Nauli Feri: Mnyika, Hata Wewe?

Nauli Feri: Mnyika, Hata Wewe?

Tuachane na mambo ya kuombana misamaa au wabunge wamesema nini, Twende kwenye gate collection mara baada ya kupandisha nauli. Mwanzo walisema wanapata M9 kwa siku na mara baada ya kupandisha nauli kwa 100% sasa wanapata takribani 18M. lakini wadau tukumbuke magari maguta na bajaji zimepanda zaidi ya mara mbili, so sitegemei gate collection kupanda mara mbili ya zamani. kimsingi sipingi ongezeko la nauli wala sipo upande wowote kati ya wabunge na Magufuri ila kilio changu ni jinsi tunavyoibiwa na hawa jamaa
 
Hapa ndio mnapokosea....Magufuli alitoa kauli ile baada ya kuzomewa! hakuna anayesema wananchi waombe msamaha kwa kuzomea.......
Umeona mbali yaani wananchi wana haki ya kumvunjia waziri heshima ila wao ndio waheshimiwe,hakuna haja ya kuomba msamaha aliyetuambia atanunua ndege hata kama wananchi watakula majani alishawahi omba msamaha?wapi na lipi?Magufuri fanya kazi ww ndio kioo cha mawazir wote wa Jk,lakusimamia madaraja yaliyoharibiwa wakat wa mafuriko hawalioni wanaliona la feri tu watu wa dar acheni Mtemvu acha unafiki,mi siamini kama wazaramo wana jina linaloanzia na mtemvu
 
So, unadhani kwa wananchi wa Kigamboni ni fair kabisa kuchangishwa nauli kusaidia usafiri wa watu wa Bagamoyo? Kwa nini wasichangishwe hizo nauli ziwajengee daraja ili kuepukana na kero ya usafiri? Which fair: Wananchi wa Kigamboni kuchangishwa ili kununua kivuko cha watu wa Bagamoyo au kuchangishwa ili kujengewa daraja na kuachana na karaa za pantoni?

Hivi ni kwa nini tunafikiri tu kuwa wanaotumia kivuko kile ni wakaazi wa Kigamboni peke yao? kuna vitega uchumi pale, na kuna watu wanaofanya kazi sehemu nyingine ya mji wakiishi kule, na kuna wanaoishi sehemu za mbali kama Tegeta wakifanya kazi pale kwenye hoteli za kitalii. Na kuna wawekezaji ambao si wa kipato cha chini, na kuna watalii pia ambao wanatumia kivuko kile. Kwa hiyo kujilazimisha kufikiria kuwa kivuko kinawasaidia wakazi wa Kigamboni peke yao si jambo la maana sana, hata kama kuna ukweli kuwa wao wanaweza kuwa wengi.

Kabla ya kupandishwa nauli, mapato toka vivuko vingine yalukuwa yanatumika kutoa ruzuku kwa kivuko cha Kigamboni, ndiyo maana hata mapato yao yanaweza kutumiwa kuendeleza sehemu nyingine pia.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mchambuzi,
Ahsante kwa mada 'serious' na sio sensitive kama ulivyosema. Wakati mjadala ukipamba moto naomba niweke kumbu kumbu sawa kwasababu kuna mambo tunayasahau au kuyafumbia macho.

1. Hoja ya awali ya mbunge wa Kigamboni ilikuwa kueleza kuwa magufuli hakufuata taratibu kupandisha nauli na kwamba hilo ni jukumu la SUMATRA. Hoja haikuwa kiwango bali utaratibu.

2. Magufuli amenukuliwa na gazeti moja akisema dhumuni hasa ni kukusanya pesa ili ziweze kununua boti itakayohudumia Bagamoyo na Dar kupunguza msongamano. Hajasema kuna tatizo kivukoni bali ana 'source' vyanzo vingine kwa ajili ya Bagamoyo

3.Hakuna anayejua pesa za maegesho za Kingunge zilitumika kuhudumia nini hadi leo, watu walilipa.
Ubungo terminal bado tunalipa tukiingia bila ruzuku

4. Tunatumia usafiri wa dala dala usio na ruzuku ya serikalini. UDA ilikuwa na ruzuku kama shirika la umma.
Kwahiyo mkazi wa mbagala anayefanya kazi ubungo hana ruzuku ya usafiri kama mkazi wa kigamboni anayefanya kazi Ilala,Temeke,Kinondoni

5. Tulikubali bilioni 100 alipwe mtu, hatukuona mshikamano wa wabunge kimkoa au kitaifa.

6. Ongezeko la posho za wabunge katika malaki ni asilimia 200. Ongezeko la nauli za feri katika mia ni asilimia 100.
Ikumbukwe 'charity begins at home'. Hatujaona mshikamano wa wabunge kwenye posho

7. Kuna vivuko vingine nchini vina nauli kubwa kuliko ya feri Kigamboni.
 
It doesn't matter whether is doing business or delivering services. A responsible government should gradually increase the price of its services to equate it to the economic cost of running them. A gradual increase in prices to allows the consumers to adjust to the changes and also provide time for consumers to find alternatives. Siyo unakaa miaka 14 kimya, halafu unapandisha bei ghafla bila hata transparency and effective participation. Au kwa vile wananchi wa Kigamboni wana limited alternatives za usafiri ndio wabambikiwe nauli mpya ghafla?

EMT
What a crap! The government should have done long time a go but politics was to blame; the minister was very clear on whole issue let face the reality, what about other Tanzanians who pays more; and they don`t have other alternatives at least Kigamboni residents have choices to make; 100% increase does not mean anything, Kigamboni residents have enjoyed free ride for a while so let them pay; same as Pangani residents, favors has to go for good!

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Kwa nini tuna-avoid maswali magumu? Comparison yako ya kutopandisha nauli kwa miaka 14 na kutojenga daraja kwa miaka hamsimi naona kama ni absurd. Hapa serikali ilikuwa na uwezo wa kupandisha nauli kulingana na gharama za uendeshaji lakini haikufanya hivyo kwa muda wa miaka 14.
Hapana mkuu sio absurd hata kidogo ikiwa umenielewa nadhani wewe umechukulia hivyo..

Maana yangu kimtazamo, Serikali ilikuwa na uwezo wa kujenga daraja miaka 50 iliyopita ukitaka kutazama sababu unazotumia, Hadi leo wamenunua Pantoni ngani, gharama zilitupata kwa miaka hiyo bora daraja lingejengwa miaka 30 au 20 iliyopita..Haya ni mawazo ya mtu upande wa pili ambaye anajiuliza ana reasonout kama wewe ktk swala hili..Hoja kama hii ina mantiki na sii ya kupuuza lakini hatuwezi ku question mtu anayetaka kujenga daraja leo kwa kutumia sababu WHY NOW?

Magufuli hakuwa waziri wa wizara hii kwa miaka 14 iliyopita..Swali lako ni sawa na lile ya JK alipotembelea wizara ya Magufuli na aliposikia bomoabomoa alimuuliza Magufuli mlikuwa wapi miaka yote mtu anajenga msingi, anapandisha nyumba sasa ndio mnataka kuzibomoa?... Sasa ukifikiria kwa makini halikuwa jukumu la Magufuli miaka 14 iliyopita maana hakuwa waziri wa wizara hiyo wakati watu wanahamia Jangwani ama kujenga vibanda vya maduka hadi barabarani...

Mawaziri waliopita ndio walifanya uzembe, hivyo Magufuli hawezi kuacha kutangaza bomoabomoa kwa sababu uzembe uliisha fanyika toka zamani basi na aache kama ilivyo...na kama swali ni kwa serikali ukimuuliza JK atakwambia he was not President 14 Years ago, hivyo unataka aache vitu kama vilivyo maadam walifanya uzembe.. Hapa huoni kama tunapoteza maadili ya Accountability, kama kila mmoja wetu atauliza kwa msemo huo...

Hivi ndivyo nilivyokuelewa na ndio majibu yangu yanakuja ktk mtiririko huo.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Hivi unafananisha vipi Hiace na Bus? Ni watu wangapi wanavuka Pangani kwa kila trip moja na ni watu wangapi wanavuka Kigamboni? Naamini hiyo 100 kwa Kigamboni ni sawsawa na na hiyo 200 kwa Pangani itakuwa sawa kwa sababu kuna muda hiko cha pangani Kinavuka tupu kwenda upande wa pili kufuata abiria likini hiki cha Kigamboini kikienda ni NYOMI na kiki rudi pia ni NYOMI.

Ukiongea kwa mantiki hiyo unataka Kigamboni walipe tshs 50? Hoja yako ni kwamba kwasababu Kigamboni kinajaza mapato yanayakusanywa ni mengi na yanakidhi gharama za uendeshaji? Ukisema hivyo wananchi wa sehemu ambao walipa zaidi wanaweza kudai kwasababu wao wanapungufu ya shughuli za kiuchumi kitu ambacho serikali imechangia kwa kiasi kikubwa wasifiri bure; hivi labda nikuulize hiyo tsh 200 ina thamani gani sasa hivi? Ukiangalia thamani ya shs ni kama bado wanavuka bure.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Mchambuzi,
Ahsante kwa mada 'serious' na sio sensitive kama ulivyosema. Wakati mjadala ukipamba moto naomba niweke kumbu kumbu sawa kwasababu kuna mambo tunayasahau au kuyafumbia macho.

1. Hoja ya awali ya mbunge wa Kigamboni ilikuwa kueleza kuwa magufuli hakufuata taratibu kupandisha nauli na kwamba hilo ni jukumu la SUMATRA. Hoja haikuwa kiwango bali utaratibu.

2. Magufuli amenukuliwa na gazeti moja akisema dhumuni hasa ni kukusanya pesa ili ziweze kununua boti itakayohudumia Bagamoyo na Dar kupunguza msongamano. Hajasema kuna tatizo kivukoni bali ana 'source' vyanzo vingine kwa ajili ya Bagamoyo

3.Hakuna anayejua pesa za maegesho za Kingunge zilitumika kuhudumia nini hadi leo, watu walilipa.
Ubungo terminal bado tunalipa tukiingia bila ruzuku

4. Tunatumia usafiri wa dala dala usio na ruzuku ya serikalini. UDA ilikuwa na ruzuku kama shirika la umma.
Kwahiyo mkazi wa mbagala anayefanya kazi ubungo hana ruzuku ya usafiri kama mkazi wa kigamboni anayefanya kazi Ilala,Temeke,Kinondoni

5. Tulikubali bilioni 100 alipwe mtu, hatukuona mshikamano wa wabunge kimkoa au kitaifa.

6. Ongezeko la posho za wabunge katika malaki ni asilimia 200. Ongezeko la nauli za feri katika mia ni asilimia 100.
Ikumbukwe 'charity begins at home'. Hatujaona mshikamano wa wabunge kwenye posho

7. Kuna vivuko vingine nchini vina nauli kubwa kuliko ya feri Kigamboni.

1. kwenye GUTA ni Asilimia ngapi?
hilio ndio lina beba Viazi na Maembe kuja huku uswahilini kwetu kutoka kibada.

2. Ni kwa sababu huko hakuna abiria, unakuta kivuko kinavusha watu wawili na gari moja kwa siku , unategemea nini?
 
Ukiongea kwa mantiki hiyo unataka Kigamboni walipe tshs 50? Hoja yako ni kwamba kwasababu Kigamboni kinajaza mapato yanayakusanywa ni mengi na yanakidhi gharama za uendeshaji? Ukisema hivyo wananchi wa sehemu ambao walipa zaidi wanaweza kudai kwasababu wao wanapungufu ya shughuli za kiuchumi kitu ambacho serikali imechangia kwa kiasi kikubwa wasifiri bure; hivi labda nikuulize hiyo tsh 200 ina thamani gani sasa hivi? Ukiangalia thamani ya shs ni kama bado wanavuka bure.

Chama
Gongo la Mboto DSM

NDIO!!
Sasa kwanini tunaongeza nauli? hili ile ipatikane ya kuendesha cha Pangani? Kilombero? au?
Magufuli si alisema kuwa Kigamboni inaendeshwa kwa hasara na ina hudumiwa na vivuko vingine?
huoni kuwa katu danganya?

Thamani ya 200 huioni?
Pople sana ndugu yangu unless wewe ni Fisadi au ni mzee wa Rushwa,
Tajiri yeyote na mtu yeyote anayejali matumizi na bajeti kwa vyovyote 200 ni kubwa sana, just Imagine ni watu wangapi kwa siku wana vuka pale? Ndio maana huwa tunaibiwa sana, Fikiria kampuni ya simu inawateja 5Mil ikiwaibia wateja wake wote kila mmoja ndani ya wiki 200 200, ni shilingi ngapi? Tuache dharahu!!!!
 
Jamani eeeeh, nchi yetu bado ipo ktk utawala wa central Government, mauzo yote yanakusanywa na kisha kugawiwa wizara na idara zake bila kujali nani kachangia ngapi na apewe nafuu gani bali kuna vigezo vyake nahavihusiani kabisa na utengano.

Sasa mnapoanza kugawanya kati ya Kigamboni, Ubungo na Pangani - mara sijui hili ni swala la wakazi wa Kigamboni tu na kadhalika... Hii ni dalili kubwa kuonyesha tumefika wapi ktk Utengano baina yetu...Inaonyesha jinsi sisi wenyewe tulivyo wafinyu wa kufikiria kwamba hili ni swala la wakazi wa Kigamboni na halituhusu wengine kwa nini basi lisaidie wengine!

Tafadhalini sana tulizungumze swala hili kama swala la Kitaifa na kusema kweli binafsi sioni makosa ya Mnyika kulizungumzia maana linamhusu yeye pia..Let's stick to the point ya upandaji wa nauli za Pantoni na sii kutazama nje ya hoja hiyo maana tunaharibu...tuwe na uvumilivu wakati tunamsubiri Mnyika.
 
Mkuu vivuko vingi hapa nchini vimenunuliwa kwa mkopo toka World Bank. Ni vichache sana tumenunue kwa pesa zetu. Lakini jamani mbona hatujiulizi ni kwa nini bei ya sukari imepanda kutoka 500 hadi 2,000 kwa kilo ma hatukugoma. Watu wa kigamboni waligoma kulipa bei ya sukari baada ya kupanda? Sishangilii kupanda kwa nauli kwa kuwa kuna kiloo kwamba kuna ivujaji wa mapato hapo feri. Serikali ingeziba kwanza mianya kisha ikapandisha nauli
Tatizo langiu ni Nauli ya GUTA linalo beba, VIAZI, MAGIMBI, EMBE na mazao mengine kuja huku soko la TANDALE kwa nauli ya kutoka 300 mpaka 1800 , sijuhi bei itapanda vipi?
 
Tatizo langiu ni Nauli ya GUTA linalo beba, VIAZI, MAGIMBI, EMBE na mazao mengine kuja huku soko la TANDALE kwa nauli ya kutoka 300 mpaka 1800 , sijuhi bei itapanda vipi?
Itabidi wafanya biashara mbadilishe utamaduni wa kutumia guta badala yake mtumie usafiri wa magari yanayobeba vyakula na kusambaza sehemu hizo...Wakulima waunde Union au cooperative ambayo watakuwa wakikusanya mazao yao tuseme soko la Kariakoo na wanunuzi wanatoa Order zao za vyakula kisha magari yatasambaza mji mzima hadi Kigamboni.

Wenye guta watafanya usafiri mdogo mdogo wa ndani baina ya vituo kwa mfano kuwepo na soko jingine Kigamboni na majimbo mengine yote na wakulima ndio wawe supplier ktk masoko hayo na wenye guta watakuwa wakazi wa Kigamboni kusambaza Kigamboni..

Nadhani itakuwa hatua ya maendeleo zaidi kulingana na mfumko wa bei kuliko kuendelea kuithaminisha shilingi kwa mlalahoi wakati hailingani wala haikidhi matumizi makubwa ya uendeshaji biashara zao wala Pantoni..Mishahara iongezwe kulingana na upandaji wa maisha na tukubali ku face the real value of our currency..
 
Mchambuzi,

..nadhani kivuko cha Kigamboni kina wateja wengi zaidi na ndiyo maana it makes sense kutoza nauli ndogo zaidi ya huko Pangani au Kilombero. naamini hata mtu binafsi atapenda kufanya biashara Kigamboni as compared to Kilombero.

..nauli zilizopanda siyo za abiria tu, bali hata za maguta, magari makubwa na madogo etc etc. sijui kwani watu wameshikana mashati kwenye nauli za abiria tu.

..kinachotakiwa kufanyika ni uhakiki wa mapato na gharama za uendeshaji wa kivuko cha kigamboni. Wabunge wamependekeza kufanyike uhakiki huo kabla ya kupandisha nauli lakini Magufuli amekataa.

NB:

..MAGUFULI AACHE LUGHA ZA KEJELI NA DHARAU KWA WALE WANAOTOFAUTIANA NAYE. MIMI NI MTU MZIMA KIDOGO NA NAKUHAKIKISHIA SIJAWAHI KUONA WAZIRI ASIYE MSIKIVU NA ALIYEKOSA STAHA KTK MAJIBU YAKE KAMA JOHN POMBE MAGUFULI.
 
Mchambuzi,

..nadhani kivuko cha Kigamboni kina wateja wengi zaidi na ndiyo maana it makes sense kutoza nauli ndogo zaidi ya huko Pangani au Kilombero. naamini hata mtu binafsi atapenda kufanya biashara Kigamboni as compared to Kilombero.

..nauli zilizopanda siyo za abiria tu, bali hata za maguta, magari makubwa na madogo etc etc. sijui kwani watu wameshikana mashati kwenye nauli za abiria tu.

..kinachotakiwa kufanyika ni uhakiki wa mapato na gharama za uendeshaji wa kivuko cha kigamboni. Wabunge wamependekeza kufanyike uhakiki huo kabla ya kupandisha nauli lakini Magufuli amekataa.

NB:

..MAGUFULI AACHE LUGHA ZA KEJELI NA DHARAU KWA WALE WANAOTOFAUTIANA NAYE. MIMI NI MTU MZIMA KIDOGO NA NAKUHAKIKISHIA SIJAWAHI KUONA WAZIRI ASIYE MSIKIVU NA ALIYEKOSA STAHA KTK MAJIBU YAKE KAMA JOHN POMBE MAGUFULI.
Mkuu wangu unajua vizuri sana kwamba nyumba za Msajili au NHC zinapangishwa chini ya kiwango chake na watu wengi sana wana abuse mteremko waliopewa wakipangisha nyumba hizo hizo kwa wahindi in dollars up to 1,500 a month..

Sasa serikali inapopandisha bei za pango na kuharamisha upangishaji haramu wananchi wamelalamika sana na wengine hata kutaka uhai wa kiongozi aliyeweka bei mpya ambazo hazifiki hata hiyo 1,500 ambayo kusema kweli ndio market rate. Lakini kwa mtu alozoea kulipa Laki 2 huyu ataona anaonewa japokuwa yeye anapangisha kwa dollar..Tukiendelea kusikia vilio vya watu hatuweza fanya mabadiliko maana watu wanataka tuishi kama tulivyoishi siku tulopata Uhuru au wakati wa Nyerere.

Kama bei za Guta na magri zinaonekana kubwa ni kwa sababu ya thamani ya shilingi yenyewe tunataka sana kuithaminisha wakati hailingani na matumizi.. pengine Tsh 1800 ni kubwa sana lakini basi tulizungumzie hilo basi na magari kutozwa 2,000. Na amini maneno yangu ya kwamba hata matumizi ya ununuzi wa vipuli na vifaa nyote toka nje ikiwa nipamoja na mafundi kutoka nje hayawekwi ktk matumizi ya pantoni kwa sababu yanalipwa nje ya mfuko wa Pantoni. Kinachopigwa hesabu ni matumizi ya direct na pantoni lakini nje ya hapo hayamo...

Wee subiri report ya mapato namatumizi yake utaona kwa sababu najua kabisa kwamba wizara chini ya Central government ina cover matumizi mengine.
 
Wabunge wapo sahihi,na unapozungumzia juu ya nauli usiishie tu kuitaja ile 200,angalia pia gharama za mizigo,bajaji,gari n.k.pia usisahau na nauli nyingine kutoka pale feri kwenda maeneo mengine mara kurudi,yaani mfano mwenge,mabibo n.k,inawezekana wanaopingana na wabunge hawa upeo wao wa kufikiri ndio umeishia hapo,tunawasamehe.
 
embu tuliweke hili suala kwenye context ifuatayo, maana tufike mahali tuwe tunalinganisha maembe kwa maembe (samahani kama input ya namna hii tayari imekwishatolewa na mchangiaji mwingine)...........

mimi ni mkazi wa dar, naishi manzese. sina uwezo wa kulipa nauli ya daladala kila siku kwenda kariakoo ambako ndipo ipo maskani ya kupatia riziki yangu. kutokana na bajeti yangu kutomudu daladala kila siku, nina option ya tz11 (kwenda kwa miguu), na nimekuwa nikiitumia miaka nenda rudi. suits me ok.

binamu yangu kombo anaishi kigamboni. ndiyo mdau mwenzangu kwenye maskani yetu pale kariakoo. nauli ya kivuko ndiyo hiyo imependa na bajeti haimruhusu ku-accomodate hii rise. kwa bahati mbaya, binamu kombo hana option ya tz11 kama yangu na (btw) hajui kuogelea hata kwenye dimbwi achilia mbali bahari.

sa naomba mnisaidie nimshauri vipi ndugu yangu kombo!?
 
embu tuliweke hili suala kwenye context ifuatayo, maana tufike mahali tuwe tunalinganisha maembe kwa maembe (samahani kama input ya namna hii tayari imekwishatolewa na mchangiaji mwingine)...........

mimi ni mkazi wa dar, naishi manzese. sina uwezo wa kulipa nauli ya daladala kila siku kwenda kariakoo ambako ndipo ipo maskani ya kupatia riziki yangu. kutokana na bajeti yangu kutomudu daladala kila siku, nina option ya tz11 (kwenda kwa miguu), na nimekuwa nikiitumia miaka nenda rudi. suits me ok.

binamu yangu kombo anaishi kigamboni. ndiyo mdau mwenzangu kwenye maskani yetu pale kariakoo. nauli ya kivuko ndiyo hiyo imependa na bajeti haimruhusu ku-accomodate hii rise. kwa bahati mbaya, binamu kombo hana option ya tz11 kama yangu na (btw) hajui kuogelea hata kwenye dimbwi achilia mbali bahari.

sa naomba mnisaidie nimshauri vipi ndugu yangu kombo!?

Kwa mujibu wa Magufuli either apige mbizi au azungukie Kongowe.
 
embu tuliweke hili suala kwenye context ifuatayo, maana tufike mahali tuwe tunalinganisha maembe kwa maembe (samahani kama input ya namna hii tayari imekwishatolewa na mchangiaji mwingine)...........

mimi ni mkazi wa dar, naishi manzese. sina uwezo wa kulipa nauli ya daladala kila siku kwenda kariakoo ambako ndipo ipo maskani ya kupatia riziki yangu. kutokana na bajeti yangu kutomudu daladala kila siku, nina option ya tz11 (kwenda kwa miguu), na nimekuwa nikiitumia miaka nenda rudi. suits me ok.

binamu yangu kombo anaishi kigamboni. ndiyo mdau mwenzangu kwenye maskani yetu pale kariakoo. nauli ya kivuko ndiyo hiyo imependa na bajeti haimruhusu ku-accomodate hii rise. kwa bahati mbaya, binamu kombo hana option ya tz11 kama yangu na (btw) hajui kuogelea hata kwenye dimbwi achilia mbali bahari.

sa naomba mnisaidie nimshauri vipi ndugu yangu kombo!?
Je angekuwa hana 100 angefanyaje?
 
Wabunge wapo sahihi,na unapozungumzia juu ya nauli usiishie tu kuitaja ile 200,angalia pia gharama za mizigo,bajaji,gari n.k.pia usisahau na nauli nyingine kutoka pale feri kwenda maeneo mengine mara kurudi,yaani mfano mwenge,mabibo n.k,inawezekana wanaopingana na wabunge hawa upeo wao wa kufikiri ndio umeishia hapo,tunawasamehe.

Na ndio maana tunasubiria wenye upeo zaidi waturudie na ufafanuzi zaidi. Vinginevyo, usisahau kwamba kiini cha huu mjadala ni ongezeko la shillingi 100, miaka 14 baadae, suala la maguta, magari, baiskeli, pamoja na umuhimu wake, sio sehemu kuu ya mjadala kwa sasa.

Mh. Mnyika alisema atazungumza na waandishi wa habari leo (jumapili), hatujamsikia. Nadhani amesogeza iwe kesho. Vinginevyo aliahidi kuturudia mara baada ya kujibu hoja za magufuli mbele ya waandishi wa habari.
 
Kupinga kwamba wananchi wa Kigamboni (beneficiaries of the ferry services ) wasilipie in fully running cost a.k.a operating expenditure (OPEX) za vivuko ni sawa na kusema Kalimanzira wa Kigoma au Tabora, Bububu ambaye hafaidiki na hicho kivuko na yeye pia alipie kuzipa hilo pengo la operating cost...

Naomba niwakumbushe operating cost za kivuko ni pamoja ---depreciation ya kivuko...

In fact wa-Bububu tutaenda mahakamani kupinga kulipia indirect cost zisizotuhusu., na mturudishie chenji yetu ya miaka hiyo mliyokuwa mnapata subsidy.... we can only allow watoto na vikongwe wapati subsidy lakini sio kila mtu.
 
Back
Top Bottom