Mjomba Malume
JF-Expert Member
- Apr 8, 2025
- 903
- 1,317
Wakuu salamuni.
Nimeamua kuanzisha huu uzi baada ya kuona hii hali imeanza kunipa usumbufu mkubwa kwenye maisha yangu ya kila siku. Kuna baadhi ya vitu navifanya kwa kurudia rudia sana kiasi kwamba vinanichosha na kunipotezea muda bila sababu ya msingi.
Mfano nikifunga mlango, baada ya kuondoka nahisi kama sijaufunga vizuri hivyo narudi tena kwenda kuangalia. Wakati mwingine narudia mara mbili hadi tano kuhakikisha tu umefungwa. Pia nikizima switch au vifaa vya umeme, lazima nijiridhishe mara nyingi kama kweli nimezima. Hata nikishaangalia bado mawazo yananilazimisha nirudi tena kuhakiki.
Hii hali imekuwa ikinifanya nichelewe mambo mengi, nipoteze muda kwenye vitu vidogo vidogo na wakati mwingine nikose kabisa amani ya moyo na raha ya kawaida. Kinachoniumiza zaidi ni kwamba akili yangu huwa inajua kabisa kuwa tayari nimefanya hicho kitu, lakini bado kuna msukumo wa kutaka kurudia kuhakiki tena na tena.
Nilijaribu kuwauliza baadhi ya watu kuhusu hii tabia, wengi wakaniambia huenda ni tatizo la OCD. Ndiyo maana nimekuja kwenu wakuu, labda kuna mwenye experience au uelewa kuhusu hili aniambie namna ya kupambana nalo au kupata solution yake.
Karibuni ushauri wenu wakuu.
Nimeamua kuanzisha huu uzi baada ya kuona hii hali imeanza kunipa usumbufu mkubwa kwenye maisha yangu ya kila siku. Kuna baadhi ya vitu navifanya kwa kurudia rudia sana kiasi kwamba vinanichosha na kunipotezea muda bila sababu ya msingi.
Mfano nikifunga mlango, baada ya kuondoka nahisi kama sijaufunga vizuri hivyo narudi tena kwenda kuangalia. Wakati mwingine narudia mara mbili hadi tano kuhakikisha tu umefungwa. Pia nikizima switch au vifaa vya umeme, lazima nijiridhishe mara nyingi kama kweli nimezima. Hata nikishaangalia bado mawazo yananilazimisha nirudi tena kuhakiki.
Hii hali imekuwa ikinifanya nichelewe mambo mengi, nipoteze muda kwenye vitu vidogo vidogo na wakati mwingine nikose kabisa amani ya moyo na raha ya kawaida. Kinachoniumiza zaidi ni kwamba akili yangu huwa inajua kabisa kuwa tayari nimefanya hicho kitu, lakini bado kuna msukumo wa kutaka kurudia kuhakiki tena na tena.
Nilijaribu kuwauliza baadhi ya watu kuhusu hii tabia, wengi wakaniambia huenda ni tatizo la OCD. Ndiyo maana nimekuja kwenu wakuu, labda kuna mwenye experience au uelewa kuhusu hili aniambie namna ya kupambana nalo au kupata solution yake.
Karibuni ushauri wenu wakuu.