Ni ngumu sana kumpata Mwanamke kama Tulia Ackson. Ana uwezo mkubwa, anafaa kuwa Rais

Nashukuruuu Sanaaaa kwa kuliona hilo ambalo wengine tulishaliona tangia muda mrefu sana na kuandika sana humu jukwaani kwa kurudia rudia sana ,katika kueleza uwezo mkubwa wa kiakili na kiuongozi alio nao Mheshimiwa Dkt Tulia Acksoni Mwansasu Dada wa Taifa na Nguli wa sheria kuwahi kutokea nyanda za juu kusini.

Bora wewe umejisemea ukweli maana mimi nikiandika naambiwa kuwa namtetea na kumpamba sana. Ok ngoja nisiandike sana leo.
 
Hamna kitu hapo. Watu mnasifia ujinga tu sijui mumelipwa Shillingi ngapi? Huyo Tulia bila LIFT ya Magufuli asingefika hapo alipofika. Alimfanyia nini Magufuli hadi akampa u Naibu Spika, ni siri yao

Kwenye duru za sheria wala siyo nguli kihivyo, nenda kaulize UDSM uone kama ana machapisho. Ukikuta ana machapisho nenda kayatest kwa Plagiarism application ndiyo uje hapa.

Watu eti wanamsifia kushinda kesi ya muta 200 mwaka 2015. Ile kesi hata mwanafunzi wa first year Law School angeshinda tu kwa kuwa tayari Jaji wa High Court alikuwa na maelekezo.
Usijipe shida...
Vigezo vya Watanzania kusema mtu fulani ana uwezo mkubwa ni vya kipekee...
 
Shida ninayoona anayo, ni kuna muda anafanyaga mambo kukomoa yani ni kwamba utafanya nini sasa nimefanya.
Hana tofauti sana na ndungai.
Yani kama hakupendi basi atakukomoa hata kama anajua anachofanya si sahihi.
Kama anafanya kukomoa wale anaopingana nao, basi tukubaliane Dr. Tulia ni kiongozi dhaifu, anayeshindwa kujiongoza kihisia ili kukabiliana na wale anaopingana nao kwenye hoja mbalimbali.

Kwanini asiutumie huo uwezo wake wa kujenga hoja mnaosema anao kukabiliana nao, badala ya kutumia nafasi yake kuwaumiza, mimi simkubali kabisa Spika Tulia, hawezi kujiongoza wala hana msimamo, na pale maslahi ya serikali na bunge yanapotakiwa kuwekwa tofauti, hujigeuza mtumishi wa serikali bila aibu.
 
Habari za Sabato!

Sijawahi kumfahamu Mwanamke yeyote kwa hapa Tanzania mwenye uwezo kama Tulia Akson. Sisemi ili wengine wamuonee Wivu, wala sisemi ili yeye awe na Kiburi. Ila naongea kila ambacho ninaokiona Kwa Tulia mwenyewe. na uwezo wa kuongoza.

Tulia Akson anauwezo wa kushika nafasi ya Urais katika nchi yetu na sio hivyo tuu hata kuongoza Nchi yoyote hapa Duniani. Kwa sababu anasifa za level za kimataifa.

Nimemaliza
Naunga mkono hoja,

P
 
Kama anafanya kukomoa wale anaopingana nao, basi tukubaliane Dr. Tulia ni kiongozi dhaifu, anayeshindwa kujiongoza kihisia ili kukabiliana na wale anaopingana nao kwenye hoja mbalimbali.

Kwanini asiutumie huo uwezo wake wa kujenga hoja mnaosema anao kukabiliana nao, badala ya kutumia nafasi yake kuwaumiza, mimi simkubali kabisa Spika Tulia, hawezi kujiongoza wala hana msimamo, na pale maslahi ya serikali na bunge yanapotakiwa kuwekwa tofauti, hujigeuza mtumishi wa serikali bila aibu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Mkuu mimi sijawahi mkubali kwa sababu mara nyingi nainaga hayuko fair kuzuia mijadara bungeni kama vile ni mwenyekiti kwenye vikao vya chama.
Nadhani wizara ya sanaa na michezo inamfaa maana anapenda sana kuroll na kupiga picha na wasanii
 
Tulia Kwa profession ni Mwanasheria.

Na Mahali pekee ambapo tulitarajia kuona akionyesha ubobevu na HAKI katika kusimamia Serikali ni BUNGENI.

Ikiwa ameshindwa kujua kitu kidogo tu kuwa Wabunge wasio na chama hawatakiwi kuwa bungeni, atawezaje kuaminiwa position ya juu zaidi?

Mahali panapomfaa Tulia ni DARASANI kufundisha, baas.
 
Kama anafanya kukomoa wale anaopingana nao, basi tukubaliane Dr. Tulia ni kiongozi dhaifu, anayeshindwa kujiongoza kihisia ili kukabiliana na wale anaopingana nao kwenye hoja mbalimbali.

Kwanini asiutumie huo uwezo wake wa kujenga hoja mnaosema anao kukabiliana nao, badala ya kutumia nafasi yake kuwaumiza, mimi simkubali kabisa Spika Tulia, hawezi kujiongoza wala hana msimamo, na pale maslahi ya serikali na bunge yanapotakiwa kuwekwa tofauti, hujigeuza mtumishi wa serikali bila aibu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Mkuu mimi sijawahi mkubali kwa sababu mara nyingi nainaga hayuko fair kuzuia mijadara bungeni kama vile ni mwenyekiti kwenye vikao vya chama.
Nadhani wizara ya sanaa na michezo inamfaa maana anapenda sana kuroll na kupiga picha na wasanii
 
Habari za Sabato!

Sijawahi kumfahamu Mwanamke yeyote kwa hapa Tanzania mwenye uwezo kama Tulia Akson. Sisemi ili wengine wamuonee Wivu, wala sisemi ili yeye awe na Kiburi. Ila naongea kila ambacho ninaokiona Kwa Tulia mwenyewe.

Kama utapata Nafasi ya Kumsikia Tulia Akson akizungumza iwe kwa kuhojiwa au kuhutubia, utagundua kuwa hana tofauti na kina Kamala Harris au kina Hilary Clinton.

Utulivu!
Kujiamini!
Umahiri!
Hoja!
Ubobevu!,

Nimeona Watu wengi wanapokutana na Tulia katika mijadala wakimshindwa kwa Hoja. Unapozungumzia hoja Unazungumzia uwezo wa akili ya mtu kujenga mantiki, yaani kitu kieleweke. Wakati mwingine kwa lugha rahisi.

Tulia sijawahi kumsikia akijali uanamke wake au maumbile yake kama sehemu 6a kikwazo katika kazi zake.
Tena yeye hupendelea changamoto anapokutana na sisi wanaume.

Tulia hatajali kama wewe ni Waziri au Mheshimiwa, ukiwa bungeni kama ataona kuna jambo hujalitolea maelezo yaliyonyooka au hakuna hoja anauthubutu wa kukukosoa au kutaka kukuweka Sawa.
Kujadiliana na Tulia Akson itakupasa uwe na uwezo mkubwa kama yeye au umzidi ili usije ukaaibika.

Kwa mwanaume mwenye upeo mdogo lazima amwone Tulia kama Mjuaji, hasa pale atakaposhindwa kwa Hoja.

Tunaposema Wanawake wapewe nafasi tunahitaji wanawake wa mfano wa Tulia Akson. Wanawake wenye uwezo.

Sio Mwanamke anayelalamika hajapewa haki yake. Tunahitaji Wanawake wenye uwezo wa kudai haki zao wenyewe bila kusaidiwa. Hao ndio watakuwa na uwezo wa kuongoza.

Tulia Akson anauwezo wa kushika nafasi ya Urais katika nchi yetu na sio hivyo tuu hata kuongoza Nchi yoyote hapa Duniani. Kwa sababu anasifa za level za kimataifa.

Nimemaliza
Yaani umeamua kutuchora tutanawazaje au??? Labda sijaelewa nini unamaanisha kaka mtibeli labda utumie muda kunielewesha.... Kwani wewe huwezi kuwa kiongozi wa nchi hiii??? Nakuonaga ukosmart sana ila leo nimekuvua nyota zote aseee
 
Kwa lile bunge legelege sijui umetumia kigezo gani kupima uwezo wa Tulia kwenye kujenga hoja.

Nina wasiwasi unamchukulia Tulia vile alivyo na tabia za kidikteta, kuingilia mazungumzo ya wale anaozungumza nao, ndio unamuona ana uwezo wa kujenga hoja.

Sijui kama uliwahi kumuona yule Tulia aliyeliongoza bunge kupitisha ule mkataba haramu na DPW unaolalamikiwa na wengi mpaka leo, yule alikuwa kuwadi wa watanganyika aliyejipendekeza kwa serikali ili kufanya kile serikali inachotaka.

Akiwa kama spika wa bunge alitakiwa kuwa kama refarii, awaongoze wote wanaopinga hoja na kuunga mkono hoja, lakini badala yake Tulia bila aibu akasimama na wale wanaounga mkono hoja kutoa bandari zetu, huyu ni kiongozi wa hovyo kabisa nina wasiwasi na upeo wako kumsifia.

Watu waliokuwa wakipinga kama Mpina ndio hawakupewa hata hiyo nafasi ya kutoa mchango wao kwa mdomo, kama Tulia anajiamini kwenye kujenga hoja kwanini akawazuia wale wenye kupinga uuzwaji wa bandari zetu wasiongee bungeni siku ile?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Changamoto kubwa ya Tulia ni Uongee aidha kwa hoja au kwa Reference hapo ndipo wengi hushindwa kwa sababu wengi huzungumza vitu kama wapo vijiweni. Porojo.
 
Habari za Sabato!

Sijawahi kumfahamu Mwanamke yeyote kwa hapa Tanzania mwenye uwezo kama Tulia Akson. Sisemi ili wengine wamuonee Wivu, wala sisemi ili yeye awe na Kiburi. Ila naongea kila ambacho ninaokiona Kwa Tulia mwenyewe.

Kama utapata Nafasi ya Kumsikia Tulia Akson akizungumza iwe kwa kuhojiwa au kuhutubia, utagundua kuwa hana tofauti na kina Kamala Harris au kina Hilary Clinton.

Utulivu!
Kujiamini!
Umahiri!
Hoja!
Ubobevu!,

Nimeona Watu wengi wanapokutana na Tulia katika mijadala wakimshindwa kwa Hoja. Unapozungumzia hoja Unazungumzia uwezo wa akili ya mtu kujenga mantiki, yaani kitu kieleweke. Wakati mwingine kwa lugha rahisi.

Tulia sijawahi kumsikia akijali uanamke wake au maumbile yake kama sehemu 6a kikwazo katika kazi zake.
Tena yeye hupendelea changamoto anapokutana na sisi wanaume.

Tulia hatajali kama wewe ni Waziri au Mheshimiwa, ukiwa bungeni kama ataona kuna jambo hujalitolea maelezo yaliyonyooka au hakuna hoja anauthubutu wa kukukosoa au kutaka kukuweka Sawa.
Kujadiliana na Tulia Akson itakupasa uwe na uwezo mkubwa kama yeye au umzidi ili usije ukaaibika.

Kwa mwanaume mwenye upeo mdogo lazima amwone Tulia kama Mjuaji, hasa pale atakaposhindwa kwa Hoja.

Tunaposema Wanawake wapewe nafasi tunahitaji wanawake wa mfano wa Tulia Akson. Wanawake wenye uwezo.

Sio Mwanamke anayelalamika hajapewa haki yake. Tunahitaji Wanawake wenye uwezo wa kudai haki zao wenyewe bila kusaidiwa. Hao ndio watakuwa na uwezo wa kuongoza.

Tulia Akson anauwezo wa kushika nafasi ya Urais katika nchi yetu na sio hivyo tuu hata kuongoza Nchi yoyote hapa Duniani. Kwa sababu anasifa za level za kimataifa.

Nimemaliza
Uwezo unaousema ni huko kuvunja Katiba kwa kuwahifadhi COVID 19 au uwezo wa kutonenepa na kuwa mwembamba milele au kwako wewe uwezo ni kitu gani hasa ?
 
Shida ninayoona anayo, ni kuna muda anafanyaga mambo kukomoa yani ni kwamba utafanya nini sasa nimefanya.
Hana tofauti sana na ndungai.Yani kama hakupendi basi atakukomoa hata kama anajua anachofanya si sahihi.
Siyo kuna muda,inaeleweka wewe nyoosha maelezo kwamba hayo kwenye bold ni hulka ya kike.

Ndiyo maana hata aliyepo sasa akibanwa sana anakaa kimya akidhani anamkomoa mtu kumbe ndiyo anazidi kuvuruga au anakimbilia kusema watu wanamdharau kwa sababu mwanamke.
 
Back
Top Bottom