Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
Habari za Sabato!
Sijawahi kumfahamu Mwanamke yeyote kwa hapa Tanzania mwenye uwezo kama Tulia Akson. Sisemi ili wengine wamuonee Wivu, wala sisemi ili yeye awe na Kiburi. Ila naongea kila ambacho ninaokiona Kwa Tulia mwenyewe.
Kama utapata Nafasi ya Kumsikia Tulia Akson akizungumza iwe kwa kuhojiwa au kuhutubia, utagundua kuwa hana tofauti na kina Kamala Harris au kina Hilary Clinton.
Utulivu!
Kujiamini!
Umahiri!
Hoja!
Ubobevu!,
Nimeona Watu wengi wanapokutana na Tulia katika mijadala wakimshindwa kwa Hoja. Unapozungumzia hoja Unazungumzia uwezo wa akili ya mtu kujenga mantiki, yaani kitu kieleweke. Wakati mwingine kwa lugha rahisi.
Tulia sijawahi kumsikia akijali uanamke wake au maumbile yake kama sehemu 6a kikwazo katika kazi zake.
Tena yeye hupendelea changamoto anapokutana na sisi wanaume.
Tulia hatajali kama wewe ni Waziri au Mheshimiwa, ukiwa bungeni kama ataona kuna jambo hujalitolea maelezo yaliyonyooka au hakuna hoja anauthubutu wa kukukosoa au kutaka kukuweka Sawa.
Kujadiliana na Tulia Akson itakupasa uwe na uwezo mkubwa kama yeye au umzidi ili usije ukaaibika.
Kwa mwanaume mwenye upeo mdogo lazima amwone Tulia kama Mjuaji, hasa pale atakaposhindwa kwa Hoja.
Tunaposema Wanawake wapewe nafasi tunahitaji wanawake wa mfano wa Tulia Akson. Wanawake wenye uwezo.
Sio Mwanamke anayelalamika hajapewa haki yake. Tunahitaji Wanawake wenye uwezo wa kudai haki zao wenyewe bila kusaidiwa. Hao ndio watakuwa na uwezo wa kuongoza.
Tulia Akson anauwezo wa kushika nafasi ya Urais katika nchi yetu na sio hivyo tuu hata kuongoza Nchi yoyote hapa Duniani. Kwa sababu anasifa za level za kimataifa.
Nimemaliza
Sijawahi kumfahamu Mwanamke yeyote kwa hapa Tanzania mwenye uwezo kama Tulia Akson. Sisemi ili wengine wamuonee Wivu, wala sisemi ili yeye awe na Kiburi. Ila naongea kila ambacho ninaokiona Kwa Tulia mwenyewe.
Kama utapata Nafasi ya Kumsikia Tulia Akson akizungumza iwe kwa kuhojiwa au kuhutubia, utagundua kuwa hana tofauti na kina Kamala Harris au kina Hilary Clinton.
Utulivu!
Kujiamini!
Umahiri!
Hoja!
Ubobevu!,
Nimeona Watu wengi wanapokutana na Tulia katika mijadala wakimshindwa kwa Hoja. Unapozungumzia hoja Unazungumzia uwezo wa akili ya mtu kujenga mantiki, yaani kitu kieleweke. Wakati mwingine kwa lugha rahisi.
Tulia sijawahi kumsikia akijali uanamke wake au maumbile yake kama sehemu 6a kikwazo katika kazi zake.
Tena yeye hupendelea changamoto anapokutana na sisi wanaume.
Tulia hatajali kama wewe ni Waziri au Mheshimiwa, ukiwa bungeni kama ataona kuna jambo hujalitolea maelezo yaliyonyooka au hakuna hoja anauthubutu wa kukukosoa au kutaka kukuweka Sawa.
Kujadiliana na Tulia Akson itakupasa uwe na uwezo mkubwa kama yeye au umzidi ili usije ukaaibika.
Kwa mwanaume mwenye upeo mdogo lazima amwone Tulia kama Mjuaji, hasa pale atakaposhindwa kwa Hoja.
Tunaposema Wanawake wapewe nafasi tunahitaji wanawake wa mfano wa Tulia Akson. Wanawake wenye uwezo.
Sio Mwanamke anayelalamika hajapewa haki yake. Tunahitaji Wanawake wenye uwezo wa kudai haki zao wenyewe bila kusaidiwa. Hao ndio watakuwa na uwezo wa kuongoza.
Tulia Akson anauwezo wa kushika nafasi ya Urais katika nchi yetu na sio hivyo tuu hata kuongoza Nchi yoyote hapa Duniani. Kwa sababu anasifa za level za kimataifa.
Nimemaliza