Arsis Jamiix Hayo maneno ni dua nzuri sana kwa ajili ya kujikinga na madhara na ubaya. Ntajitahidi kuweka maana yake.
KIARABU - بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لَا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
YANAVYOTAMKWA - "Bismillahi lladhi la yadurru ma'a ismihi shay'un fil-ardi wala fissama'i wa huwa as-sami'ul-'alim."
ENGLISH TRANSLATION - In the Name of Allah, Who with His Name nothing can cause harm in the earth nor in the heavens, and He is the All-Hearing, the All-Knowing.
TAFSIRI YA KISWAHILI - "Kwa jina la Allah, ambaye, Kwa jina Lake hakidhuru chochote kilicho ardhini wala mbinguni, naye ni Mwenye Kusikia na Mwenye kujua."
Tafsiri ya Maneno
- بِسْمِ اللَّهِ (Bismillahi) - Kwa jina la Allah
- الَّذِي (alladhi) - Ambaye
- لَا يَضُرُّ (la yadurru) - Hakidhuru
- مَعَ اسْمِهِ (ma'a ismihi) - Kwa jina Lake
- شَيْءٌ (shay'un) - Kitu
- فِي الْأَرْضِ (fi al-ardi) - Katika ardhi
- وَلَا فِي السَّمَاءِ (wala fissama'i) - Wala mbinguni
- وَهُوَ (wa huwa) - Naye ni
- السَّمِيعُ (as-sami') - Mwenye kusikia
- الْعَلِيمُ (al-'alim) - Mwenye kujua/maarifa
Tafsiri ya Jumla
Dua hii inasema kwamba, kwa jina la Allah, jina Lake linatoa kinga dhidi ya madhara yoyote katika ardhi na angani, kwani Yeye ni Msikivu na Mwenye maarifa yaani mwenye kujua..