Nawahurumia sana viumbe hai ninapowakuta kwenye matatizo

We saidia tu sababu kila mtu ana jambo lake ambalo likiwekwa wazi au ukifikiria kwann anafanya unaona ni tatizo tu la akili.

kuna wanaozungumza na watu wasioonekana,

kuna ambaye akiona kioo anaanza kufanya vituko,

kuna wanaojirikodi wakiimba huku wanabinua mdomo,

kuna wanaorikodi dashbord ya gari ikiwa na mziki na kuweka status huku kila saa akiview wangapi wameona dashbord n.k n.k
 
We saidia tu sababu kila mtu ana jambo lake ambalo likiwekwa wazi au ukifikiria kwann anafanya unaona ni tatizo tu la akili.

kuna wanaozungumza na watu wasioonekana,

kuna ambaye akiona kioo anaanza kufanya vituko,

kuna wanaojirikodi wakiimba huku wanabinua mdomo,

kuna wanaorikodi dashbord ya gari ikiwa na mziki na kuweka status huku kila saa akiview wangapi wameona dashbord n.k n.k
Kuzungumza na watu wasioonekana imenitokea sana!!usikariri
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Kuzungumza na watu wasioonekana imenitokea sana!!usikariri
Hilo ni jambo lako mm nilikariri la nn?

Mm nimesema kila mtu na jambo lake ambalo kwa mwingine ukilifikiria analiona kama tatizo la afya ya akili.

Kama huwa unazungumza na wasio onekana endelea tu na vikao vyenu.
 
Hii dunia ina mambo ya ajabu sana. Mfano mimi ni baba zima na midevu yangu na nina mke na watoto, ila naogopa KUKU balaa..! Yaani nipo radhi nipambane na simba, chui, nyati, dubu nk lakini KUKU nikimuona tu miguu inagongana yaani naishiwa nguvu kabisa siwezi kumsogelea wala kumshika na akinifata natoka nduki kali..!
wangu umepitiliza, siku moja niko na mamdii wangu tuko njiani taratibu tunaelekea mahali, mara paap konokono mbele yangu anajikongoja taratibu kuelekea upande wa pili. Nlichofanya nilizuga naokota kitu, kumbe namuokota konokono ili asikanyagwe na shubaamiti bodaboda. Nikimaliza hilo zoezi nahisi kama vile nimeokoa dunia 😂
 
Endelea kuishi hivyo mkuu siyo kila mtu hupenda vitu vinavyomzunguka
Ninaimani tulipewa akili ya kuvitawala viumbe vya ardhini na majini wala siyo nguvu ya kuviangamiza
 
kuongea na wasionekana inakuwa vipi
Unakuta tu Kuna sauti inakuja inakuongelesha, mnaongea , sauti unaisikia lakini huoni mtu mara nyingi ni mizimu ya kwenu huko!
Unaweza kuagizwa ufanye hivi au vile!!
 
Hivyo ndivyo wanadamu tunapaswa kuwa......bahati mbaya tunaishi katika Dunia iliyojaa unyama mpaka WEMA unaonekana jambo la ajabu sana..........

Ulimwengu tulionao waungwana na wema hawapendwi bali wanatumiwa na wanaojua kuyatumia hayo madhaifu hayo.......ndio maana nyakati hizi watu WEMA wanaonekana wajinga na wasiojielewa na watu wabaya wanaonekana wajanja........

Ukiokota mali ya mtu ukamtafuta mwenyewe utaonekana boya hata Kwa mkeo au mumeo lakini ukiificha utaonekana mjanja.,......
 
Pamoja na moyo wote huo, ukiulizwa umesomea nini si ajabu umesomea ufundi redio...

Nenda kasomee mambo ya wanyama Mweka, uwe hata zoo keeper...
 
Mm mpaka wanangu nimeshawakataza km mdudu hana madhara kwako kwa nn umuue maana waswahili tuna ujinga mwingi sana wadudu wana mishe zao ww unaenda kuwakanyaga ama kuwaua bila sababu maalumu huu mm hua naona ni ukatili
 
Habari wanajamvi,

Nina hali ambayo sijui niiterm kama tatizo au ya kufurahisha.

Ninajikuta navionea huruma sana viumbe hivi visivyokuwa na hatia wanyama, ndege na wadudu wa aina zote (kufugwa na wasiofugwa), ninapokutana navyo vikiwa kwenye hali yoyote itakayohatarisha uhai wao.
Nikupe scenarios ninazokutana nazo au ambazo nimewakuta hawa viumbe nikajikuta nawasaidia bila kujali aina ya kiumbe.

1: Kuwasaidia kuvuka barabara/njia. Vinyonga na konokono nikikutana nao anajitahaidi kuvuka njia kuelekea upande wa pili, najikuta nasimama na kuwasaidia kuvuka kwa kuwabeba kwa kijiti au kushika na mikono yangu. Nafanya hivyo coz najua mpita njia/boda zitakanyaga na kuwau.

2: Mende, nzi, mbu na wadudu wengine warukao nawanasua wanapokuwa wamenasa kwenye maji au kushindwa kuruka. Niliwahi ishi mabibo, choo kilikuwa na mende wengi hivyo nikikuta wale wanaoshindwa kutembea nakuwa na kazi ya kuwabinua na kuwanasua ili watembee. Nzi nkiwaona wamenasa kwenye ndoo za maji nawatoa na kuwaacha waende zao. Siui mbu wa mchana.

3: Mbwa, paka nanwanyama wengine wadogo wanaofanana na hao. Nikiwa nimepanda boda au daladala mwenye akili mbovu waopenda kugonga hawa viumbe huwa nahamaki kwa kelele huku nmeshika kende zangu nkiamini hatagogwa. Asipogongwa nafurahi sana, mimi ni introvert lkn kwa hilo huwa nakuwa mkali gafla. Inapotokea nkaona mbwa au paka kafa njiani kwa kugongwa ninaumia sana.

4: Nkikuta kuku na vifaranga wake wako barabarani nawafukuza ili wasigongwe.

5: Ni mfugaji mzuri, changamoto inapokuja kwenye kuuza naumia moyoni sana. Sichinji kuku....lkn nyama nakula

6: Nyoka na wadudu hatari, nikiitwa niue endapo kakutwa kwenye mazingira ya watu nitawazuga na kumtengenezea mazingira mpk nyoka akimbie.

Hali ya kutaka kusaidia hutokea gafla sana akilini, kiasi kwamba siangalii niko mazingira gani na kiumbe huyo ana hatari gani kwangu.

Kwa sehemu ninaposhindwa either nmekuta kafa au hali hairuhusu kumsaidia naumia sana. Najikuta najiuliza ni tatizo la akili au lkn nakumbuka mwenye tatizo la akili hawezi jitambua kama ana tatizo

Ni jambo jema na Huna shida, ila jifunze kwamba huwezi control mazingira yote, kaa kwenye eneo lako la ubinadam na binadam wenzako.
 
Pamoja na moyo wote huo, ukiulizwa umesomea nini si ajabu umesomea ufundi redio...

Nenda kasomee mambo ya wanyama Mweka, uwe hata zoo keeper...
kama ulijua vile, lakini bado sijachelewa kurudi kwenye lane yangu
 
Back
Top Bottom