Watanzania tuna kasumba mbaya sana juu ya elimu. Utasikia mtu anasema Bakhresa mbona hajasoma lakini ni tajiri! Au Diamond mbona anaishi vizuri tu bila elimu! Ni hivi: Hatusomi shule ili tuwe matajiri, au tuwe na fedha nyingi na tuishi maisha ya kuponda raha. Hili siyo lengo la shule hata kidogo na ndiyo maana watu wengi wanakwama. Utajiri na fedha nyingi za kutesa ni vitu ambavyo mtu yoyote anaweza kuvipata ili mradi tu awe na malengo na afanye kazi kwa bidii. Kwa kifupi tunaenda shule ili tuelimike. Ina maana watu waliofika vyuo vikuu hawaoni faida ya elimu zao? Mimi mbona nimefika tu chuo, sina utajiri wowote lakini kila siku ijayokwa Mungu na-enjoy sana elimu niliyopata? Nadhani kwa sababu watu wetu wengi wamezaliwa na kukulia kwenye mazingira ya umaskini ndiyo maana wanachukulia fedha nyingi kama ndiyo kipimo cha mafanikio kielimu!