Samahani...nadandia treni kwa mbele...! Mkuu hii ya 40,000 kumuona daktari umeshaisema mara nyingi na kama kumbukumbu zangu hazijakosea ulishawahi kusema pia kuna wakati mlishindwa kumlipia mgonjwa wenu kwenye hizi hospitali zinazopokea ruzuku ikabdi mumpeleke India... Hivi hauwezi kweli kutuambia jina la hiyo hospitali? Ni hilo tu.
- Mkuu sielewi nia yako lakini kama nisemavyo sina Unafiki, nitasema kweli daima uongo kwangu ni mwiko..
kuna kesi mbili hapa tofauti, ipo ile ya kwenda India (Apollo) ambayo tulianza na KCMC na ipo ya mdogo wangu kutibiwa Muhimbili ambayo tulilipa Tsh 40,000 kumwona Daktari baada ya kupata vipimo toka kwa daktari mwingine mhindi ni kilema yuko Upanga kwa Tsh 80,000 kisha akafanyiwa Operation ndogo kwa Tsh 600,000 lakini bado hajapona. Tumefanya tena vipimo kujaribu kutazama haswa kinachosmbua ni kitu gani maana miaka mingi sasa.
Ningeungana sana na madaktari kama madai yao yangekuwa dhidi ya serikali na hayahatarishi maisha ya wananchi. Unagoma kudai haki yako bila kuathiri sheria nyingine, ndivyo sheria zilivyo tungwa kwa kutazama uzito wa swala. Kenya wamewahi kufanya mgomo lakini waliweza kuendelea kutibia wananchi wenye ulazima wa kupata matibabu..
Yes, yawezekana kabisa madai ya hawa madaktari yakawa na msingi lakini unapomtumia mwananchi kama humanshield ktk vita baina yako na serikali hapo mkuu wangu sintokubaliana nao kabisa acha mbali najua fika hakuna daktari bingwa nchini mwenye maisha mabaya - hakuna!..
Madaktari wanazo njia nyingi sana ambazo ni haramu ktk viapo vya Udaktari lakini zimehalalishwa nchini kutokana na Azimio la Zanzibar. Mtu kasomeshwa bure kwa gharama zaidi ya Usd 120,000 na kodi za wananchi, anapewa nyumba, maji na umeme bure bado wanaweka madai kwa sababu ya wajinga wengine WABUNGE ambao nao ati wanajiita wasomi wanalishwa bure na kodi za wananchi bila hata aibu wanajitapa kwamba wao ndio serikali (wabunge ndio mawaziri). Yaani mfumo mzima wa RUKSA ndio sababu kubwa ya migogoro na nchi yetu kuingia bondeni tukakwama. Na kwa ujinga ule ule wa Ruksa, tunabishana sana juu ya viti , nauli zetu na dereva awe nani badala ya kutazama tutaliondoa vipi gari letu toka ktk shimo hili tulokwama. Usafiri ni gari sio maisha ya kila mtu wakati hatuwezi tembea kwa miguu kwenda tunakotaka.
Hii nchi kweli inatawalika au ndio akili za wasomi wetu.