
Na hiyo misemo yako ni kama mtu aliye-left group.
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, angekuwapo, na angekuwa kaumba ulimwengu huu, upumbavu usingeweza kuwapo, popote, kwa yeyote, muda wowote.

Uwepo wa upumbavu, wowote, popote, kwa yeyote, ni uthibitisho Mungu huyo hayupo.

Ila, wewe huwezi kujua hilo.

Kwa sababu unakataa kutumia logic.
 
Athibitishe ili iweje?

Sisi tunaamini Mungu yupo, wewe unaumia nini kwa sisi kuamini hivi?

Kama wewe huamini basi Ishi maisha yako, sisi tayari tumemuona Mungu kwenye maisha yetu siyo lazima na wewe umuone au utake kila muda tukuthibitishie ili iweje? Kama wewe umeshindwa kumthibitisha basi endelea na maisha yako.

Ni ngumu kubadili kitu kinachoaminiwa na kukubaliwa na zaidi ya watu asilimia 98 duniani.

Waache watu waendelee na imani zao na wewe endelea na imani yako.

Kila mtu atazikwa kivyake hivyo amini unachoamini bila kusumbua wengine
Kuamini unaweza kuamini unachotaka, hata uongo.

Kwako nyumbani, msikitini, kanisani, kwenye faragha yako kiimani.

Ila, ukija hapa public square imani yako ni yako, hapa tunadai risiti, tunataka facts, tunataka uthibitisho.

Mimi nimewaacha watu waendelee na imani zao, hata hapa sikutaka kuchangia.

Ila, nimeitwa hapa. Watu wametaka kujua mawazo yangu kuhusu hii mada.

Na mimi imani yangu ni kuhoji imani kujua kama ni za msingi wa kweli ama la.

Sasa na wewe ukiniingilia katika kuhoji kwangu huoni unaniingilia katika imani yangu?

Huelewi wapi?
 
Kuamini unaweza kuamini unachotaka, hata uongo.

Kwako nyumbani, msikitini, kanisani, kwenye faragha yako kiimani.

Ila, ukija hapa public square imani yako ni yako, hapa tunadai risiti, tunataka facts, tunataka uthibitisho.

Mimi nimewaacha watu waendelee na imani zao, hata hapa sikutaka kuchangia.

Ila, nimeitwa hapa. Watu wametaka kujua mawazo yangu kuhusu hii mada.

Na mimi imani yangu ni kuhoji imani kujua kama ni za msingi wa kweli ama la.

Sasa na wewe ukiniingilia katika kuhoji kwangu huoni unaniingilia katika imani yangu?

Huelewi wapi?
Hivi Google ile AI yake ameipa jina gani vile?
 
Je wewe Kiranga unaweza kukaa wiki 2 bila kutumia mawasiliano (simu, computer, etc) na ukajisikia vizuri kabisa?
Swali hili linatokea wapi?

Lina uhusiano gani na mada iliyopo hapa?

Lina umuhimu gani?

Mbona kama linatoka kwenye mada na kumfanya Kiranga kuwa mada?
 
Swali hili linatokea wapi?

Lina uhusiano gani na mada iliyopo hapa?

Lina umuhimu gani?

Mbona kama linatoka kwenye mada na kumfanya Kiranga kuwa mada?
Basi mkuu yameisha

Mimi Naamini Mungu yupo na silazimiki kukuthibitishia chochote wewe

Kama wewe huwezi kumuamini mpaka upate uthibitisho ni maamuzi yako binafsi tusisumbuwane

Wala mimi sikushawishi au kukulazimisha kumuamini Mungu, Ishi maisha yako kama ulivyoamua

Have a great day.
 
Basi mkuu yameisha

Mimi Naamini Mungu yupo na silazimiki kukuthibitishia chochote wewe

Kama wewe huwezi kumuamini mpaka upate uthibitisho ni maamuzi yako binafsi tusisumbuwane

Wala mimi sikushawishi au kukulazimisha kumuamini Mungu, Ishi maisha yako kama ulivyoamua

Have a great day.
Hayajaisha mpaka ujibu maswali.

Swali hili linatokea wapi?

Lina uhusiano gani na mada iliyopo hapa?

Lina umuhimu gani?

Mbona kama linatoka kwenye mada na kumfanya Kiranga kuwa mada?
 
Hayajaisha mpaka ujibu maswali.

Swali hili linatokea wapi?

Lina uhusiano gani na mada iliyopo hapa?

Lina umuhimu gani?

Mbona kama linatoka kwenye mada na kumfanya Kiranga kuwa mada?
Jinsi ulivyo hukujipangia, hukuanza tu kuwa mpenda sayansi na mawasiliano

Nyota yako ipo hivyo, you are a Gemini na una akili ya pekee kwa kuzaliwa (by nature), unaongozwa na sayari ya mawasiliano inaitwa mercury.

Najua huamini masuala ya Nyota na pengine unaweza hata kunitukana but I have studied you for so long huwezi kumaliza masaa 24 hujaingia Jf

You are in this way by natural design not by your will.

Pia kuna sehemu nimekuona unatetea mambo ya ubinadamu (mfano unakemea sana mauaji na unyanyasaji) hivi vitu havitokei tu they are in your DNA by the natural design (siyo kila mtu yupo hivi).

You are humanitarian by nature though sometimes you act as a gaidi it's all part of your design (ni mapacha wewe).

Kwahiyo my friend ni uwezo wako wa asili wa kuwa na akili nyingi sababu ya Nyota yako (gemini) ndiyo umekufanya kupenda sayansi na kuhoji kila kitu hadi kuhusu Mungu

Najua utanijibu >nonsense (I know you).
 
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, angekuwapo, na angekuwa kaumba ulimwengu huu, upumbavu usingeweza kuwapo, popote, kwa yeyote, muda wowote.

Uwepo wa upumbavu, wowote, popote, kwa yeyote, ni uthibitisho Mungu huyo hayupo.

Ila, wewe huwezi kujua hilo.

Kwa sababu unakataa kutumia logic.
Nini umeelewa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote?
Vipi unaweza kuzungumzia kuhusu hiari ya mwanadamu?
 
Habari za mahakama na Mungu hazina uhusiano.

Wewe unakataa kwamba Mungu hayupo, halafu kuthibitisha Mungu yupo huwezi.

Sasa unataka nini?

Una simama wapi?
Bado narudia kusema kwamba hatutoweza kuelewana ikiwa bado una mtazamo usio sahihi kuhusu uthibitisho.
 
"kua mwema kwa viumbe hai hata visivyoonekana"

Sasa unakataa MUNGU hayupo kwasababu humuoni halafu hapo hapo unaamini kuna viumbe visionekana!
 
Back
Top Bottom