Niliyoyashuhudia leo Muhimbili

Niliyoyashuhudia leo Muhimbili

Juzi nilienda na mgonjwa mwananyamala nikaambiwa nikaanzie hospitali ya Kambangwa au Magomeni, Mwananyamala ni hospitali ya mkoa. Nikafikiria kama mgonjwa mwenyewe angekuwa amezidiwa ingekuwaje!
 
Duuuuh
Hawa wengine mbona wanajulikana tu kweupee....!!! Jinsi wanavyogeuza vyama vya siasa kuwa mali yao binafsi; Wanavyojisultanisha uongozi wa milele wa chama, na wanavyofisidi ruzuka za chama, huku wakiwapatiliza ama kuwafunga midomo wanaohoji matumizi yasiyofaa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuuuh
Yule mzee aliyejificha chato alidhania kupambana na corona ni kazi rahisi

Sasa inabidi agawe mavazi ya kujikinga na corona kwa madaktali na manesi wote wa Tanzania nzima

Maana hata kama wewe unaumwa maralia doctor ataamini vipi kama wewe huna corona na atakutibia vipi wakati yeye amevaa tisheti na jinsi tu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mgonjwa huwa anatibiwa muhimbili. Ana file hapo
Naamini umeleta taarifa hiyo kishabiki tu na siyo kiuhalisia. Taarifa za uchochezi hazikusaidai kamwe kufikia lengo lako.

Unajua fika Muhimbili ni hospitali ya rufaa. Wagonjwa wanaopokelewa hapo wanapaswa kuwa walio na rufaa tu. Kuimarishwa kwa hospitali za Wilaya na Mikoa, Vituo vya afya na Zahanati nchi nzima, Muhimbili imebaki na jukumu lake la msingi. Hivyo basi, kama ni kweli ulimpeleka mgonjwa wako, ni kwa kimazoea, ndiyo maana umekwama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Eti 'kama anampiga mwizi' Umenichekesha
Niliwahi kuandika humu nilienda tu Zahanati ya karibu kupima Malaria na nilikuwa na kikohozi cha kawaida kutokana na hali ya hewa, Daktari niliyemkuta alikuwa ananiuliza maswali akiwa na jazba kama anahoji mwizi.

Madaktari wapo katika hali ya taharuki kwa kukosa vifaa vya kujilinda na mazingira wezeshi, sasa hivi kama kuna uwezekano wa kujitibia ukiwa nyumbani ni bora ukae na dawa zako za kutosha.

Watu wengi watapoteza maisha kwa hali za utata kwa magonjwa ya kawaida kwa sababu ya kukosa huduma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mgonjwa huwa anatibiwa muhimbili. Ana file pale
Ambacho hajatuambia ni kuwa alimpeleka mgonjwa muhimbili akiwa katokea wapi. Kama ni moja kwa moja si rahisi kupokelewa bila kuwa na rufaa kutokea temeke au hospitali ya chini yake. Vinginevyo angeelekezwa kufuata route ya private palepale muhimbili na mgonjwa angetibiwa kama private

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja
Asee pole sana mkuu! kwa kifupi sasa hivi kila mgonjwa anayekwenda hospitali kwa ajili ya matibabu anakuwa suspected kama mgonjwa wa Covid19, na hii inatoa picha halisi kujua jinsi gani hili janga limeshaenea kiasi kikubwa,.Yani serikali imeshalemewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom