Nilimwambia atakufa akafa kweli

Nilimwambia atakufa akafa kweli

Duh..Mkuu mshana unatutisha humu?

Maana utafanya watu wakuogope zaidi ya kawaida
 
Ewaaa....

Damu ya Yesu itufunike kila Mshana akitaka kuturoga aone taswira yake mwenyewe.... Mungu wewe ni Mkuu, naomba utulinde na babu yangu, tufiche kwenye mbawa zako mfalme wa amani.... Katika jina la Yesu naomba na kuamini Aaaaammmeenn

Eiiimeeeeeennnn!!
images
 
Imepita miaka mitano sasa lakini bado nakumbuka hili tukio
Ilikuwa ni mchana mmoja siku ya ijumaa nilikwenda bar ya Igongwe pale Mwenge karibu na vinyago kupata lunch
Kufika pale nikahudumiwa na binti mgeni hata wa kuhudumia, ndani ya nususaa alikuwa keshaniambia historia yake yote lakini wakati huohuo akiwa keshagonga safari 3,
Nilibaki pale mpaka saa kumi muda aliosema anatoka huku nikiwa nimeshamaliza mzinga wa konyagi... Alikuwa kanihoji na mimi kama ni mwenyeji mitaa ile nikamdanganya nikamwambia mimi mgeni
Baada ya hapo tukaondoka kuelekea Cafe la Tino si mbali sana kutoka pale
Cha ajabu na cha kushangaza kufika pale akajifanya amelewa na mimi ni mpenzi wake.. Mbele za rafiki zangu akawapa cheo cha mashemeji
Kugundua hili nikaamua kumtelekeza kiaina.... Lakini loh kufika tu kwenye gari huyo naye kafika
Nikamkatalia kupanda lakini timbwili alilofanya pale aliishia polisi mabatini
Pale Cafe la Tino alidai ana mimba yangu halafu najifanya kumtoroka, hiyo mimba atalea na nani? Duu .... Siku hiyo nilikuwa nimeingia cha shoga wallah
Kwa hasira nikamwambia kama kweli una mimba yangu mimi nitakufa ila kama hata kama unasema uongo na hatufahamiani kabisa basi utakufa!
Alikaa mahabusu Ijumaa ile mpaka jumatatu nilipoenda kufuta kesi... Alifariki ijumaa ya wiki ile aliyotoka selo! Alilala getho la Igogwe akiwa mzima.. The next day jumamosi ilikuwa zamu yake kufanya usafi, wenzake walipojaribu kumuamsha alikuwa wa juzi ..... Nilipata habari kwa meneja na nikatoa mchango wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi kumbe mwenye mamlaka ya kufuta kesi ni mlalamikaji?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu sishangai, Yuko Boss wangu mmoja akikwambia kitu lazima kitokee, akikwambia huyu atavunja hiki, basi kinavunjika, akikwambia huyu ataleta madhara haya kwenye kazi lazima itokee..

Na mwenyewe anasemaga msinikere, Mimi na mdomo mbaya!
kiki hizo!
 
haya mambo yanawezekana kuwepo

mamangu alinambia unaenda shule lakini hauna muda mrefu utafukuzwa (nilikuwa nimemkera jambo fulani) na kweli wakanifukuza wala hakuonesha kushangaa.

aliwahi mwambia dadangu maneno flani na yakawa ivo, huwa anaogopa kunena mabaya kwa mtu maana hutokea.

kilicho nishangaza ni nduguze wakiugua ama watoto wao humpigia simu na kumuomba awanenee mazuri na kuwaombea wapate nafuu na kupona na huwa ivo.

mkuu leo niambie ni uchawi ama ni nini?
 
Hivi kumbe mwenye mamlaka ya kufuta kesi ni mlalamikaji?

Sent using Jamii Forums mobile app
Iko hivi baada ya kutokea lile timbwili simu ilipigwa kituo kidogo cha Mwenge wakaja askari wa patrol na defender, wakajaribu kumtuliza lakini akawa kiburi na kuwaporomoshea matusi mazito kabisa.. Kwahiyo akabebwa huku sisi tukidrive,
Tulipofika Mwenge akazidisha fujo ndio tukaenda mabatini, kesi ikafunguliwa mimi nikiwa mlalamikaji na kutakiwa kurudi Jumatatu yake
Niliporudi nikaulizwa kama nina interest ya kuendelea na ile kesi nikasema hapana, ikafutwa
Mlalamikaji ana haki hiyo ila jamhuri ikiamua inaweza kufungua kesi upya kwakuwa msamaha haufuti kosa husika kwa mujibu wa katiba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom