FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 36,063
- 40,724
Wazazi walinihadithia kwamba hapo zamani, wazazi wao wa kiume(babu zangu) walikuwa wanatabia ya kukimbia na kujificha maporini pale ambapo walikuwa hawajalipa kodi ya kichwa, maana familia ilikuwa ni kubwa, na hapakuwa na pesa ya ziada ya kwenda kulipa kodi ya kichwa, hivyo kuna kipindi iliwabidi kuwaacha na mama zao ili wao waende kufanya vibarua sehemu mbalimbali na as soon as wanapopata pesa ya kulipa kodi ya kichwa ndio walirudi majambani mwao.
Kwa wale ambao hawakulipa na hawakutoroka mafichoni, walikamtwa na maaskari wa mkoloni na kwenda kulimishwa kwenye mashamba ya chai, pamba na kadhalika hadi pale deni litakapoisha. Mkoloni alitumia reli kusafirisha pamba , chai , katani nk. hadi kwenye bandari na kuzisafirisha kwa meli hadi Uingereza na kuwapa utajiri wa kufuru.
Hiyo ni miaka ya ya kabla na baada ya ukoloni , 1950’s kuendelea. Sasa fastfoward hadi kipindi cha Mkapa, uamuzi ukafanyika kwamba kodi ya kichwa ihamishiwe kwenye bidhaa (Vat na kadhalika), ambapo kwa hivi sasa, hata mtoto mdogo akinunua soda tu (japo hana TIN number) tayari analipa kodi na inakwenda serikalini. Hivyo kwa mantiki hiyo, hakuna MTanzania ambae halipi kodi, hata kama hana TIN number, bado analipa kodi kupitia bidhaa anazonunua.
Sasa jamani, leo hii mtu anatoroka milembe kimagendo magendo tu, kwa njia anazojua yeye, bila ruhusa ya daktari ili kudhibitisha kama akili zake zipo sawa, anakuja huku uraiani leo hii 2022 anasema waTanzania wasio na TIN hawalipi kodi, tena hao hao ambao kila siku wanakatwa pesa za miamala, yeye anasema halipi kodi, hivyo wote wapewe TIN number ili waanze kulipa kodi.
Kwahiyo tumerudi miaka ile ya 1950’s ambapo kwa sasa njia inayotumika ni kutupa mikopo ‘HEWA’ , mfano mkopo wa chanjo wa Trillion 2 na vifaa tiba vya kupima chanjo, mkopo ni hewa maana hata ugonjwa ni hewa, hata Barakoa Rais havai tena, malengo yametimia, na ili kulipa mkopo huo ndio wanarudisha kodi ya kichwa kwa style hii, na mwisho wa siku trillion 10 kila mwaka inayokusanywa, ni ya kulipa madeni na riba juu, yaani badala ya kupeleka pamba, chai na katani, tunapeleka pesa kama watumwa, mariba matupu!!!
Hii nchi amani itakuja kutoweka, THERE IS A LIMIT, hata kondoo ana uvumilivu wake!!!
USHAURI: Ulinzi uongezwe Mirembe, pafungwe CCTV, wagonjwa wanatoroka hovyohovyo!
Kwa wale ambao hawakulipa na hawakutoroka mafichoni, walikamtwa na maaskari wa mkoloni na kwenda kulimishwa kwenye mashamba ya chai, pamba na kadhalika hadi pale deni litakapoisha. Mkoloni alitumia reli kusafirisha pamba , chai , katani nk. hadi kwenye bandari na kuzisafirisha kwa meli hadi Uingereza na kuwapa utajiri wa kufuru.
Hiyo ni miaka ya ya kabla na baada ya ukoloni , 1950’s kuendelea. Sasa fastfoward hadi kipindi cha Mkapa, uamuzi ukafanyika kwamba kodi ya kichwa ihamishiwe kwenye bidhaa (Vat na kadhalika), ambapo kwa hivi sasa, hata mtoto mdogo akinunua soda tu (japo hana TIN number) tayari analipa kodi na inakwenda serikalini. Hivyo kwa mantiki hiyo, hakuna MTanzania ambae halipi kodi, hata kama hana TIN number, bado analipa kodi kupitia bidhaa anazonunua.
Sasa jamani, leo hii mtu anatoroka milembe kimagendo magendo tu, kwa njia anazojua yeye, bila ruhusa ya daktari ili kudhibitisha kama akili zake zipo sawa, anakuja huku uraiani leo hii 2022 anasema waTanzania wasio na TIN hawalipi kodi, tena hao hao ambao kila siku wanakatwa pesa za miamala, yeye anasema halipi kodi, hivyo wote wapewe TIN number ili waanze kulipa kodi.
Kwahiyo tumerudi miaka ile ya 1950’s ambapo kwa sasa njia inayotumika ni kutupa mikopo ‘HEWA’ , mfano mkopo wa chanjo wa Trillion 2 na vifaa tiba vya kupima chanjo, mkopo ni hewa maana hata ugonjwa ni hewa, hata Barakoa Rais havai tena, malengo yametimia, na ili kulipa mkopo huo ndio wanarudisha kodi ya kichwa kwa style hii, na mwisho wa siku trillion 10 kila mwaka inayokusanywa, ni ya kulipa madeni na riba juu, yaani badala ya kupeleka pamba, chai na katani, tunapeleka pesa kama watumwa, mariba matupu!!!
Hii nchi amani itakuja kutoweka, THERE IS A LIMIT, hata kondoo ana uvumilivu wake!!!
USHAURI: Ulinzi uongezwe Mirembe, pafungwe CCTV, wagonjwa wanatoroka hovyohovyo!
Serikali: Kila Mtanzania mwenye umri wa zaidi ya miaka 18 na mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi
"Kila mtanzania mwenye umri wa zaidi ya miaka 18 na mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi. Ili kutimiza amza hiyo, Serikali inakusudia kutoa namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) kwa kila mtanzania mwenye umri wa kuanzia miaka 18 au zaidi" "Kwa kuwa utaratibu wa usajili wa namba ya utambulisho...
www.jamiiforums.com
Tahadhari: Ipo siku hewa tunayovuta tutailipia kodi ili ipatikane pesa ya kulipa mikopo chechefu
Hii mikopo tunayobugia kwa pupa hivi tutakuja kuilipa kupitia puani. Tanzania yakopa Tsh trilioni 2.4 kutoka IMF Muda wa kulipa ukifika, tunaweza hata kuambiwa tulipie hii hewa tunayovuta, maana ni rasilimali ya serikali na tulipe kama tunavyolipa kodi ya ardhi. Unapimwa uzito wako kisha...
www.jamiiforums.com