Nilimwambia atakufa akafa kweli

Nilimwambia atakufa akafa kweli

Sina roho ya kisasi inawezekana kabisa siku zake zilifika

Sent using Jamii Forums mobile app
Yote yanawezekana na yasiwezekana.Yanawezaekana kwa sababu kwenye bibilia tunaambiwa maneno ni uzima tena ni roho(yanaishi)Neno lako liliishi kwake ndo maana kweli akafa.

Kama asingekufa pengine tungesema siku zake hazikufika au Mungu alikua na kusudi lake.Ndo maana tunaambiwa tuwe makini na ndimi zetu.Nadhani lilitimia kwasababu uliimaanisha kweli na ulikua na hasira juu yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mimi nikuulize tu mshana jr , ilikuwaje hadi muondoke wote uje umtelekeze? hata mimi ningesema wewe mpenzi wangu kabisa, huwezi nitoroka mbele za watu aibu nipate mwenyewe

teh teh
 
Imepita miaka mitano sasa lakini bado nakumbuka hili tukio
Ilikuwa ni mchana mmoja siku ya ijumaa nilikwenda bar ya Igongwe pale Mwenge karibu na vinyago kupata lunch
Kufika pale nikahudumiwa na binti mgeni hata wa kuhudumia, ndani ya nususaa alikuwa keshaniambia historia yake yote lakini wakati huohuo akiwa keshagonga safari 3,
Nilibaki pale mpaka saa kumi muda aliosema anatoka huku nikiwa nimeshamaliza mzinga wa konyagi... Alikuwa kanihoji na mimi kama ni mwenyeji mitaa ile nikamdanganya nikamwambia mimi mgeni
Baada ya hapo tukaondoka kuelekea Cafe la Tino si mbali sana kutoka pale
Cha ajabu na cha kushangaza kufika pale akajifanya amelewa na mimi ni mpenzi wake.. Mbele za rafiki zangu akawapa cheo cha mashemeji
Kugundua hili nikaamua kumtelekeza kiaina.... Lakini loh kufika tu kwenye gari huyo naye kafika
Nikamkatalia kupanda lakini timbwili alilofanya pale aliishia polisi mabatini
Pale Cafe la Tino alidai ana mimba yangu halafu najifanya kumtoroka, hiyo mimba atalea na nani? Duu .... Siku hiyo nilikuwa nimeingia cha shoga wallah
Kwa hasira nikamwambia kama kweli una mimba yangu mimi nitakufa ila kama hata kama unasema uongo na hatufahamiani kabisa basi utakufa!
Alikaa mahabusu Ijumaa ile mpaka jumatatu nilipoenda kufuta kesi... Alifariki ijumaa ya wiki ile aliyotoka selo! Alilala getho la Igogwe akiwa mzima.. The next day jumamosi ilikuwa zamu yake kufanya usafi, wenzake walipojaribu kumuamsha alikuwa wa juzi ..... Nilipata habari kwa meneja na nikatoa mchango wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mshana. Mdomo unanguvu kubwa sana ya kuumba vitu. Ndo mana hata mimi binafsi nakuwa makini sana na maneno ninayosema.

Nakumbuka nilishawahi kuwa na mahusiano na mtoto mmoja mzuri sana. Hata wewe ukimwona lazma ushtuke lakini tukajagombana na nikamtamkia maneno mabaya sana. Kwamba hutokuja kuolewa kamwe na hadi leo bila bila hajaolewa licha ya kuwa na uzuri uliopitiliza. Hayo maneno niliyasema almost 8 years back. Nikikaaga nae kupiga stori anasema anataka sana kuolewa lkn hapati mtu.

Ingawa bado tuna urafiki, ila amekuwa mchepuko wangu tu sio njia kuu. Nikifikiria huwa nasikitika sana
 
Back
Top Bottom