Hali kama hiyo nimeiona kwa rafiki yangu ila yeye anaota na kuona vitu vinavyodhuru ukoo wake.
Alijaribu kuombewa ikashindikana,mchungaji mmoja akwambia hayo ni maono na sio kitu kibaya
Sasa yupo kama mlinzi wa ukoo wake
Usiogope mimisa. Kuna watu wamejaaliwa kuoneshwa baadhi ya vitu kupitia ndoto. Hiyo ni karama Mungu amekupa.
Usiogope ila mshukuru Mungu na kufanya maombi kila uotapo. Mungu atakutumia zaidi na zaidi katika kufanikisha kusudi lake.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Usihofu, kuna watu wanaota ndoto zinakuwa za kweli na wengine zinakuwa za uongo au ni opposite kwa ile ndoto. Hiyo ni strength kwako. Vipi na ndoto nyingine ukiacha za msiba unaota? Na majibu yake unayapata? Unajua wewe unalalamika ndoto ila kuna wengine pia wakisema jambo huwa linatimia. Mimi binafsi nikisema jambo kwa kudhamiria huwa linatimia hasa la kama nimeonewa!!!! Kwa mfano ukinidhulumu mali yangu na kama ni kweli na ikifikia mwoshowe nikakuambia kuwa sitakudai tena ila itapeperuka kama upepo, na itatokea kweli. Kama ni jambo jema pia ninataka kumwomba Mungu anifanyie nikiaminia huwa linatokea. Kwa hiyo huwa mara nyingi najitahidi sana kuchunga ulimi wangu pale ninapopata hasira ya jambo la mtu kuniudhi au kunidhulumu maana nikitamka haipiti muda inaanza kutumia. Kwa mantiki hii binadamu kila mtu ana kitu ambacho kipo kwenye asili yake. Cha msingi pia omba Mungu na tafuta watumishii wa Mungu wakuombee waifunge hiyo ndoto ya mauti. Pole sana. binafsi naota mara chache sana na sijawahi kuona zikitimia!!!! Nikilala ni fofo fofo kama mtoto mdogo.
Wana jamvi naandika hapa nikiwa na hofu na mashaka juu yangu mwenyewe..
hili jambo limekua likinitatiza sana..mwaka 2006,nikiwa shule niliota nyumbani tunalia,tumefiwa,haikuchukua hata wiki mbili..nikapigiwa simu kujulishwa msiba,bibi yangu mzaa mama amefariki..
Mwaka uliofuata nikaota mjomba wangu kafariki..wiki kadhaa baadae mtoto wa mjomba wangu nlomuota (binamu yangu sasa)alifariki kwa kupigwa na radi..nikaanza kujistukia lakini sikumuambia mtu..Mwaka jana niliota kuna msiba umetokea kwao my best frnd kabisa wa toka utoto (tumekua kama ndugu sasa)..haukupita muda,kaka yake akafariki..miezi miwili baada ya huo msiba,nikaota tena msiba tena..baba yake na my best huyo huyo akafariki..
Leo usiku,nimelala usingizi wa mang'amu ng'amu..nimeota niko msibani nalia..sasa hivi tuu nimepata ujumbe wa simu mjomba wa rafiki yangu (sio alofiwa na kaka na baba) amefariki..
Jamani ni nini hii?..wengine husema wakiota msiba maana yake ni jambo la heri mbona mm sio hivo?
Hapa sina amani..
Mokoyo hujamalizia when a dream is from your flesh inakuaje.
Please share kidogo.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Pole sana. Hii hali inaweza kuelezeka vizuri zaidi kama mtu akifahamu imani yako katika Jina la Yesu. Inabidi utambue kuwa kuna maono na kuna roho za utambuzi. Unaweza ukawa na vyote hivi au kimoja wapo lakini haimaanishi kuwa lazima viwe vinatoka kwa Mungu. Kama wewe ni msomaji wa Biblia utakumbuka kuna mahali pameandikwa yupo mtu aliyewaambia kina Petro mambo yanayowahusu japo hakuwafahamu kutokana na roho ya utambuzi aliyokuwa nayo. Hata hivyo kina Petro waliikemea ile roho ikamtoka sbb haikutokana na Mungu. Ila kama wewe unaimani na nimcha Mungu basi ujue hayo yanakuwa mafunuo toka kwa Mungu akikupasha habari za mambo yajayo ili uombe. Kuota ndoto hizi nakukaa kimya badala yakuomba rehema juu ya uliyemuota nakuvunja roho ya mauti inakuwa deni kubwa kwako mbele za Mungu. Mungu hakuonyeshi ili uangalie nakukaa kimya ila anakuonyesha ili kupitia maombi yako hizi roho zipone na mauti. Ni somo pana sana hili ila usipoomba utadaiwa mbele za Mungu. Unaweza kunipm kama utataka ushauri zaidi.
mimisa hilo jambo lisikutishe mpenzi, hilo ni liroho lichafu la mauti uko nalo unachotakiwa kufanya, kabla hujalala anza kulikemea na kuomba ulinzi wa malaika kwa watu woote hata kama kuna nguvu za kishetani zisiwapate na nguvu za mungu zitawale...!!!!
asante hekimatele
Inamaanisha kwamba kiroho umekufa. Sasa cha kufanya, jaribu kwenda kanisa la kiroho karibu yako wakujaze roho mtakatifu atakayekusimamia nasa kuondoa hizo ndoto zako za kuzimu. 2. Ukiota mambo kama hayo kama ukistuka muda huo anza kuomba ukifuta hiyo ndoto yako. For more information ni PM nikutumie Dream Codes usome ujue maana ya hizo ndoto zako na jinsi ya kuomba.
Pole sana.