Nilimwambia atakufa akafa kweli

Nilimwambia atakufa akafa kweli

haya mambo yanawezekana kuwepo

mamangu alinambia unaenda shule lakini hauna muda mrefu utafukuzwa (nilikuwa nimemkera jambo fulani) na kweli wakanifukuza wala hakuonesha kushangaa.

aliwahi mwambia dadangu maneno flani na yakawa ivo, huwa anaogopa kunena mabaya kwa mtu maana hutokea.

kilicho nishangaza ni nduguze wakiugua ama watoto wao humpigia simu na kumuomba awanenee mazuri na kuwaombea wapate nafuu na kupona na huwa ivo.

mkuu leo niambie ni uchawi ama ni nini?
Sio uchawi ni supernatural powers! Nguvu ya kuumba kwa maneno

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu sishangai, Yuko Boss wangu mmoja akikwambia kitu lazima kitokee, akikwambia huyu atavunja hiki, basi kinavunjika, akikwambia huyu ataleta madhara haya kwenye kazi lazima itokee..

Na mwenyewe anasemaga msinikere, Mimi na mdomo mbaya!
Dua mbaya haombewi mtoto, huwezi jua kila mtu ana mdomo wake kina wengine wakikuapiza tu basi yanakutikea kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi wakristo tunashauriwa kulinda vinywa vyetu daima. Yaani mwanadamu alipewa mamlaka ya kuvipa vitu majina na hakika vyote viwe na majina na sifa za majina hayo. (mwanzo 1-2).Adamu aliambiwa awape viumbe wote majina. Hii ina maana ukizoea kumtukana mwanao ukimuita mbwa, paka, kondoo, kichaa, mbuzi, kuku nakadhalika lazima abebe sifa na tabia za wanyama hao.
Lakini mamlaka hizo huambatana sana na mtu ambaye nafsi yake iko ktk haki si kwa wote.
Tujifunze biblia inasema sisi ni Miungu hivyo tunayo sehemu ya mamlaka ya Mungu ikiwa tunayafanya yaliyo mapenzi yake.
Angalizo:Kwenda kanisani ama msikitini kila siku si tiketi ya kufanya mapenzi ya Mungu bali wafanyao mapenzi ya Mungu waweza kuwa popote na wakatambulika kwa matendo yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulimi kiungo kidogo, lakini matatizo yake ni makubwa sana.
 
Natoa ridhaa, ushafurahi?

Hujajibu swali langu. Nani hatakufa?

Hali ngumu ya nchi yangu hainihusu. I am actually embarassed by how much money I make while people are screaming hali ngumu.

Ijumaa tu nimetengeneza faida ya $3,800. That is US dollars. Kwa hela zenu za madafu huko, kwa exchange rate ya leo bongo hiyo ni Tanzanian shillings 8,512,000.

Hiyo ni faida niliyoongeza kwa siku moja. Si msingi, si faida ya mwaka. Ni faida ya siku moja tu.

Na nina uwezo wa kupiga hata mara tano ya hiyo hela kwa siku.

Sasa kama wewe umekwama na hali ngumu ya huko kwenu niombe mkopo tu.

Usifikiri kila mtu ana hali ngumu.
Aiseeeee upo wapi kaka nikufate sio kwa mihela hiyo jamani😉😉
 
Iko hv Mshana kwanza ulikosea sana kumtamkia mtu kifo kwani hakimu wa haki wa mambo yetu yote yawe mazuri au maovu ni Mungu tu. Ndo maana sisi wakristo tuliomwamini Mungu kupitia kazi ya msalaba Mungu anasema kisasi ni juu yake.
Lkn inakupasa ujue kuwa Mungu anasema hafurahii kufa kwake mtu mwovu heri atùbu na kuacha njia yake mbaya. Hvyo Mungu anavuta subira watu wamwamini si matamanio yake wanadamu wapotee japo watapotea kwa kutokuamini kwao.

Hvyo basi ukimtamkia mwenzako mabaya usijedhani eti kwavile ww Mkristo basi ni Mungu ametenda ila ni Adui ametake advantage ya mashambulizi yako kwa mwingine anatakeleza hasa pale ambapo amiyenenewa hana maarifa ya kucounter attack maneno hayo.

So pls tuwe makini tusitumie kauli zetu vby. Ww mwenyewe hapo umethibitisha. Sitarajii ulifurahia kufa kwake yule dada na kama ulifurahia aiseeèeeeee!!!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom