Vionjo vya Arsis 5-5
nilivyokutanishwa na majini ya Kingazija (Comoros) na Kipemba Kojani.
Alipoondoka Jini 1 nikakaa nikajifikiria niende au nisiende kwa Arsis, nikaamua niende, linalowezekana leo lisingoje kesho.
Nikampigia kijana mshikaji nikampa dili ya kupeleka gari Upanga nikamwambia ukiningoja sehemu nitakupitia turiudi wote, aua ukirudi mwenyewe sawa. Nikamwambia akimaliza huko anipigie anicheki niko wapi, niakua mitaa sio mbali na Upanga.
Nikatoka nikaitoa gari ya Dokta nje, kijana akaja nikamkabidhi aipeleke, nikampigia Dokta, nikahisi kama alikua usingizini, nikamueleza, akanishukuru akasema alikua anafikiria asubuhi atakwendaje kwenye kazi zako. Nikamwabia usijali, akikufikishia huyo kijana nipigie hata saa ngai unijulishe, na alichelewa ikipita lisaa limoja kuaniza sasa nijulishe. Akasema sawa.
Mimi nikaondoka kuelekea kwa Arsis. Kufika langni oshen roodi, kama kawaida nikaita akaja kwa sauti tu.
Arsis: Vipi hali, Simba?
Mimi: Sio poa.
Arsis; Huku anacheka, nimeona babu yako kakupatia mchumba mpya. Unasemaje.
Mimi: Arsis sipo hapa kwa kufanyiana utani, nimekuja hapa nikuulize vitu.
Arsis: Unafikiri natania, hio ndio fikira za babu yako. haya uliza.
Mimi: Arsis, majini wako wamenielezea mengi kuhusu huyo Dokta na mazee Ali lakini kuna mengine wamenambia nikuulize wewe.
Arsis; Nafahamu, kuna vitu hawajui, uliza tu Sumba.
Mimi; Nani huyu Dokta?
Arsis: huyo ni Dokta kweli ytena Daktari bungwa amesoma Urusi, Japan, Australia na ameishi sana Uingereza, kweli ameolewa na madakatari wawili zamni, mmoja ndio mume wake wa kwanza na ni dokta mkubwa sana Tanzania. Huyo wa pili aliolewa kama hasira tu alipoachika na mumewe wa kwanza, Huyo wa pili mtu wa kwenu anga, walikutana walikua wanafanya kazi pamoja. lakini wameachana pia. Ngumu sana huyo kukaa na mume. Ana mengi sana.
Mimi ; Hilo ndio swali langu, kwanini hakai na mume?
Arsis: Huyoi ana mtu alimpoenda sana lakini huyo mtu sio kiwiliwili ni nafsi tu. Ni binadam alaieuliwa lakini nafsi yake haijaingia kwenye umauti.
Mimi: hapo unanichanganya Arsis.
Arsis: naahamu, kwa kua hauna elimu ya majini. Majini wengi sana ni nafsi za watu. Huyo kija n wa Kiarabu ni katika waliouliwa wakati wa mapinduzi Unguja, alidhulumiwa maisha yake, nafsi ipo hai lakini mwilli umekufa na umezikwa kwenye mashimo ya halaiki, Ni kijana wazazi wake walikua kwenye baraza la Sultan lakini hawakua serikalini ni washauri tu. nafsi yake ikawa inatembea tembea sana mpaka leo, huko Unguja, hususan sehemu alipomuona mara ya kwanza Dokta, na maeneo ya nyumbani kwao huyo kijana, karibu ya forishani kwenye majumba ya matajiri siku hizo. Alipomuona Dokta, siku hizo mwanafunzi sekondari, akampenda ndio akawa hatoki kwa Dokta.
Mimi: hatoki vipi?
Arsis: Yupo nae karibu na akamuoa kivuli chake, kwa sababu hawezi kumuoa mwili wake, mpaka sasa anaamini ni mkwe na aana wivu sana hataki mwili wa Dokta uolewe au utembee na mwanamme wengine, akiokewa akitemnbea na wanaume wengine, huyo kijana anatuma rafiki zaake wa kijini wahuni wanamtesa sana Dokta, mpaka imefikia hapendi kabisa wanaume. Kwa bahati mbaya sana mpka akajatribu usagaji lakini hakuupenda akaachana nao kabisa. Alifanya lajini kwa muda tu, alikua na mwanamke wa kibindam mmoja Zanzibar, akaachaa nae kwa ajili ya huyo kijana, alimtesa sana huyoi mwanamke na marafiki zake, ytule mwanamke akaamkimbia Dokta. hataki hata kusikia sauti yake, anamuogopa kabisa.
Huyu wa pili wa hapa hapa Dar, huyu muhunimuhuni sana, huytu hatraki mapenzi ya kweli anatagfuta pesa tu, ni rafiki yake Dokta, lakini hata yeye sio masagaji wa kweli ni muhuni tu, ndio akapna huyu hana mume na mzuei hivi labda msagaji, akaanza kumjribu waksagana ndio wakaanza hivyo, yule anajua jua ni juhuni sana. Dokta nae alihjifunza funza kwa yule wa Unguja, sasa mara moja wakawa wakikuta wanasgana. Lakini haikuchukua muda, Dokta akawa anajichukia kufanya huo uchafu akaacha kabisa, miaka mingi sana sasa. Alikua anaogopa binti yake anakua halafu amuone vile mamake, analala chumba kimoja narafiki yake. Dokta akajifikiria sana akamuomba Mwenyezi Mungu akamuondoshe ahyo kabisa. Akasema boira hayo majini ya ndotoni kuliko huu ushenzi.
Maana yule kijana anakuja kuingiliana nae kwa kivuli, hio ndio inakua ndoto tu. Umeelewa?
Mimi: Inaingia akailini lakini sijaelewa vizuri.
Arsis" Sio lazima uelewe kila kitu mara moja, utaelewa tru kidogo kidogo. Dunia iina siri nyingi sana.
Mimi: sasa hao majini wa kwao hawajauia hio hali ya kuingiwa na jini wa Unguja na hawa wanawake wasagaji?
Arsis: Majini ya kibuki ya ukoo wale hayaingilii kabisa mambi yake binafsi, wenyewe hao vibuki wapo wasagaji wapo mashoiga, hawaingiliaa maisha ya mtu binafsi, wao yao ni starehem kuvaa vizuri, kula vizurui, kua na pesa na kujionesha tu. Wanapenda sa harusi na misiba. Ni majini wasio na akli labda wale waliojaaliwa kutoka kizani. Wana mila za ajabu sana haoi Simba.
Hao hua wanaalikana kulewa tu ili kumkaribisha binadamu mwenye kibuki. Bila pombe hapo yule boinadam hakubaliwi. Na ukiwakubalki hao ukiwapa mapombe wanajuana wenyewe kama ile jini yenu ya Simba. Kila kitu utaona inakwenda vizuri.
Mimi: sasa yeye kwanini wanamtesa?
rsis: Wale kibuki wanaubaguzi sana, wapo ukoo wa baba yake na wapo ukoo wa mama yake, kila mmoja anataka kujionesha nani zaidi. Halafu wote koo hizo wanakubaliana kitu kimoja, kua huyu ni wa kwao halafu mpaka leo hajaolewa kwa ada yao ya harusi.
Mimi ; Ndio nini hiyo?
Arsis: Muoe wewe utajua ndio nini hiyo.
Mimi: Arsis sitaki utani, mi simtaki kumuoa kabisa.
Arsis: usikasirike ni mwanamke mzuri na ataemuoa akifanya ada yao ya Kingazija, atafaidi sana na yule nafsi ya jini haitamsumbua tena si uliambiwa wana mikataba yao?
Mimi; Siiji, hio ndio nilitaka kukuuliza.
Arsis; Nafsi wamekubaliana na hawa kibuki wasiingiliane na hiyo nafsi haiwei kumuoa huyu ibaki hukohuko imeoana na kivuli la sivyo ikimuingilia sana huyiu mwanamke maboi yake ya kibdamu inakua hio nafsi inawatia matatani hao binadam wengine. inaoatuma kupitia majini washenzi. Nfasi hizo zinaonana Arsis, kama wewe unavyonana na miili ya wengine. Hmuingilini mmbo yenu. Ni hivyo hivyo kwa nafasi na zinawea kua na mahusianoi kama nyinyi mlio na miili, hakuna togfauti.
Mimi: sasa wewe Arsis unamsaidia vipi?
Arsis: kana tunataka kuingia makubaliano na majini wakubwa wa vile viujini vya Mzee Ali viondoke x)visimfatefate kabisa. Ndio tunataka wewe umsindikiz Kojani, ipo safari karibu sana.
Mimi: kwani mimi")?
Arsis: kwa sababu wewe ukiwepo huko na yeye anakua kaona mtu mwingine anemfahamu anaiukua hana wasiwasi sana. Hawa(ezi kwenda peke yake, na mambo yaliomtokea kwa marafiki zake, sasa hivi anaogopa hata kua na rafiki wa karibu mwanamme au mwanamke, kapitia mengi sana huyo Dokta, kama isingekua majini hya kwao kumlinda na wachawi, sasa hivi huyo wehu au matrehemu.
Mimi; kwanini?
Arsis: huyo mumewe wa pili alikua na mke, huyo mwanamke akaanza kumrpga kwa kila aina ya waganga na wachawi lakini amtokeo yake huyu Dokta hajadhurika kashurika mumewe na yeye, lakini walishaacha yule mwanamke akamini iau amemshinda huyu kwa aganga wake. Hajijui masiki ya Mungu. N huyu Dokta alikua anota ota anafanyiwwa uchawi lakini alikua anaona ndoto tu hizo. Ni mamboi mengi lakini cha muhimu, sasa anahitaji aolewe, ndio njia ya kumsaidia na arudishe furaha na amani yake asiogope tena binadam wenzie. Na hio ni rahisi sana. Kwanza waondoke vijini vya Mzee Ali, muongo tu tapeli yule. Mimi nashauri kabla hujaenda Pemba nenda Unguja ukaonane na mkubwa wa vibuki vya upoanda wa babake, ukiend tu pale watajua umefata nini na hawatamvumbua tena, sisi tutakua tayari tunfanya mikataba nao. Lakini mimi nataka uende ukaione dunia, siku mbili tu inakutosha. Ukaone na sherehe yao ya pombe, lakini huyu atakua ytauari hataki hio sherehe, akiifanya huko basi kataka mwenyewe tu sio vibuki. Fanyta uende huko.
Mim: msiniinginze kwenye mamboi yenu, sitaki vita na majini.
Arsis; hakuna jini duniani anaeweza kufanya vita na wewe, akiona hio ete tu wanakimbia mbali sana na wanakuheshimu sana, Madini ya hio pete sio ya kawaida hata Mafalme wa kijini wanayatak hawayapati. Wafalme akijini wakiipayta hio peyte ulioivaa wapo tayari kukyufanya tajiri mkubwa duniani, wao wanachotaka ni hicho kito na hio chuma iliochnganywa hapo, waiyeyusha hio hawajali muhuri uliopo hapo, watan)vunja nia za mwasiliano tulizoiwekea, itakua saa watafanya mawasilano na watu wanaotaka wao, na sana ni watu hatari na wenye nguvu duniani. Simba kwa sasa inatisha, lazima uende Unguja, vipi mimi sijui, mimi nakushairi tu nenda ili urudishea maisha ya mtu huyu muhimu sanakwenye hadhi yake.
Mimi; Ana umuhimu gani?
Atsis: huyo dakatariamesoma sana na ana ubunifu sana kwenye kazi yake, ndio maana hata Wazungu wanamtaka duniani huko, huyo sasa hivu yupo Tanzania lakini amaeajiriwa na chuo kikubwa cha Wamarekani, unafikri watamuajiri mtu hovyo hovyo? Sasa kanini asiajiriwe na Srerikali ya tanzania ikawa fanida kwa Watanzania? Fikiri hilo, isiache hizo safari mbi na ya tatu itakua ngazija, ukaone ada ya harusi za wangazzija labada itakujia hamu ya kuoia mngazija.
Mimi: Arsis; kwaheri.
Arsis; kwaheri huku anacheka.
mimi nikaondoka pel kufika kwenye gari nikatazama zi,mu yangu nikakuta yule dokta alinipigia muda si mrefu kama dakika kumi nyuma na yile kijana kama nusu saa nyuma. Nikaanza na Dokta, nikampigia hata haikuita mata)ra mbili aka[pokea.
Dokta: Hello, Simba? Nilikupigia kukujulisha tari imeletwa, Ahgsante sana. Sasa hivi nipo fresh kabisa, imekua viuri nilichukua wale kuku pale hivi nawala sasa hivi, nimeipenda juisi yao.
Mimi: Okay poa, hakuna shida, si umeshapajua pale?
Dokta; Napajua pale siku nyingi lakini ndio mpaka niende na wenzangu. Lakini nilikua sijawahi kunywa hii jiuisi yake, nilikua naagiza soda tu.
Mimi: Nikahisi kama anahamu ya kuongea zaidi, nikamkatiz; Sawa Dokta, mradi gari imefika salama na wewe upo salama tuombeane dua tu.
Dokta; Kuna kitu nilitaka kukuuliza kuhusu Mzee Ali.
Mimi: Dokta naendesha sasa hivi nimesimama kuona miss call yako, tu tuongee kesho, samahani.
Dokta: Bila samahani, nitakupigia kesho, niasmehe sana.
Mimi; No problrm ahsante.
Tukaagana pale nikampigia mshikaji aliepeleka gari.
Mshikaji: Hoyaa Simba, mimi nishaondoka s)muda mregfu nimempa gari yule dada, nilitamani anikaribishe ndani, yupo bomba kishenzi. Nitum tana kwake.
Mimi; Ushafika ilala?
Mshikaji: bado natumiampesa alionipa, yule dada ana poesa ndefu sio njaa njaa kama wewe.
Mimi: Unatumia peke yako? Nambi uko wapi na mimi nije.
Mshikaji: Wewe hupawezi hapa tunapotumia sisi nipo kariakoo, wewe nenda tu tutaonana mitaani.
Mimi: kariakoo sehemu gani mimi ndio nakaribia mitaa ya Kariakoo.
Mshikaji: Unapjua Pajero bar? ndio nipoa hapa na mipashkuna ya Kariakoo inaimba taarabu.
Mimi: Mshikaji mpaka unajimwaga hivyo, itakua mshiko mrefu basi?
Mshikaji: Bia za kuzugia ninazo leo lakini za ofa ndio sina au utapiata uniachie kitu?
Mimi; Sipajui wala sipiti kwenye ma bar.
Mshgikaji: Wewe usiingie, piata nje mimi nitatoka?
Mimi: Ipo wapi kwnai, akanielekeza.
Mimi; Pole, sana hapo umeumizwa, napajua sasa. Sipiti njia hio, mimi nipo Mtaa wa Lingdi sasa naelekea nyumbani. Tuwasilane kesho unipe micha[o ya Pajero, kuna moja hili halitoki hapo linaitwa Nusura, jeupoe kama tto kla kigiriki.
Mshikaji; Yupo hapoa na mabwana zake anachuna na mashga zake kibao. Sijui kapata shamba gani la kutokea wapi sijui limaitwa haruna, linatumia hilo kama halina akili vizuri, sijui jambazi hili. Tushapigwa raundi tatu bar nzima hii na hilo jamaa.
Mimi: kwaheri utanipa michapo kesho.
Mshkaji: Hakuna noma, nitume kwa yule DSada saa yypote hata nimepekee ndizi sokini kwa pesa zangu, sitaki uasafiri wala unilipe kitu, ile ndi mi dada ya kujuana nayo si hii ya Pajero, inanuka mibia.
Mimi; kwaheri, nikakata simu, nikajua huyo kishalewa, hanyamazi.
Simba.
...5.6