Sijui ni Zanzibar ipi wanaitaka maana hata mapinduzi sasa wanasema ni ya Nyerere, lakini wanasherehekea kila mwaka na waasisi wao wanawaenzi.Tatizo la Wazanzibar wengi ni kuimba nyimbo wasizojua tungo zake. Maswali ya MM hakuna anayejibu bali tunasikia wanaonewa.Inasikitisha kuwa hakuna Mzanzibar anayeongelea kwa uchache faida za muungano.Sidhani muungano huu ni dudu linalaowaumiza Wazanzibar bila kuwa na hata faida moja.
Hii inatokana na kulishwa chuki ambazo ukiuliza hakuna anayeweza kuzifafanua, lakini zipo mioyoni mwao kwasababu ya kupandikizwa tu.
Nimefauatilia majadiliano mengi ya Wazanzibar, wao wanataka Tanganyika irudi, na sijui ni kwanini kwasababu lengo lao ni 'kuirudisha' Zanzibar. Hili la Tanganyika ni la Watanganyika na Tanganyika au Tanzania zinaweza kubaki hivyo endapo wahusika watakubali, ni majina tu.
Wanzanzibar hawasemi hatutaki muungano, wanachosema ni kuwa muungano kama upo uwe wa mambo fulani. Hii maana yake ni kuwa hawataki muungano lakini wanataka ushirikiano kwa mambo wanayodhani nje ya muungano yatawaumiza sana. Wanajua wazi kuwa ni kupitia muungano kuna fursa wanazofaidika nazo,lakini wamependikizwa chuki ya kuchukia tu hata yale mema yanayotokana na muungano, na kuaminishwa kuwa kusema hili ni faida ya muungano ni sawa na kufru na dhambi mbele ya S.W.T.
Sioni kwanini walalame, wana baraza la wawakilishi linalofanya kazi kikamilifu na kubadili kila wakitakacho. Wanashindwa nini kuamua mambo ya muungano? mfano ni kuzuia wabunge wa JMT kutoka Zanzibar, kumrejesha makamu wa rais JMT, wao kuondoka bara na kurejea kwao, kuwatimua wabara kutoka visiwani, kutangaza pesa yao kama wimbo wao wa taifa n.k.
Nimekuwa nauliza hili swali mara nyingi na sitachoka, Wazanzibar niambieni Mtanganyika ataathirika vipi kwa kuvunjika muungano! tukizingatia kuwa Wazanzibar 500,000 wanaishi bara wana ajira na biashara, na wanafaidika na huduma zote za kodi za wabara kama elimu ya juu n.k. Tafadhali nifahamisheni, Tanganyika itaathirika vipi.