KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 18,141
- 32,850
Habari za muda huu wapendwa
Bila shaka kwenye safari ya maisha kila mmoja wetu amewahi kukumbana na visa na mikasa mbali mbali kwenye purukushani za maisha
Mikasa ambayo imekuwa ikitupa mafunzo na mafundisho maishani mwetu na wakati huo huo kubadilisha kabisa mitazamo ya maisha yetu juu ya watu.
Watu wetu wa karibu ni watu tunaowategemea kwenye maisha yetu Kwa mambo mbali mbali lakini pia watu hao hugeuka na kutuletea vilio vya kudumu vyenye machungu maishani mwetu.
Je umewahi kufanyiwa mkasa, kisa au tukio Gani baya na ndugu au mtu wako wa karibu?
Mimi niliwahi kuchomewa utambi kazini na mtu wangu wa karibu...ambaye nilikuwa na share mambo yangu kibao na hata niliwahi kumpa mtaji wa biashara, lakini kumbe alikuwa anachukia mafanikio yangu tangia hapo nikabadilisha kabisa mtazamo wangu juu ya marafiki na watu wangu wa karibu. Kwa kifupi nikawa na chujio mdomoni mwangu na kichwani mwangu.
Bila shaka kwenye safari ya maisha kila mmoja wetu amewahi kukumbana na visa na mikasa mbali mbali kwenye purukushani za maisha
Mikasa ambayo imekuwa ikitupa mafunzo na mafundisho maishani mwetu na wakati huo huo kubadilisha kabisa mitazamo ya maisha yetu juu ya watu.
Watu wetu wa karibu ni watu tunaowategemea kwenye maisha yetu Kwa mambo mbali mbali lakini pia watu hao hugeuka na kutuletea vilio vya kudumu vyenye machungu maishani mwetu.
Je umewahi kufanyiwa mkasa, kisa au tukio Gani baya na ndugu au mtu wako wa karibu?
Mimi niliwahi kuchomewa utambi kazini na mtu wangu wa karibu...ambaye nilikuwa na share mambo yangu kibao na hata niliwahi kumpa mtaji wa biashara, lakini kumbe alikuwa anachukia mafanikio yangu tangia hapo nikabadilisha kabisa mtazamo wangu juu ya marafiki na watu wangu wa karibu. Kwa kifupi nikawa na chujio mdomoni mwangu na kichwani mwangu.