Sitaki kuamini kuwa aliyetuumba alituumba ili tumuabudu, bali alikuwa na malengo mengine na inawezekana viumbe hai wote kwake ni mifugo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,015
144,372
Mtanisamehe kwa mada hii inayoweza kuleta ukakasi ila hili ni Jukwaa huru.

Tumekuwa tukiambiwa kuwa alietuweka hapa duniani alifanya hivyo ili tumuabudu. Binafsi hili swala kwangu linanifanya nikjiule maswali mengi sana;

1. Yaani alijichosa kisa tu kuabudiwa?
Na kama ni kweli ili tumuabudui, basi ni wazi ananufaika na sisi kumuabudu na hapa hoja yangu sisi viumbe hai kuwa kama mifugo kwake inapopata nguvu nyingine.

2.Kama alituumba ili kumuabudu, vipi kuhusu wanyama ambao wala hawatambui uwepo wake?
Hapa naendelea kupata imani kuwa sisi wanadamu na viumbe wengine wote alituumba kwa makusudi fulani na hii dunia ni kama zizi na sisi viumbe hai wote kwake ni mifugo, mifugo inayompa faida fulani.

Pia, ukichunguza, utagundua aliyeuumba huu ulimwengu, aliweka mazingira ya kuhakikisha hakuna siku hii dunia itakuwa na ombwe la viumbe hai, na moja ya mbinu hiyo ni kufanya tendo la ndoa(tendo la kujaamiiani) kuwa ni tendo la burudani(lenye utamu) ili viumbe hai wazaliane.

Hakuishia hapo, bali alihakikisha kila kiumbe hai naturally kinakuwa na upendo na watoto wake na zaidi kila kiumnbe hai naturally kinahakikisha mtoto wake anakuwa salama na anakua mpaka kujitegemea. Hapa lengo ni kuhakikisha kiumbne hai kikizaliwa kikue na kijaze hiii dunia ndio maana hata kuku anaweza kukudonoa unapotishia uhai wa kifaranga chake(this is work of nature).

Jambo lingine ni kuhakikisha hakuna tukio,ugomjwa au jambo lolote linaloweza kuangamiza kabisa uwepo wa vimbe hai hapa duniani.

Hii ni sababu kwanini tangu kuumbwa kwa hii dunia, hakuna ugonjwa uliowahi kutokea na kuangamiza aina yote ya kiumbe hai iwe ni binadamu, wanyama au wadudu. Likitokea gonjwa tishio, mwisho wa siku ama litatoweka au dawa yake kupatikana, na ndio maana akatupa mpaka maarifa ya kujitubu huku hata wanyama nao wakijitibu kwa kula majani na vitu vingine kama dawa,

Kwa kifupi, yako mambo mengi ya kiasili yanayohakikisha viumbe hai wanaendelea kuwepo hapa duniani, na wasitoweke kabisa licha ya species chache kudaiwa na wanasayansi kutoweka au kuwa katika tishio la kutokweka(extinction)

Pia, ukichunguza, utaona kabisa Nature ilishajipanga tangu kuambwa kwa hii dunia kuhakikisha viumbe hai wanaendelea kuwepo hapa duniani katika mazingiora yoyote na zaidi viumbe hai wasiwe wengi kuliko uwezo wa dunia kuwa-accomodate na bila shaka hii ni sababu kwanini viumbe hai wote hufa,

Kewahiyo, hapa conclusion yangu ni kuwa, hii dunia ni kama zizi, na sisi viumbe hai ni mifugo, mifugo ambayo inamnufaisha aliyetuumba kwa namna ambayo sisi hatuelewi kama ambavyo ng'ombe unaemfuga haelewi namna anavyokunufaisha.

Nawasilisha.
 
Mungu akamaliza kuumba mbingu na nchi na vitu vyote siku ya 6,akaona kwamba vyapendeza.

Pointi yako iko hapa mkuu

Siku ya 7 kamfugo kamoja kakamliziwa.
Halafu kama ni kuabudiwa, kwanini ahangaike kuumba wazungu, wachina, waafrika, n.k?

Hakika maswali ni mengi sana.
 
Huwa najisemea, waliotunga vitabu vitakatifu ni moja ya binadamu waliojaliwa akili nyingi sana duniani.

Waliweza kuiteka dunia nzima kuamini vitu ambavyo kiuhalisia ni myths tu. Yaani yeye anataka tu kutukuzwa, kusifiwa na kuabudiwa...come to think of it!!
 
Biblia ni kitabu ambacho mwanadamu amepewa ili amfahamu Mungu,namna alivyo na anavyotenda kazi!.

Shida ni kwamba wanadamu hawataki kuisoma Biblia ambayo imetoa muongozo wa namna ya kuishi,kula,kuvaa,kuoa,kunywa,kuishi na hata kifo wao wanajiendea wenyewe kwa akili zao!.

Hapo ndipo tatizo lilipo!

Mtu anauliza maswali ambayo Biblia inayo majibu,halafu anataka majibu kwa watu walewale ambao hawaelewi chochote kuhusu Mungu!
 
Sijaona haja ya msingi hapo zaidi zaidi unajipeleka mwenyewe kwenye Maandiko yaan Biblia na misaafu.

Ukizungumza uumbaji au unaposema alituumba ili tuwe mifugo,Kumbuka mifugo inachinjwa na kuliwa kama kitoweo kama dhana ndio hiyo Mungu angekua anachinja wanadamu na kuwala kama kitoweo huku akifurahia na malaika wake.


Ukienda mbali zaidi utagundua Mungu alituumba tuvitawale viumbe vyote na sisi (Wanadamu) tumuabudu yeye,

Ndio maana katika maandiko kuna sehem Mungu alituagiza kuchinja wanyama kama sadaka.

Kama hoja nikuzaliana wako wapi Dinosaur? Je mfugaji yuko tayari mifugo yake ipotee?

Hakika Mungu yupo na anatutizama
 
Dhumuni la Kuumbwa binadamu sio Kumuabudu Muumba maana Muumba hana haja na ibada zako mwanadamu,

Dhumuni kubwa la mtu kuumbwa ni kurestore idadi ya malaika wasariti waliopunguzwa wakiwa pamoja na shetan.

Ndiomaana Amri kuu aliyoamrishwa Kiumbe wa kwanza(Mtu) ambaye wazungu wanamuita Adamu, aliambiwa AKAZAE NA KUIJAZA DUNIA WHY? sababu kuu ni kurudisha idadi ama kujazia nafasi iliyotolewa na hao malaika wasaliti, mnatakiwa kujua kuwa binadamu naye ni malaika wa mwisho kuumbwa kwa Ushirika wa Muumba pale alipoumbwa huyo Adamu ambaye nae anaendeleza uzazi(uumbaji) ndiomaana tunawaita wazazi Mungu wa pili kwakuwa wanashiriki uumbaji wa kibinadamu, uumbaji wa kwanza ni ule wa Muumba alioumba Roho ya Adamu ambayo ndio hii inaendeleza uzazi wa wanadamu dunian kupitia uumbaji wa pili wa kibinadamu wa Miili baada ya tendo la ndoa.

Idadi kamili ya wanadamu itakapojazia ile nafasi iliyotolewa na malaika wasariti basi na ule mwisho ndipo utakapofika, hakuna cha yesu kurudi wala nini, bali idadi maalumu ya binadamu kujazia nafasi aliyoamrishwa adamu kuijaza.


Kinachochelewesha idadi kutimia ni ushenzi wetu wanadamu kuacha njia sahihi za maisha na kukumbatia maovu na imani za kijinga kama dini za wazungu na upumbavu wa utandawazi
 
Dhumuni la Kuumbwa binadamu sio Kumuabudu Muumba maana Muumba hana haja na ibada zako mwanadamu,

Dhumuni kubwa la mtu kuumbwa ni kurestore idadi ya malaika wasariti waliopunguzwa wakiwa pamoja na shetan.

Ndiomaana Amri kuu aliyoamrishwa Kiumbe wa kwanza(Mtu) ambaye wazungu wanamuita Adamu, aliambiwa AKAZAE NA KUIJAZA DUNIA WHY? sababu kuu ni kurudisha idadi ama kujazia nafasi iliyotolewa na hao malaika wasaliti, mnatakiwa kujua kuwa binadamu naye ni malaika wa mwisho kuumbwa kwa Ushirika wa Muumba pale alipoumbwa huyo Adamu ambaye nae anaendeleza uzazi(uumbaji) ndiomaana tunawaita wazazi Mungu wa pili kwakuwa wanashiriki uumbaji wa kibinadamu, uumbaji wa kwanza ni ule wa Muumba alioumba Roho ya Adamu ambayo ndio hii inaendeleza uzazi wa wanadamu dunian kupitia uumbaji wa pili wa kibinadamu wa Miili baada ya tendo la ndoa.

Idadi kamili ya wanadamu itakapojazia ile nafasi iliyotolewa na malaika wasariti basi na ule mwisho ndipo utakapofika, hakuna cha yesu kurudi wala nini, bali idadi maalumu ya binadamu kujazia nafasi aliyoamrishwa adamu kuijaza.


Kinachochelewesha idadi kutimia ni ushenzi wetu wanadamu kuacha njia sahihi za maisha na kukumbatia maovu na imani za kijinga kama dini za wazungu na upumbavu wa utandawazi
Mungu anao uwezo wa kuwaumba hao malaika wa kufanya replacement ya wale waliosaliti.

Swali ni kwa nini hiyo kazi akamuachia Adamu na Eva, wakati anajua Adamu na Eva wangepata changamoto kutoka kwa Malaika Ibilisi?

Yani Mungu aliamua tuu kujichelewesha mwenyewe kwa kumuachia Adamu?

Na kwamba Mungu hakuona kwamba Adamu atapata mtihani kutoka kwa Ibilisi?

Kama ali-anticipate kwa nini alitake hiyo risk?
 
Mtanisamehe kwa mada hii inayoweza kuleta ukakasi ila hili ni Jukwaa huru.

Tumekuwa tukiambiwa kuwa alietuweka hapa duniani alifanya hivyo ili tumuabudu. Binafsi hili swala kwangu linanifanya nikjiule maswali mengi sana;

1. Yaani alijichosa kisa tu kuabudiwa?
Na kama ni kweli ili tumuabudui, basi ni wazi ananufaika na sisi kumuabudu na hapa hoja yangu sisi viumbe hai kuwa kama mifugo kwake inapopata nguvu nyingine.

2.Kama alituumba ili kumuabudu, vipi kuhusu wanyama ambao wala hawatambui uwepo wake?
Hapa naendelea kupata imani kuwa sisi wanadamu na viumbe wengine wote alituumba kwa makusudi fulani na hii dunia ni kama zizi na sisi viumbe hai wote kwake ni mifugo, mifugo inayompa faida fulani.

Pia, ukichunguza, utagundua aliyeuumba huu ulimwengu, aliweka mazingira ya kuhakikisha hakuna siku hii dunia itakuwa na ombwe la viumbe hai, na moja ya mbinu hiyo ni kufanya tendo la ndoa(tendo la kujaamiiani) kuwa ni tendo la burudani(lenye utamu) ili viumbe hai wazaliane.

Hakuishia hapo, bali alihakikisha kila kiumbe hai naturally kinakuwa na upendo na watoto wake na zaidi kila kiumnbe hai naturally kinahakikisha mtoto wake anakuwa salama na anakua mpaka kujitegemea. Hapa lengo ni kuhakikisha kiumbne hai kikizaliwa kikue na kijaze hiii dunia ndio maana hata kuku anaweza kukudonoa unapotishia uhai wa kifaranga chake(this is work of nature).

Jambo lingine ni kuhakikisha hakuna tukio,ugomjwa au jambo lolote linaloweza kuangamiza kabisa uwepo wa vimbe hai hapa duniani.

Hii ni sababu kwanini tangu kuumbwa kwa hii dunia, hakuna ugonjwa uliowahi kutokea na kuangamiza aina yote ya kiumbe hai iwe ni binadamu, wanyama au wadudu. Likitokea gonjwa tishio, mwisho wa siku ama litatoweka au dawa yake kupatikana, na ndio maana akatupa mpaka maarifa ya kujitubu huku hata wanyama nao wakijitibu kwa kula majani na vitu vingine kama dawa,

Kwa kifupi, yako mambo mengi ya kiasili yanayohakikisha viumbe hai wanaendelea kuwepo hapa duniani, na wasitoweke kabisa licha ya species chache kudaiwa na wanasayansi kutoweka au kuwa katika tishio la kutokweka(extinction)

Pia, ukichunguza, utaona kabisa Nature ilishajipanga tangu kuambwa kwa hii dunia kuhakikisha viumbe hai wanaendelea kuwepo hapa duniani katika mazingiora yoyote na zaidi viumbe hai wasiwe wengi kuliko uwezo wa dunia kuwa-accomodate na bila shaka hii ni sababu kwanini viumbe hai wote hufa,

Kewahiyo, hapa conclusion yangu ni kuwa, hii dunia ni kama zizi, na sisi viumbe hai ni mifugo, mifugo ambayo inamnufaisha aliyetuumba kwa namna ambayo sisi hatuelewi kama ambavyo ng'ombe unaemfuga haelewi namna anavyokunufaisha.

Nawasilisha.
Umejiuliza na umejijibu bado unauliza majibu uliyonayo. Sasa kama ameweka tendo la kujamiana ni burudan ili tuendelee kuwepo naturally kwanini hiyo kumuabudu usiamini nayo imewekwa naturally ili tuweze kuwa nae karibu kushiriki baraka zake.
 
Mtanisamehe kwa mada hii inayoweza kuleta ukakasi ila hili ni Jukwaa huru.

Tumekuwa tukiambiwa kuwa alietuweka hapa duniani alifanya hivyo ili tumuabudu. Binafsi hili swala kwangu linanifanya nikjiule maswali mengi sana;

1. Yaani alijichosa kisa tu kuabudiwa?
Na kama ni kweli ili tumuabudui, basi ni wazi ananufaika na sisi kumuabudu na hapa hoja yangu sisi viumbe hai kuwa kama mifugo kwake inapopata nguvu nyingine.

2.Kama alituumba ili kumuabudu, vipi kuhusu wanyama ambao wala hawatambui uwepo wake?
Hapa naendelea kupata imani kuwa sisi wanadamu na viumbe wengine wote alituumba kwa makusudi fulani na hii dunia ni kama zizi na sisi viumbe hai wote kwake ni mifugo, mifugo inayompa faida fulani.

Pia, ukichunguza, utagundua aliyeuumba huu ulimwengu, aliweka mazingira ya kuhakikisha hakuna siku hii dunia itakuwa na ombwe la viumbe hai, na moja ya mbinu hiyo ni kufanya tendo la ndoa(tendo la kujaamiiani) kuwa ni tendo la burudani(lenye utamu) ili viumbe hai wazaliane.

Hakuishia hapo, bali alihakikisha kila kiumbe hai naturally kinakuwa na upendo na watoto wake na zaidi kila kiumnbe hai naturally kinahakikisha mtoto wake anakuwa salama na anakua mpaka kujitegemea. Hapa lengo ni kuhakikisha kiumbne hai kikizaliwa kikue na kijaze hiii dunia ndio maana hata kuku anaweza kukudonoa unapotishia uhai wa kifaranga chake(this is work of nature).

Jambo lingine ni kuhakikisha hakuna tukio,ugomjwa au jambo lolote linaloweza kuangamiza kabisa uwepo wa vimbe hai hapa duniani.

Hii ni sababu kwanini tangu kuumbwa kwa hii dunia, hakuna ugonjwa uliowahi kutokea na kuangamiza aina yote ya kiumbe hai iwe ni binadamu, wanyama au wadudu. Likitokea gonjwa tishio, mwisho wa siku ama litatoweka au dawa yake kupatikana, na ndio maana akatupa mpaka maarifa ya kujitubu huku hata wanyama nao wakijitibu kwa kula majani na vitu vingine kama dawa,

Kwa kifupi, yako mambo mengi ya kiasili yanayohakikisha viumbe hai wanaendelea kuwepo hapa duniani, na wasitoweke kabisa licha ya species chache kudaiwa na wanasayansi kutoweka au kuwa katika tishio la kutokweka(extinction)

Pia, ukichunguza, utaona kabisa Nature ilishajipanga tangu kuambwa kwa hii dunia kuhakikisha viumbe hai wanaendelea kuwepo hapa duniani katika mazingiora yoyote na zaidi viumbe hai wasiwe wengi kuliko uwezo wa dunia kuwa-accomodate na bila shaka hii ni sababu kwanini viumbe hai wote hufa,

Kewahiyo, hapa conclusion yangu ni kuwa, hii dunia ni kama zizi, na sisi viumbe hai ni mifugo, mifugo ambayo inamnufaisha aliyetuumba kwa namna ambayo sisi hatuelewi kama ambavyo ng'ombe unaemfuga haelewi namna anavyokunufaisha.

Nawasilisha.
Umeshawahi kuwa na watoto halafu hawatambui thamani yako maishani mwao? Ulijisikiaje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom