Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

Hicho mnachoita demokrasia ni propaganda za mabeberu kuleta ukoloni mamboleo kuendeleza maslahi yao ya kiuchumi, kijamii na kisiasa, hakuna cha ziada.
 
Msio ijua history na Ukweli wa mambo hua nawaonea huruma Sana.
Gaddafi hakutolewa na nguvu ya umma, bali ni mabeberu wakitumia NATO, na walibya wanajuta kwa sasa, kama hujui Jambo ni bora kunyamaza kulinda heshima yako kuliko Kuonyesha uzuzu wako hadharani
Hivi unajua kuwa hata hapa kwa hali hii wakipata uchochezi na support toka nje ni rahisi kugeuka na kuihujumu serikali iliyopo? Upendo a nchi yao umeshapotezwa kwani nchi haiwapendi wala kuwaheshimu tena.
Sasa hivi watu hawa wenye chuki na Polisi au wakuu kama Makonda wakipata wanao washawishi kutega mabomu ofisi zao ipo sababu kweli ya kukataa na kulinda utaifa?
Tunaipoteza Amani yetu kwa kubweteka kuwa ulinzi wa dola unaweza kutufanya tuwafanyie wengine chochote.
Au kitendo cha Makonda watu wake kuonyesha bastola aliyofunga kiunoni kuwa ni ufahari hadharani na ulinzi wa kutosha.
Tunaangamia kwa kukosa maarifa
 
Tatizo hampo kwenye system ndomana hamjui kitu kazi kuwatukuza wanasiasa..
1) unajua toka magufuli aingie kabadili system ndan ya jeshi? Je mtazamo wa wanajeshi unajua ukoje juu yake?
2)unajua kwann Tanzania inakubali tu kuendelea na UN missions Congo,Sudan,Lebanon na central Africa?
3) unajua kitu chochote kilichotokea ngome house mwaka huu mpaka wanajeshi kupgana risasi wao kwa wao?
Daaah wanasiasa wanapoteza Tz yetu...gas imeondoka, uranium imeondoka, madini yameondoka
watoto wa kula kunya hawa,watajua wapi.
 
Hakuna haja ya kuwahukunu dawa yao ni Barrage Kutoka kwenye Grad launcher usiku kucha kukipambazuka huo msitu umegeuka jangwa na mizoga ya pipoz mainzi.
Hiyo grad launcher mlipouziwa nyie wauzaji waliacha kuuza?
 
Ni wapumbavu tu wale walindwao na wanadamu wenzao kisha wakajiamini sana kwa kudhani kuwa wanayajua yale yaliyomo katika mioyo ya hao wanaowalinda, na wakajidanganya kuwa wana uwezo wa kuwacontrol muda wote muda wowote, wanajidanganya!!. Dhulma ni mbaya tena ni mbaya sana!!. Kuna watu kwa sababu ya ubabe utokanao na ulevi wa madaraka wanataka kuharibu nchi !. Kwa matendo yao Ipo siku watakinywea kikombe wanachokitengeneza!!
 
Hiyo grad launcher mlipouziwa nyie wauzaji waliacha kuuza?
Hizo zimejaaa hata Amini wa uganda alipewaa na ghadafi lakini tuliziteka kwa ulainiii kwanza hawajui kuzitumia mimi nadhani majeshi yaliyokuwa ni waataalamu wa kutumia silaha hizi za kjmbari ni Somalia.
 
Hebu tuone hekima za Sun Tzu kwenye kitabu cha sanaa za kivita anasemaje kitabu kinaitwa " Art of war" kwa kiingereza

Sun Tzu anasema askari ni moyo kabla ya silaha, Ukiwa na moyo basi silaha na chakula utavikuta kwenye himaya ya "adui".

Sun Tzu anasema ni rahisi kwa jeshi dogo lenye sababu za msingi za kupigana kuweza kulishinda jeshi la wengi na lenye nguvu lakini lenye kupigania kulinda yasiyo na maana,hii ni kweli maana kwa mfano jeshi la Vietnam liliweza kuwapiga Wamarekani wenye zana nzito, Wamarekani walikuwa wanapigania kulinda kibaraka wao huko south Vietnsm wakati wa Vietnam walikuwa wakipigania kulinda uhuru na kujitawal au jeshi la Kagame la Kagame lilipoishinda jeshi serikali, Kagame alikuwa anapigania kuondoa manyanyaso dhidi ya watusi na kukomesha Genocide wakati jeshi la serikali lilikuwa likiendesha chinjachinja dhidi ya Watusi, au Waafghanistan dhidi ya Wasoviet

Sun Tzu anasema askari ni kama Simba hazoeleki, ukijiaminisha kuwa unammiliki ipo siku anaweza kukuchenjia akakutafuna

Sun Tzu anasema jemedari shupavu ana uwezo wa kumfanya mtu yoyote yule legelege kuwa mtu hatari sana mpaka usimdhanie kama huyu mtu ndiyo yule aliyekuwa legelege
 
Kama kijana nayeipenda nchi yangu, nayependa amani, demokrasia na maendeleo nafanyaje?

Nafanyaje Askari wanaposherehekea ushindi wa dhulma wa chama tawala kwa kuimba 'soldier nyakua'?

Nafanyaje mheshimiwa rais anapotoa ilani ya kumshughulikia Mkurugenzi atakayemtangaza mpinzani kuwa mshindi kwenye uchaguzi?

Nafanyaje napoona viongozi wangu wa chama, wapenda demokrasia na amani, wakidhalilishwa na polisi kila leo,wakinyang'anywa Mali zao kwa nguvu, wakilazimika kuzunguka mahakamani kila uchao na wakidhalilishwa wao na familia zao?

Nafanyaje napoona vijana wenzangu wa Rika wakishawishiwa na kushawishika kwamba demokrasia haina nafasi Bali siasa za visasi, hujuma na matumizi ya nguvu ya dola ndio mtindo wa kileo?

Nitaendeleaje kuamini katika uchaguzi huru na wa haki wakati tume yenyewe ya uchaguzi haiamini Wala vyombo vya dola haviamini?

Kwanini wakati wa apartheid vijana wa Afrika kusini walikuja kujifunza hapa mbinu za uasi?
Kwanini hawakuitisha tu mikutano ya siasa nchini kwao na kwenda kupiga kura?

When democracy has no chance, it is the responsibility of everyone and anyone to give it a chance!

SOLDIER NYAKUA, NYAKUA!
Unafikirisha!
 
Vita ya uasi uisikie na kuona kwenye picha tu. Gharama za vita hazivumilki nchi haijafikia level hiyo. Mtoa maada kama umechoka so uandamane au kuasi?
 
Back
Top Bottom