Wengi hatutaki kuujadili ukweli. Kiuhalisia si CHADEMA pekee hata vyama vingine vya upinzani pia havina organization ya kueleweka. Kuanzia uendeshaji wake ni wenye kutia mashaka ya hali ya juu. Ipo mifani kadhaa ambayo inaongeza wasiwasi.
1. Wkt wa harakati za kutafuta mgombea wa Urais, CHADEMA walimpitisha mgombea wao na kuwakilisha jina NEC hata kabla ya kuidhinishwa na Mkutano Mkuu. (Hii ndio dhana ya rubber stamp).
2. Mgombea wa Urais alimtaja M/Kiti wa CHADEMA wa Iringa kuwa alijitoa baada ya kupewa rushwa. Hapa pamoja na kumtaja tulitarajia kuona CHAMA kinachukua hatua na kumfikisha mahakamani maana yaelekea ushahidi wanao.
3. Mkutano Mkuu uliofanyika hivi karibuni ulionyesha ni namna gani CHADEMA inataka nani aendelee kuongoza.
Haya na mengineyo hayana tofauti na CUF.
Kiuhalisia CHAMA kinahitaji muundo imara na DEMOKRASIA inayoonekana na si kusemakana. CHAMA kinahitaji muundo ambao ni imara na uliona uwakilishi wa sehem kubwa ya nchi. CHAMA kinachoweza kutambuliwa km CHAMA na si km mtu na ambacho kwa namna yoyote ile kinaweza kujitofautisha na kutofautishwa na kabila au dini fulani. CHAMA ambacho wanachama wanaweza wakatoka mbele na kujisifia (hapa namaanisha wasomi maana wao ndio waoga kuliko wasiosoma).
Mjengwa yupo sahihi kiasi fulani ingawa si lazima uwe mti mrefu km watu wanavyotarajia wapime height la hasha anamaanisha mti unaoonekana. Ingawa CONCEPT yake is prune to critism kwamba extent ya urefu wa mti (kwangu mie naona bora ustawi wa mti) inatakiwa isizidi miti mingine.
FMES,
Hata mimi nimeelewa hivyo toka mwanzo lakini hainingii akili mtu mzima kufikiria kwamba Chadema (msitu) ni Dr.Slaa ambaye tumekuja mchagua hivi majuzi tu kwa riidhaa ya wanaChadema. Dr.Slaa ni mgombea kiti cha Urais kwa tiketi ya Chadema hivyo sielewi huo msitu unaozungumziwa ni Chadema au Tanzania.
Pili, Mbowe ni mwenyekiti wa Chadema, kweli yawezekana ana matatizo yake lakini la muhimu ni kutazama katiba ya nchi inasema nini sio katiba au mpangilio wa Chadema. Sasa kama Katiba inasema kwamba rais akifa kesho basi anayeshika madaraka ni Mwenyekiti wa Chadema hapo tunaweza kujadili hata kama Mbowe atakuwa Waziri mkuu.
Ifahamike tu kwamba Chadema kama chama kitafuata katiba ya nchi hadi hapo watakapo badilisha Katiba hiyo na kutenganisha Mawaziri na Wabunge na bado Mbowe ni mbunge, hivyo wasiwasi iko wapi.
Na pengine fikra hizi zinakuja kutokana na wengi kufikiria kwamba CCM umeweza kusimamisha miti mingi kina Dr.Shein ambao hatukuwafahamu before wameshika madaraka, iweje leo tufikirie Chadema na Dr.Slaa lakini wazito sana kufikiria CCM na JK. Mathlan JK akiondoka leo nani atakuwa rais?..Kwa fikra na jicho hilo hilo tunamkuta ni Lowassa..Haya CUF je akiondoka Lipumba nani atakuwa rais? Seif Sharrif Hamad maanake ndio wanaoviendesha vyama.
Sasa iweje tu watu mnaitazama Chadema hali kila chama kina mtu anayewapeleka watu puta? Ndiyo yawezekana Mbowe hana maamuzi yanayopendwa na wengi lakini chama chochote kinatakiwa kiongozi mwenye msimamo na pengine jeuri ili kuweka displine kwani kila mtu anayekuja ndani ya chama huwa na mawazo yake. Na rahisi sana kukivuruga chama hasa ikiwa wapo baadhi wenye ambition..
Halafu jamani huyu Mbowe na ukorofi wake kaweza kuachia kugombea kiti cha Urais, jambo ambalo nina hakika hakuna kiongozi yeyote Tanzania angeweza kufanya hivyo.. hakuna, hata JK mwenyewe asingeweza. tatizo kubwa ni wapambe wa Mbowe hili nina hakika nalo sana hawa jamaa wanatafuta sana sifa na kukibomoa chama kwa maslahi ya vitu fulani fulani... sina haja ya kuendelea huko.
Hivyo haiwezekani kabisa mti mmoja kuwa msitu wala msitu sii idadi ya miti inayofanana unless miti hiyo ni pandikizi...Na hata siku moja binadamu hawawezi kufananishwa na mti au msitu ndio maana nikasema mandela hawezi kusema ujinga huo..
Mkuu sioni kabisa Usahihi wa lolote lile kwani huwezi fananisha binadamu na mti au misitu ambayo haina mahusiano baina yake labda tu ktk concept ya mchumia tumbo kwani kila mti ktk msitu mzima hujitegemea..hakuna mahusiano baina ya mti mmoja kwenda mwingine zaidi ya kuona msitu mkubwa hali miti yote inategemea kulishwa mvua na rutuba iliyopo..Wengi hatutaki kuujadili ukweli. Kiuhalisia si CHADEMA pekee hata vyama vingine vya upinzani pia havina organization ya kueleweka. Kuanzia uendeshaji wake ni wenye kutia mashaka ya hali ya juu. Ipo mifani kadhaa ambayo inaongeza wasiwasi.
1. Wkt wa harakati za kutafuta mgombea wa Urais, CHADEMA walimpitisha mgombea wao na kuwakilisha jina NEC hata kabla ya kuidhinishwa na Mkutano Mkuu. (Hii ndio dhana ya rubber stamp).
2. Mgombea wa Urais alimtaja M/Kiti wa CHADEMA wa Iringa kuwa alijitoa baada ya kupewa rushwa. Hapa pamoja na kumtaja tulitarajia kuona CHAMA kinachukua hatua na kumfikisha mahakamani maana yaelekea ushahidi wanao.
3. Mkutano Mkuu uliofanyika hivi karibuni ulionyesha ni namna gani CHADEMA inataka nani aendelee kuongoza.
Haya na mengineyo hayana tofauti na CUF.
Kiuhalisia CHAMA kinahitaji muundo imara na DEMOKRASIA inayoonekana na si kusemakana. CHAMA kinahitaji muundo ambao ni imara na uliona uwakilishi wa sehem kubwa ya nchi. CHAMA kinachoweza kutambuliwa km CHAMA na si km mtu na ambacho kwa namna yoyote ile kinaweza kujitofautisha na kutofautishwa na kabila au dini fulani. CHAMA ambacho wanachama wanaweza wakatoka mbele na kujisifia (hapa namaanisha wasomi maana wao ndio waoga kuliko wasiosoma).
Mjengwa yupo sahihi kiasi fulani ingawa si lazima uwe mti mrefu km watu wanavyotarajia wapime height la hasha anamaanisha mti unaoonekana. Ingawa CONCEPT yake is prune to critism kwamba extent ya urefu wa mti (kwangu mie naona bora ustawi wa mti) inatakiwa isizidi miti mingine.
Sasa mkuu umesema Slaa na Lipumba wana same shot kwenye presidency,lakini mbona hujasema Dr Slaa na yeye ana nguvu ukanda gani?kama ulivyotolea mfano wa umaaruf wa Lipumba huko kanda ya kusini?Ama ni ukanda wa kaskazini?jmushi1,
..nimesoma kwamba kampeni za CUF na Prof.Lipumba zimepokelewa vizuri sana ukanda wote wa kusini mwa Tanzania.
..kwa upande mwingine, Prof makes a lot of sense katika mambo mengi anayoyazungumzia. he would have helped himself kama angeamua kujijenga kwanza kama mbunge kabla ya 2010.
..sasa, ukiweka mapenzi ya chama pembeni, ukasikiliza hoja kwa hoja, baina ya JK,Prof.Lipumba,na Dr.Slaa, naamini kabisa you will end up with a toss up btn Lipumba and Slaa.
..kwa upande wangu nadhani kura za Uraisi hazitatofautiana sana baina ya vyama vitatu CCM,CUF,na Chadema.
Sasa ile agenda ya Independent Candiates ambayo wengi wameililia sana hadi mahakama ya rufaa inakuwa irrevant hapa? Mie naungana kabisa na yule asemaye msitu basi uwe wananchi; otherwise tukubali kuwa agenda ya Independent Candidates haitakuwepo katika demokrasia yetu!- Tukisimamia hoja hii thread ina mengi mazuri, lakini tatizo linaletwa na ushabiki, unashia kuiharibu kabisaa hii thread halafu inaudhi kweli!
Es!
Kwani mjadala ukiwa hauna mwelekeo inakuwaje? Anageuziwa aliye uleta.hana lolote huyo acid
watanzania tumefunzwa ustaarabu na kuaminisshwa sote ni ndugu kinyume cha uadui ambao anautaka huyo mpumbavu acid, upenzi wake kwenye vyama umempofua mpaka anatamani uadui kuliko udugu loh hasara yake.
tukija kwenye mada, kuna ya kujifunza mengi tu, chama au kikundi chochote imara si mtu mmoja peke yake, maana sawa na sehemu yenye chemni moja tu na watu wote wanategemea kuona kupitia chemni hio, sasa ikizima watu wote wako gizani, hilo ndio alilomaanisha
na nnachofahamu yeye amenukuu maneno ya mandela na nnataraji vyama vina haki ya kujifunza na kujikosoa ikiwemo chama changu CCM kujipanga na kuwanoa makada wake vyema kuelewa misingi ya chama na kujipanga iwapo yeyote anaondoka mapambano yanaendelea tena yanaendelea kwa kufata misingi ya chama husika sio kila mtu anakuja na umaarufu wake pasipo kuelewa misingi ya chama husika
tuwe watu ambao kweli ni wasomi na sio wapumbavu, chadema kwa mfano ina watu wachache ambao ni vinara na nnamini wengi wao wanatumia umaarufu wao na huenda nata ili misingi ya chama chenyewe hawakijui.
tujadili mada badala ya mtu.
kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi. Ebu niambie kwenye kura za maoni ya sisi m si kulikuwa na side ya upinzani vile vile! hao walikuwa ni wakina nani? Maana, maana ya upinzani ni kuwa kuna side mbili zinapingana. Sasa ebu niambie kule Dodoma wapinzani kwenye kambi ya sisi m alikuwa nani na angeungana na nani? kwi kwi kwi kwi- Bob Heshima yako kaka, mimi nimejaribu kuielewa hoja ya Majjid kuhusu mti mrefu, hayo mengine siyajui sijaenda that far maana ninaamini bila kuungana Wapinzani na kuwa kitu kimoja kwa sababu nia yao ni moja kama sikosei, basi itakwua ni kupoteza muda na pesa nyingi za kuimarisha vyama, kwa maoni yangu!
Es!
Maggid huyoooooooooooo kesha waacha mparurane macho. Yuko wapi kutetea hoja? Ngoja nimtafute acid
Sio tu uchambuzi wa kisiasa unakushinda kuandika bali hata makala zisizo za siasa....wewe si mwandishi mzuri kwani uwezo wako wa kufikiri uko chini ya unaojaribu kuwaandikia!!!!!Ndugu Yangu Mchukia Fisadi,
Sijawaacha. Nimeanzisha mada hii na naifuatilia kwa makini sana. Nasoma kila kinachoingizwa. Haya tunayoyajadili hapa ni mambo mazito na ya muhimu sana kwa taifa letu. Kuyachukulia kwa wepesi wepesi na mzaha mzaha ni hatari sana. Maana, katika siku zisizozidi 21 Watanzania tunakwenda kufanya maamuzi magumu, makubwa na mazito yatakayoamua mustakabali wa nchi yetu.
Tukifanya makosa, tutasubiri miaka mingine mitano au hata kumi kurekebisha makosa hayo. Nilijiunga hapa JF baada ya kusikia sifa za mahali hapa, kwamba JF ni "The Home of Great Thinkers, Where People Dare to Talk Openly!"
Na kwa staili yangu nazileta hizi mada humu ili ' Great Thinkers' wazichambue, wazijadili, waje na mawazo na mengineyo yenye manufaa kwa taifa. Nilifahamu, kuwa ' Kwenye msafara wa mamba na kenge wamo ". Kwamba miongoni mwa 'Great Thinkers' wa JF kuna wasiofanana na jina hilo, na wakati mwingine hawafanani hata na kenge, bali mijusi.
Ndio hao, mara wanapoona hoja imewasilishwa, basi, wanakimbilia kumshambulia mtoa hoja. Ni wavivu wa kufikiri. Kufanya kazi ya kuisoma kwa makini hoja husika, kuikubali au kuikataa kwa hoja.
Katika mada hii nimeona hatua ya maana imeanza kupigwa. Watu wameanza kujadili "Urefu wa mti", hivyo basi, wanajadili hoja. Naona kuna ambao wamenielewa, tena vizuri sana. Kuna ambao hawajanielewa hadi sasa, naamini watakuja kunielewa vema mbele ya safari.
Ndugu zangu,
Hii ni nchi yetu. Ni nchi yetu sote, kama Watanzania sisi ni ndugu. Nchi ni kama mama, hatuwezi kuchagua mama. Ndio maana tunaipenda nchi yetu. Inahusu Watanzania zaidi ya milioni 40. Kumchagua Mtanzania atakayepewa jukumu la kushika dhamana ya watu milioni 40 si sawa na kucheza ' ngoma ya lelemama'. Tuwe makini, na wakati mwingine si vibaya tukagombana kwa hoja.
Kwangu mimi kutoka Jangwani peke yangu na kupandisha Magomeni ilihali nikijua nitakutana na umati wa watu usio na mtazamo kama wangu ni kazi ya kuutafuta umakini huo. Tuanze kujadili.
Ni bahati mbaya, kuwa kila unapotoa hoja, watu hukimbilia kukutafutia droo ya kabati la kukuingizia; CCM, CUF, CHADEMA, Dini, Kabila, Ufisadi na kadhalika. Wengi tumelisahau droo muhimu sana katika kabati letu; Droo la Tanzania.
Mimi nimo kwenye droo hilo. Katika kila nifanyalo; naangalia kwanza, kama lina maslahi kwa Tanzania. Wanaojihangaisha ni wale wanaonitafutia droo nyingine za kuniweka na kuliacha droo langu la Tanzania. Ni kwa vile hawanijui.
Sio tu uchambuzi wa kisiasa unakushinda kuandika bali hata makala zisizo za siasa....wewe si mwandishi mzuri kwani uwezo wako wa kufikiri uko chini ya unaojaribu kuwaandikia!!!!!
Joka Kuu said:..kwa upande wangu nadhani kura za Uraisi hazitatofautiana sana baina ya vyama vitatu CCM,CUF,na Chadema.
kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi. Ebu niambie kwenye kura za maoni ya sisi m si kulikuwa na side ya upinzani vile vile! hao walikuwa ni wakina nani? Maana, maana ya upinzani ni kuwa kuna side mbili zinapingana. Sasa ebu niambie kule Dodoma wapinzani kwenye kambi ya sisi m alikuwa nani na angeungana na nani? kwi kwi kwi kwi
Na Maggid Mjengwa,
" One tall tree does not make a jungle"- Nelson Mandela.
Hakika, na mimi naamini, kuwa Chama cha kisiasa chenye nguvu kinatokana na kazi ya timu iliyoandaliwa vema. Na si mtu mmoja.
Tujiulize; Je, chama cha siasa ni nini? Katika harakati za kisiasa kuna aina mbili za vyama; Chama cha Ukombozi na Chama cha Uongozi. TANU, FRELIMO, ANC ni mifano ya vyama vya ukombozi vilivyokuja kugeuka kuwa vyama vya uongozi. CCM, CUF, CHADEMA ni mifano michache ya vyama vya uongozi.
Chama imara cha ukombozi kinatakiwa kijenge uwezo wa kuwa chama cha uongozi mara ile kitapotwaa madaraka. Hufanya hivyo kwa kuweka mkazo juu ya mafunzo kwa makada wake. TANU, FRELIMO na ANC viliweza kujenga uwezo huo. Kielelezo cha nguvu na umakini wa chama cha kisiasa ni uwingi na ubora wa makada wake. Chama ni makada kwa vile chama ni itikadi, malengo na shabaha na wala si nasaba na umaarufu wa mtu mmoja mmoja ndani ya chama.
Chama chenye makada wengi wenye kuielewa itikadi, malengo na shabaha ya chama, huwa hakimtegemei mtu mmoja katika kuwepo kwake. Hakimtegemei mtu mmoja katika kufanikisha ushindi wa chama. Hakimtegemei mtu mmoja katika kuhamasisha wanachama au umma. Chama hicho hujiamini. Edward Mondlane, kiongozi wa kwanza wa Frelimo alipouawa kwa bomu la barua, Frelimo walijua watafanya nini, walijua mchakato gani utumike katika kumpata mrithi wake. Na hata Samora Machel, alipotoweka ghafla kwa ajali ya ndege, FRELIMO walijua watafanya nini.
Na kama Nyerere angekufa wakati wa TANU, bila shaka, TANU walikuwa wamejindaa vema na cha kufanya. TANU haikuwa na ukame wa jeshi la makada. Nguvu ya Frelimo kama ilivyokuwa kwa TANU zilikuwa ni makada wake. Na ieleweke, kuwa makada ni roho ya chama. Chama kikianza kupungukiwa na idadi ya makada wake wakereketwa, basi, chama hicho hakina mustakabali ulio salama, kitayumba, kitaangukia kaburini.
Kuna mfano wa chama kisichokuwa na nguvu ya makada. Wakati John Garang wa SPLM alipouawa kwa ajali ya ndege, hakuna ndani ya SPLM aliyekuwa na hakika ya nini kifanyike. Kwamba ni mke na mtoto wa John Garang waliosimama mbele ya kamera za waandishi wa kimataifa kujaribu kuelekeza nini John Garang angependa kifanyike kilidhihirisha udhaifu wa SPLM. Kwamba SPLM ni John Garang na kinyume chake. SPLM ilikuwa ni chama mtu. Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid,
Msamvu, Morogoro