Je, kupewa TIN ni sawa na kodi ya kichwa?

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
670
Waziri wa Fedha na Mipango amependekeza kugawa TIN kwa watu wa kuanzia miaka 18 na kuendelea, na taarifa hizi ziende sawa na NIDA ili kulipa kodi kwa usahihi.

Baadhi ya watu wamehusianisha namna hii ya ukusanyaji kodi na Kodi ya kichwa, kitu ambacho naona ni kupotosha ukweli kuhusu kodi ya kichwa.

Kwanza lazima tujua kuwa na namba ya mlipa kodi haimaanishi unalipa kodi, kwa mfano kila mwenye leseni ya udereva ana namba ya mlipa kodi, ila sio kwamba wanalipa kodi.

KODI YA KICHWA
Kodi hii ilikuwa inalipwa na kila mtu mwenye kichwa na unapewa kibali, hivyo ukikosa kibali unashtakiwa kwa kutolipa kodi. Ni kodi ambayo ilikuwa na udhaifu mkubwa kwa kuwa watu wa kijijini na porini walikuwa ni ngumu kufikiwa ili kulipa kodi hiyo.

Kodi inayopendekezwa ktk bajeti ya mwaka 2022/23 ni kila mtu anapofanya muamala, sio kuwa atalipa kutokana na umri wake, bali ni kuongeza wigo wa kufanya malipo yanayofanyika yakatwe kodi.

Hakuna mtu ambaye atafuatwa kudaiwa kodi kwa sababu ana namba ya mlipa kodi. Kumbuko kwenye kodi ya kichwa unafuatwa kuhakikisha kama una kibali.

Kwa sababu hiyo, wale wanaodhani kuwa kodi hii ni sawa na kodi ya kichwa wanapotosha.

Signed OLS
 
Nadhani ulicho shindwa kuelewa ni kuwa imebadilishwa jina kutoka kwenye kodi ya kichwa kuingia kwenye habari ya namba ya mlipa kodi na unapo sema kodi ya kichwa ilikuwa ikitozwa kwa kila mtu nadhani unaweza kuwa bado mdogo hivyo kwenye makuzi yako hukuwahi ona watu wakitozwa kodi ya kichwa ilitozwa kwa kila mtu mwenye utimamu mwenye umri wa miaka 18.

Asie mwanafunzi na aise mzee kwahiyo tini ni sawa na kichwa tu maana kichwa kimoja TIN moja hakuna mtu anae miliki namba zaid ya moja ya TIN vivyo hivyo hakuna binadamu anae miliki vichwa zaidi ya kimoja akaitwa mmoja nachelea kuingiza uccm

Hapa maana hata wakati wa tozo mlishangilia na kupiga makofi mkiisifia ni tozo za maendeleo na kutaja madaraja na mabarabara halafu baadae mlipo ona malalamiko makubwa kwa watu mkageuka tena
 
Lugha tu imebadilishwa!

TIN ni kifupi cha Taxpayer Identification Number, kiswahili chake ni Nambari ya Utambulisho wa Mlipa kodi.

Hii ni nambari anayopewa mlipa kodi pekee. Ama niseme hivi, kila anaepewa Nambari hii ni mlipakodi.
 
Lugha tu imebadilishwa!

TIN ni kifupi cha Taxpayer Identification Number...
Moja ya hoja ni kuwa, kila mwenye leseni ya udereva ana namba ya mlipa kodi.

Je, umeshawahi kuona dereva kafuatwa alipe kodi?
 
Endesha gari kwa leseni iliyoisha muda wake halafu trafiki akukamate, ndio utajuwa kama unafuatwa kulipa kodi au hufuatwi
Suala ni leseni ikiisha muda na hauna gari, you are good to go. So kuwa na TIN sio ulazima wa kulipa kodi.

Ni kupotosha kwamba mtu akiwa na TINI basi ni lazima atalipa.

Kodi ya kichwa ilikuwa kwamba unalipia kichwa chako, kwa hiyo ukiepuka miaka kadhaa wakikudabua watataka uoneshe ushahidi kuwa ulilipa miaka iliyotangulia.

In fact hata kwa sasa ni muhimu kwa mtu kuwa na TIN, though wengi hawana
 
Moja ya hoja ni kuwa, kila mwenye leseni ya udereva ana namba ya mlipa kodi. Je umeshawahi kuona dereva kafuatwa alipe kodi?
Leseni ya udereva inatolewa bure?
Jamani mbona mnajitoa ufahamu au hamna akili kweli? Basi nchi hii tumekwisha!
 
Hii itafanya watu wasipeleke pesa zao benki mfano mtu kauza nyumba yake kutokana na matatizo halafu hizo pesa akiziweka benki anakatwa kodi juu kwa juu! Sasa ikiwa hivyo si ndiyo unamuongezea matatizo wakati labda walielewana na mnunuzi kodi zote atazibeba mnunuzi.
 
Waziri wa Fedha na Mipango amependekeza kugawa TIN kwa watu wa kuanzia miaka 18 na kuendelea, na taarifa hizi ziende sawa na NIDA ili kulipa kodi kwa usahihi.

Baadhi ya watu wamehusianisha namna hii ya ukusanyaji kodi na Kodi ya kichwa, kitu ambacho naona ni kupotosha ukweli kuhusu kodi ya kichwa.

Kwanza lazima tujua kuwa na namba ya mlipa kodi haimaanishi unalipa kodi, kwa mfano kila mwenye leseni ya udereva ana namba ya mlipa kodi, ila sio kwamba wanalipa kodi.

KODI YA KICHWA
Kodi hii ilikuwa inalipwa na kila mtu mwenye kichwa na unapewa kibali, hivyo ukikosa kibali unashtakiwa kwa kutolipa kodi. Ni kodi ambayo ilikuwa na udhaifu mkubwa kwa kuwa watu wa kijijini na porini walikuwa ni ngumu kufikiwa ili kulipa kodi hiyo.

Kodi inayopendekezwa ktk bajeti ya mwaka 2022/23 ni kila mtu anapofanya muamala, sio kuwa atalipa kutokana na umri wake, bali ni kuongeza wigo wa kufanya malipo yanayofanyika yakatwe kodi.

Hakuna mtu ambaye atafuatwa kudaiwa kodi kwa sababu ana namba ya mlipa kodi. Kumbuko kwenye kodi ya kichwa unafuatwa kuhakikisha kama una kibali.

Kwa sababu hiyo, wale wanaodhani kuwa kodi hii ni sawa na kodi ya kichwa wanapotosha.

Signed OLS
Kijana unajua sheria za kodi za tz na duniani kote kasome income tax act na tax administration act,kisha ndo uwakosoe watu au kawaulize wataalamu wa kodi kisha ndo utambue unachotetea ni ujinga
 
Hii itafanya watu wasipeleke pesa zao benki mfano mtu kauza nyumba yake kutokana na matatizo halafu hizo pesa akiziweka benki anakatwa kodi juu kwa juu! Sasa ikiwa hivyo si ndiyo unamuongezea matatizo wakati labda walielewana na mnunuzi kodi zote atazibeba mnunuzi.
Mtu ukimuuzia nyumba au kulipia kodi wewe ni agent wa TRA unajukumu la kukusanya kodi na kuwapelekea
 
Back
Top Bottom