Nchi yangu Tanzania na wasomi wake wapi tunatamani kufika?

Siri yangu

JF-Expert Member
Jul 22, 2023
1,031
2,038
Mungu ibariki nchi hii na watu wake, Mungu mbariki mmiliki wa mtandao huu na timu nzima ya kazi inayofanywa hapa ili sisi tupate sehemu ya kutolea dukuduku zetu.

20230724_121432.jpg
Ndugu zangu Kwa heshima na taadhima nipo mbele yenu nami kule kero yangu hapa kwa viongozi na wataalamu wetu tuliowapa nafasi watutumikie na wawe na maono ya kesho na mbele zaidi, hiyo picha hapo juu mnaoiona ni barabara za kutengenezwa kwa greda ambazo ni za mtaa.

Hapa ni manispaa ya Kahama mji ambao unakimbia kwa kasi ya ajabu sana, eneo hili lipo Mhungula karibu kabisaa na shule ya msingi Ilindi na ni Mbugani namaanisha mbuga kabisaa ya kulimia mpunga na nyakati za masika watu wanapata taabu kukatisha hayo maeneo.

Nimekuja kwenu na kuandika makala haya ili nijijue kama labda mimi ndio nimepungukiwa na akili au tuliowapa nafasi wamepungukiwa kidogo na sio sana, Mwaka 1998 wakati mvua kubwa na mpaka ikafikia kuitwa jina Elinino ilinyesha na maeneo haya ilikuwa ni kama bahari tu hakuna mtu aliekatiza hapa pembezoni kabisaa ndio kulilimwa mpunga na watu walivuna sana mwaka huo,.

Leo hii ukifika maeneo haya serikali imeruhusu watu kuwa na viwanja humo na kutoa vibali vya ujenzi katikati ya mbuga ambayo mvua kidogo tu maji yanajaa tena kwenye mikondo wa maji na watu wanajenga na halimashauri inabariki jambo hili.

Maswali yangu ya kijinga
1. Je, Tumejenga miundombinu ya kudhibiti maji siku ikitokea mvua kubwa?
2. Je, mmejiandaa na misaada kipindi wananchi wanapigwa na mafuriko haya?
2. Je, tumejiandaa kuja kuwalaumu wananchi wetu kuwa kwanini walijenga na ili hali ninyi ndio mnatoa vibali?
3. Je, tumeshawahi jiuliza iwapo mvua za Elinino zikija na kwa bahati mbaya ikaja usiku ikanyesha mvua kwa masaa 5 nini kitatokea kwenye nchi hii?
4. Watu wetu hawana elimu kabisaa na hawajawahi kuwaza mbali je tutawalaumu ?
5. Ofisi ya waziri mkuu kitengo cha maafa unafurahia kuja kula posho na kutoa ahadi zisizotekelezeka kama Mwakata?
6. Au na hizi fedha za maafa mtazipiga kama mlivyopiga za Bukoba ?
7. Mwisho watu wa mipango miji mlienda kufanya nini shuleni au mnakula mishahara kwa kazi gani?

Maswali ni mengi sana naweza andika hadi kesho kutwa ila naomba niishie hapa kwa umri wangu mdogo huu naombeni kama nimekosea nikosoeni kwa staha na naomba msamaha.

Wenu katika ujenzi wa Taifa
Mpitimbi ndio kwetu ukipitia Ughandi
 
Mungu ibariki nchi hii na watu wake, Mungu mbariki mmiliki wa mtandao huu na timu nzima ya kazi inayofanywa hapa ili sisi tupate sehemu ya kutolea dukuduku zetu.

Ndugu zangu Kwa heshima na taadhima nipo mbele yenu nami kule kero yangu hapa kwa viongozi na wataalamu wetu tuliowapa nafasi watutumikie na wawe na maono ya kesho na mbele zaidi, hiyo picha hapo juu mnaoiona ni barabara za kutengenezwa kwa greda ambazo ni za mtaa.

Hapa ni manispaa ya Kahama mji ambao unakimbia kwa kasi ya ajabu sana, eneo hili lipo Mhungula karibu kabisaa na shule ya msingi Ilindi na ni Mbugani namaanisha mbuga kabisaa ya kulimia mpunga na nyakati za masika watu wanapata taabu kukatisha hayo maeneo.

Nimekuja kwenu na kuandika makala haya ili nijijue kama labda mimi ndio nimepungukiwa na akili au tuliowapa nafasi wamepungukiwa kidogo na sio sana, Mwaka 1998 wakati mvua kubwa na mpaka ikafikia kuitwa jina Elinino ilinyesha na maeneo haya ilikuwa ni kama bahari tu hakuna mtu aliekatiza hapa pembezoni kabisaa ndio kulilimwa mpunga na watu walivuna sana mwaka huo,.

Leo hii ukifika maeneo haya serikali imeruhusu watu kuwa na viwanja humo na kutoa vibali vya ujenzi katikati ya mbuga ambayo mvua kidogo tu maji yanajaa tena kwenye mikondo wa maji na watu wanajenga na halimashauri inabariki jambo hili.

Maswali yangu ya kijinga
1. Je, Tumejenga miundombinu ya kudhibiti maji siku ikitokea mvua kubwa?
2. Je, mmejiandaa na misaada kipindi wananchi wanapigwa na mafuriko haya?
2. Je, tumejiandaa kuja kuwalaumu wananchi wetu kuwa kwanini walijenga na ili hali ninyi ndio mnatoa vibali?
3. Je, tumeshawahi jiuliza iwapo mvua za Elinino zikija na kwa bahati mbaya ikaja usiku ikanyesha mvua kwa masaa 5 nini kitatokea kwenye nchi hii?
4. Watu wetu hawana elimu kabisaa na hawajawahi kuwaza mbali je tutawalaumu ?
5. Ofisi ya waziri mkuu kitengo cha maafa unafurahia kuja kula posho na kutoa ahadi zisizotekelezeka kama Mwakata?
6. Au na hizi fedha za maafa mtazipiga kama mlivyopiga za Bukoba ?
7. Mwisho watu wa mipango miji mlienda kufanya nini shuleni au mnakula mishahara kwa kazi gani?

Maswali ni mengi sana naweza andika hadi kesho kutwa ila naomba niishie hapa kwa umri wangu mdogo huu naombeni kama nimekosea nikosoeni kwa staha na naomba msamaha.

Wenu katika ujenzi wa Taifa
Mpitimbi ndio kwetu ukipitia Ughandi
Unazungumzia Mji ninaoufahamu vizuri sana.

Shida ya Kahama inaendelea kujipika. Na kwa haya yanayoendelea ninaingoja siku isiyokuwa na jina.. na ninawaasa wanasheria wa Kahama wawaambie wateja wao kutunza nyaraka zao za vibali vya ujenzi na nyaraka yoyote ya kubariki itokayo serikalini... Maana siku hizo zitakuwa za kulia kwa muda na kucheka kwa sana.

Miji huanzishwa kwa kuzingatia suitability analysis, kung'amua hatari zinazoweza kuleta shida kwa wakazi na aidha kuzitafutia ufumbuzi wa kidumu kabla ya kuruhusu Mji kuanzishwa eneo lolote au kukataza matumizi ya makazi kwa eneo lenye shida.

Kijiografia Mji wa Kahama ni mkusanyiko wa mabonde yenye miinuko midogo midogo inayokusanya na kupeleka maji katika ziwa Nyanza. Hivi karibuni pressure ya watu kujenga imeigeuza Manispaa shingo na Sasa Manispaa imedanganyika na mapato ya vibali.. sweet.. only until it's time to cough the change.

Athari zake kubwa ukiachilia devastation ya watakaokumbwa na shida ni pamoja na watu kupachukia, kuhama eneo au Mji, kufunga biashara kwa watakaokumbwa na changamoto kwenye maeneo ya uzalishani na kubwa kuliko ni kupunguza morale ya watu kuwekeza Tena kwenye maeneo mengi ya Mji kwa kuhofia Matokeo ya usahaulifu na kukosa umakini.

Na Kahama isipokuwa makini na kufanya

1) proper master plan haraka iwezekanavyo,

2) kutekeleza mpango wa ujenzi wa series of water catchment ponds maeneo kama ya Mhungula, Zongomela, Majengo chini na sehemu za Sofi na Nyashimbi, kupanda miji katika njia za maji na kuziacha wazi, kubainisha na kuzifungua njia zote kubwa za maji mengi (Storm water drains)

3) kuwekeza katika mfumo wa maji taka kabla hata hawajaanza kuwekeza kwenye mabarabara, huwezi kuwa na Mji wa watu laki nne halafu wote wanapanga kinyesi ...hakioti sana kinafanya Ardhi inakuwa saturated tu na maji na Mji kuwa na harufu mbaya.

4) mfumo wa maji taka, hasa kwa Kata za mjini kati utachochea Compact development ambayo kwa. Sasa ni ngumu kujenga Majengo makubwa sana kwa kuhofia water treatment na cost ya ununuzi wa maneno makubwa mjini ili kupata nafasi ya water treatment

5) mwisho ni kuondoa stand ya CDT na eneo la kuegesha magari la Uwanja Wa Taifa ..hakuna Mji unakosa kuwa na open spaces, na maeneo haya yalitengwa kuwa maeneo ya wazi ..Mji unakosa definition kwa sababu ya tamaa ya mapato.

Na TARURA na Manispaa kwa ujumla wazingatie kujenga miundombinu rafiki kwa waenda kwa miguu. It's as if kila wakijenga barabara basi watu waipite barabarani maana inakuwa ni hatari Bora hata ingekuwa ya vumbi.. or barabara ya mhongolo kutokea pale mashine I i hatari sio tu kwa magari hata kwa waenda kwa miguu.

Kuwa Mji sio mapato, Wala wingi wa watu ni namna watu wako wanavyobehave. Moshi Haina watu wengi kama Kahama ila Moshi ni mjini kuliko Kahama... Ni namna watu wanavyobehave.. na tabia za watu no reflection ya viongozi wao.

Let's go Kahama.
 
Unazungumzia Mji ninaoufahamu vizuri sana.

Shida ya Kahama inaendelea kujipika. Na kwa haya yanayoendelea ninaingoja siku isiyokuwa na jina.. na ninawaasa wanasheria wa Kahama wawaambie wateja wao kutunza nyaraka zao za vibali vya ujenzi na nyaraka yoyote ya kubariki itokayo serikalini... Maana siku hizo zitakuwa za kulia kwa muda na kucheka kwa sana.

Miji huanzishwa kwa kuzingatia suitability analysis, kung'amua hatari zinazoweza kuleta shida kwa wakazi na aidha kuzitafutia ufumbuzi wa kidumu kabla ya kuruhusu Mji kuanzishwa eneo lolote au kukataza matumizi ya makazi kwa eneo lenye shida.

Kijiografia Mji wa Kahama ni mkusanyiko wa mabonde yenye miinuko midogo midogo inayokusanya na kupeleka maji katika ziwa Nyanza. Hivi karibuni pressure ya watu kujenga imeigeuza Manispaa shingo na Sasa Manispaa imedanganyika na mapato ya vibali.. sweet.. only until it's time to cough the change.

Athari zake kubwa ukiachilia devastation ya watakaokumbwa na shida ni pamoja na watu kupachukia, kuhama eneo au Mji, kufunga biashara kwa watakaokumbwa na changamoto kwenye maeneo ya uzalishani na kubwa kuliko ni kupunguza morale ya watu kuwekeza Tena kwenye maeneo mengi ya Mji kwa kuhofia Matokeo ya usahaulifu na kukosa umakini.

Na Kahama isipokuwa makini na kufanya

1) proper master plan haraka iwezekanavyo,

2) kutekeleza mpango wa ujenzi wa series of water catchment ponds maeneo kama ya Mhungula, Zongomela, Majengo chini na sehemu za Sofi na Nyashimbi, kupanda miji katika njia za maji na kuziacha wazi, kubainisha na kuzifungua njia zote kubwa za maji mengi (Storm water drains)

3) kuwekeza katika mfumo wa maji taka kabla hata hawajaanza kuwekeza kwenye mabarabara, huwezi kuwa na Mji wa watu laki nne halafu wote wanapanga kinyesi ...hakioti sana kinafanya Ardhi inakuwa saturated tu na maji na Mji kuwa na harufu mbaya.

4) mfumo wa maji taka, hasa kwa Kata za mjini kati utachochea Compact development ambayo kwa. Sasa ni ngumu kujenga Majengo makubwa sana kwa kuhofia water treatment na cost ya ununuzi wa maneno makubwa mjini ili kupata nafasi ya water treatment

5) mwisho ni kuondoa stand ya CDT na eneo la kuegesha magari la Uwanja Wa Taifa ..hakuna Mji unakosa kuwa na open spaces, na maeneo haya yalitengwa kuwa maeneo ya wazi ..Mji unakosa definition kwa sababu ya tamaa ya mapato.

Na TARURA na Manispaa kwa ujumla wazingatie kujenga miundombinu rafiki kwa waenda kwa miguu. It's as if kila wakijenga barabara basi watu waipite barabarani maana inakuwa ni hatari Bora hata ingekuwa ya vumbi.. or barabara ya mhongolo kutokea pale mashine I i hatari sio tu kwa magari hata kwa waenda kwa miguu.

Kuwa Mji sio mapato, Wala wingi wa watu ni namna watu wako wanavyobehave. Moshi Haina watu wengi kama Kahama ila Moshi ni mjini kuliko Kahama... Ni namna watu wanavyobehave.. na tabia za watu no reflection ya viongozi wao.

Let's go Kahama.
Ahsante kiongozi kwa hili pia napata faraja kuniunga mkono kuona kosa linalofanyika kwenye Mji wa Kahama
 
Back
Top Bottom