Nchimbi yuko wapi? Serikali na CCM tunataka majibu

Nchimbi yuko wapi? Serikali na CCM tunataka majibu

Umeenda nyumbani kwake umemkosa?
Kwani unadhani mtu akiacha kazi huwa anaenda wapi?

Bi Kidude alisema eti mna katiba nzuri mnaweza fanya power transition bila mgogoro inakuaje sasa mtu tuliyeambiwa amejiuzulu haji hata kukabidhi hiyo ofisi ambayo alikuwemo japo kiharamu?

Gachagua alikua impeached ambayo ni njia mojawapo ya kutoka ofisini tumeendelea kumuona hata baada ya kutoka ofisi aliyochaguliwa ni mwaka wa pili sasa hadi kaunda chama na anaendelea na siasa kama kawaida na anazumgumza muda wowote anapojisikia bila hofu.

Iweje machawa mshangilie mtu aliyejiuzulumu kwa hiyari yake [kama ni kweli ] ghafla anafukuzwa chama chenu mnashangilia na tukiwauliza kosa lake hamlijui ?
 
Hivi kwani Nchimbi hana familia au marafiki wa kufika kwake na kumuulizia badala ya kupiga simu. Yaani hakuna anayepajua kwake!
..tunaomtakia mema kiroho tunashangaa kutokumuona kwenye jumuiya zetu za kiroho, si lazima familia au rafiki, ni ndugu yetu kiroho, tusipomuona lazima tuulize ili wenye dhamana ya usalama wa raia watujibu wanachojua..
 
..tunaomtakia mema kiroho tunashangaa kutokumuona kwenye jumuiya zetu za kiroho, si lazima familia au rafiki, ni ndugu yetu kiroho, tusipomuona lazima tuulize ili wenye dhamana ya usalama wa raia watujibu wanachojua..
Kama ni mwenzenu sidhani kamq ni kosa nyie kwenda kwake nq kumuuliza kuliko mwana jumuiya mwenzetu. Ama ni mwenzenu lakini hamruhusiwi kufika kwake?
 
Wiki chache zilizopita tulitangaziwa kuwa aliyekuwa makamu wa Rais, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi amejiuzulu nafasi hiyo. Siku chache baadaye CCM wakatutangazia kuwa wamemfukuza Nchimbi uanachama wa chama chao! Ajabu ni kuwa CCM katika taarifa yao kwa wanahabari hawakutoa fursa ya maswali.

Tangu tukio hilo kutokea Watanzania hawajapata fursa ya kumsikia wala kumuona Nchimbi mwenyewe hadharani; haijukikani kama yuko kizuizini, amekufa au yuko hai; waliojaribu kumtafuta kama alivyofanya mzee Warioba wanadai hata kwenye simu hapatikani!

Makamu wa Rais ni cheo kikubwa sana nchini, haiwezekani kutoweka bila wananchi kujua yuko wapi, huu ni uhalifu kwa taifa. Haifikiriki mtu kama Nchimbi kutoweka na kunyamazishwa kimyakimya bila serikali na au vyombo vya dola kutuambia yuko wapi.
Kuna tetesi kuwa Nchimbi hajajiuzulu; hii inaweza kuwa kweli kwa sababu yeye mwenyewe hajasikika wala kuonekana hadharani kulizungumzia suala hili. Ajabu kuu hakuna mamlaka wala taasisi yoyote imejitokeza kuhoji uhalali wa kuondolewa kwenye nafasi yake au hata mustakabali wa uhai wake; haijulikani kama yuko hai ama amekufa, kama ni mgonjwa au yuko kizuizini.

Mwaka 1984, wakati wa mfumo wa Chama kimoja, Aboud Jumbe aliyekuwa Makamu wa Rais JMT na rais wa Zanzibar alivuliwa umakamu wa raus wa JMT, urais wa Zanzibar na kuwekwa kwenye kizuizi cha nyumbani hadi mauti yalipomkuta miaka ya 2000; angalau ilijulikana yuko wapi. Mwaka 2015, aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowasa, alijiuzulu na kuihama CCM, hatukuona kitu kama hiki maana aliendelea na harakati za kisiasa kama kawaida; sasa hili la Nchimbi mbona limekaa hivi? Watanzania wana haki ya kujua, kiongozi wao yuko wapi? Yuko hai? Yuko kizuizini? Yu mgonjwa?

Vv
Mimi naunga mkono hoja yako kabisa , ifike mda utu kwanza mengine badae bila kujali itikadi ya Mtu , dini n.k .

Hali sio shwari kwa Taifa hasa itokeapo endensha mambo kihuni kwenye Taifa huru .

Hii inamanisha nini

Sasa Kupitia hili ,Mabeberu wanaanza kujiridhisha Tz ni ya namna gani ungiunganisha dot kibao anza 29 Oct, Lissu kupewa kesi ya uhaini na kupigwa marisasi, watu kutekwa ,kupotea na kuuwawa.

Hawa jamaa wanaharibu badala ya kujenga ,ok twende tu ila watakiona cha mtema kuni ni swala mda tu.

Najiuliza kila siku kweli tz watu smart wameisha katika mifumo yetu ? Wakusema ichi ndio ,ichi kibaya tuache?
 
Wiki chache zilizopita tulitangaziwa kuwa aliyekuwa makamu wa Rais, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi amejiuzulu nafasi hiyo. Siku chache baadaye CCM wakatutangazia kuwa wamemfukuza Nchimbi uanachama wa chama chao! Ajabu ni kuwa CCM katika taarifa yao kwa wanahabari hawakutoa fursa ya maswali.

Tangu tukio hilo kutokea Watanzania hawajapata fursa ya kumsikia wala kumuona Nchimbi mwenyewe hadharani; haijukikani kama yuko kizuizini, amekufa au yuko hai; waliojaribu kumtafuta kama alivyofanya mzee Warioba wanadai hata kwenye simu hapatikani!

Makamu wa Rais ni cheo kikubwa sana nchini, haiwezekani kutoweka bila wananchi kujua yuko wapi, huu ni uhalifu kwa taifa. Haifikiriki mtu kama Nchimbi kutoweka na kunyamazishwa kimyakimya bila serikali na au vyombo vya dola kutuambia yuko wapi.
Kuna tetesi kuwa Nchimbi hajajiuzulu; hii inaweza kuwa kweli kwa sababu yeye mwenyewe hajasikika wala kuonekana hadharani kulizungumzia suala hili. Ajabu kuu hakuna mamlaka wala taasisi yoyote imejitokeza kuhoji uhalali wa kuondolewa kwenye nafasi yake au hata mustakabali wa uhai wake; haijulikani kama yuko hai ama amekufa, kama ni mgonjwa au yuko kizuizini.

Mwaka 1984, wakati wa mfumo wa Chama kimoja, Aboud Jumbe aliyekuwa Makamu wa Rais JMT na rais wa Zanzibar alivuliwa umakamu wa raus wa JMT, urais wa Zanzibar na kuwekwa kwenye kizuizi cha nyumbani hadi mauti yalipomkuta miaka ya 2000; angalau ilijulikana yuko wapi. Mwaka 2015, aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowasa, alijiuzulu na kuihama CCM, hatukuona kitu kama hiki maana aliendelea na harakati za kisiasa kama kawaida; sasa hili la Nchimbi mbona limekaa hivi? Watanzania wana haki ya kujua, kiongozi wao yuko wapi? Yuko hai? Yuko kizuizini? Yu mgonjwa?

Vv
Subiri usikie "kafia hospital fulani"alikukuwa anapatiwa matibabu baada ya kujiskia vibaya
 
Kama ni mwenzenu sidhani kamq ni kosa nyie kwenda kwake nq kumuuliza kuliko mwana jumuiya mwenzetu. Ama ni mwenzenu lakini hamruhusiwi kufika kwake?
Hatuhitaji kwenda kwake, tumemkosa kwenye mikusanyiko yetu maana yake hata nyumbani hayupo, ndio maana tunawauliza hao waliomwachisha uanachama watuambie alipo wao ndio wanampangia hata walinzi wake..kwani kusema wanachojua kuna ugumu gani, wasituletee mambo ya zama za kina salmin amour hapa..NO!
 
Hatuhitaji kwenda kwake, tumemkosa kwenye mikusanyiko yetu maana yake hata nyumbani hayupo, ndio maana tunawauliza hao waliomwachisha uanachama watuambie alipo wao ndio wanampangia hata walinzi wake..kwani kusema wanachojua kuna ugumu gani, wasituletee mambo ya zama za kina salmin amour hapa..NO!
Kwa sasa kama yeye mwenyewe kaamua kukaa kimya bila kujitokeza hadharani ili atulize kichwa kwanza, nani anawajibu wa kutoa taarifa ya wapi yupo? Tusiseme Serikali in general tuwe specific kuwa flani/taasis flani/wizara flani ndiyo wana wajibu wa kutuambia Mh Nchimbi yuko wapi. Tukiwachekea hawa watu tumekwisha.
 
Kwa sasa kama yeye mwenyewe kaamua kukaa kimya bila kujitokeza hadharani ili atulize kichwa kwanza, nani anawajibu wa kutoa taarifa ya wapi yupo? Tusiseme Serikali in general tuwe specific kuwa flani/taasis flani/wizara flani ndiyo wana wajibu wa kutuambia Mh Nchimbi yuko wapi. Tukiwachekea hawa watu tumekwisha.
Kwanza hao waliojibu barua yake ya kujiuzulu, pili hao waliomwachisha uanachama, hawezi kukaa kimya km yuko huru..kwa nafasi yake analindwa kisheria, hao wenye wajibu wa kumlinda kwa nini wanakaa kimya..hajafanya makabidhiano ya ofisi yake, km walipokea barua yake kujiuzulu wanashindwaje kumtaka akabidhi ofisi hadharani..mtu aliyeandika anataka kujihudhuru na akakubaliwa anawezaje tena kukataa kukabidhi ofisi..? si alikubaliwa alichoomba! Wasilete maigizo hapa..No!
 
Back
Top Bottom