Nifanyeje niwe na uelewa mdogo?

Nifanyeje niwe na uelewa mdogo?

Yaani kuwa na uelewa wa mambo mbambali ni mateso makubwa hasa kwenye nchi ya Tanzania nimegundua watu wenye uelewa mdogo wa mambo (ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kisayansi) wana raha kubwa sana na wanafurahia maisha vizuri, yaani kwao bora liende hawajui chochote kinachoendelea.

Kuna mambo mengi makubwa yanatokea tena yakuogopesha kwa mtu mwenye kufikiri vizuri, lakini wenzagu wenye uelewa mdogo wala hawapati machungu yoyote yale maisha kwao yanasonga mbele kama vile hakuna kinachotokea, kiufupi wenzagu raha wanayo.

Sasa naomba mnipatie mbinu ya kuondoa uelewa wa kutafakari na kuchambua mambo, ili niwe kama zezeta fulani na mi nifurahie maisha.
Nimeona njia pekee ya kufurahia maisha apa Bongo ni kuwa na uelewa mdogo wa mambo.
Omba upatiwe kadi ya uwanachama wa CCM
 
Uchanganyeko na kabangi mpwa maana hii nchi kweli ukiwa na akili safi na ukawa unapenda mambo yaende kwa usawa hutosita kupata mgonjwa kama presure, msongo wa mawazo, insomnia pia hata kujiua [emoji23] [emoji23] [emoji23]

Kikubwa zaidi wakikugundua wanakurestisha au kukubambikia kesi na kwenda kukutesa
 
umeeleweka Mkuu.
Wa Jana tuu, utafiti sio lazima ufanyiwe waweza kufanya mwenyewe.
Jana nilijikita kusoma post 100 za siasa hapa jf na kuona watu 97 wapenzi wa Ccm wako happy hata ukiwaambia hospitalini hakuna dawa, wao wanasema hapakazituu.
 
watu kama hawa ndio wanaishi kwa rahaa zao.@jambazi
 
Sheria za nchi haziruhusu bangi.
 
Ni kweli kuna jamaa nilimuliza rais alikuwa kenya juzi jamaa akasema hamna kitu kama hicho

Nikamwambia mwana bungeni mambo yamesha haribika Mbowe kakinukisha jamaa ananijibu acha ujinga kwani bunge lilisha anza vikao vyake?

Yaani kuna raia wahajui nini kinacho endelea humu duniani tofauti na kuangalia maisha yake!

Kuna watu flani wanaishi maporini Wahazabe yaani hawa jamaa ndiyo funika wanajua rais ni Nyerere hadi leo! Enzi za Nyerere alikuwa anaenda kuwatembelea anawapelekea asali!
Next week, nina safari ya kwenda kwa wahazabe
 
Yaani kuwa na uelewa wa mambo mbambali ni mateso makubwa hasa kwenye nchi ya Tanzania nimegundua watu wenye uelewa mdogo wa mambo (ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kisayansi) wana raha kubwa sana na wanafurahia maisha vizuri, yaani kwao bora liende hawajui chochote kinachoendelea.

Kuna mambo mengi makubwa yanatokea tena yakuogopesha kwa mtu mwenye kufikiri vizuri, lakini wenzagu wenye uelewa mdogo wala hawapati machungu yoyote yale maisha kwao yanasonga mbele kama vile hakuna kinachotokea, kiufupi wenzagu raha wanayo.

Sasa naomba mnipatie mbinu ya kuondoa uelewa wa kutafakari na kuchambua mambo, ili niwe kama zezeta fulani na mi nifurahie maisha.
Nimeona njia pekee ya kufurahia maisha apa Bongo ni kuwa na uelewa mdogo wa mambo.
Mia kwa mia mkuu.
 
Mwambie Bitukinao akupe limbwata,,utapata tu uelewa mdogo
 
Back
Top Bottom