Ni mstari gani kwenye biblia unautumia sana upitiapo nyakati ngumu katika Maisha

Von Bismarck

JF-Expert Member
Jul 11, 2018
3,074
6,254
Bwana wetu Yesu kristo asifiwe wana Jf

Katika maisha yetu hapa duniani kuna wakati tunapitia nyakati zilizo na mambo magumu sana, kiasi kwamba kwa uwezo wetu unakosa majibu na kubaki kujiuliza maswali magumu yasiyo na majibu.

Nyakati kama za Kufukuzwa kazi, Ugumu wa maisha, kupoteza wapendwa wetu tuliowapenda sana. Usaliti katika maisha ya mahusiano na ndoa, kukosa kazi, kupakaziwa maneno yasiyo na ukweli pengine ugonjwa wa muda mrefu.

Tunapitia dhiki, mateso na maumivu katika maisha. Ukipata hiki unakosa kile ndivyo maisha yalivyo.

Natumaini letu linabakia kwa Muumba wetu.

Je ni mstari gani kutoka kwenye biblia unautumia sana kukupa faraja mpendwa.

Kwa upande wangu, Mstari unaoniongoza kila siku ni

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Zaburi 23:6

Karibu.
Tusichoke kutenda wema.
 
Back
Top Bottom