Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Tafsiri:
Utakuja kua tajiri mkubwa sana kushinda hao wakina bill gates,
'upo ndani ya jeneza' yani utakua kwny kiti cha ufalme,
'watu wanalia sana' yani watu watakua wanakushangilia kila upitapo,
'ukashtuka usingizini' yani utajiri wako utakaa kwa muda mfupi, utakua kapuku,
'kichwa kikauma sana' yani mawazo yatakusonga mpk utachizika.

Mmmh ngoja nisubiri Kama ni kweli
 
Usiku wa kuamkia leo nimeota ndoto ambayo siyo nzuri sana na imenitisha sana.

Nimeota nimekufa niko ndani ya jeneza kwenda kuzikwa na watu wanalia sana. Ghafla nikashtuka toka usingizini. Nikajaribu kuinua kichwa kikawa kizito baada ya muda kichwa kikaniuma sana.

Naomba unipe tafsiri ya hii ndoto maana imeninyima raha kabisa.

Nawasilisha.
ipuuzie hiyo binti, mimi nina idadi kubwa sana ya ndoto za kutisha lakini hakuna chochote cha ajabu kilichonitokea baada ya hizo ndoto
kuna siku nimeota nimepigwa risasi ya kichwa ila nikaamka na maisha yakaendelea kawaida tu
hicho kichwa kuuma sana ni kutokana na mshtuko wa hiyo ndoto au kutokana na uliyofanya jana yake
 
Kwa mujibu wa kitabu cha tafsiri ya ndoto,, ndoto yako ni kwamba Siku za mbele utakuwa kiongozi ktk kundi la watu Fulani, ,,,,,maybe mtawala ,,,,,,ILA TUMEFUNDISHWA UKIOTA NDOTO AMBAYO UNA HOFU NAYO KWAKUWA HUJUI KITU KTK TAFSIRI YAKE ,,,BAS INATAKIWA KUMUOMBA MUNGU AKUEPUSHE NA SHARI ITOKANAYO NA IYO NDOTO,,NA KM INA KHERI NDANI YAKE PIA UNAMUOMBA MUNGU AJALIE IWE KHERI ZAIDI,,,,,,, ,
 
Pole sana.Mimi si mfasiri wa ndoto ila nitatoa sababu ya ndoto za namna hiyo.Kwanza hiyo ndoto bila shaka ni ya KISHETANI.Mashetani WANAKUFANYA wanavyotaka,wanakufanyia fujo za kila namna ili uingie kwenye mitego yao yaani USHIRIKINA.Na mashetani kutufanyia fujo sana usiku ni sisi wenyewe tunajitakia kwa sababu tunalala kienyeji.Wengi wetu tunajitupia kitandani kama magunia ya mkaa bila ya kwanza kuomba ulinzi wa Mwenyezi Mungu.
 
Mimi ninauwezo wa kukitafsilia sema unamtaka mshana jr
Mmh mercky ngoja tu niseme neno kwamba hiyo ndoto ilikuwa na maana mbili
1. Alikuwa anawangiwa ndio maana kaamka kichwa kinamuuma
2. Ni ndoto tu ya kawaida inayomtabiria mema kwakuwa kuna baadhi ya ndoto tafsiri huwa kinyume
 
Dah!! Chief hiyo ndoto maana yake ni ONYO.

1. Kama una deni lipa mara moja kwani mdai wako ameishachoka na ahadi zako sasa anapanga akufanyie kitu mbaya.

2. Kama unamchapia mtu acha mara moja kwani mwenyewe ameanza kunusa hilo.

Kwa niaba ya Profesa mshana jr
Hahahhaa wewe kitengo hujakiweza bado! Mbona vitisho vingi kiasi hicho?
 
Punguza maasi hapo unaonywa juu ya matendo yako mavaya uyatendayo,pili inawezekana umerogwa au mti wako wa karibu karogwa,
 
nipo Mumbai, ntakuletea "Kurta"
Tafsiri:
Utakuja kua tajiri mkubwa sana kushinda hao wakina bill gates,
'upo ndani ya jeneza' yani utakua kwny kiti cha ufalme,
'watu wanalia sana' yani watu watakua wanakushangilia kila upitapo,
'ukashtuka usingizini' yani utajiri wako utakaa kwa muda mfupi, utakua kapuku,
'kichwa kikauma sana' yani mawazo yatakusonga mpk utachizika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom