Nguvu za kioo na miujiza yake: Wale wenye imani zenu njooni hapa

BANDOKITITA

JF-Expert Member
Oct 4, 2022
1,177
2,281
Vioo tunavyotumia kujitazamia au vilivyoko ktk nyumba zetu inasemekana kuwa na uwezo mkubwa wa kiroho. Soma hapa na utoe maoni yako.

Kioo ni kitu ambacho kinatakiwa kutunzwa na kutazamwa kwa umakini zaidi kwakuwa ni kitu Flagile yaani kinavunjika kwa urahisi.

Tujue kwanza kioo hutengenezwa na nini? Kioo kimetengenezwa na Material asilia ya aina tatu yaani Mchanga, Soda ash na Limestone ambavyo huchanganywa na kuunguzwa na moto mkali ndipo hutokea Kioo! Tuachane na Utengenezwaji wake tuje kwenye matumizi yake.

Kuna vioo vya kujitazama na vioo vya urembo halafu kuna vioo kwa ajili ya matumizi ya nyumba kama mlango ama madirisha. Vioo vya urembo hivi huwa na rangi rangi nyingi tofauti ambavyo hutengenezwa kwa ustadi na kuning'inizwa nje mlangoni au dirisha. Mara hivi hutumika kutambua uwepo wa roho eneo husika kwani utakuta hakuna upepo ila vinatikisika na kutengeneza mlio flani hapo wataalamu hukwambia kuna uwepo wa Roho na milio inapo sikika

mtaalamu huwa na uwezo wa kusoma ujumbe kupitia milio hiyo! Tafuta muvi inaitwa BABA YAGA utatambua nachokiongea. Kioo ni kifaa cha Magic Power kwa Wazungu sio Asili ya afrika sisi tulikuwa hatutumii vioo vya kutengeneza bali tulitumia vioo vya asilia. Asili inauwezo wa kutengeneza kioo yaani kioo cha asili kutoka kwenye natural Stone ndio hizo Almasi n.k. Sasa Wapuuzi wasio jua nguvu ndio wakaamua kutengeneza vioo kutoka kwenye natural stones. Kioo hutokana na madini na madini yana roho ndani yake so isione ajabu kioo kikahitaji damu katika eneo hilo.

Wachawi wa kizungu na ma Sorcerer walitumia vioo kutazama matukio yajayo ama kutazama matukio yaliyopita na yaliyopo. Kupitia kioo waliweza kuita mizimu ama kutuma uchawi kwa njia ya kioo. Waliweza kuhifadhi roho mbaya na nzuri kwenye vioo. Kioo kinauwezo mkubwa wa kusababisha mauaji. Sasa Wakushi hatukuwahi kutumia vioo katika utaalamu wa namna hiyo kwakuwa vioo vya Asili ni vichache kinyume chake Wakushi walitumia maji yaliyitulia either ya mto uliotulia ama ya Bwawani ambayo ni maji yasiyokuwa na movement. Baadhi ya Wakushi pia hutumia Maji kwenye Beseni, Bakuri ama Ndoo n.k.

Sasa turudi kwenye Vioo. Katika kila kioo kuna Roho ndani yake, jiulize kioo kimoja hutazamwa na watu wangapi? Ile Image unadhani haibaki kwenye kioo? Unadhani ni kitu gani kina leta ile reflexion ya wewe ama kitu? Kioo kinaweza kuamrisha mtu kufanya tukio la kujiua.

ANGALIZO

1. Usitumie kioo ambacho Pembe zake hazijafunikwa mfano kama kina pembe nne hakikisha kila pembe imeshikiliwa na ubao au chuma kisichokuwa na reflexion.

2. Usitumie kioo ambacho hakijazungushiwa cover ya aina yeyote.

3. Kioo kikivunjika tupa vipande vyote usibaki na kipande cha kioo ndani ya nyumba ama chumba chako.

4. Reflexion ya aina yeyote inaweza kutumika kuita mzimu ama mtu aliyembali ama roho yoyote katika taswira yake na kuongea nayo.

5. Watu wenye vibrations za karibu wanauwezo wa ku sense Roho zilizopo kwenye kioo na hutulia tu endapo kioo kitafunikwa ama kugeuzwa muelekeo ambao sio walipo wao.

6. Wachawi hutumia vioo ambavyo vipo majumbani mwa watu kuleta madhara katika familia husika au watu husika.

7. Kioo kikivunjika kwenye Dressing table ondoa dakika hiyo hiyo kioo kizima katupe kisha weka kioo kingine usiendelee kutumia kwa ubahili madhara yake ni makubwa zaidi. Unaweza ukaona mambo ndani ya nyumba hayaendi na usijue shida ni nini kumbe ni Kioo kibovu.

8. As below so Above. Ukisimama na kutazama mbele kwenye ukuta bila kioo utaona ukuta ila tukileta kioo utajiona wewe kiuhalisia pale unapoona ukuta kuna another version of you anakutazama ila wewe humuoni mpaka uletewe kioo. Ila ukiletewe kioo ambacho ni transparent utaendelea kuona ukuta halafu anaother version of you (Taswira) utaiona kwa kufifia kama kivuli hivi Taswira unayo iona ni wewe katika mfumo wa Roho. Sasa wachawi huitumia hiyo kufanyia mambo yao.

9. Umewahi kusikia kwamba kwenye bwawa flani kuna chunusi ana nyonya damu za watu. Kiuhalisia kwenye bwawa lenye maji yaliyotulia kuna Roho ambazo muda flani hazihitaji kubugudhiwa kwa namna yoyote ile, sasa mkienda kuoga ni lazima ziondoke na mtu na mkienda kwa maana ya kuabudu mtawasiliana nazo na kupewa maelekezo ya nini cha kufanya kwa utaratibu.

10. Kioo kinaweza kukuonesha matukio yajayo, yaliyopo na yaliyopita kwa kunuia maneno.

11. Mwisho kabisa japo yapo mengi unaweza kumuita Mtu aliyekufa akatokea kwenye kioo na mkaongea naye ukamueleza shida zako akakuelekeza namna ya kufanya kutatua shida zako ila unatakiwa kuwa na ujasiri kwakuwa tukio hilo unatakiwa kulifanya usiku wa kuanzia saa sita kamili mpaka sa tisa hapo kati au sehemu ambayo imetulia sana hakuna kelele."

Mdau mmoja naye katoa ya moyoni

Fact kabisa kioo kina nguvu kubwa ya kiasili na ukitaka kuamin amka usik kuanzia sa 9-10 nenda kajiangalie kenye kioo km dk 10 elekeza(concentrate) fikra zako hapo utaona kama kivuli nyuma yako kimesimama kama huamin kafanye na kama unatumia kioo chenye cracks(mipasuko) katupe sahv tafut kioo kipya.

NB:
Tutoe ushuhuda au maoni bila mihemuko ya kiimani.
 
angalizo hili

Unapomaliza kutumia kioo Kwa kujiangalia kifunike yaani usikiache wazi ni kama kioo kipande kifunike juu chini na kama vya dressng table tafuta jinsi ya kukifunika na kitambaa au panzia aina yeyote ilee ila usipendelee kutumia kioo na ukakiacha wazi
 
Vioo tunavyotumia kujitazamia au vilivyoko ktk nyumba zetu inasemekana kuwa na uwezo mkubwa wa kiroho. Soma hapa na utoe maoni yako.

yake.
hata ukininunulia K-VANT kubwa siwezi kufanya jaribio la kumwita marehem kwenye kioo usiku!! ata kama umetupiga fix lakini jaribio hilo siliwezi ata ukininunulia kitimoto cha kuchoma!! lol!!
 
angalizo hili

Unapomaliza kutumia kioo Kwa kujiangalia kifunike yaani usikiache wazi ni kama kioo kipande kifunike juu chini na kama vya dressng table tafuta jinsi ya kukifunika na kitambaa au panzia aina yeyote ilee ila usipendelee kutumia kioo na ukakiacha wazi
Hii ni kweli kabisa!
 
hata ukininunulia K-VANT kubwa siwezi kufanya jaribio la kumwita marehem kwenye kioo usiku!! ata kama umetupiga fix lakini jaribio hilo siliwezi ata ukininunulia kitimoto cha kuchoma!! lol!!
Na msibani ulikuwa unalia unafiki au?! 😀😅😅😅👍🏾
 
Back
Top Bottom