Mr simple M
JF-Expert Member
- Sep 18, 2020
- 2,066
- 4,280
Keep up as long as u feel passionate doing it
Kuzungumza na watu wasioonekana imenitokea sana!!usikaririWe saidia tu sababu kila mtu ana jambo lake ambalo likiwekwa wazi au ukifikiria kwann anafanya unaona ni tatizo tu la akili.
kuna wanaozungumza na watu wasioonekana,
kuna ambaye akiona kioo anaanza kufanya vituko,
kuna wanaojirikodi wakiimba huku wanabinua mdomo,
kuna wanaorikodi dashbord ya gari ikiwa na mziki na kuweka status huku kila saa akiview wangapi wameona dashbord n.k n.k
Hilo ni jambo lako mm nilikariri la nn?Kuzungumza na watu wasioonekana imenitokea sana!!usikariri
wangu umepitiliza, siku moja niko na mamdii wangu tuko njiani taratibu tunaelekea mahali, mara paap konokono mbele yangu anajikongoja taratibu kuelekea upande wa pili. Nlichofanya nilizuga naokota kitu, kumbe namuokota konokono ili asikanyagwe na shubaamiti bodaboda. Nikimaliza hilo zoezi nahisi kama vile nimeokoa dunia 😂
Unakuta tu Kuna sauti inakuja inakuongelesha, mnaongea , sauti unaisikia lakini huoni mtu mara nyingi ni mizimu ya kwenu huko!kuongea na wasionekana inakuwa vipi
Habari wanajamvi,
Nina hali ambayo sijui niiterm kama tatizo au ya kufurahisha.
Ninajikuta navionea huruma sana viumbe hivi visivyokuwa na hatia wanyama, ndege na wadudu wa aina zote (kufugwa na wasiofugwa), ninapokutana navyo vikiwa kwenye hali yoyote itakayohatarisha uhai wao.
Nikupe scenarios ninazokutana nazo au ambazo nimewakuta hawa viumbe nikajikuta nawasaidia bila kujali aina ya kiumbe.
1: Kuwasaidia kuvuka barabara/njia. Vinyonga na konokono nikikutana nao anajitahaidi kuvuka njia kuelekea upande wa pili, najikuta nasimama na kuwasaidia kuvuka kwa kuwabeba kwa kijiti au kushika na mikono yangu. Nafanya hivyo coz najua mpita njia/boda zitakanyaga na kuwau.
2: Mende, nzi, mbu na wadudu wengine warukao nawanasua wanapokuwa wamenasa kwenye maji au kushindwa kuruka. Niliwahi ishi mabibo, choo kilikuwa na mende wengi hivyo nikikuta wale wanaoshindwa kutembea nakuwa na kazi ya kuwabinua na kuwanasua ili watembee. Nzi nkiwaona wamenasa kwenye ndoo za maji nawatoa na kuwaacha waende zao. Siui mbu wa mchana.
3: Mbwa, paka nanwanyama wengine wadogo wanaofanana na hao. Nikiwa nimepanda boda au daladala mwenye akili mbovu waopenda kugonga hawa viumbe huwa nahamaki kwa kelele huku nmeshika kende zangu nkiamini hatagogwa. Asipogongwa nafurahi sana, mimi ni introvert lkn kwa hilo huwa nakuwa mkali gafla. Inapotokea nkaona mbwa au paka kafa njiani kwa kugongwa ninaumia sana.
4: Nkikuta kuku na vifaranga wake wako barabarani nawafukuza ili wasigongwe.
5: Ni mfugaji mzuri, changamoto inapokuja kwenye kuuza naumia moyoni sana. Sichinji kuku....lkn nyama nakula
6: Nyoka na wadudu hatari, nikiitwa niue endapo kakutwa kwenye mazingira ya watu nitawazuga na kumtengenezea mazingira mpk nyoka akimbie.
Hali ya kutaka kusaidia hutokea gafla sana akilini, kiasi kwamba siangalii niko mazingira gani na kiumbe huyo ana hatari gani kwangu.
Kwa sehemu ninaposhindwa either nmekuta kafa au hali hairuhusu kumsaidia naumia sana. Najikuta najiuliza ni tatizo la akili au lkn nakumbuka mwenye tatizo la akili hawezi jitambua kama ana tatizo