Nawashangaa Sana wanawake wanaojiuza

Nawashangaa Sana wanawake wanaojiuza

Ugumu na dhiki za maisha si kigezo cha mtu kufanya uhalifu.
Wizi, udokozi, ukibaka, umalaya, ukahaba ni ishu ya tabia ( roho ).
Ukimpa kibaka au malaya milioni 20 mpe miezi miwili tu hata buku hana.
Pana watu wana maisha magumu kuliko hao na wanakaza hadi wanatoboa.
Point nzuri, maana ukiangalia wapo wenye shida na hawajiuzi, ni tabia inayotokana na malezi mabovu pia roho chafu
 
Kudadeki ivi unawazaga nini tajir yangu
Inagawa anachosema sio kweli! Dhambi ya Kwanza ya Binadamu ni kiburi tunda alilokula eve na kumgawia Adam ilikua ni kiburi (kukataa agizo la Mungu) ukisoma biblia dhambi ya Adam na Hawa inakuja Baada ya Mungu kuwa ameshawapa Maagizo ya kuzaa na kuujaza ulimwengu pamoja na kuvitiisha viumbe vyote!

Baada ya ukaidi na kiburi wakajikuta naked ndio Mungu anawalaani mwanamke atazaa kwa uchungu na mwanaume atatfuta kwa jasho na nyoka atapondwa kichwa kwa kisigino!
Kwa maana Hiyo yumkini wasigekaidi Maagizo ya Mungu mwanamke asingezaa kwa uchungu na Wala masela tusingekua tunatuma na ya kutolea na uadui Kati ya huyo mwanamke na nyoka usingewekwa!
Asomaye na aelewe
 
Sahihi a ndio maana wasichana wengi wamejikuta wakiwa na tamaa sana ya mali na mwisho kuzalishwa hovyo na kuona kama Ndoa na mapenzi ni kitu kibaya.

Wanaone wenzao wakiwa na maisha mazuri kwa vivuli vya ujasiriamali n.k
Na ndo chanzo cha single mothers
 
Penda hela kwa sababu hela ndo zinaendesha maisha yetu.

Lakini ubinadamu usikutoke , kwamba hela ndo kila kitu chako cha kwanza, bila kujali kuna uhai na maisha ya watu wengi.

Usiziabudu maana ukiziabudu unaweza kufanya kitu chochote kile.

Kwahiyo mimi nawaasa pendeni hela kwasababu zinarun maisha yetu lakini tuwe na mipaka kwenye kuzitafuta na namna tunavyotaka zituendeshee maisha yetu.

Tukumbuke kuna kesho yake ...
Tamaa mbele mauti nyuma...
Umemaliza mkuu
 
Back
Top Bottom