vamda
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 864
- 534
Salamu wote. Corona imetuletea tafrani kubwa. Leo nimempeleka Muhimbili mgonjwa mwenye presha ya kushuka.
Alikuwa mahututi, hawezi hata kuongea. Kufika mapokezi dr mmoja (jina lake sikufanikiwa kulijua) aligoma kumpokea akidai kwamba twende hospitali ya Temeke au Mwananyamala.
Nikamuuliza dr kwa hali ya mgonjwa ilivyo huoni kama akichelewa kupata tiba yanaweza kutokea mengine. Jibu alilonipa nilichoka. Alijibu kwamba mgonjwa bado hajazidiwa na hawezi kumtibu hivyo tuondoke.
Sikuwa na jambo lingine la kufanya zaidi kumpeleka mgonjwa hospitali ya private. Siku hizi ukimpeleka mgonjwa hospitali nyingi (za serikali) akiwa mahututi, ma-dr na ma-nesi wanaogopa kumuhudumia, wanahukumu kwamba kila mtu ameambukizwa Corona.
Wizara ya afya imeshindwa kutoa huduma bora kwa wakati. Wagonjwa wengi wanakufa kwa kukosa matibabu.
Hayo nimeshuhudia kwa macho yangu leo tarehe 30 Machi, 2020 hospitali ya MUHIMBILI saa 7 mchana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Alikuwa mahututi, hawezi hata kuongea. Kufika mapokezi dr mmoja (jina lake sikufanikiwa kulijua) aligoma kumpokea akidai kwamba twende hospitali ya Temeke au Mwananyamala.
Nikamuuliza dr kwa hali ya mgonjwa ilivyo huoni kama akichelewa kupata tiba yanaweza kutokea mengine. Jibu alilonipa nilichoka. Alijibu kwamba mgonjwa bado hajazidiwa na hawezi kumtibu hivyo tuondoke.
Sikuwa na jambo lingine la kufanya zaidi kumpeleka mgonjwa hospitali ya private. Siku hizi ukimpeleka mgonjwa hospitali nyingi (za serikali) akiwa mahututi, ma-dr na ma-nesi wanaogopa kumuhudumia, wanahukumu kwamba kila mtu ameambukizwa Corona.
Wizara ya afya imeshindwa kutoa huduma bora kwa wakati. Wagonjwa wengi wanakufa kwa kukosa matibabu.
Hayo nimeshuhudia kwa macho yangu leo tarehe 30 Machi, 2020 hospitali ya MUHIMBILI saa 7 mchana.
Sent using Jamii Forums mobile app