Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

Kama kijana nayeipenda nchi yangu, nayependa amani, demokrasia na maendeleo nafanyaje?

Nafanyaje Askari wanaposherehekea ushindi wa dhulma wa chama tawala kwa kuimba 'soldier nyakua'?

Nafanyaje mheshimiwa rais anapotoa ilani ya kumshughulikia Mkurugenzi atakayemtangaza mpinzani kuwa mshindi kwenye uchaguzi?

Nafanyaje napoona viongozi wangu wa chama, wapenda demokrasia na amani, wakidhalilishwa na polisi kila leo,wakinyang'anywa Mali zao kwa nguvu, wakilazimika kuzunguka mahakamani kila uchao na wakidhalilishwa wao na familia zao?

Nafanyaje napoona vijana wenzangu wa Rika wakishawishiwa na kushawishika kwamba demokrasia haina nafasi Bali siasa za visasi, hujuma na matumizi ya nguvu ya dola ndio mtindo wa kileo?

Nitaendeleaje kuamini katika uchaguzi huru na wa haki wakati tume yenyewe ya uchaguzi haiamini Wala vyombo vya dola haviamini?

Kwanini wakati wa apartheid vijana wa Afrika kusini walikuja kujifunza hapa mbinu za uasi?
Kwanini hawakuitisha tu mikutano ya siasa nchini kwao na kwenda kupiga kura?

When democracy has no chance, it is the responsibility of everyone and anyone to give it a chance!

SOLDIER NYAKUA, NYAKUA!
Ivi wale walikua wanashabikia ushindi wa mwanasiasa gani na wa Jimbo lipi mm niliona tu wakishabikia lakini sikufaham ni mwanasiasa gani, naomba kujuzwa aisee, maana tunakoelekea sipo kabisa
 
Ni hatari sana watu wanapowekwa katika mazingira ya kuanza kufikiri "uasi" kama njia ya kupata haki!

Waliopewa dhamana ya kulinda usalama wa Taifa hili nashangaa wanaacha dhulma zinatamalaki ndani ya nchi!. Dhulma na uonevu ndivyo vitu vinavyotishia usalama na amani, ni mambo ya aibu, ni mambo ya kinyama, ni mambo ya watu wasiostaarabika!

Kuna watu somewhere ni compliant wa udhalimu ndani ya mipaka yetu au hawatimizi wajibu wao, watalaaniwa na kila kizazi kijacho kwa kuipeleka nchi yetu katika direction ya uharibifu na maangamizi!. Ni huzuni sana kuona nchi yetu polepole inaelekea kusiko!
 
Ingieni msituni nina hamu na minofu ya bavicha
Kufikia asubuhi msitu umelala ndio mtatujua kwanini tunaogopwa na nchi zote za kiafrika na asia.
View attachment 870037
Labda wanadhani kuwa nchi imeshindwa kutawalika. Hapa wala hakuna haja ya kujadiliana na mtu mwenye fikra za uasi. Huyo ni kumsubiri aasi kisha kumkamata na kumuhukumu kadri ya matendo yake.
 
Kama kijana nayeipenda nchi yangu, nayependa amani, demokrasia na maendeleo nafanyaje?

Nafanyaje Askari wanaposherehekea ushindi wa dhulma wa chama tawala kwa kuimba 'soldier nyakua'?

Nafanyaje mheshimiwa rais anapotoa ilani ya kumshughulikia Mkurugenzi atakayemtangaza mpinzani kuwa mshindi kwenye uchaguzi?

Nafanyaje napoona viongozi wangu wa chama, wapenda demokrasia na amani, wakidhalilishwa na polisi kila leo,wakinyang'anywa Mali zao kwa nguvu, wakilazimika kuzunguka mahakamani kila uchao na wakidhalilishwa wao na familia zao?

Nafanyaje napoona vijana wenzangu wa Rika wakishawishiwa na kushawishika kwamba demokrasia haina nafasi Bali siasa za visasi, hujuma na matumizi ya nguvu ya dola ndio mtindo wa kileo?

Nitaendeleaje kuamini katika uchaguzi huru na wa haki wakati tume yenyewe ya uchaguzi haiamini Wala vyombo vya dola haviamini?

Kwanini wakati wa apartheid vijana wa Afrika kusini walikuja kujifunza hapa mbinu za uasi?
Kwanini hawakuitisha tu mikutano ya siasa nchini kwao na kwenda kupiga kura?

When democracy has no chance, it is the responsibility of everyone and anyone to give it a chance!

SOLDIER NYAKUA, NYAKUA!
Kimsingi tumechelewa sana, yaliyotokea monduli juzi yalishawahi kutokea wakati fulani na Nassary alipigwa vibaya wakati huo lowasa ndo sterling wa ccm monduli.

Kimsingi lowasa anaijua vizuri siasa na wapiga kura wa Tz, alifahamu fika kuwa ccm itachukua nchi kwa gharama yoyote ile na yeye akibaki ccm ndo mwisho wake kisiasa, solution, hamia cdm gombea urasi na status yake kwenye national politics itabaki kuwa juu na amefanikiwa sana.

Cdm wanaelewa sana ugumu wa kuitoa ccm madarakani kwa karatasi ya kura, so yoyote anakuja kwao hata km ni mbaya kiasi gani, ukweli ni kwamba hakuna ubaya wa mtu utakaoweza kuizidi ule wa ccm na mfumo wake, hivyo pokea wote including lowasa na sumaye aliyewahi kusema 'ukitaka mambo yako yaende vizuri ingia ccm'.

Hapa sina lengo la kuwalaumu cdm wala kina lowasa na wenzake bali ni kujaribu kuonesha ni kwa kiasi gani tumechelewa sana kudai true democracy kwa njia yoyote ile. Mifano ni mingi sana kuelewa kuwa uhuru wa 1961 niwakubadili tu utawala ila mifumo ya ukoloni bado inatutawala kupitia watu weusi.

Kwa urahisi kuwa ccm haiwezi kutoka madarakani kwa kura hata km uchumi ufe kiasi gani angalia Zimbabwe pale ambapo jina ccm bado haijachokwa na siku ikichokwa angalia yaliyotokea Kenya. Kabla kanu haijafa, iliua upinzani wa kweli ikatengeneza kwa kwake chini ya kibaki ambaye miaka yote toka uhuru amekuwa kanu km waziri na makamu wa raisi. Sasa yupo kenyata ambaye 2002 alikuwa mgombea uraisi wa kanu, 2008-2013 waziri wa fedha chini ya kibaki na 2013-leo ni raisi, jiulize ni lini kanu ilikufa?

Mwisho, ccm haiwezi kuachia madaraka kwa njia ya kawaida ya karatasi ya kura kwa sababu kuu tatu; #1. Ujinga na umaskini bado ni mkubwa sana, yaani bado wapo wengi tu wanaoipa kura, #2. Mfumo wa uchaguzi haiko huru na kamwe hawatauweka huru kwa kuombwa, #3. Bado mfumo wa utawala unaendelea kujali interests za wakubwa duniani.

Mwisho kabisa, exception, #1. inawezekana ccm kuondoka pale ambapo tutapa mgombea uraisi ambaye ataungwa mkono na idadi ya kutosha, at least 75% ya wapiga kura wote nchi nzima ktk nafasi zote yaani udiwani, ubunge na uraisi, #2. Siku wakiaamya kuvunja mfumo unalinda interests za wakubwa duniani.

Kwa mapni yangu, hii exception #1 tuipatie nafasi 2020 kupitia Tundu Lissu, alishawahi kuifuta ccm jimbo kwake, anaweza kuifuta Tz.
 
Upo sawa kabisa, shida vijana wengi wa leo vipao mbele vyetu ni hamisa mobeto na voice note za mganga au gigiy money na mo jay au dogo janja na airine uwoya, mambo ya siasa tunasema hayatuhusu!!


Ilimradi tuna vicomputer tunaweka nyimbo kwenye simu tupate bando lakusoma udaku na tumeruhusiwa kuchuuza bidhaa bila kulipa kodi kwa kuzitandika mpaka ofisi ya mkuuwa wilaya mengine hayatuhusu!!

Sasa hayo ya siasa usituambie we tuambie habari za kuvaa vijinzi vinaitwa kamatia chini, na mambo ya vikuku na nk!!!

Ilimradi tumeamka asubui tunapata hela yakula, basi inatosha!!! Uo uasi kaaanao, utakuwa wewe peke yako, naivi tumemaliza form four na zero zero hatuitaji hayo mambo!!!


Hiiinchi kati ya watu milioni 50 wenye uelewa ni milion 5 usitegemee unacho fikiri!!
Uko sahihi ila fahamu kuwa hata ukisubiri miaka elfu bado ratio itakuwa hiyo ya 1:10 na kwamba kazi ya hao wachache ni kuwakomboa the rest
 
Msio ijua history na Ukweli wa mambo hua nawaonea huruma Sana.
Gaddafi hakutolewa na nguvu ya umma, bali ni mabeberu wakitumia NATO, na walibya wanajuta kwa sasa, kama hujui Jambo ni bora kunyamaza kulinda heshima yako kuliko Kuonyesha uzuzu wako hadharani
Yaani unaandika yote haya ili kutetea uhuni unaofanyika katika taifa hili ambao athari zake hata wewe mwenyewe zinakugusa hata kama unajikausha? Gadafi alitolewa na nguvu ya umma. Nyingine ni nyongeza tu. Hii habari ya kwamba walibya wanajuta, ni propaganda tu kama zile za "Tunatekeleza" huku nchi ikiingia kwenye madeni makubwa ambayo hayawekwi wazi, lakini ni lazima kesho na keshokutwa tutalazimika kuyalipa!
 
Sasa bro ulitakiwa kujua kitu kimoja katika mapambano. Kiasili mapamo ya kumtoa mtawala huwa hayataki kushindwa na yanataka maandalizi.

Musa pale alikuwa anandoa uovu sababu alikuwa na uwezo wa kufanya,na ndio maana baada ya tukio hilo hapakutokea umwagaji damu.

Yaani aliondoa uovu bila kuruhusu uovu mwingine utokee.

Sasa nyinyi mnaotaka kuasi mnaweza kufanya kama lile alilofanya Musa ? Yaani mnaweza kuondoa uovu bila kusababisha hatari kubwa zaidi kutokea ?

Na hapa ndipo siri ya mapambano ambayo wengi hawaijui.

Nasubiri jibu.

Mtoa maada alipozungumzia uasi hakusema ni uasi wa aina gani, uasi uko wa aina nyingi.
Kuna uasi bila kumwaga damu, kuna uasi hutokea na damu kumwagika za wenye hatia na wasio na hatia, kuna uasi kwa damu za wenye hatia pekee kumwagika, kuna uasi wa damu za wasizo na hatia pekee kumwagika.. Mtoa maada ana options nyingi za uasi anaotaka kuufanya cha muhimu ni sababu za huo uasi..
 
Yaani unaandika yote haya ili kutetea uhuni unaofanyika katika taifa hili ambao athari zake hata wewe mwenyewe zinakugusa hata kama unajikausha? Gadafi alitolewa na nguvu ya umma. Nyingine ni nyongeza tu. Hii habari ya kwamba walibya wanajuta, ni propaganda tu kama zile za "Tunatekeleza" huku nchi ikiingia kwenye madeni makubwa ambayo hayawekwi wazi, lakini ni lazima kesho na keshokutwa tutalazimika kuyalipa!
Acha porojo nyuma ya keyboards lianzishe tuone umwamba wako,na kwa taarifa yako muulize Sugu na wasafwa wake,habari wanayo
 
Ingieni msituni nina hamu na minofu ya bavicha
Kufikia asubuhi msitu umelala ndio mtatujua kwanini tunaogopwa na nchi zote za kiafrika na asia.
View attachment 870037
Haaaaa huna lolote unalojisifia nalo hivi unazan hao waasi ni RAIA au, Hivi unajua kwamba hata jeshini watu hawafurahishwi na uzandiki huu wa wanasiasa lakn lazima afate order but am sure one day they will ignore the order
 
Wadhalimu wakisherehekea na mitutu
Screenshot_20180917-205548.jpg
 
Back
Top Bottom