Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

.......Tunataka zanzibar yetu ileeee kabla ya muungano.zanzibar kabla ya Muungano tulikua na Balozi za nje 14.Na pia tulikua na kiti chetu umoja wa Mataifa.tumekubali kufuta hadhi za kibalozi zote tuliokua nazo na kupoteza kiti chetu umoja wa mataifa na kuchukuliwa na hio inayoitwa sasa Tanzania.
Tunaitaka zanzibar yetu ili hadhi na heshma tulokua nayo kabla Muungano irudi.
 
Kwahiyo serikali ya mapinduzi na BLW,wimbo wa Taifa, bendera ya Znz, Rais na Makamu hivyo havitoshi kuwa ni Znz.
Muungano umeidumaza znz,tunahitaji ufahamu, ni kwa vipi kama si kuisadia.
Pili, je muungano hauna lolote jema na kama lipo ni lipi.

Ni wakati ule karafuu ilikuwa 'hot' na Znz kuitwa spice island, karafuu inazalishwa kwa ubora na mataifa mengi,kudorora kwa uchumi wa znz ni matokeo ya kudhani ndiyo pekee inayoweza kuzalisha karafuu. Pesa zikatumika kuwekeza katika TV za rangi na ya kwanza Africa.
Tanganyika imepata vitu kama hivyo miaka 20 iliyopita, lakini waliwekeza katika elimu, afya n.k. Ndiyo maana viongozi wote wa Znz wame elimikakupitia Tanganyika.

Hakuna Mtanganyika anayeing'ang'ania ZNZ, nieleze kwa lipi linaloweza kukosekana kwa znz kutokuwepo? Hoja kuu hapa ni uchumi ambao nimeshaueleza kuwa haukidhi haja ya kung'ang'ania ZNZ.
.
Wanapokwenda Kenya ni tofauti na wakiwa bara. Waulize wafanyabiashara kwanini wanapenda bara zaidi ya Kenya. Mznz hawezi kusoma vidudu hadi chuo kikuu Kenya kama utambarare wakiwa bara. Hawabaguliwi na ni sehemu ya wananchi wa kawaida. Waulize Wznz wa kawaida wanaoishi bara watakueleza.
Jiulize kwanini waagize bidhaa za kilimo kutoka bara na si mombasa au Lamu.

Ndani ya muungano kuna GNU nje ya muungano wapo wanaosema mapinduzi daima na wapo wanaosema mapinduzi ya Okello na Nyerere. Ndiyo maana nimekuuliza swali kabla, je mapinduzi mnayathamini au ni ya Nyerere na Okello.?(Huna jibu)
Ndani ya muungano ni Wznz, nje ya muungano wapo wzn weusi waunguja na wamanga wapemba.Wapemba wanasisitiza kuwa hawana mkataba na Unguja, juzi tu wamerudia hayo. Je GNU ni kutoka katika muungano au ni ya kudumu.?

Kipi kinashindikana kupeleka mswada wa kuvunja muungano ili wasing'ang'aniwe na Tanganyika.

Mswada umepingwa vikali bara, si kwa ajili ya muungano tu, bali maudhui yote. Tofauti na Znz bara wametumia kauli,na Znz wametumia hisia za vurugu. Kuna uwezekano wa kusema 'hapana' bila rabsha.

Kinachowaudhi watu ni kauli za ukoloni, tunaonewa n.k. Fikiria umembeba mtu mgongoni bado anarusha mateke na kejeli.
Kinachoudhi ni kuwa kwanini msirudi kwenu, mkatumia BLW na kusema basi.

Sidhani kama kunahitajika mfumo wa ushirikiano, upi labda na kwa vipi, nifafanulie.

Wznz walio wengi na wakawaida wanatumia fursa za muungano hawapendi ufe, wanachotaka ni kuurejea na kuangalia mapungufu.
Wznz wanaoishi nchi za nje wanataka ufe wakijua kuwa watakaporejea nyumbani na elimu zao au kuongea kiingereza watapata fursa za vyeo.!!!(mzalendo.net)

Wasichokijua znz ni kuwa eneo lao na population ni matatizo katika siku za mbeleni. Biashara zao zinategemea majirani hasa Tanganyika.Kama watajenga uchumi bado utakuwa tegemezi.

Misaada toka uarabuni ambako wengi wanadhani znz ni sehemu ya, itasadia sana kuinua uchumi nakurudisha ukoloni wa Sultan.

Fursa zote mnaziziona,nje ya muungano ni ushindani.
Kujitenga kwa znz ni sababu ya hisia za kuwepo mafuta. Haya hatukuyaona wala wakati mishahara ikitoka bara. Fanyeni maamuzi haraka mpate nchi yenu yenye asali na maziwa, ila tu isije kuwa nchi ya kufikirika.
Kuna Visiwa vingapi kandokando ya Afrika? Jee, hivi Visiwa vinategemea kuwepo kwa Tanganyika? Jee, hivi Visiwa vinapata ruzuku yeyote kutoka Tanganyika ? Je, viwango vya maisha ni sawa kama Tanganyika? Unajua GDP ya kisiwa kama Mauritius? Tanganyika iko nafasi ya ngapi kiuchumi katika Afrika?
Mafuta yakiwepo yasiwepo,Zanzibar itaendelea na harakati za kujikomboa...MPAKA KIELEWEKE... HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE ...
 
Kuna Visiwa vingapi kandokando ya Afrika? Jee, hivi Visiwa vinategemea kuwepo kwa Tanganyika? Jee, hivi Visiwa vinapata ruzuku yeyote kutoka Tanganyika ? Je, viwango vya maisha ni sawa kama Tanganyika? Unajua GDP ya kisiwa kama Mauritius? Tanganyika iko nafasi ya ngapi kiuchumi katika Afrika?
Mafuta yakiwepo yasiwepo,Zanzibar itaendelea na harakati za kujikomboa...MPAKA KIELEWEKE... HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE ...


Hapo kwenye red, Zanzibar inaweza ikafanana na Comoro pia msiwe too optimistic. Mauritius wameinvest kwenye Utalii. Lakini utalii unautamaduni wake. Kwa jinsi mnavyotaka kuipeleka Zanzibar kuwa nchi ya Kiislam, mkitakata kuinvest kwenye utalii itawalazimu kukyuka baadhi ya maadili mengi ya Kiislam. Watalii wengi wanapenda kuvitumia visiwa kama sehemu ya starehe, za kupindukia. Sasa jiandaeni kupisha sheria zitakazokuwa zinaruhusu nudity na sun-bathing kwani huo ndio utalii wa beach. Utalii wa bara ukiondoa kwenye beach, hauitaji sunbathing wala nudity kwani huwezi panda mlima kilimanjaro wala kwenda serengeti ukiwa nude. Ni bora pia mkafikiria hayo kabla hamjapanga hiyo mikakati yenu ya uchumi wa kisiwa chenu
 
Ilikwishatabiriwa kwamba bila muungano hakuna zanzibar, bali kuna unguja na pemba, kwa hiyo hiyo zanzibar wanayoidai nje ya muungano haipo, hivyo hawataipata daima.
 
ile ya wakati wa Marehemu Mzee Abeid Amani karume ilipokuwa watanganyika hawana sauti zidi ya wazanzibar wanachokifanya au kuwamuwa na isitoshe walikuwa wanaingia kwa pass
 
ile ya wakati wa Marehemu Mzee Abeid Amani karume ilipokuwa watanganyika hawana sauti zidi ya wazanzibar wanachokifanya au kuwamuwa na isitoshe walikuwa wanaingia kwa pass

Ni nani alioondoa hiyo pass?
 
Kuna Visiwa vingapi kandokando ya Afrika? Jee, hivi Visiwa vinategemea kuwepo kwa Tanganyika? Jee, hivi Visiwa vinapata ruzuku yeyote kutoka Tanganyika ? Je, viwango vya maisha ni sawa kama Tanganyika? Unajua GDP ya kisiwa kama Mauritius? Tanganyika iko nafasi ya ngapi kiuchumi katika Afrika?
Mafuta yakiwepo yasiwepo,Zanzibar itaendelea na harakati za kujikomboa...MPAKA KIELEWEKE... HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE ...


Unapokuwa na jazba unapoteza thamani ya mjadala na hata hoja zako zinavurugika na kupandana.
Niliposema uchumi utategemea kwa kiwango kikubwa uhusiano na Tanganyika, halikuwa na maana ya kudhalilisha bali upo ukweli ambao werevu wanautambua.Kwa bahati nzuri huko Mauritius na Zanzibar nimekaa kwahiyo nafahamu vema kile ninachoongelea.

Nitakufafanulia kidogo. Visiwa havitegemei uwepo wa Tanzania kwani vingine havikaribiani kabisa. Mauritius nimeishi sehemu inaitwa (Katrebon kwa kifaransa) nimeona maisha ya mtu wa kawaida na maisha ya matajiri. GDP unayoiongelea ni nzuri sana lakini si kama unavyoona kwenye internet.Nimeona utamaduni wao, uchumi na mahusiano yao na wafaransa.
Comoro ambayo ina ukaribu sana na ZNZ si kama Mauritius na ni mshiriki mzuri wa biashara na Bara, ungejiuliza kwanini si msumbiji.

Kampuni ya Maersk iliwahi kukataa mizigo ya kwenda Znz, na walitoa sababu kuwa ni bora konteina 14 za Znz zikashushwe Dar iwe sehemu ya konteina 400. Na hivi tunapoandika wafanyabiashara wengi kutoka Znz wantumia bandari ya Dar pamoja na ubovu na uzembe uliopo. Hapa ndipo unapaswa kujiuliza kwanini! ili hali kuna bandari huru nchi ya neema Znz.

Kampuni ya Zantel iliyojinasibu kuwa mkombozi wa cellphone visiwani kwa tech ya satellite kutoka uarabuni, ilifikia mahali serikali ya ZNZ kuzusha zogo kwanini isisajiliwe Bara. Hii ni kufuatia hofu ya Zantel kutaka kufunga virago kutokana na volume ya biashara. Sasa na makao makuu wanahamisha kabisa. Ni bora kuwa na soko la watu laki moja wa Ilala wenye nguvu katika biashara na si vinginevyo.

Si Znz, hata Tanganyika inawashirika wake inawategemea kiuchumi. Kufutwa kwa ubaguzi South Africa kumeifanya Zambia isitumie Tanganyika na matokeo yake ni kuangaka kwa biashara ya Tanganyika. Kenya nayo pia inaitegemea Tanganyika kama soko lake, Uganda inategemea Kenya. Kama ilivyo US inategemea Canada na Mexico ndivyo Japan inategemea US na China inalenga Africa.Ni mahusiano ya kibiashara yanayonifanya niseme Znz itaathirika kwa kiasi fulani.

Rwanda na Burundi ambazo hatukuwa na mahusiano kwa misingi ya mipaka na tamaduni za kikoloni, zimepigana sana kuwa ndani ya EA. Si kwasababu nyingine bali kwa fursa zilizopo. Huu ni mfano tu wa kuonyesha ni jinsi gani size na population vinavyohusika kiuchumi.

Kwa mwekazaji yoyote atakayetaka kuwekeza Zanzibar, kwanza hata angalia Znz bali nchi jirani. Kwa jinsi ilivyo Tanganyika itapewa jicho la kwanza kwa kuzingatia vigezo vyote vya kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi vinavyoshabihiana sana na Znz.
Hata kufikiri kwa kiwango cha kawaida, wznz wenye biashara bara haina maana hawawezi kufanya kenya au kwao, lakini kuna sababu za msingi wao kufanya hivyo, na labda kawaulize ili wakupe jibu wao wenyewe.

Yote hapo juu ni mifano ya kuweka sawa mjadala na neno 'tegemezi'. Ni lazima ukweli uitwe ukweli hata kama unauma.
Pamoja na yote haya ni muhimu sana mkaomba mswada wa kura ya maoni ili muamue hatima ya nchi yenu yenye mito na asali.
 
Kuna watu naamini wanaishi wakiwa wamefungwa na kale; Baadhi ya watu wanaodai hii "Zanzibar" hawalilii Zanzibar Mpya wanataka Zanzibar ya kale. Wenyewe wanaita "Utukufu wa Zanzibar". Ukiwauliza hawa utaona wanakumbushia jinsi maisha yalivyokuwa mazuri Zanzibar "wakati ule" na watataja mambo yale matamu ya wakati ule ambayo yaliimbwa katika nyimbo na kutungiwa tenzi.

Hivyo kwa hawa Zanzibar inabakia kuwa kama Jiji la Atlantis tunaloambiwa lilipotea katika historia ya kale na kuwa lilikuwa ni jiji lililokuwa limepiga hatua kubwa sana na kwa miaka maelfu sasa limebakia likisimuliwa katika njozi juu ya utukufu wake. Hii ndio Zanzibar ambayo watu wanaitamania. Ni Zanzibar yenye kwenye njozi ambayo iliishi katika utukufu ambapo watu wake waliishi kama wamoja, wakipendana, bila dhulma, hiana au mgongano wowote. Ni Zanzibar tukufu ambayo historia yake tunaambiwa ni ya kale sana.

Zanzibar hii ya kale utukufu wake unahusishwa zaidi na ujio wa Waarabu na Uislamu. Licha ya utukufu wa mambo ya maisha kuna utukufu ambao unaendana hisia ya kustaarabika na ukiwasoma baadhi ya watu wanaobeza watu wa bara wanabeza kutoka katika misingi ya kuwa Zanzibar ilistaarabika mapema kuliko bara kwa kupokea ustaarabu wa Kiarabu ambao ulijengwa katika misingi ya Imani ya Kiislamu. Hata hivyo, Wazanzibari hawa wenye utukufu hawajivunii Zanzibar kwa sababu ya Uislamu kwa sababu kama hiyo ingekuwa kweli watu wa bara wengi tu nao wangeweza kujivunia Uislamu wao kwani maneo kama Kilwa (iliyoko bara) yanaweza kujivunia Uislamu ule ule wa Zanzibar na kuna wengine ambao wanadai kuwa Zanzibar yenyewe (kama maswali yangu hapo juu nilivyoashiria) haikuwa inakoma kwenye visiwa viwili tu vya Unguja na Pemba kama wengi wanavyotaka tuamini bali ilihusisha hata baadhi ya miji ya mwambao wa Afrika ya Mashariki.

Tatizo kubwa ni kuwa watu wengi wa bara hawajui historia yao na wanaamini kuwa historia yao ilikuja na kuanza na ujio wa Waarab. Wengi wetu wala hatujui kuwa kuanzia karne ya kwanza kabisa pwani ya Afrika ya Mashariki ilikuwa na jamii zake nyingine nazo zilipotea katika historia kama jiji la Atlantis. Kwa mfano watu wengi wa bara hawajawahi kusikia jina la Prof. Felix Chami ambaye amefanya utafiti mkubwa sana katika eneo la pwani ya Afrika ya Mashariki hasa maeneo ya Kilwa na Delta ya Rufiji huko. Dr. Chami ndiye ambaye miaka ya hivi karibuni amepindua kabisa historia ya Afrika ya Mashariki ambayo tumejaribu kulazimishwa kuaminishwa kuwa ndio "historia sahihi" kuwa ustaarabu na mahusiano na nje ya Afrika ya Mashariki yamekuja baada ya Waarabu.

Hivyo, wanaotaka Zanzibar bado hawajaweza kujibu kuwa ni ipi hasa wanayoitaka. Wanaosema wanataka Zanzibar "iliyoungana na Tanganyika" Zanzibar hiyo ni ile ya Mapinduzi yaliyomng'oa Sultani katika tukio la umwagikaji wa damu mkubwa. Zanzibar hii iliyojeruhiwa na kuumizwa na kuwagawa Zanzibar kinasaba na kwa damu, haiwezekani iwe ni Zanzibar ambayo hawa ndugu zetu wanaitaka. Watakuwa wanataka Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi. Lakini Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi haikuwa ni Zanzibar ya watu wote. Waliojifunza historia wanajua kabisa kugawanyika kwa Wazanzibar hakukusababishwa na Muungano wala hakukusababishwa na Nyerere.

Hawa vijana wa leo wanaomlaumu Nyerere hawaambiwi historia yao kweli. Wengi hata hawajui kuwa umwagikaji damu Zanzibar haukuja mwaka 2001 tu au mwaka 1964; wanaofahamu historia wanajua damu ilishamwagika na vurugu kutokea Zanzibar kufuatia uchaguzi visiwani mle. Kwani hata hiyo inayoitwa "serikali ya Shamte" haikuungwa mkono na Wazanzibari wote - ushahidi ni matokeo ya chaguzi mbalimbali visiwani mle. Matokeo ya uchaguzi wa 1957, wa 1961 na hata wa 1963 ulionesha wazi mgawanyiko kati ya vyama vikuu vya Zanzibar ambavyo mtu yeyote anayejua historia anajua vilihusiana na nasaba za watu. ASP, ZPPP na ZNP viliwaganya Wazanzibari. Na hata kilichofanyika mwaka 1963 kuunda "serikali ya mseto" ya Shamte tunajua hakikuwa sababu ya furaha kwa Wazanzibari wote. Lakini wapo wanaotaka tuamini kuwa uchaguzi wa 1963 uliwaunganisha Wazanzibari!

Hapana, Wazanzibar leo hii kama Nyerere alivyosema wanaunganishwa na chuki yao dhidi ya Muungano na dhidi ya watu wa Bara ambao wengine ni ndugu zao wa damu. Wanaunganishwa na chuki ambayo yaweza kuwa pia ina msingi wa udini vile vile lakini nafikiri zaidi ni msingi wa ubora (superiority complex) ambayo tulioishi maeneo ya pwani tunajua baadhi ya watu wanavyojiona bora kwa sababu ya nasaba zao. Bado watu wanawaona watu weusi kuwa ni duni kwao. Na bara kuwa na sehemu kubwa ya watu wake ni watu weusi inaonekana kana kwamba ni uduni wa aina fulani na watu wanaitaka "Zanzibar mpya". Tukumbuke kuwa kinyume na kule Marekani ambapo sheria ya "tone moja la damu ya mtu mweusi" inakufanya uwe mtu mweusi kule Zanzibar na hata maeneo mengi ambayo watu walichanganya damu na waarabu utawakuta wapo wetu weusi tii ambao wamejiaminisha kuwa wao ni Waarabu - si kwa maana ya tamaduni na imani bali kwa maana ya nasaba. Kwani Uarabu kama inavyosemwa na watu wengi siyo suala la damu. Lakini wapo watu ambao hujitambulisha kuwa ni waarabu kwa maana ya kwamba katika familia zao wamechangia damu ya waarabu na hivyo wanawaona weusi wenzao kuwa si wenzao!

Tatizo hata hivyo ni kuwa chuki haiwezi kuunganisha. Inaunganisha tu kwa kadiri ya kwamba kile mnachokichukia bado kipo. Ndio maana Nyerere katika ile hotuba yake ya kinabii (natumia neno nabii loosely) alisema wazi kuwa dhambi ya kubaguana haikomi. Yule unayembagua akishaondoka unatafuta mwingine wa kumbagua. Zanzibar wanaweza kuamua kabisa wakawa nje ya Muungano. Ni haki yao kama binadamu na ni haki yao kufanya uamuzi huo. Lakini anayefikiria kuwa baada ya kutoka kwenye Muungano Wazanzibari watarudi kuwa wamoja - hawajawahi kuwa wamoja anyway - wanajidanganya. Zanzibar ya 1963 ilikuwa imegawanyika - ikirudi ile ile itagawanyika.

Nilikuwa nasikiliza Clouds FM juzi tu hapa na watu wengine walikuwa wanaanza kuzungumzia Jamhuri ya Pemba. Hawa ni Wapemba ambao wanaona kuwa Unguja inajjipa madaraka makubwa juu yao na kama sote tunavyofahamu ni chini ya CCM kwa mara ya kwanza Mtawala wa Zanzibar anatokea Pemba (niko tayari kusahihishwa katika hilo). Wapo waunguja ambao wanaona Wapemba ni duni kwao na wapo Wapemba ambao wanaona Waunguja ni kama watu tofauti kabisa na wao. Na hizi tofauti haziondoki kwa sababu Muungano umekufa - zitarudi kwa nguvu pamoja na maneno matamu kuwa "Zanzibar yetu sote" sijui "Zanzibar ni moja".

Binafsi mimi ni Unionist. Siaminii katika serikali tatu kama wengine, wala siamini katika serikali ya Tanganyika - kwa sababu nilizowahi kuzianisha huko nyuma. Ninaamini katika taifa na serikali ambayo ni zao la wananchi wote wa nchi hiyo. Kama Zanzibar wanataka kujitoa ni ndugu zetu, tuna historia nao, wala historia hiyo haifutiki kwa sababu hatuna Muungano. Tena naamini tunaweza kuwa na uhusiano mzuri kabisa wa kidugu hata wa kulindana kwa damu kama ulivyo wa Wamarekani na Waingereza licha ya kuwa Marekani ilijitangaza huru kutoka falme ya Mwingereza. Leo hii Wamarekani watakufa kuwalinda Waingereza na Waingereza watakufa kuwalinda Wamarekani.

Sipendi wanaozungumza kwa misingi ya kupandiza chuki kati ya Wabara na Wazanzibari. Kuna watu wengi wako Zanzibar ambao wanatoke Bara na kuna watu wengi wa Bara wanaotokea Zanzibar hawa wenye kuzungumza kwa chuki hizi za "Ubara' na "Uzanzibari" au "Uzanzibara" ni watu wa kuogopwa tu. Muungano uliundwa na binadamu, tukiona haufai tunauvunja na tukaendelea kuwa na mahusiano mazuri tu tena yanaweza kuwa na maana zaidi. Jamani Rwanda na Burundi ziliwahi kuwa chini ya utawala mmoja na Tanganyika. Leo hii tuna mahusiano na nchi hizo kwa karibu tu. Jamani tuna mahusiano na waliokuwa wakoloni wetu Wajerumani na hata Waingereza. Tuna mahusiano na nchi zilizochukua wazee wetu utumwa kwanini tuhisi hatuwezi kuwa na mahusiano mazuri na ndugu zetu wa Zanzibar ambao wanaweza kutaka kujitoa kwenye Muungano?

Ninaamini kuna kura moja tu inayohitaji kuamuriwa aidha kuungana kuwa nchi moja kabisa - mifumo tofauti ya utawala au kuvunja Muungano ili tuwe na nchi mbili rafiki, ndugu na zenye mikabata ya makubaliano ya ushirikiano labda kuliko na nchi nyingine yoyote ile. Hili linawezekana. Lakini haya mambo ya kufanyana duni na watu kujiona bora ni hisia zisizo na msingi na zinajaribu kung'ang'ania masimulizi ya kale kuliko ukweli wa kihistoria.
 
the znz issue always amazes me!
Sijawahi hata siku moja kuelewa nini kinatakikana na kila mhusika na kwa sababu gani!

Sehemu mbili zikiungana/kuunganishwa kisha ikatokea kuwa hazishikamani - je ni vema kuongeza gundi kulazimishia kuunganisha..au ni kuangalia ni vipi sehemu hizo zibakie kivyakevyake?

Huenda gundi imechoka, kuongezea zaidi hakutatua sababu inayofanya gundi kuachia...
nafikiri tuwaache kwanza peke yao alafu baadae yuwaulize kama wanataka muungano, maana sikuzote wanalalamika kwamba wanaonewa, kumbuka ngombe asipokatika mkia wake hajui thamani yake.
 
nafikiri tuwaache kwanza peke yao alafu baadae yuwaulize kama wanataka muungano, maana sikuzote wanalalamika kwamba wanaonewa, kumbuka ngombe asipokatika mkia wake hajui thamani yake.


Kwa muda wa miaka 47 hakuna tusichokijua kuhusu huu "Muungano" na hatuhitaji muda zaidi.

Wazanzibari hawajaona faida ya "Muungano" huu isipokuwa viongozi wachache na wapambe wao.

Wakati umefika Zanzibar kujiamulia mambo yake na kuondokana na ukoloni wa Tanganyika.

Zanzibar for Zanzibaris
 
Wanaitaka nchi "yao" ya Zanzibar; Wanataka kurudia "utukufu wa Zanzibar" kwa kuwa hapa walipo sasa hawaoni manufaa "yoyote" kwa Zanzibar. Wanasema wanaitaka nchi yao waliyonyang'anywa na Wadanganyika (ati Watanganyika). Wanataka warudishiwe nchi yao waliyonyang'anywa na Nyerere na watu wa bara.

Ni Zanzibar ipi hiyo wanayoitaka?


  • Zanzibar ya historia ya kale (Zenj - nchi ya weusi?) ambayo ni zaidi ya visiwa vya Unguja na Pemba bali na mwambao wa Afrika ya Mashariki
  • Zanzibar ya Sultani(ambaye naye utawala wake ulizidi mipaka ya Unguja na Pemba)
  • Zanzibar ya Sultani chini ya Mwingereza
  • Zanzibar ya baada ya Uhuru na Sultani akiwa bado ni Mkuu wa Nchi na serikali ya Mseto
  • Zanzibar ya Mapinduzi kabla ya Muungano
  • Zanzibar "mpya" ambayo haijawahi kuwepo yaani ya baada ya muungano

Ni ipi hasa wanayoitaka? Ni ipi hasa Zanzibar "proper". Isije kuwa ni kama nchi ya ahadi ambayo iko katika fikra za watu tu lakini haijawahi kuwepo; yaani ile nchi imiminikayo maziwa na asali na kwamba watu wa bara na dunia nzima wanataka kuwanyang'anya Wazanzibari. Na labda hapa itabidi tulijibu swali pia kuwa Mzanzibari ni nani hasa?

Kwenye Red. Mzanzibari ametajwa kwenye Katiba ya Zanazibar ya 1984, sambamba na Sheria ya Zanzibaris Act no. 5 of 1985.
 
Bila shaka ni zanzibar ya kabla ya muungano maana hizo nyingine ni zanzibar za wakati wa mkoloni na wasingependa kurudi kwenye makucha ya mkoloni. Mimi nawashauri kama kweli wana nia ya dhati na wanaona kuwa hawanufaiki na muungano basi wawasilishe mapendekezo yao kwa maandishi bungeni ili tujadiliane, ifanyike referendum na matokeo yatakayokuja yaheshimike. Waache kumunyamunya midomo au waache kupigia kelele uvunguni. Wasimame kidete na hadharani waseme wanataka na kuhitaji nini. Tanganyika haikuomba muungano bali udhaifu wa serikali ya karume wakati ule ndiyo ulimfanya kukimbilia kwa nyerere kuomba msaada huku akijificha makwapani kwake ili serikali yake isipinduliwe. Tukiachana bado nadhani tutakuwa marafiki na tutakuwa na diplomasia ya kweli na kushirikiana katika hili na lile. Nawatakieni kila la heri katika kudai zanzibar yenu!
 
Bila shaka ni zanzibar ya kabla ya muungano maana hizo nyingine ni zanzibar za wakati wa mkoloni na wasingependa kurudi kwenye makucha ya mkoloni. Mimi nawashauri kama kweli wana nia ya dhati na wanaona kuwa hawanufaiki na muungano basi wawasilishe mapendekezo yao kwa maandishi bungeni ili tujadiliane, ifanyike referendum na matokeo yatakayokuja yaheshimike. Waache kumunyamunya midomo au waache kupigia kelele uvunguni. Wasimame kidete na hadharani waseme wanataka na kuhitaji nini. Tanganyika haikuomba muungano bali udhaifu wa serikali ya karume wakati ule ndiyo ulimfanya kukimbilia kwa nyerere kuomba msaada huku akijificha makwapani kwake ili serikali yake isipinduliwe. Tukiachana bado nadhani tutakuwa marafiki na tutakuwa na diplomasia ya kweli na kushirikiana katika hili na lile. Nawatakieni kila la heri katika kudai zanzibar yenu!


Mkuu hapa unapotosha ukweli au itakuwa umemeza propaganda zenu za CCM

Aliekuja na proposal ya Muungano ni Nyerere na kwa vitisho vya kuwa Karume atapinduliwa na Waarabu watarudi, Karume akameza ndoana iliotukaa mpaka leo. Pia lilikuwepo shindikizo la Western Powers wakati wa Cold War na wakati huo Nyerere alikua kibaraka wao.

Lakini ilifika wakati hata huyo Nyerere aliwahi kumwambia Dr. Omar (the late VP) maneno haya:

"Viongozi wetu hawana la maana kuwaeleza wananchi wao, isipokuwa Hizbu,imefanya hili na Sultani alikuwa akifanya lile na lile.Jee, jamani vijana wetu tuliokuwa nao, hivi sasa ni nani anaeijuwa Hizbu ni nani anaemjuwa Sultani? Hivi kweli hamna zaidi ya haya kuwaeleza wananchi?"

Wakati wa Nyerere na Karume umepita na sasa vijana wanataka yale sisi yaliotushinda na hamuwezi kuyazuia tena kama alivyosema Mzee Hassan Nassor Moyo hivi karibuni:

"Ule wakati wetu na Nyerere tlikuwa tunakubali lakini hawa vijana wa leo hwakubali, Bw. Sitta, ITS OVER".
Na hatua zimeanza kuchukuliwa ingawa kuna wanaoona ni hatua hafifu "|(Mabadiliko ya 10):
Katiba ya Zanzibar inasema;

(9)(i) Zanzibar itakuwa ni NCHI ya kidemokrasia na haki za kijamii.

(9)(2)(a) Mamlaka ya kuendesha NCHI ni ya wananchi wenyewe …

(10) Kwa madhumuni ya kuendeleza umoja na maendeleo ya watu na ustawi wa jamii katika NCHI itakuwa ni wajibu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar:

(10)(3) Itadhibiti uchumi wa NCHI kufuatana na misingi na madhumuni yaliyoelezwa na katiba hii.

(12)(3) Haki za raia, wajibu na maslahi ya kila mtu yatalindwa na kuamuliwa na mahkama pamoja na vyombo vya NCHI na vinginevyo vilivyowekwa na sheria.

(21)(i) Kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa NCHI…

(23)(2) Kila mtu ana wajibu wa kulinda maliasili ya Zanzibar, mali ya NCHI pamoja na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi…


Zanzibar for Zanzibaris

 
Unapokuwa na jazba unapoteza thamani ya mjadala na hata hoja zako zinavurugika na kupandana.
Niliposema uchumi utategemea kwa kiwango kikubwa uhusiano na Tanganyika, halikuwa na maana ya kudhalilisha bali upo ukweli ambao werevu wanautambua.Kwa bahati nzuri huko Mauritius na Zanzibar nimekaa kwahiyo nafahamu vema kile ninachoongelea.

Nitakufafanulia kidogo. Visiwa havitegemei uwepo wa Tanzania kwani vingine havikaribiani kabisa. Mauritius nimeishi sehemu inaitwa (Katrebon kwa kifaransa) nimeona maisha ya mtu wa kawaida na maisha ya matajiri. GDP unayoiongelea ni nzuri sana lakini si kama unavyoona kwenye internet.Nimeona utamaduni wao, uchumi na mahusiano yao na wafaransa.
Comoro ambayo ina ukaribu sana na ZNZ si kama Mauritius na ni mshiriki mzuri wa biashara na Bara, ungejiuliza kwanini si msumbiji.

Kampuni ya Maersk iliwahi kukataa mizigo ya kwenda Znz, na walitoa sababu kuwa ni bora konteina 14 za Znz zikashushwe Dar iwe sehemu ya konteina 400. Na hivi tunapoandika wafanyabiashara wengi kutoka Znz wantumia bandari ya Dar pamoja na ubovu na uzembe uliopo. Hapa ndipo unapaswa kujiuliza kwanini! ili hali kuna bandari huru nchi ya neema Znz.

Kampuni ya Zantel iliyojinasibu kuwa mkombozi wa cellphone visiwani kwa tech ya satellite kutoka uarabuni, ilifikia mahali serikali ya ZNZ kuzusha zogo kwanini isisajiliwe Bara. Hii ni kufuatia hofu ya Zantel kutaka kufunga virago kutokana na volume ya biashara. Sasa na makao makuu wanahamisha kabisa. Ni bora kuwa na soko la watu laki moja wa Ilala wenye nguvu katika biashara na si vinginevyo.

Si Znz, hata Tanganyika inawashirika wake inawategemea kiuchumi. Kufutwa kwa ubaguzi South Africa kumeifanya Zambia isitumie Tanganyika na matokeo yake ni kuangaka kwa biashara ya Tanganyika. Kenya nayo pia inaitegemea Tanganyika kama soko lake, Uganda inategemea Kenya. Kama ilivyo US inategemea Canada na Mexico ndivyo Japan inategemea US na China inalenga Africa.Ni mahusiano ya kibiashara yanayonifanya niseme Znz itaathirika kwa kiasi fulani.

Rwanda na Burundi ambazo hatukuwa na mahusiano kwa misingi ya mipaka na tamaduni za kikoloni, zimepigana sana kuwa ndani ya EA. Si kwasababu nyingine bali kwa fursa zilizopo. Huu ni mfano tu wa kuonyesha ni jinsi gani size na population vinavyohusika kiuchumi.

Kwa mwekazaji yoyote atakayetaka kuwekeza Zanzibar, kwanza hata angalia Znz bali nchi jirani. Kwa jinsi ilivyo Tanganyika itapewa jicho la kwanza kwa kuzingatia vigezo vyote vya kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi vinavyoshabihiana sana na Znz.
Hata kufikiri kwa kiwango cha kawaida, wznz wenye biashara bara haina maana hawawezi kufanya kenya au kwao, lakini kuna sababu za msingi wao kufanya hivyo, na labda kawaulize ili wakupe jibu wao wenyewe.

Yote hapo juu ni mifano ya kuweka sawa mjadala na neno 'tegemezi'. Ni lazima ukweli uitwe ukweli hata kama unauma.
Pamoja na yote haya ni muhimu sana mkaomba mswada wa kura ya maoni ili muamue hatima ya nchi yenu yenye mito na asali.

Kwa kifupi ni kwamba wanachotaka Zanzibar kurudisha mamlaka yake ...Serikali ya SMZ kwa mfumo uliyopo sasa wa Muungano haina uwezo wowote. Haiwezi kufanya direct contact na Mashirika ya Kimataifa bila ya kupitia serikali ya muungano. Kuna project ambazo Zanzibar walitaka kuzifanya Serikali ya Muungano wame zizuwia . Kwa madai ambayo hayaeleweki au wanzibari hawaelewi.

Muungano umekuwa ikitumiwa kwa maslahi ya Tanganyika kwanza kisha ndio wanaangalia Zanzibar. Wazanzibari sio wazembe au watu wasio elewa kama hivyo mnavyo fikiria. Kama Muungano ungekuwa na manufaa ya kweli basi kusingekuwa na malalamiko yote haya. Mfano mzuri ni Muungano wa Ulaya , kila nchi ina utaifa wake na uongozi wake na sio nchi moja kuwaamilia wengine eti nyinyi ni kidogo tu, eti nyinyi ni kama ka-wilaya tu.

Luxembourg imo katika umoja wa Ulaya population 500,000 tu. Inashiriki kama member kamili wa Ulaya na unapofika mzunguko wa kuchukua urais wa Ulaya na wao wanaweka AGENDA zao . Hata makubaliano ya Muungano wa tanganyika na Zanzibar yalikusudiwa katika mantiki kama hii. Lakini kumbe ile ndani ya mioyo yenu kuna kile mncho amini kwamba Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika lakini wakoloni ndio waliigawa blah blah...By the way, hata Mwanakijiji aliwahi kuandika katika thread zake za nyuma...

Kwa ufupi wazanzibari wameshachoka kuburuzwa na huu Muungano " fake". Kinacho wazuia mpaka sasa ni utawala wa mabavu wa CCM.
kwani kila unapofanyika uchaguzi vikosi vya JWTZ hu miminwa Zanzibar kutishia usalama wa raia. IT IS ABOUT TIME THE PEOPLE'S POWER WILL TAKE OVER SOON.
Wanao zuwia kura ya maoni ni CCM makao makuu . Lakini tayari mwanga unaoneka "at the end of tunnel". Tunawaombea dua iko siku na hapa Tanganyika wata zinduka katika usingizi wao wa muda mrefu. with all respects naomaba kuwasilisha...
 
kweli kuna waZanzibari wenye asili ya Tanganyika, lakini hii haina maana lazima wakubali muungano na Tanganyika... ukweli wa mambo ni kuwa waZanzibari ni watu mchanganyiko...Watu wenye asili ya sehemu mbali mbali ikiwemo, India,Iran,Yemen,Oman,Pakistan,Kenya,Uganda,Somali,Ethiopia,Malawi,Zambia na Comoro. Wamekua na utamaduni wao ambao influenced by Islam (brought by Oman)...

Duh! ama kweli kazi kweli kweli maana maneno hayo hapo juu yameniacha hoi...Kumbe ni hawa watu wahamiaji ndio wanakuja kudai nchi yao!
 
Hapo kwenye red, Zanzibar inaweza ikafanana na Comoro pia msiwe too optimistic. Mauritius wameinvest kwenye Utalii. Lakini utalii unautamaduni wake. Kwa jinsi mnavyotaka kuipeleka Zanzibar kuwa nchi ya Kiislam, mkitakata kuinvest kwenye utalii itawalazimu kukyuka baadhi ya maadili mengi ya Kiislam. Watalii wengi wanapenda kuvitumia visiwa kama sehemu ya starehe, za kupindukia. Sasa jiandaeni kupisha sheria zitakazokuwa zinaruhusu nudity na sun-bathing kwani huo ndio utalii wa beach. Utalii wa bara ukiondoa kwenye beach, hauitaji sunbathing wala nudity kwani huwezi panda mlima kilimanjaro wala kwenda serengeti ukiwa nude. Ni bora pia mkafikiria hayo kabla hamjapanga hiyo mikakati yenu ya uchumi wa kisiwa chenu

Nini na vipi Zanzibar iwe watakao amua ni wazanzibari wenyewe sio Straatkasyambe wala Nguruvi3 wala Mwanakijiji . Miaka 47 ya Muungano kilichopatikana ni kuengezeka kwa umasikini na hali ngumu ya maisha sio Zanzibar tu, bali hata hapa Tanganyika. Kutafuta solution ya kutatuwa matatizo ya watu milioni moja ( 1,000,000) ni rahisi kuliko watu milioni 40... Kitu cha mwanzo ni uhuru mengine yatafuata ....HIZI SIO ZAMA ZA NYERERE , MPAKA KIELEWEKE.
 


Duh! ama kweli kazi kweli kweli maana maneno hayo hapo juu yameniacha hoi...Kumbe ni hawa watu wahamiaji ndio wanakuja kudai nchi yao!

hata hapa tanganyika wako wenye asili Kenya, Uganda,Malawi, Burundi,Somalia, Msumbiji, India,Pakistan, Ruwanda,Zaire (Congo) South-Afrika na sehemu nyengine... Au matanganyika lazima awe Mchaga au Mzaramo?
 
Kuna watu naamini wanaishi wakiwa wamefungwa na kale; Baadhi ya watu wanaodai hii "Zanzibar" hawalilii Zanzibar Mpya wanataka Zanzibar ya kale. Wenyewe wanaita "Utukufu wa Zanzibar". Ukiwauliza hawa utaona wanakumbushia jinsi maisha yalivyokuwa mazuri Zanzibar "wakati ule" na watataja mambo yale matamu ya wakati ule ambayo yaliimbwa katika nyimbo na kutungiwa tenzi.

Hivyo kwa hawa Zanzibar inabakia kuwa kama Jiji la Atlantis tunaloambiwa lilipotea katika historia ya kale na kuwa lilikuwa ni jiji lililokuwa limepiga hatua kubwa sana na kwa miaka maelfu sasa limebakia likisimuliwa katika njozi juu ya utukufu wake. Hii ndio Zanzibar ambayo watu wanaitamania. Ni Zanzibar yenye kwenye njozi ambayo iliishi katika utukufu ambapo watu wake waliishi kama wamoja, wakipendana, bila dhulma, hiana au mgongano wowote. Ni Zanzibar tukufu ambayo historia yake tunaambiwa ni ya kale sana.

Zanzibar hii ya kale utukufu wake unahusishwa zaidi na ujio wa Waarabu na Uislamu. Licha ya utukufu wa mambo ya maisha kuna utukufu ambao unaendana hisia ya kustaarabika na ukiwasoma baadhi ya watu wanaobeza watu wa bara wanabeza kutoka katika misingi ya kuwa Zanzibar ilistaarabika mapema kuliko bara kwa kupokea ustaarabu wa Kiarabu ambao ulijengwa katika misingi ya Imani ya Kiislamu. Hata hivyo, Wazanzibari hawa wenye utukufu hawajivunii Zanzibar kwa sababu ya Uislamu kwa sababu kama hiyo ingekuwa kweli watu wa bara wengi tu nao wangeweza kujivunia Uislamu wao kwani maneo kama Kilwa (iliyoko bara) yanaweza kujivunia Uislamu ule ule wa Zanzibar na kuna wengine ambao wanadai kuwa Zanzibar yenyewe (kama maswali yangu hapo juu nilivyoashiria) haikuwa inakoma kwenye visiwa viwili tu vya Unguja na Pemba kama wengi wanavyotaka tuamini bali ilihusisha hata baadhi ya miji ya mwambao wa Afrika ya Mashariki.

Tatizo kubwa ni kuwa watu wengi wa bara hawajui historia yao na wanaamini kuwa historia yao ilikuja na kuanza na ujio wa Waarab. Wengi wetu wala hatujui kuwa kuanzia karne ya kwanza kabisa pwani ya Afrika ya Mashariki ilikuwa na jamii zake nyingine nazo zilipotea katika historia kama jiji la Atlantis. Kwa mfano watu wengi wa bara hawajawahi kusikia jina la Prof. Felix Chami ambaye amefanya utafiti mkubwa sana katika eneo la pwani ya Afrika ya Mashariki hasa maeneo ya Kilwa na Delta ya Rufiji huko. Dr. Chami ndiye ambaye miaka ya hivi karibuni amepindua kabisa historia ya Afrika ya Mashariki ambayo tumejaribu kulazimishwa kuaminishwa kuwa ndio "historia sahihi" kuwa ustaarabu na mahusiano na nje ya Afrika ya Mashariki yamekuja baada ya Waarabu.

Hivyo, wanaotaka Zanzibar bado hawajaweza kujibu kuwa ni ipi hasa wanayoitaka. Wanaosema wanataka Zanzibar "iliyoungana na Tanganyika" Zanzibar hiyo ni ile ya Mapinduzi yaliyomng'oa Sultani katika tukio la umwagikaji wa damu mkubwa. Zanzibar hii iliyojeruhiwa na kuumizwa na kuwagawa Zanzibar kinasaba na kwa damu, haiwezekani iwe ni Zanzibar ambayo hawa ndugu zetu wanaitaka. Watakuwa wanataka Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi. Lakini Zanzibar ya kabla ya Mapinduzi haikuwa ni Zanzibar ya watu wote. Waliojifunza historia wanajua kabisa kugawanyika kwa Wazanzibar hakukusababishwa na Muungano wala hakukusababishwa na Nyerere.

Hawa vijana wa leo wanaomlaumu Nyerere hawaambiwi historia yao kweli. Wengi hata hawajui kuwa umwagikaji damu Zanzibar haukuja mwaka 2001 tu au mwaka 1964; wanaofahamu historia wanajua damu ilishamwagika na vurugu kutokea Zanzibar kufuatia uchaguzi visiwani mle. Kwani hata hiyo inayoitwa "serikali ya Shamte" haikuungwa mkono na Wazanzibari wote - ushahidi ni matokeo ya chaguzi mbalimbali visiwani mle. Matokeo ya uchaguzi wa 1957, wa 1961 na hata wa 1963 ulionesha wazi mgawanyiko kati ya vyama vikuu vya Zanzibar ambavyo mtu yeyote anayejua historia anajua vilihusiana na nasaba za watu. ASP, ZPPP na ZNP viliwaganya Wazanzibari. Na hata kilichofanyika mwaka 1963 kuunda "serikali ya mseto" ya Shamte tunajua hakikuwa sababu ya furaha kwa Wazanzibari wote. Lakini wapo wanaotaka tuamini kuwa uchaguzi wa 1963 uliwaunganisha Wazanzibari!

Hapana, Wazanzibar leo hii kama Nyerere alivyosema wanaunganishwa na chuki yao dhidi ya Muungano na dhidi ya watu wa Bara ambao wengine ni ndugu zao wa damu. Wanaunganishwa na chuki ambayo yaweza kuwa pia ina msingi wa udini vile vile lakini nafikiri zaidi ni msingi wa ubora (superiority complex) ambayo tulioishi maeneo ya pwani tunajua baadhi ya watu wanavyojiona bora kwa sababu ya nasaba zao. Bado watu wanawaona watu weusi kuwa ni duni kwao. Na bara kuwa na sehemu kubwa ya watu wake ni watu weusi inaonekana kana kwamba ni uduni wa aina fulani na watu wanaitaka "Zanzibar mpya". Tukumbuke kuwa kinyume na kule Marekani ambapo sheria ya "tone moja la damu ya mtu mweusi" inakufanya uwe mtu mweusi kule Zanzibar na hata maeneo mengi ambayo watu walichanganya damu na waarabu utawakuta wapo wetu weusi tii ambao wamejiaminisha kuwa wao ni Waarabu - si kwa maana ya tamaduni na imani bali kwa maana ya nasaba. Kwani Uarabu kama inavyosemwa na watu wengi siyo suala la damu. Lakini wapo watu ambao hujitambulisha kuwa ni waarabu kwa maana ya kwamba katika familia zao wamechangia damu ya waarabu na hivyo wanawaona weusi wenzao kuwa si wenzao!

Tatizo hata hivyo ni kuwa chuki haiwezi kuunganisha. Inaunganisha tu kwa kadiri ya kwamba kile mnachokichukia bado kipo. Ndio maana Nyerere katika ile hotuba yake ya kinabii (natumia neno nabii loosely) alisema wazi kuwa dhambi ya kubaguana haikomi. Yule unayembagua akishaondoka unatafuta mwingine wa kumbagua. Zanzibar wanaweza kuamua kabisa wakawa nje ya Muungano. Ni haki yao kama binadamu na ni haki yao kufanya uamuzi huo. Lakini anayefikiria kuwa baada ya kutoka kwenye Muungano Wazanzibari watarudi kuwa wamoja - hawajawahi kuwa wamoja anyway - wanajidanganya. Zanzibar ya 1963 ilikuwa imegawanyika - ikirudi ile ile itagawanyika.

Nilikuwa nasikiliza Clouds FM juzi tu hapa na watu wengine walikuwa wanaanza kuzungumzia Jamhuri ya Pemba. Hawa ni Wapemba ambao wanaona kuwa Unguja inajjipa madaraka makubwa juu yao na kama sote tunavyofahamu ni chini ya CCM kwa mara ya kwanza Mtawala wa Zanzibar anatokea Pemba (niko tayari kusahihishwa katika hilo). Wapo waunguja ambao wanaona Wapemba ni duni kwao na wapo Wapemba ambao wanaona Waunguja ni kama watu tofauti kabisa na wao. Na hizi tofauti haziondoki kwa sababu Muungano umekufa - zitarudi kwa nguvu pamoja na maneno matamu kuwa "Zanzibar yetu sote" sijui "Zanzibar ni moja".

Binafsi mimi ni Unionist. Siaminii katika serikali tatu kama wengine, wala siamini katika serikali ya Tanganyika - kwa sababu nilizowahi kuzianisha huko nyuma. Ninaamini katika taifa na serikali ambayo ni zao la wananchi wote wa nchi hiyo. Kama Zanzibar wanataka kujitoa ni ndugu zetu, tuna historia nao, wala historia hiyo haifutiki kwa sababu hatuna Muungano. Tena naamini tunaweza kuwa na uhusiano mzuri kabisa wa kidugu hata wa kulindana kwa damu kama ulivyo wa Wamarekani na Waingereza licha ya kuwa Marekani ilijitangaza huru kutoka falme ya Mwingereza. Leo hii Wamarekani watakufa kuwalinda Waingereza na Waingereza watakufa kuwalinda Wamarekani.

Sipendi wanaozungumza kwa misingi ya kupandiza chuki kati ya Wabara na Wazanzibari. Kuna watu wengi wako Zanzibar ambao wanatoke Bara na kuna watu wengi wa Bara wanaotokea Zanzibar hawa wenye kuzungumza kwa chuki hizi za "Ubara' na "Uzanzibari" au "Uzanzibara" ni watu wa kuogopwa tu. Muungano uliundwa na binadamu, tukiona haufai tunauvunja na tukaendelea kuwa na mahusiano mazuri tu tena yanaweza kuwa na maana zaidi. Jamani Rwanda na Burundi ziliwahi kuwa chini ya utawala mmoja na Tanganyika. Leo hii tuna mahusiano na nchi hizo kwa karibu tu. Jamani tuna mahusiano na waliokuwa wakoloni wetu Wajerumani na hata Waingereza. Tuna mahusiano na nchi zilizochukua wazee wetu utumwa kwanini tuhisi hatuwezi kuwa na mahusiano mazuri na ndugu zetu wa Zanzibar ambao wanaweza kutaka kujitoa kwenye Muungano?

Ninaamini kuna kura moja tu inayohitaji kuamuriwa aidha kuungana kuwa nchi moja kabisa - mifumo tofauti ya utawala au kuvunja Muungano ili tuwe na nchi mbili rafiki, ndugu na zenye mikabata ya makubaliano ya ushirikiano labda kuliko na nchi nyingine yoyote ile. Hili linawezekana. Lakini haya mambo ya kufanyana duni na watu kujiona bora ni hisia zisizo na msingi na zinajaribu kung'ang'ania masimulizi ya kale kuliko ukweli wa kihistoria.


Mkuu Mwanakijiji , usipoteshe watu kwa falsafa zako za uongo na kweli... Kilio cha wazanzibari ni Matatizo ya ki-UCHUMI ,SIASA NA MAENDELEO. Hakuna mtu anabaguliwa Zanzibar eti mweusi ,sio kweli . Mimi nimeshi kote Tanganyika na Zanzibar sijaona hicho kitu. Ikienda Zanzibar ,halafu waambie hii sio nchi , kweli watakutenga hata uwe na rangi kama mzungu wa ulaya. Huo ndio ukweli wa mambao.
 
hata hapa tanganyika wako wenye asili Kenya, Uganda,Malawi, Burundi,Somalia, Msumbiji, India,Pakistan, Ruwanda,Zaire (Congo) South-Afrika na sehemu nyengine... Au matanganyika lazima awe Mchaga au Mzaramo?
Kweli wapo lakini ni wahamiaji na hawadai Tanganyika ni yao!
 
Mkuu Mwanakiji , usipoteshe watu kwa falsafa zako za uongo na kweli... Kilio cha wazanzibari ni Matatizo ya ki-UCHUMI ,SIASA NA MAENDELEO. Hakuna mtu anabaguliwa Zanzibar eti mweusi ,sio kweli . Mimi nimeshi kote Tanganyika na Zanzibar sijaona hicho kitu. Ikienda Zanzibar ,halafu waambie hii sio nchi , kweli watakutenga hata uwe na rangi kama mzungu wa ulaya. Huo ndio ukweli wa mambao.

yeah right hata historia ya Zanzibar mnataka tusahau! Hii Zanzibar ya pepo hiyo iliwahi kuwepo lini? Matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo ni nchi gani ambayo haina? Wengine tuliaminishwa kuwa nchi zote za Kiarabu ni pepo, maskini kina Khalid wametuonesha ile siri kuu. Tunaambiwa Oman ni pepo.. juzi tunaoneshwa kuwa ipo Pepo ya Wachache. Na hivi ndivyo mnavyotaka watu waamini kuwa Zanzibar ilikuwa Pepo kwa kila mtu, kumbe ilikuwa Pepo ya Wachache.

Kweli mnafikiri mkiwa nje ya Muungano ndio matatizo ya Kiuchumi, Kisiasa na Maendeleo yataondolewa? Really? SAudia na mafuta yake yote hayo imeweza vipi kuondoa matatizo yote ya Kijamii? Hata Libya, Iran, na Iraq zote ukiziangalia kwenye kipimo cha maendeleo zinaoneshwa ziko juu ya Tanzania lakini leo tunajua kuwa siyo vyote vinavyomeremeta dhahabu. Jamani msiwaadahe watu kuwa ati Zanzibar ikiwa nje ya Muungano basi pepo itarudi. Msije kujikuta mnabakia kuimbiana taarab za nyimbo za "iliyokuwa Zanzibar" huku watu wanatamani pepo isiyokuwepo.

Ushirikiano wetu unatuhakikishia sote na miye napendekeza zaidi Zanzibar a brighter future kuliko watu wanavyodanganyana.
 
Back
Top Bottom