Wewe unafikiri Nyerere aliamka asubuhi na kutangaza Azimio la Arusha? Mkuu Idadi ya watu haijengi hoja kwani leo Nyumba zilizojengwa nchini nazo zimejengwa na kanisa au serikali! vipi mkuu wangu mbona wakati wa Nyerere tulikuwa hatuna sabuni wlaa dawa ya mswaki leo Mengi anatengeneza vitu hivyo na hatumpi ruzuku?. Unataka kujenga hoja kwa sababu ya dhiki zilizopo..
Business means business! na serikali haitakiwi kuweka mkono wake. Mimi ni mhafidhina na nazungumzwa kama mhafidhina wala sio swala la Udini kama manvyofikiria. Serikali inafanya matumizi ambayo hayahitajiki kabisa, maana kanisa linaweza kabisa kujitosheleza. Wewe mgonjwa ukienda Hospital iwe ya kanisa au private ndipo serikali inatoa subsidy kwa tiba uloipata sio kutoa fungu la Bil 90 hatujui kanisa wamezitumia vipi. Hii ni nooo nooo! Sasa kama wananchi wengi hawaendei ktk hospital hizo, hizo fedha wanazifanyia nini na tunazi account vipi?..
Mimi nasema sikubaliani na Muafaka wa MoU, wewe tazama kwa jicho lolote lile lakini sio kuniita sina akili wakati wewe mwenyewe unaamini vitu vya ajabu ajabu.. na sitaki kwenda huko... lakini kubali tu kwamba serikali yetu haifungamani na dini yoyote na kutoa ruzuku kwa kuweka muafaka na kanisa ni makosa ya kikatiba. Itolewe ruzuku kwa wagonjwa iwe umekwenda KCMC, Kariuki au Hindu Mandal mgonjwa ndiye awe na chaguo la kutibiwa wapi na hiyo ruzuku yake inamfuata kule alikotibiwa - Kabish!
Ndio maana nakwambia wewe ni mjinga. Serikali haina dhamira ya kuchukua hospitali za watu bila sababu za msingi. Kairuki, Aghakan, Hindu Mandal na Ibrahim Haji ni hospitali zilizopo mjini. Lengo la serikali kutoa ruzuku ni kwa maeneo ambayo serikali haijafikisha huduma. Hospitali ulizozitaja zote zipo mjini ambako tayari serikali inao uwezo wa kutoa huduma. Tofauti hapa ni kwamba, kanisa limefika ambapo hao kina hindu mandal hawajafika. Sasa sioni ni ubongo gani unakuongoza kuona kuwa ruzuku ni fasheni. Kule kijijini mgonjwa hana chaguo, ataenda tu kwenye hospitali ya misheni kwani ndio iliopo. Kwa nini unapenda kubisha wkt hujatembea?
Kulaumu nayo ni ibada kwako, ndio maana unajiita mhafidhina bila kuwa na utashi wa kujitegemea. Wewe endelea kupinga MoU, lkn waislamu wanaotibiwa Teule Hospital hawajui unalia nini kwani wao wanatibiwa kwa gharama sawa na amana au mwananyamala. Wewe unayeishi kwa kusikia toka kwa Sheikh Isa ponda na bassaleh endelea kupinga MoU na kudai misikiti ijengwe mashuleni bila kuwa na utashi wa kujenga shule zenu.
Na unaposema 90bn hatujui kanisa wamezitumia vipi ni ujinga ndugu yangu. Mara ngapi nikueleze kuwa fedha zimetolewa kwa hospitali na sio kanisa? Mara ngapi nikueleze kuwa hata mhasibu wa hospitali inayopata ruzuku ya serikali anaajiriwa na kusimamiwa na serikali na sio kanisa? Unaposema hamjui, wewe na nani? Yule anayewajibika kujua za TANROADS zimetumikaje ndio anawajibika kujua na za BUGANDO zimetumikaje. Yule anayewajibika kujua za MEM na MEMKWA zimetumikaje ndio anawajibika kujua za KCMC zimetumikaje. Wewe na huyo mwenzio (unayemwakilisha unaposema 'hatujui') sio kigezo cha kukosekana uhalali wa MoU. Waislamu wenzako wanaotumia hizi hospitali watakushangaa kwa kuwasemea.
Na kwa kuwa unajifanya (ki unafiki) kuwa si udini unakuongoza kusema haya yooote kuhusu MoU, acha basi nikukumbushe kuwa:
1. Zile fedha zilizoaminika kurejeshwa EPA hazijulikani zilipo (bila shaka hizi unajua habari zake jinsi zilivyotumika ndio maana upo kimya)
2. Kesi ya RADA imezua mashitaka kwa waingereza waliotuuzia na wanapata kibano lkn wezi wenzao wa hapa kwetu wanatesa mjengoni (bila shaka unajua jinsi fedha za rada zilivyotumika)
3. Juzi hapa kakamatwa mtumishi wa bodi ya mikopo kwa wizi wa fedha (bila shaka unajua zinavyotumika kwa kuwa unafuatilia kama ilivyo ada ya majukumu yako)
Haya ni machache tu kati ya ambayo umeshayapitia na kuona yako sawa kwa kiyo lazima ulalamike juu ya hizi za KCMC na BUGANDO kwa kuwa wamekunyima taarifa bila kuzingatia kuwa wewe ndio unatakiwa uwe wa kwanza kujua zimetumikaje.
Eeeh Mungu nipe akili, maisha yasiwe mzigo!
Hivyo vitu vya ajabu ajabu unavyovisema juu ya imani yangu wewe viseme tu, mimi sina mashaka juu ya kile ninachoamini. Na kama imani itatakiwa iwe msingi wa maisha yetu, basi jua kuwa mimi ni mwanaume kwa hiyo sina cha kuhofia ktk ahadi za yale tunayotakiwa kuyatarajia tukifika peponi. (mabikira na wine: ni wanawake ndio hatujui wameahidiwa nini)