ZirlovimovicZirkov
Member
- Sep 3, 2025
- 48
- 85
Wakuu salaam,
Nakuja kwenu ndugu yenu, kaka yenu pia mdogo wenu kwa heshima kubwa nikihitaji msaada wenu wa mawazo nikaamini Kuna watu wanauzoefu wa namna yoyote au uelewa mkubwa kuzidi wangu.
Kwanza niweke wazi kwamba katika maisha yangu na uhai wangu huu katika kitu sipendi kukiona ni maiti, Ndio Yaani nikiona binadamu ambaye roho yake imeacha mwili Huwa najisikia vibaya sana pia huwa napoteza nguvu ya ndani, nakua naona kama maisha hayana maana tena yaani napoteza morali ya kufanya kitu chochote na hali hii niliigundua nikiwa na miaka 12.
Nilikua form one ambapo mwanafunzi mwenzetu alifariki kwahiyo shule nzima ilitulazimu kumuaga baada ya kuona ule mwili kwakweli hali yangu ilibadilika na ilinichukua muda mrefu sana mpaka kurudi hali yangu. Baada ya hapo nilifikia maamuzi kwamba sitokuja tena kuangalia maiti.
Kutokea hapo sijawahi kuangalia maiti mpaka nimefikia umri huu nilionao Leo.
Turudi kwenye maada iliyonileta kwenu. Ni kwamba hivi nilipoanza kujitambua zaidi kuna kitu nilikinotice kwenye maisha yangu. Yaani mtu anapokaribia kufariki huwa najikuta najitenga nae Yaani sitaki ukaribu wowote na huyo mtu na sio kwamba anakua ameniudhi hapana ila huwa najikuta tuu nakua nakaa mbali nae au namkwepakwepa na baada ya muda nasikia amefariki.
Jambo hili limetokea zaidi ya mara tatu sasa kwa watu tofauti ikiwepo mtoto mchanga wa miezi chini ya sita, pia hali kama niliyoielezea hapo juu imeanza kunitokea kwa mtu wangu wa karibu sana, alizoea kunipigia simu ila sasa hivi hanipigii na hata siwazi sana na zaidi sitamani tena anipigie simu, Pia Kuna siku nilimuota ananikabidhi mdogo angu wa mwisho kwamba nimlee, huyu dogo yeye pekee ndio bado anasoma, pia mara mbili nimeota tumesimama mahali ila huyu ndugu yangu yeye hayupo.
Kinachonileta kwenu ni kuomba msaada juu ya hii Hali, Yaani nawezaje kuichukulia? Je! Niwe nawafuata watu nawambia kinachoendelea mfano huyu ndugu yangu wa karibu au niendelee kubaki kuwa mtazamaji mpaka yatakapotokea? Lakini kubaki kuwa mtazamaji Bado pia huwa inanisumbua sana akilini kitu ambacho kinanifanya nitafute kwenda mbali na huyo mtu.
Kwenu wakuu naomba msaada wa ushauri au yeyote mwenye uzoefu wa haya mambo.
Karibuni.
Nakuja kwenu ndugu yenu, kaka yenu pia mdogo wenu kwa heshima kubwa nikihitaji msaada wenu wa mawazo nikaamini Kuna watu wanauzoefu wa namna yoyote au uelewa mkubwa kuzidi wangu.
Kwanza niweke wazi kwamba katika maisha yangu na uhai wangu huu katika kitu sipendi kukiona ni maiti, Ndio Yaani nikiona binadamu ambaye roho yake imeacha mwili Huwa najisikia vibaya sana pia huwa napoteza nguvu ya ndani, nakua naona kama maisha hayana maana tena yaani napoteza morali ya kufanya kitu chochote na hali hii niliigundua nikiwa na miaka 12.
Nilikua form one ambapo mwanafunzi mwenzetu alifariki kwahiyo shule nzima ilitulazimu kumuaga baada ya kuona ule mwili kwakweli hali yangu ilibadilika na ilinichukua muda mrefu sana mpaka kurudi hali yangu. Baada ya hapo nilifikia maamuzi kwamba sitokuja tena kuangalia maiti.
Kutokea hapo sijawahi kuangalia maiti mpaka nimefikia umri huu nilionao Leo.
Turudi kwenye maada iliyonileta kwenu. Ni kwamba hivi nilipoanza kujitambua zaidi kuna kitu nilikinotice kwenye maisha yangu. Yaani mtu anapokaribia kufariki huwa najikuta najitenga nae Yaani sitaki ukaribu wowote na huyo mtu na sio kwamba anakua ameniudhi hapana ila huwa najikuta tuu nakua nakaa mbali nae au namkwepakwepa na baada ya muda nasikia amefariki.
Jambo hili limetokea zaidi ya mara tatu sasa kwa watu tofauti ikiwepo mtoto mchanga wa miezi chini ya sita, pia hali kama niliyoielezea hapo juu imeanza kunitokea kwa mtu wangu wa karibu sana, alizoea kunipigia simu ila sasa hivi hanipigii na hata siwazi sana na zaidi sitamani tena anipigie simu, Pia Kuna siku nilimuota ananikabidhi mdogo angu wa mwisho kwamba nimlee, huyu dogo yeye pekee ndio bado anasoma, pia mara mbili nimeota tumesimama mahali ila huyu ndugu yangu yeye hayupo.
Kinachonileta kwenu ni kuomba msaada juu ya hii Hali, Yaani nawezaje kuichukulia? Je! Niwe nawafuata watu nawambia kinachoendelea mfano huyu ndugu yangu wa karibu au niendelee kubaki kuwa mtazamaji mpaka yatakapotokea? Lakini kubaki kuwa mtazamaji Bado pia huwa inanisumbua sana akilini kitu ambacho kinanifanya nitafute kwenda mbali na huyo mtu.
Kwenu wakuu naomba msaada wa ushauri au yeyote mwenye uzoefu wa haya mambo.
Karibuni.