Nauliza tu: Lowassa ana nini jamani?

Nauliza tu: Lowassa ana nini jamani?

Wanajamvi wenzangu humu ndani kumezuka tabia ambayoa hata kichaa anaweza kutushangaa,ikitokea amefariki mwanasiasa fulan ambaye hayuko upande wa lowassa utasikia watu wa viroba wanakuja na kebehi eti alimtukana lowassa,upuuzi mkubwa sana huu,bila evidence ya kutuonesha kua kweli alitukanwa,lakini hata hivyo lowasa ni nani asitukanwe?asisemwe?tuache kazi za MUNGU ziendelee,mambo ya kuhusisha kifo cha mtu na sababu za kijinga tuache ni dhambi.

Note:nipo kagera kwenye kuwafariji waliotapeliwa,sitaki mabishano.
Umenifurahisha jinsi ulivyomalizia
 
Lowasa:Nimwiteje Tena Ila Nieleweke?
Wale Waliompondea na Kumchulia Kifo Mwaka Jana na Uko Nyuma,Ubaya Wao Umewarudia!
Walimtukana na Kumchafua Lowasa,Wakidhani Watamuua Kisiasa,ila Sasa Imekuwa Kinyume!
Wakati Lowasa Akiwa Kimya,Kila Tukio Linalousiana na Vifo,Sherehe au Matukio ya Kisiasa ni Lazima Jina la Lowasa Litajwe!
Wale Wote Waliomtukana Hadharani Mwaka Jana,Wamebaki Kulialia Gizani!
LOWASA:NADHARIA YA KIUNGU ILIYO NA UWEZO WA KUUMBA,YENYE KUTOA UHAI NA KIFO!
 
mjukuu wangu wenyewe wanajilinda na kale kasheria kao. mweee bado napenda kuishi na bibi yako.
Bado hakajatungiwa vikanuni babuu. Usitunze sana hekima zako za kale, bora utiririke. Ushauri tu babu ila usiniombe nikusindikize shimo la tewa
 
Mjukuu wangu sasa povu la nini? na wewe kama ni mmojawapo kampigie tu magoti mzee mwenzangu Lowasa atakusamehe ila ukiendelea na ubishi me namwachia Mungu
Mi siwezi kufa sababu ya huyo mungu wako lowassa,iwe mwanzo na mwisho kutisha watu upuuzi wako huu,kufa kwangu ni mipango ya ALLAH,sio huyo mwizi wa nchi hii.
 
Nasikia wote waliomtusia sana Lowassa ni swala la muda tu, 2020 huenda wengi hawata kuwepo.. ni kweli wengi waliomsema vibaya wamekufa, sijui Mungu wa Lowassa ni yupi.. daah inatisha sana
 
Hamjambo wajukuu zangu.

Tangu nimeanza kuwa mtu mzima(18yrs) katika miaka ya 1970s sijawai ona maajabu kama haya yanayotokea sasa katika medani za siasa ya nchi ya viwanda na kutumbua majipu.

Namzungumzia Mhe Edward Ngoyai Lowasa, nguli la siasa tangu enzi za Mwlm JK Nyerere. Edward Lowasa ni mwanasiasa aliyepitia magumu mengi pengine kuliko mwanasiasa yeyote katika siasa za Tanzania. Lowasa aliwahi kuhusishwa na kashfa ya ubadhirifu AICC, Richmond, Jengo la UVCCM na kashfa nyingine nyingi nje ndani ya ccm na serikali ya Tanzania.

Ajabu lenyewe ni hili hapa. Lowasa baada ya kuhama CCM na kugombea urais kupitia UKAWA amekua ni nyota inayong'aa ambayo ina tumaini tele mbele ya watanzania wanyonge. Amekuwa kama Musa aliyewatoa wanawaisrael utumwani Misri kuelekea nchi ya ahadi.

Linalonishangaza zaidi kila aliyeinua/anayeinua kinywa chake na kumnena vibaya mtu huyu maono huwa yanamrudia mwenyewe. Kumbukeni kauli za mawaziri mbalimbali waliomtusi na kukashifu afya mtu huyu lkn wao ndo wamekuwa wa kwanza kuchungulia kaburi. Lakini pia chunguzeni kwa makini matamko yenye utata ya Mhe RC ambaye alitumia muda mwingi kumnanga na kumsimanga Lowasa ndani ya UVCCM. Mhe RC hv sasa ameanza kupoteza mwelekeo kila kauli inayotoka kinywani mwake ina ukakasi dhidi ya wananchi ama watumishi wenzake.

Namuhurumia sana mjukuu wangu wa ACT aliyemtukana Lowasa pale mwembeyanga sijui naye itakuaje tusubiri muda tu.

Babu yenu
Tanaluza
Zee zima linaendekeza imani za kishirikina. Hata aibu huna?
 
Wanajamvi wenzangu humu ndani kumezuka tabia ambayoa hata kichaa anaweza kutushangaa,ikitokea amefariki mwanasiasa fulan ambaye hayuko upande wa lowassa utasikia watu wa viroba wanakuja na kebehi eti alimtukana lowassa,upuuzi mkubwa sana huu,bila evidence ya kutuonesha kua kweli alitukanwa,lakini hata hivyo lowasa ni nani asitukanwe?asisemwe?tuache kazi za MUNGU ziendelee,mambo ya kuhusisha kifo cha mtu na sababu za kijinga tuache ni dhambi.

Note:nipo kagera kwenye kuwafariji waliotapeliwa,sitaki mabishano.
Mzee Lowasa siyo mtakatifu na hakuna mtu anayefuraia kifo cha mwingine ila ukweli utabaki kuwa ukweli kila aliyetumia afya ya Lowasa kwa kumtabiria kifo amekufa yeye na kwa hilo tunatakiwa kuchunga ndimi zetu
 
Lowassa angekuwa Rais wa hii Nchi hivi sasa, tusingekuwa kwenye hali hii ilivyo hivi sasa Nchini.
Kweli mkuu. Watu tungekuwa makazini sasa.
Lkn waliongia wana roho ya umaskini na ya kishetani.
Wao kuona mtu anateseka wanafurahia sana.
Awamu hii wamejaa na tamaa sana, wanataka hata hela za wahanga wa majanga
 
Kila amneneae mabaya ndg yake ajue amelaaniwa!!lowasa ni musa jangwan !Ccm Na dola lao ni mafarao,ni mda Tu tusubiri!
 
Wanajamvi wenzangu humu ndani kumezuka tabia ambayoa hata kichaa anaweza kutushangaa,ikitokea amefariki mwanasiasa fulan ambaye hayuko upande wa lowassa utasikia watu wa viroba wanakuja na kebehi eti alimtukana lowassa,upuuzi mkubwa sana huu,bila evidence ya kutuonesha kua kweli alitukanwa,lakini hata hivyo lowasa ni nani asitukanwe?asisemwe?tuache kazi za MUNGU ziendelee,mambo ya kuhusisha kifo cha mtu na sababu za kijinga tuache ni dhambi.

Note:nipo kagera kwenye kuwafariji waliotapeliwa,sitaki mabishano.

Tukusaidieje?
 
Back
Top Bottom