Muungano umewadumaza na kuwafikisha hapo walipo. Wazanzibari wanaitaka Zanzibar yao ambayo kuondokana na koloni la Tanganyika.
Kwahiyo serikali ya mapinduzi na BLW,wimbo wa Taifa, bendera ya Znz, Rais na Makamu hivyo havitoshi kuwa ni Znz.
Muungano umeidumaza znz,tunahitaji ufahamu, ni kwa vipi kama si kuisadia.
Pili, je muungano hauna lolote jema na kama lipo ni lipi.
Kabla ya "Muungano" huu, Zanzibar ilikuwa inajiweza kujiendesha wenyewe bila ya matatizo yoyote yale na hatukuwahi kuwa tegemezi kwa nchi yoyote ile.
Ni wakati ule karafuu ilikuwa 'hot' na Znz kuitwa spice island, karafuu inazalishwa kwa ubora na mataifa mengi,kudorora kwa uchumi wa znz ni matokeo ya kudhani ndiyo pekee inayoweza kuzalisha karafuu. Pesa zikatumika kuwekeza katika TV za rangi na ya kwanza Africa.
Tanganyika imepata vitu kama hivyo miaka 20 iliyopita, lakini waliwekeza katika elimu, afya n.k. Ndiyo maana viongozi wote wa Znz wame elimikakupitia Tanganyika.
Tanganyika inatajwa kwa sababu inaonekana inaing'ang'ania Zanzibar kwa nguvu na hili halikubaliki.
Hakuna Mtanganyika anayeing'ang'ania ZNZ, nieleze kwa lipi linaloweza kukosekana kwa znz kutokuwepo? Hoja kuu hapa ni uchumi ambao nimeshaueleza kuwa haukidhi haja ya kung'ang'ania ZNZ.
Wazanzibari wanakuja kufanya biashara bara ndio lakini pia wanakwenda Kenya kutokana na ukaribu kijiografia. Pia wanakwenda sehemu mbalimbali duniani kama wanavyokwenda Watanganyika kutafuta fursa ya kujiendeleza kimaishi
.
Wanapokwenda Kenya ni tofauti na wakiwa bara. Waulize wafanyabiashara kwanini wanapenda bara zaidi ya Kenya. Mznz hawezi kusoma vidudu hadi chuo kikuu Kenya kama utambarare wakiwa bara. Hawabaguliwi na ni sehemu ya wananchi wa kawaida. Waulize Wznz wa kawaida wanaoishi bara watakueleza.
Jiulize kwanini waagize bidhaa za kilimo kutoka bara na si mombasa au Lamu.
Sasa Wazanzibari wametamtambua adui yao na wanarekebisha makosa yao na kuundwa kwa GNU/SUK ni kielelezo tosha kwamba Wazanzibari wameamua kusahau tafauti zao na wanajiandaa kudai haki yao, jambo ambalo ni dhahir limewashtua.
Ndani ya muungano kuna GNU nje ya muungano wapo wanaosema mapinduzi daima na wapo wanaosema mapinduzi ya Okello na Nyerere. Ndiyo maana nimekuuliza swali kabla, je mapinduzi mnayathamini au ni ya Nyerere na Okello.?(Huna jibu)
Ndani ya muungano ni Wznz, nje ya muungano wapo wzn weusi waunguja na wamanga wapemba.Wapemba wanasisitiza kuwa hawana mkataba na Unguja, juzi tu wamerudia hayo. Je GNU ni kutoka katika muungano au ni ya kudumu.?
Baraza la Wawakilishi tayari wameanza kuchukua hatua unazopendekeza Mkuu Nguruvi kwa kuifanyia marekebisho Katiba yao ya mwaka 1984
Kipi kinashindikana kupeleka mswada wa kuvunja muungano ili wasing'ang'aniwe na Tanganyika.
Mjadala wa Mswada uliojadiliwa hivi majuzi ni kielelezo chengine kwamba Wazanzibari hawaridhiki na mfumo wa sasa wa Muungano.
Mswada umepingwa vikali bara, si kwa ajili ya muungano tu, bali maudhui yote. Tofauti na Znz bara wametumia kauli,na Znz wametumia hisia za vurugu. Kuna uwezekano wa kusema 'hapana' bila rabsha.
Kwanini mnakasirika pale Wazanzibari wanapodai chao?
Kinachowaudhi watu ni kauli za ukoloni, tunaonewa n.k. Fikiria umembeba mtu mgongoni bado anarusha mateke na kejeli.
Kinachoudhi ni kuwa kwanini msirudi kwenu, mkatumia BLW na kusema basi.
Wazanzibari wanaitaka Zanzibar yao kwanza, mfumo gani wa kushirikiana, hilo ni baadae
Sidhani kama kunahitajika mfumo wa ushirikiano, upi labda na kwa vipi, nifafanulie.
Wznz walio wengi na wakawaida wanatumia fursa za muungano hawapendi ufe, wanachotaka ni kuurejea na kuangalia mapungufu.
Wznz wanaoishi nchi za nje wanataka ufe wakijua kuwa watakaporejea nyumbani na elimu zao au kuongea kiingereza watapata fursa za vyeo.!!!(mzalendo.net)
Wasichokijua znz ni kuwa eneo lao na population ni matatizo katika siku za mbeleni. Biashara zao zinategemea majirani hasa Tanganyika.Kama watajenga uchumi bado utakuwa tegemezi.
Misaada toka uarabuni ambako wengi wanadhani znz ni sehemu ya, itasadia sana kuinua uchumi nakurudisha ukoloni wa Sultan.
Fursa zote mnaziziona,nje ya muungano ni ushindani.
Kujitenga kwa znz ni sababu ya hisia za kuwepo mafuta. Haya hatukuyaona wala wakati mishahara ikitoka bara. Fanyeni maamuzi haraka mpate nchi yenu yenye asali na maziwa, ila tu isije kuwa nchi ya kufikirika.