Nawaunga Mkono Madaktari

Nawaunga Mkono Madaktari

Ikiwa serikali inatoa billioni 90 kila mwaka kwa kanisa mlitegemea itapata fedha wapi zaidi za kuboresha Hospital zake..

Kanisa gani hilo?
Sikuwahi kudhani kwamba na wewe ni mdini kiasi hiki.
Afu umeanzisha thread ya kulalamika JF imechange kumbe na wewe
ni sumu kiasi hiki?
 
ukiumwa sasa hivi ukawa serious ndio utamjua kalumekenge ni nani
 
Well kuanzia sasa hivi Mkandara siye yule umjuaye tena. Mimi nalilia maslahi ya wananchi na sio ya Kanisa wala Msikiti. Tunalipa kodi zetu sasa wanagoma ili iweje kama sio tufe sisi, wakati wameshakatiwa fungu na serikali. nani anayepanga matumizi ya uendeshaji biashara zao kama sio kamati ya CSSC. Na hata wangekuwa Bakwata ningewashambulia kama navyofanya hapa maadam nachokitazama ni maslahi ya wananchi sio dini wala dhehebu.

Kama madaktari wanataka kugoma waanze na kwenda ktk menejimenti zao kujua kulikoni. Tena tunatakiwa kabisa kudai CSSC watupe matumizi ya ruzuku zetu maana mkuu wangu hata wewe Mkristu unalipia fedha hizi ktk kodi na bado unatozwa kumwona daktari. Hakuna nafuu kwako wewe wala mimi sote tunaumizwa, hivyo unapolifanya swala hili liwe la Udini ndipo napowashangaa wakati linakuumiza hata wewe. Hawa ni watu tu binadamu kama wewe mnawaogopa kitu gani?... kwa sababu viongozi wa dini!... Upuuzi mtupu ndio maana CCM itatawala milele kwa kuwagawa.


Matatizo ya madaktari na Kanisa vina ingiliana vipi mkuu?
Hapa una jaribu kufunika funika uharo ulio toa lakini wala sioni point
ya kujitetea kwa chuki zako na udini.
Duh
 
well said

uchungu wa banda la mbuzi lisiloezekwa kipindi cha mvua hauwezi kuzungumziwa na paka anayelala chumbani kwa mwenye nyumba. Acha tuzungumzie sie wenyewe! Kwani unafikiri madaktari hawajui kwamba ndugu zao wanaweza ugua huko waliko wakati huu wa mgomo na kukosa huduma? Na wao kwani ni vyuma? Wachache wafe kwa manufaa ya wengi watakaobaki. Tunataka hospitali zetu ziboreshwe. Hospitali ya taifa inakosa hata xray films! This cant be.
 
Wapi nimesema fedha zimejenga makanisa na mihadhara!... jamani huu ukumbi siku hizi vipi?..
Na kama ulivyosema ndivyo, sasa kwa nini madaktari wamegoma?.. kwa nini iwe jukumu la serikali ikiwa fedha hizo walipewa makanisa kuboresha huduma hizo..Wewe unajua hiyo kamati ya CSSC walizitumia vipi fedha hizo? na kwa nini usitake wakupe mahesabu lakini akisema Mkandara tayari ni Udini wakati hata wewe unaweza kuuliza?..

Kwa hiyo una maana makanisa ndiyo yanaendesha hospitali zote nchini pamoja na za serikali? Una maanisha nini unaposema, "kwa nini iwe jukumu la serikali wakati makanisa yalipewa hizo hela kuboresha huduma"?
 
Mkandala uliwahi kulalamika kuhusu jukwaa la siasa,....
Kwa muda nimekuwa nikifuatilia mada za hapa jukwaani inaonyesha wazi kwamba jukwaa hili linapungua nguvu zake za hoja na kuwa jukwaa la Majitaka na unafiki..Watu wengi sana waliokuwa wakichangia jukwaa hili zamani, nawaona wakiondoka mmoja baada ya mwingne taratibu tunapoteza vichwa muhimu sana ktk jukwaa hili - Kulikoni?

Hivi kweli ndio tumeishiwa au JF imebadilisha kabisa mwelekeo na kuwa kambi ya wasema ovyo, matusi na kusodoana.. Je, hii yote inatokana na maisha magumu au kitu gani?..Mimi sielewi.

Leo katika mada tofauti kabisa,isiyo husisha mambo ya dini wala udini,ukiwa mchangiaji
wa kwanza katika thread hii ukaanza kwa kusema:-

Ikiwa serikali inatoa billioni 90 kila mwaka kwa kanisa mlitegemea itapata fedha wapi zaidi za kuboresha Hospital zake..

Now,unabisha kwamba hujaongelea udini na wewe ndio ume chafua topic kabisa tofauti na
hoja uliyo itoa jukwaa la ulalamikaji kuhusu kuyumba kwa Jukwaa la siasa.

Wapi nimesema fedha zimejenga makanisa na mihadhara!... jamani huu ukumbi siku hizi vipi?..
Na kama ulivyosema ndivyo, sasa kwa nini madaktari wamegoma?.. kwa nini iwe jukumu la serikali ikiwa fedha hizo walipewa makanisa kuboresha huduma hizo..Wewe unajua hiyo kamati ya CSSC walizitumia vipi fedha hizo? na kwa nini usitake wakupe mahesabu lakini akisema Mkandara tayari ni Udini wakati hata wewe unaweza kuuliza?..


Kwanini tusiamini kwamba Una ID nyingi ambazo unatumia kueneza chuki za kidini humu
na ID nyingine una jidai mtakatifu?
 
Nionyeshe nakala hata moja inayosema serikali ilishindwa kujenga Hospitali maana haya maneno nayasoma hapa hapa JF tu.. Ni lini na waziri au rais gani alitangaza uwezo mdogo wa serikali kujenga Hospital wilayani hivyo kulitaka kanisa lifanye hivyo..kumwona Daktari unalipa Ths 40,000 hadi 50 unaona sii ghali?

Hauhitaji nakala yoyote ile.
Unacho hitaji ni kuonesha hospitali zilizojengwa na serikali
na zinatoa huduma bora ili ku-prove kwamba hospitali za ki kristo hazina umuhimu kiasi
hicho.
 
Aliyeweka roho zetu rehani wala si Madaktari wetu.

Wenye kufanya hivo ni watunga sera zetu hapo sekta ya afya, ukaidi wa Blandina Nyoni na kujiona Katibu Mkuu wa kwanza na wa mwisho Tanzania hii.

Nasema wenye kuweka roho zetu rehani ni Mizengo Peter Pinda anayeinuia kuwaongeza wabunge posho za kufa mtu licha ya sisi walipakodi kugomea jambo hili.

Ndio, nasema Waziri Mkuu anaonyesha kila dalili ya KWENDA KINYUME na matakwa ya umma huku akiendelea kuwuzia kiswahili kirefu Madaktari wetu huku asijue kwamba waalimu na University Lecturers naao wako njiani na madai mazito zaidi miezi si mingi sana.

Tunamtakia Mhe Pinda kheri katika hatua yake hiyo huku tukimsubiri njia panda tukamalizane cash cash juu ya huo ukaidi wa maoni ya umma wa nchi hii.

mm naisubiri hii ya walimu hata kesho mkuu.
Tatizo CWT wamekua watu wa porojo sana. Itafika wakati nitaamua kudai haki zangu mwenyewe bila kupitia CWT.
 
Mkandala uliwahi kulalamika kuhusu jukwaa la siasa,....


Leo katika mada tofauti kabisa,isiyo husisha mambo ya dini wala udini,ukiwa mchangiaji
wa kwanza katika thread hii ukaanza kwa kusema:-



Now,unabisha kwamba hujaongelea udini na wewe ndio ume chafua topic kabisa tofauti na
hoja uliyo itoa jukwaa la ulalamikaji kuhusu kuyumba kwa Jukwaa la siasa.




Kwanini tusiamini kwamba Una ID nyingi ambazo unatumia kueneza chuki za kidini humu
na ID nyingine una jidai mtakatifu?

Sasa mkuu nimekuelewa, naungana na wewe kwa 100% inawezekana kabisa watu wenye tabia hizi za kuwa na ID maalum kwa ajili ya uchochezi huwa wanajisahau kama yupo online kwa ID nyingine ambayo watu wanaifahamu kwa ya member mwenye upeo mkubwa, ndio maana akichangia pumba ni lazima ujiulize huyu kulikoni? kudos!
 
Mimi ni mmoja ya watu nisiyeunga mkono MGOMO wa madaktari.
Nakubaliana kwamba madai yao ni ya msingi sana na serikali ndio kiini cha yote na inatakiwa iyashughulie haraka sana. watu wamekuwa wanaunga mkono kwa ushabiki tu na sio kwa kuangalia uhalisia na uzito wa jambo, hv utajisikia mama yako au baba yako akifa kisa mgomo wa madaktari?

ushauri wangu:
Km kweli sisi wananchi tunaumizwa na madai ya madaktari inatakiwa sisi ambao ni wazima tufanye maandamano nchi nzima kushinikiza serikali iwatatulie madai yao huku wao wakiwa wanaendelea na matibabu. lakini swala la kukaa na kutafuta nani mwenye makosa au wa kumkomoa kati ya serikali na madaktari tujue tunachekelea vifo vya wajawazito, vikongwe, wagonjwa wa moyo etc. Tuache ubinafsi na ushabiki usio na maana juu ya swala muhimu la afya zetu. sidhani km muda huu ukipata ajali mbaya na ukapelekwa ICU utaendelea kuchekelea mgomo wa madaktari. wengi mnachekelea kwa kuwa ni wazima wa afya.\

nawasilisha

Wewe goto,maendeleo au mabadiliko lazima yaje na maumivu,so kama wewe unatibiwa apolo poa,ila madoctor ni sahihi kugoma tumechoka na huu utawala wa kisanii,leo ukienda nje kujitambulisha kama mtz unao aibu,tunadharaulika sana
 
huyu ni Mkandara kweli!!?? this is too low kwa level yako, hivi hapa tunaweza kukutofautisha na Maralia Sugu? kwa hiyo solution ya matatizo haya ni kuwa na Mahakama ya kadhi na tujiunge na OIC?
Nilijua tuu,mstari wa Mkandara kuna mtu utamgusa moyoni. Kheri useme kweli upate lawama,kuliko kusema uongo upate sifa...
 
Mimi ni mmoja ya watu nisiyeunga mkono MGOMO wa madaktari.
Labda useme kwamba, wewe Gwota, huungi mkono MGOMO wa aina yoyote ile na sio ule wa madaktari peke yao, hapo labda nitaweza kukuelewa.
Nakubaliana kwamba madai yao ni ya msingi sana na serikali ndio kiini cha yote na inatakiwa iyashughulie haraka sana.
Hii si kweli, ni unafiki. Huwezi kusema unaunga mkono madai yao halafu hapo hapo unapinga hatua yao ya kuchukua the only option ambayo ina nafasi ya angalau kuwapatia ufumbuzi kwani ni the most effective.
watu wamekuwa wanaunga mkono kwa ushabiki tu na sio kwa kuangalia uhalisia na uzito wa jambo, hv utajisikia mama yako au baba yako akifa kisa mgomo wa madaktari?
Sasa hapa wewe ndiye unaleta ushabiki wa kipuuzi labda kwa kuwa wewe huyo mama yako hata unao uwezo wa kumfikisha hospitalini au nje ya nchi akatibiwe. Watanzania wangapi wanakufa kila siku bila hata hiyo huduma? Asilimia ngapi ya Watanzania hawataona tofauti yoyote madaktari wagome wasigome. You cant make an omelette without breaking some eggs!
ushauri wangu:
Km kweli sisi wananchi tunaumizwa na madai ya madaktari inatakiwa sisi ambao ni wazima tufanye maandamano nchi nzima kushinikiza serikali iwatatulie madai yao huku wao wakiwa wanaendelea na matibabu.
Hapa ndipo unapoturudisha kule kule ulikoanzia, je unajua ripple effect ya mgomo wowote ule. Hao madaktari watafanyaje kazi kama hawawezi kufika hospitalini kwa sababu wanaotoa huduma ya usafiri wamegoma, watatoaje huduma kwa wagonjwa kama watu wa utilities (maji, umeme n.k.) nao watagoma...
au wa kumkomoa kati ya serikali na madaktari tujue tunachekelea vifo vya wajawazito, vikongwe, wagonjwa wa moyo etc.
Anayechekelea hivyo vifo unavyovitaja ni serikali na si wananchi, serikali ambayo kiongozi wake mkuu anaenda kutalii huku wananchi wake wanakufa - hizo milioni 300 wanazochoma kila leo huko majuu zingeweza kabisa kuwapunguzia makali ya maisha madaktari na wakaendelea kutoa huduma japo kwa shida.
Tuache ubinafsi na ushabiki usio na maana juu ya swala muhimu la afya zetu. sidhani km muda huu ukipata ajali mbaya na ukapelekwa ICU utaendelea kuchekelea mgomo wa madaktari.
Hivi unajua waziri akipata ajali mbaya hapelekwi ICU Muhimbili, anakimbizwa India...! Anayekupeleka Muhimbili ama hajali sana hata ukipoteza maisha kwani kama wanavyodai madaktari, huko kuna ukosefu mkubwa wa vifaa na dawa. Ni asilimia ngapi ya wanaopata ajali hufa kama mbwa kwa sababu hata hiyo zahanati wanaisikia tu!
wengi mnachekelea kwa kuwa ni wazima wa afya.\
Hapa ndugu yangu umechemsha na kweli akutukanaye hakuchagulii tusi, asante kwa ujasiri wako. Ukweli ni kuwa wananchi wengi kila wakiamka salama asubuhi wanamshukuru Mungu, kwani wanajua fika jinsi utoaji wa huduma mahospitalini ulivyo duni na hapa hakuna wa kulaumiwa bali serikali.
 
Hivi ina make sense kuona wabunge wanaongezwa posho mpaka Tsh. 200,000 kwa siku na wakati huo huo serikali inashindwa kuwalipa madaktari madai yao? Kweli hii serikali ni ya kipuuzi kabisa!! JK na Pinda wakiugua na familia zao wanapelekwa India ndio maana hawajali, walalahoi ndio tutazidi kufa!! Wanaotakiwa kuanzia maandamano ni Tucta ingawa hata vyama vya siasa na wanaharakati wengine inabidi wajitokeze kuunga mkono kwa sababu ni suala la kitaifa lisilojali itikadi, chama wala dini!!
 
Kwahiyo unapendekeza waislamu wanyang'anywe yale majengo ya morogoro ambayo ndio Muslim University? hivi pesa za EPA, RADA, Ndege ya Rahisi, Meremeta, Kiwira, Richmond/ Dowans haya madudu yote yanasababishwa na kanisa?
Hivi hata wewe umeingia kwenye mkumbo wa kuleta soga za kwenye kahawa? hivi hata Petrol inayopitia Bandari ya Dar es salaam kwenda Rwanda inauzwa bei ya chini kuliko Tanzania hivi bado hujui tatizo ni nini? pole sana unazeeka vibaya mno.
Tatizo la mtz ukimuambia ukweli ananuna...pole sana.
 
Well kuanzia sasa hivi Mkandara siye yule umjuaye tena. Mimi nalilia maslahi ya wananchi na sio ya Kanisa wala Msikiti. Tunalipa kodi zetu sasa wanagoma ili iweje kama sio tufe sisi, wakati wameshakatiwa fungu na serikali. nani anayepanga matumizi ya uendeshaji biashara zao kama sio kamati ya CSSC. Na hata wangekuwa Bakwata ningewashambulia kama navyofanya hapa maadam nachokitazama ni maslahi ya wananchi sio dini wala dhehebu.

Kama madaktari wanataka kugoma waanze na kwenda ktk menejimenti zao kujua kulikoni. Tena tunatakiwa kabisa kudai CSSC watupe matumizi ya ruzuku zetu maana mkuu wangu hata wewe Mkristu unalipia fedha hizi ktk kodi na bado unatozwa kumwona daktari. Hakuna nafuu kwako wewe wala mimi sote tunaumizwa, hivyo unapolifanya swala hili liwe la Udini ndipo napowashangaa wakati linakuumiza hata wewe. Hawa ni watu tu binadamu kama wewe mnawaogopa kitu gani?... kwa sababu viongozi wa dini!... Upuuzi mtupu ndio maana CCM itatawala milele kwa kuwagawa.

Ukweli ni kuwa pamoja na hiyo ruzuku ndogo ya serkali ni ghali sana kuendesha hospitali na kutoa huduma kwa viwango vinvyotolewa. Kama watu wangelipia gharama zote basi ingekuwa ni mara mbilli ya bei za sasa. Hiyo ziada ni sadaka zinazotoka huko makanisani msikotaka kusikia. Baniani mbaya kiatu chake dawa. Kama unataka kupinga kutolewa kwa ruzuku kwa hospitali za kanisa kwanza zigomeeni kwenda huko kisha dai wasipewe ruzuku. Wewe mwenyewe unajua wanatoa huduma bora ndiyo maana masheikh wote wanakimbilia huko!!!!!
 
Back
Top Bottom