Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Wakuu sasa hapana tunamlaumu Sitta as a person au systme inayomruhusu Spika hata ukiwa wewe au mimi kukaa kwenye nyumba ya gharama hiyo. Kuna institutional corruption lazima tuikemee pia. Tatizo hakuna mwenye uwezo na hakuna mechanism ya kupambana na bunge as institution.

Hapa bwana Sitta ana lawama. Kwa nini yeye akubali kuishi kwenye nyumba ya bei kubwa kiasi hicho wakati Bunge linakabiliwa na ukata. Hao waliofanya mpango wa kuitafuta ama wanajikomba kwake au nao wana dili la nguvu. Kwa hiyo ni vizuri tukaijua hiyo hadhi ya Spika na gharama yake (in terms of monetary value) ili tujue kweli kama anastahili kula $8K kwa pango la nyumba (rent) kwa mwezi. Pia tuwekwe wazi hiyo nyumba ni mali ya nani na mchakato wa kuipata ulikuwaje? Ikiwezekana tuoneshwe nyumba yenyewe (kama kuna mtu ana photo atuwekee tafadhali). Vinginevyo jamaa wamechonga dili la kupata pesa ili Mzee asiukose ubunge 2010 au akalazimika kulamba viatu vya RA. Hiyo bei naamini inashindana na zile za DC au NY wakati mji wenyewe ni Dom. Nitakuwa mtu wa mwisho au kiazi kuamini kuwa hili suala ni kweli (it's real) na si ulaji mwingine wa kufyonza besi za umma kiulaini.

Ila hili la mhasibi kihiyo kufanya kazi za bunge nalo ni hatari. Mhhh, Bongo Dar ni kila mahali!!
 
Habari wanabodi,

Ni muda sijaingia humu sababu ya majukumu makubwa niliyokabidhiwa miezi mitatu iliyopita,Muda wa kupitia humu unakuwa mdogo sana.

Hii ya spiika kutumia zaidi ya milion 700 kwa muda wa miaka matano kwa malazi tu ni jambo la kupigwa vita.

Nchi ya mandondocha..sijui tumerogwa!

Mwanakijiji fuatilia hili,hiyo nyumba inamilikiwa na nani na je tender ilitangazwa kupata mzabuni.Unawez akuta hiyo ni nyumba ya kigogo wa serikali..tayari dar sasa hivi kuna nyumba za dola 8000??aisee..

Karibu mkuu Gembe. Kweli tumeku-miss. Mkuu hii ni episode nyingine ya Bongo Darisalam!!
 
Ehee,kazi tunayo waafrika,hivi Tanzania ni nchi ya ngapi vile kutoka chni kwa umasikini.?....i'm stumped,nashindwa kuamini hii figure...au kuna typing error? may be ni 800$. Wakuu anayeweza kutuletea picha japo ya nje tu na ajitahidi basi...
 
Kama jamaa hana shule ya kutosha kwanini msitangaze kazi hiyo muone watu watakavyopangana na hizo CPA mnazoclaim? TZ kuna CPA nyingi tu siku hizi ambazo naamini kwa kazi kama hiyo watakuja chap chap. Please tangazeni hiyo vacant post wanaostahili walambe kazi mara moja!
 
Karibu mkuu Gembe. Kweli tumeku-miss. Mkuu hii ni episode nyingine ya Bongo Darisalam!!

Mkulu dar city,

Pamoja sana mkuu,Nimepitia kurasa nyingi sana toka ausbuhi hapa na nimeona kuna membr wengi wapya na wa zamani kama wanapotea..Mchungaji haonekani kabisa ..

watu wako busy wanaandaa ilani kuelekea 2010.Mie nataka uandaye ya kwetu hapa JF ili tuwagawie Wananchi.Mwanakijiji kazi kwako na ushirikiane na Rev.
 
Nchi inatisha, kila mahali na kila idara ya serikali na mihimili yote ni wizi na ufisadi kwa kwenda mbele! Sasa nani aliyebaki kuhakikisha kuwa hata makombo yatamfikia mlalahoi kabla ya kutupiwa mbwa na kuku wa wakubwa!

Jibu rahisi, "rais ndiye aliyepitisha". Hii ni aibu kubwa!

Tunahitaji madiliko makubwa!
 
Ndo maana kwenye hotuba ya Obama alisema kua "Africa needs strong institution not strong men" sasa kwa bongo naona ma strong men kibao......wadanganyika lini tutaamka????
 
Huyu anayelipiwa na Sipila Sita ama ni mutu gani hii ? Yule jamaa ambaye huwa anawaka sana mbele kwamba ana uchungu na Nchi ?Duh no wonder Msekwa alitaka kuendelea kuwa Sipika
 
Jamani siyo sitta peke yake, angalia maprofesa wote wa vyuo vikuu ni kwamba wanalipwa hela ya kupanga nyumba sh. 1,000,000/- kwa mwezi lakini wanakaa ktk nyumba zao walizo kwisha jenga. Je, hiyo ni sawa??

Ndiyo maana ufisadi hauwezi kuisha na utaendelea. Kwamnza muulizeni VC wa mzumbe mbona ameacha nyumba yake ya kikazi pale MU na sasa anaishi Moro mjini na wakati huo huo analipwa pesa ya nyumba (housing allowance) kila mwezi??

Miafrika ndivyo tulivyo!!!!
 
Kama kweli anaishi kwenye nyumba ya milioni nane, ni fisadi hana cha kutwambia.
 
8000 x 12 x 5 = usd 480,000 in five years only housing; kweli masikini hajijui kuwa ni masikini; hata akili haifanyi kazi. Hata Raisi hana akili!

Hiki ni kiasi kikubwa sana kwa pango hakikubaliki,hivi wakati wanaidhinisha matumizi haya je hawakumbuki kuwa kuna watanzania ambao hawahimili milo miwili kwa siku tena makao makuu ya Serikali Dar let alone mikoani.

Huu ni ubinafsi wa hali ya juu,mimi nafikiri wameshachoka kuongoza na inabidi wapumzishwe haya matumizi hayakubaliki kabisa kwenye nchi kama ya kwetu.

Hadhi ya Spika kwani akikaa kwenye nyumba ya gharama ndiko kunakomuongezea hadhi au ni utendaji uliotukuka kwa kuthamini hali halisi na kulinda utu wa watanzania ndiko kunakomuongezea hadhi.Kwa kweki wamekengeuka na ni vipofu ambao hawastahili kutuongoza,.Hali hii haikubaliki kabisa.
 
viongozi wa hovyo huwekwa na wananchi wa hovyo

Ndugu yangu wapigakura walio wengi hii nchi yetu ni mbumbumbu. Wao hawajui kabisa kinachoendelea katika hii nchi. Hata magazeti hayawafikii, wala TV hawana, ugumu wa maisha waliyonayo hawajui chanzo ni nini. Wamezaliwa katika mazingira hayo na wanaona ni kawaida tu kuishi hivyo. Kumbuka statement ya Mkuchika wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo kule Busanda hivi majuzi; nanukuu "Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyie wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu," Alifoka Mkuchika.

Kwahiyo bado tuna safari ndefu sana ya kuwaondoa madarakani hawa viongozi wabovu wasio na uchungu na wananchi wao kwa kufuja mali za umma.
 
Hapo kazi ipo. Lakini nahisi huu ni mchezo wa kuchafuana tu ulioanzishwa na kundi la waathirika wa Richmond. Ngoja tusubiri ushahidi.
 
Ubinafsi umezidi kuliko kuwaza maendeleo ya nchi na wananchi unaowatumikia. Hiyo ya Spika ni baadhi tu ya mambo ovyo ovyo yanayofanywa na viongozi katika kutumia vibaya pesa kujinufaisha.
Ndo mana baadhi ya watu wakipata ulaji(cheo kikubwa) ni kukimbilia kujilimbikizia maana ndo akili zilivyokariri, ubinafsi kuanzia mawazo!..
No wonder bakuli haliachi kutembea, matumizi ovyo.
 
Nyumba za serikali si wameshajiuzia sasa wanabaki kupangisha.. hii akili ya viongozi wetu sijui imekaaje. chunguzeni vizuri utakuta hiyo nyumbani aliyopangishiwa ni ya hao hao tu hakuna kitu hapo ni mchezo tu wanatuchezea watanzania.
Inamaana hiyo hadhi anayotaka spika kwa kuhamishiwa nyumba ambayo alikuwa anakaa tayari na kupangishiwa nyingine hiyo ya mamilioni ni hadhi gani huyu jamaa ataitaka.
Waafrika kweli akili hatuna.. mbona mtoni kiongizo wa juu tu anakaa kwenye nyumba kama raia tu mwingine. Hiyo ni "game" tu wamecheza.. hizo hela wanajilipa wenyewe hakuna kitu hapo.. no body can agree kulipa mtu kiasi chote hicho kwa pango.. imekuwa ikulu hiyo..????

Yaani viongozi wetu wa kiafrika huwa wanapenda hadhi ambazo sijui zitawapeleka wapi. Kama ulivyosema mkuu ni kweli huku ughaibuni mawaziri na viongozi mbalimbali wanaishi uraiani kabisa. Tunapanda nao treni/mabasi kama kawaida tena wengine achilia mazoezi wanakwenda mahali kwa baiskeli. They are so simple na hawako mbali na raia wao kama ilivyo kwetu Afrika, maana Afrika kiongozi na raia ni maadui kwasababu viongozi wetu wanajua kuwa hawawatendei haki wanaowaongoza. Wamajijengea tabaka lao tofauti. Inauma sana. Viongozi wa kiafrika ni miungu watu, ni watu waliojaa ubinafsi usioneneka. Hivi kweli inaingia akilini mtu ukae kwenye nyumba ya milioni 10 kwa mwezi wakati mwalimu/polisi hata laki 3 kwa mwezi haipati achilia watu wanaoamka hawajui kama watakula siku hiyo.

Acheni wazungu wazidi kubarikiwa. Ukitaka kujua siri hii soma signature yangu.
 
Kweli hawa viongozi wetu hawana uchungu na kodi zetu, hiyo nyumba ina nini hasa? Na kama unaworthy 10ml kwa nini wanunue na thamani tena za ml 200!?
Namna hii hatuendi popote

Rafiki mambo yanayoendelea serikalini yanatia uchungu. Huwezi kuamini hata Laptop ya USD 900 hununuliwa kwa USD 3000 n.k. Hii ina maana kuwa tunapoteza pesa nyingi sana kwa njia za wizi.
 
<p>
Hiki ni kiasi kikubwa sana kwa pango hakikubaliki,hivi wakati wanaidhinisha matumizi haya je hawakumbuki kuwa kuna watanzania ambao hawahimili milo miwili kwa siku tena makao makuu ya Serikali Dar let alone mikoani.</p> <p>&nbsp;</p> <p>Huu ni ubinafsi wa hali ya juu,mimi nafikiri wameshachoka kuongoza na inabidi wapumzishwe haya matumizi hayakubaliki kabisa kwenye nchi kama ya kwetu.</p> <p>&nbsp;</p> <p>Hadhi ya Spika kwani akikaa kwenye nyumba ya gharama ndiko kunakomuongezea hadhi au ni utendaji uliotukuka kwa kuthamini hali halisi na kulinda utu wa watanzania ndiko kunakomuongezea hadhi.Kwa kweki wamekengeuka na ni vipofu ambao hawastahili kutuongoza,.Hali hii haikubaliki kabisa.
</p> <p>&nbsp;</p>
 
Kwa takwimu za matumizi ya Spika, Tanzania siyo nchi masikini kabisa. Hiyo hela ya kodi peke pamoja na samani kwa mwaka mmoja vingetosheleza kununua au kujenga nyumba ya kudumu ya Spika. Vielvile huyo mhasibu kutokuwa na sifa ni kisingizio tu kwani taratibu za Ofisi ya Bunge si zinaainisha sifa za Mhasibu? Iweje muda wote awe kazini halafu leo kumetokea tuhuma ndiyo anasemwa kuwa hana sifa?
Halafu, "gari, nyumba vyenye hadhi ya Spika" maana yake ni nini? Wenzetu wa nchi zilizoendelea walishatoka huko, wanasafiri kwa treni kama wananchi wengine na wanatumia magari ya kawaida tu. Tatizo viongozi wetu wamesahau kuwa uongozi ni kutumikia na siyo kutumikiwa.
 
Nani mwandishi wa hii habari? Kwani Shellukindo ni Mwenyekiti wa kamati gani vile......au anashikilia wenyeviti wa kamati mbili? Nina mashaka na chanzo cha habari ili kuweka kumbukumbu sahihi.
 
Back
Top Bottom