Nauli Feri: Mnyika, Hata Wewe?

Ndio maana nikawarudisha watu nyuma wakumbuke kwamba UDA ilikufa kwa sababu - WALISEMA -Nyerere sio mchumi huwezi kutoza watu Tsh 1 kwa usafiri japokuwa dollar ilikuwa Tsh17 hiyo ilikuwa kama senti 6 kisha ikapandishwa hadi Tsh 5 bado haikutosha leo hii watu tunalalamika na kuongezeka kufikia senti 13 ya dollar...

Jamani hata ile shilingi moja ya Nyerere ilikuwa kubwa mara ngapi ukilinganisha na Tsh 100 ya leo?... Ni sawa na senti ngapi 6 na ushee, watu wote wanalia ingawa binafsi hata hiyo Tsh 300 ya daladala bado ni ndogo sana haifiki hata senti 20 ya dollar...Halafu tunaambiwa ati nchi imeendelea tunapaa.. haya ebu wekeni kiwango cha daladala sawa na wakati wa Nyerere ihata senti 30 tu ya dollar (Tsh 800) tuone hicho kilio cha wananchi -Tumeendelea!

Mkandara.
Kufa kwa UDA ni matokeo ya kuwa viongozi dhaifu na wenye tamaa; walipoamua kuiua UDA hawakuangalia maslahi ya Taifa na wananchi; usafiri wa ndani ya miji ni muhimu kwa wakazi husika; hii inawasaidia kupunguza gharama za maisha; mtu ambaye hajawahi kutembea ndiye atakayekubaliana nao. Moja ya sababu ya kupanda gharama za maisha Dar es salaam ni usafiri wa daladala; wananchi wengi hivi sasa wanashindwa kupanda daladala kutokana na nauli, sasa jiulize mfanyakazi wa kawaida ambaye ana watoto wawili atayamudu vipi maisha? Hapa ndipo rushwa inapoanza tukumbuke wafanyakazi hawalipwi kulingana na hali ya maisha; tukurudi kwenye UDA ilikuwa inatoa huduma kwa wananchi, lazima tukubali kuna baadhi ya huduma ni serikali tu ndio inayoweza kumudu kuzitoa; hivi tujiulize kwa nini nchi kama Marekani pamoja na kuwa na sera za kibepari hairuhusu watu binafsi kutoa huduma za usafiri ndani miji? Ukienda San Franscisco Bay area, Washington DC metro area, Houston , Boston miji yote ina metro buses ambazo zinatoa huduma, serikali kuu na serikali za majimbo ndizo zinazogharimia uendeshaji; kimsingi nauli za usafiri ndani miji mikubwa kinachoangaliwa sio FAIDA inaangaliwa ni HUDUMA. Mwl. Nyerere alioona mbali zaidi.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Why not now? Kwa sababu wangeweza kupandisha nauli kwenye hiyo miaka 14 iliyopita. Nini kilikuwa kinawazuia kupandisha nauli? Kama ni kupanda kwa mishahara ya wafanyakazi kama alivyodai magufuli, kwani hiyo mishahara imeanza kupanda mwaka huu? Kwani gharama za undeshaji wa kivuko zimeanza kupanda mwaka huu?

Hujanielewa. Serikali inatakiwa kufanya mabadiliko kwa kuendana na wakati. Sio kukaa miaka 14 bila kufanya chochote huku ikipoteza public money kama ruzuku ya kuendesha kivuko. Serikali ilikuwa wapi kipindi chote cha miaka 14 wakati taxpayers money ikiteketea pale feri?

The fact kuwa Magufuli hakuwa kwenye hiyo wizara, does not exempt the government from liability. Serikali sio Magufuli pekee. BTW Magufuli kaendesha hiyo wizara kwa miaka mingapi?
Kwanini sitting allowances zifutwe now? why now? and not 2003? au 2008?
Unakubali kuwa shilingi 100 hazitoshelezi gharama za kukiendesha kivuko? kama hukubaliani nalo basi tupe mahesabu yanayokufanya uone kuwa shs 100 zinatosheleza. Zaidi ya hapo, yatakuwa ni malumbano yasiyo na takwimu za kimahesabu which is ..... nonsense.
 
Tujue kwanza kinacholalamikiwa ndio tujadili mada!!
Issue sio kupanda kwa bei, bali mchakato uliotumika kuipandsha hiyo bei!!! Ulishirikisha wakazi wa pale??
Jana nimevuka pale nikapiga story na wale wahudumu, wakaniambia kua Bakhresa alilamikia kodi ya vibaiskeli vyake vya ice-cream basi ikashuka mpaka Tshs 300, tuseme kwakua wenye maguta hawana wa kuwatetea hivyo waendelee kutaabika tu???
Yaani bora upite na GX 110 utalipa less kuliko Guta, ni haki kweli hii???

Exactly. Pamoja na lack of transparency and participation kwenye mchakato mzima, I am shocked that serikali hawaijawahi kupandisha nauli kwa muda wa miaka 14. Why?
 
Serikali ilikuwa wapi muda wote wa miaka 14 isipandishe nauli kama walivyokuwa wanapandisha sehemu nyingine? Why now?

Hilo ni swali la msingi; lakini usisahahu serikali inatoa huduma ya kivuko haiendeshi biashara ya kivuko.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Mkandara.
Kufa kwa UDA ni matokeo ya kuwa viongozi dhaifu na wenye tamaa; walipoamua kuiua UDA hawakuangalia maslahi ya Taifa na wananchi; usafiri wa ndani ya miji ni muhimu kwa wakazi husika; hii inawasaidia kupunguza gharama za maisha; mtu ambaye hajawahi kutembea ndiye atakayekubaliana nao. Moja ya sababu ya kupanda gharama za maisha Dar es salaam ni usafiri wa daladala; wananchi wengi hivi sasa wanashindwa kupanda daladala kutokana na nauli, sasa jiulize mfanyakazi wa kawaida ambaye ana watoto wawili atayamudu vipi maisha? Hapa ndipo rushwa inapoanza tukumbuke wafanyakazi hawalipwi kulingana na hali ya maisha; tukurudi kwenye UDA ilikuwa inatoa huduma kwa wananchi, lazima tukubali kuna baadhi ya huduma ni serikali tu ndio inayoweza kumudu kuzitoa; hivi tujiulize kwa nini nchi kama Marekani pamoja na kuwa na sera za kibepari hairuhusu watu binafsi kutoa huduma za usafiri ndani miji? Ukienda San Franscisco Bay area, Washington DC metro area, Houston , Boston miji yote ina metro buses ambazo zinatoa huduma, serikali kuu na serikali za majimbo ndizo zinazogharimia uendeshaji; kimsingi nauli za usafiri ndani miji mikubwa kinachoangaliwa sio FAIDA inaangaliwa ni HUDUMA. Mwl. Nyerere alioona mbali zaidi.

Chama
Gongo la Mboto DSM
Nakubaliana na wewe 100% lakini pia tunashindwa kutazama upande wa uendeshaji. Wewe unalo gari nyumbani I assume (bongo) V6 ukiweka mafuta ya Tsh 5,000 kama unaishi Ubungo unakwenda mjini na bahati ukirudi nyumbani bado yapo sasa kama unatoa huduma ya usafiri kupakia abiria utawatoza kiasi gani watu unaowapakia?..Na ukimwambia mtu gharama hizi hatokubali atakuona mwizi mbali na hayo kila kipuli cha gari ni imported kinauzwa bei sawa na Ulaya sasa hizi nauli za Tsh100 kweli zinaweza kuendesha huduma..

Tatizo liko wapi? tatizo ni mishahara, fedha yetu haina thamani kabisa na ndio maana leo viuongozi wanapokea mabillioni wakihesabiwa ama kukisiwa kwa dollar wakati wananchi wanapokea Tsh 150,000 na graduate akifanikiwa sana atapewa Millioni moja. Hivyo tunapozungumzia usafiri wetu ghali, sii ghali kusema kweli bali mishahara ya wafanyakazi haitoshi na hakuna uuwiano wa maisha na mapato kiasi kwamba wanyonge maskini wanabanwa wao wakaze mikanda lakini wakubwa wakitumbua maisha na kudai posho zaidi..

Na kusema kweli ktk hali tuliyokuwa nayo leo haitakiwi hata kufikiria kuunda shirika la usafiri ikiwa nauli zenyewe ndio Tsh 300 hazitoshi ku run Transportation Compnay na ndio maana unaona watu wote wanakimbilia kununua semi trailers kwa sababu zinalipa na sio daladala. daladala ni biashara ya mama kwa matajiri yaani apate hela ya matumizi nyumbani.. Uliona wapi mentatlity ya huduma muhimu kama hii watu wafikirie ni fedha ya kununua mboga..Who is gonna invest?

Kwa hiyo naelewa sana jambo hili na kama ulikuwepo BCS mwaka 2001 niliwahi kuponda daladala watu wakaniijia juu kichizi kwamba sielewi hali ya usafiri dar na jinsi daladala zilivyokuja kufanikisha tatizo la Usafiri. Yaani kuna watu hapa hawakutaka kabisa kusikia UDA ingawa mimi nilikuwa na mtazamo kama wako wewe, lakini hawakuniamini na nilionekana mzuka!
 
Kwanini sitting allowances zifutwe now? why now? and not 2003? au 2008?
Kwani anayetaka sitting allowance zifutwe ni nani?

Unakubali kuwa shilingi 100 hazitoshelezi gharama za kukiendesha kivuko? kama hukubaliani nalo basi tupe mahesabu yanayokufanya uone kuwa shs 100 zinatosheleza. Zaidi ya hapo, yatakuwa ni malumbano yasiyo na takwimu za kimahesabu which is ..... nonsense.

That is not my point. Sijasema sh 100 zinatosheleza. Point yangu ni kwamba wakati serikali inapandisha nauli kwenye vivuko vingine kama Pangani kwa nini haikufanya hivyo kwa kivuko cha feri for 14 years? Kwa ni gharama za kivuko cha feri zimeanza kupanda mwaka huu?
 
Kwani anayetaka sitting allowance zifutwe ni nani?



That is not my point. Sijasema sh 100 zinatosheleza. Point yangu ni kwamba wakati serikali inapandisha nauli kwenye vivuko vingine kama Pangani kwa nini haikufanya hivyo kwa kivuko cha feri for 14 years? Kwa ni gharama za kivuko cha feri zimeanza kupanda mwaka huu?
Mkuu swali gumu sana kulijibu maana aliyetaka gharama zipande ni nwaziri Magufuli... Ni sawa na Magufuli tena amneanza kujenga daraja useme kwa nini miaka 50 ya Uhuru hawakutaka kujenga hadi sasa?..
Maadam swala hili lilikwenda Bungeni na aliyeliwakilisha ni waziri ambnaye wengi tunajua ni mchapa kazi sioni tatizo liko wapi hasa kwa kuzingatia kiwango chenyewe..
Kama ni swala la Guta kama ndilo kikwazo lizungumziwe lakini sio kulaaqani kitendo kizima kama ilivyotokea ktk bomoa bomoa ya Magufuli matokeo yake tumepoteza roho ngapi kule Jangwani na Kigogo?
 
Hilo ni swali la msingi; lakini usisahahu serikali inatoa huduma ya kivuko haiendeshi biashara ya kivuko.

Chama
Gongo la Mboto DSM

It doesn't matter whether is doing business or delivering services. A responsible government should gradually increase the price of its services to equate it to the economic cost of running them. A gradual increase in prices to allows the consumers to adjust to the changes and also provide time for consumers to find alternatives. Siyo unakaa miaka 14 kimya, halafu unapandisha bei ghafla bila hata transparency and effective participation. Au kwa vile wananchi wa Kigamboni wana limited alternatives za usafiri ndio wabambikiwe nauli mpya ghafla?
 
Kwani anayetaka sitting allowance zifutwe ni nani?



That is not my point. Sijasema sh 100 zinatosheleza. Point yangu ni kwamba wakati serikali inapandisha nauli kwenye vivuko vingine kama Pangani kwa nini haikufanya hivyo kwa kivuko cha feri for 14 years? Kwa ni gharama za kivuko cha feri zimeanza kupanda mwaka huu?
Huo ni mfano tu. Kama unauliza why now?... utaulizwa why not now kwa kila jambo.
wether it's now or not, the fact is 100 shs hazikidhi gharama

saupload_oil_price_graph.png


Kwa mfano angalia rate ya bei ya mafuta duniani, rate ya kupanda kwake tangu 2007 si sawa na from 1996 to 2006. Unaweza kusema kwa miaka kumi tangu '96 mafuta yamepanda kwa 40$ a barrel, average ya 4$ a year per barrel (roughly, it was almost flat for 6yrs).
Na kutoka 2006 mpaka leo ni 103$ per barrel. Amost 10$ a year average..... don't you think that the cost somehow skyrocketed?

Kivuko cha kigamboni ni muhimu kwa uchumi wa Tanzania kulinganisha na vivuko vingine combined, so I will understand the government's hesitation kwenye kuongeza bei as a means to stimulate trade, but when the costs outweighs the benefits ningeomba wanasiasa wakae pembeni wawaachie wataalam.

Naomba mungu mawaziri wasihusishwe na siasa tena!! this is weird.
 
It doesn't matter whether is doing business or delivering services. A responsible government should gradually increase the price of its services to equate it to the economic cost of running them. A gradual increase in prices to allows the consumers to adjust to the changes and also provide time for consumers to find alternatives. Siyo unakaa miaka 14 kimya, halafu unapandisha bei ghafla bila hata transparency and effective participation. Au kwa vile wananchi wa Kigamboni wana limited alternatives za usafiri ndio wabambikiwe nauli mpya ghafla?
That applies only if the operating costs were increasing gradually and not abruptly...
On your side too we need some transparency!

Show us how gradual the operating costs were increasing, then mabbe you can tell us how gradual the price would've increased.
 
Mkuu swali gumu sana kulijibu maana aliyetaka gharama zipande ni nwaziri Magufuli... Ni sawa na Magufuli tena amneanza kujenga daraja useme kwa nini miaka 50 ya Uhuru hawakutaka kujenga hadi sasa?..
Maadam swala hili lilikwenda Bungeni na aliyeliwakilisha ni waziri ambnaye wengi tunajua ni mchapa kazi sioni tatizo liko wapi hasa kwa kuzingatia kiwango chenyewe..
Kama ni swala la Guta kama ndilo kikwazo lizungumziwe lakini sio kulaaqani kitendo kizima kama ilivyotokea ktk bomoa bomoa ya Magufuli matokeo yake tumepoteza roho ngapi kule Jangwani na Kigogo?

Kwa nini tuna-avoid maswali magumu? Comparison yako ya kutopandisha nauli kwa miaka 14 na kutojenga daraja kwa miaka hamsimi naona kama ni absurd. Hapa serikali ilikuwa na uwezo wa kupandisha nauli kulingana na gharama za uendeshaji lakini haikufanya hivyo kwa muda wa miaka 14.
 
Huo ni mfano tu. Kama unauliza why now?... utaulizwa why not now kwa kila jambo.
wether it's now or not, the fact is 100 shs hazikidhi gharama

Kama ni why not now kwa nini then Magufuli anasema bei za vivuko vingine zimepandishwa zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1997, lakini cha Kigamboni kimekuwa kikitoza bei ya sh. 100 kwa mtu mmoja?

Kwa mfano angalia rate ya bei ya mafuta duniani, rate ya kupanda kwake tangu 2007 si sawa na from 1996 to 2006. Unaweza kusema kwa miaka kumi tangu '96 mafuta yamepanda kwa 40$ a barrel, average ya 4$ a year per barrel (roughly, it was almost flat for 6yrs). Na kutoka 2006 mpaka leo ni 103$ per barrel. Amost 10$ a year average..... don't you think that the cost somehow skyrocketed?

Kivuko cha kigamboni ni muhimu kwa uchumi wa Tanzania kulinganisha na vivuko vingine combined, so I will understand the government's hesitation kwenye kuongeza bei as a means to stimulate trade, but when the costs outweighs the benefits ningeomba wanasiasa wakae pembeni wawaachie wataalam. Naomba mungu mawaziri wasihusishwe na siasa tena!! this is weird.

Kwa nini serikali haikusema hivyo basi?

That applies only if the operating costs were increasing gradually and not abruptly...
On your side too we need some transparency! Show us how gradual the operating costs were increasing, then mabbe you can tell us how gradual the price would've increased.

Kwa hiyo, gharama za opereshesni ya kivuko cha feri imeongezeka ghafla ndio maana serikali ikaamua kuongeza nauli ghafla? Kwa mfano katika kujitetea kwale Magufuli alisema yeye haoni sababu ya nauli hizo kupigiwa kelele, kwani hata kitumbua kilichokuwa kikiuzwa awali Sh 20 sasa kinauzwa Sh 250. Hivyo vitumbua vilipanda bei abruptly kutoka sh. 20 had sh 250?
 
Ninamheshimu sana Mchambuzi,lakini nashawishika kusema ameingia kichwa kichwa katika vita dhidi ya Chadema,na ndio maana mashambulizi yake yote ameyapeleka kwa Mnyika.Ninachomshangaa anafanya fitina zake kwa kuangalia ongezeko la nauli za abiria tu.Lakini hamfikirii kijana aliyepandishiwa gharama ya kusafirisha guta kutoka 200 hadi 1800.Namshauri mchambuzi kama katumwa kumsafisha Magufuli kwa kumchafua Mnyika kakosea sana.Magufuli hana tofauti na Lyatonga Mrema katika papara za uongozi.

Haya maguta ni ya biashara, swali linekuwa wanaingiza bei gani kwenye hizo biashara zao? kuna watu wengi wanazaraulika kwa NATURE ya biashara wanazofanya, lakini mwisho wa mwezi wana take home kubwa kuliko ya mpiga suti, ila malengo na matumizi inaweza kuwa tatizo hasa kwa kuzingatia bank ni mifuko yao ya suruali, sisemi kwamba wanakula good time, lakini rukuzu inapotumika lazima kuwe na ukombozi kiuchumi, kama mtu anaendesha guta basi lina mlipa, tuhache makuzi, wasaidie mahesabu na matumizi wengi wanazipoteza hizo pesa kusikofaa, hao ni wengi
 
Kama ni why not now kwa nini then Magufuli anasema bei za vivuko vingine zimepandishwa zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1997, lakini cha Kigamboni kimekuwa kikitoza bei ya sh. 100 kwa mtu mmoja?



Kwa nini serikali haikusema hivyo basi?



Kwa hiyo, gharama za opereshesni ya kivuko cha feri imeongezeka ghafla ndio maana serikali ikaamua kuongeza nauli ghafla? Kwa mfano katika kujitetea kwale Magufuli alisema yeye haoni sababu ya nauli hizo kupigiwa kelele, kwani hata kitumbua kilichokuwa kikiuzwa awali Sh 20 sasa kinauzwa Sh 250. Hivyo vitumbua vilipanda bei abruptly kutoka sh. 20 had sh 250?

serikali haina hela ya rukuzu uchumi wetu huko hoi,
kulinganisha bei ya kitumbua na bei za kivuko sio sahihi sana, kitumbua au aina nyingine yoyote uzalishaji hisiyo na subsidy ghamala upanda kutokana na ghalama za uzalishaji na faida,
lakini hapa kwenye kivuko kuna rukuzu inasaidia kuweka mambo sawa, mapato ya kivuko hayakidhi ghalama za uendeshaji, Hivyo basi kama rukuzu ikipungua au ghalama za uendeshaji zikipanda lazima nauli au ruzuku iwe affected.#
Nilichoona mimi kwenye ili suhala la kivuko kuna kificho sana, ilipashwa kujulika ghalama za uendeshaji ni kiasi gani (ni hakika zimepanda kutokana na kupolomoka kwa shillingi) na mapato ni kiasi gani kutokana na nauli, na ruzuku kutoka serikali ni kiasi gani ( hii inaweza kuwa imepunguzwa au kutokwenda sambamba na kupanda na ghalama za uendeshaji zilizopanda) na hapo matokeo yake ni ongelezeko la nauli.
Kwa ujumla Nauli za Magufuli ziko sahihi maana sioni sababu babu yangu aliyepo mtukula kuendelea kumlipia nauli mkazi wa kigamboni kupitia rukuzu (kodi) kisa ni masikini eti ana biashara ya guta
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Kama ni why not now kwa nini then Magufuli anasema bei za vivuko vingine zimepandishwa zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1997, lakini cha Kigamboni kimekuwa kikitoza bei ya sh. 100 kwa mtu mmoja?



Kwa nini serikali haikusema hivyo basi?



Kwa hiyo, gharama za opereshesni ya kivuko cha feri imeongezeka ghafla ndio maana serikali ikaamua kuongeza nauli ghafla? Kwa mfano katika kujitetea kwale Magufuli alisema yeye haoni sababu ya nauli hizo kupigiwa kelele, kwani hata kitumbua kilichokuwa kikiuzwa awali Sh 20 sasa kinauzwa Sh 250. Hivyo vitumbua vilipanda bei abruptly kutoka sh. 20 had sh 250?
Mkuu tatizo siyo kupanda ghafla.
Tatizo wanalolisema wabunge (hakumtaja mdee lakini nyinyi mnaona kama CDM wanalengwa) ni kuwa wakazi wa kigamboni wanaonewa na serikali, kwamba shilingi 100 inatosha. Je, wewe unakubaliana nalo? Kama siyo, je huoni kuwa wabunge wameingiza siasa bila data?
Tupinge wanasiasa kujiingiza kwenye taaluma, haya mambo ndiyo yanayopingwa hapa...... wana access na data lakini hawazitumii.
Kinachosikitisha, ni ulimbukeni wa wanasiasa, ndiyo maana mnaulizwa, Mnyika hata wewe?
 
Serikali ilikuwa wapi muda wote wa miaka 14 isipandishe nauli kama walivyokuwa wanapandisha sehemu nyingine? Why now?

EMT,
Kujibu swali lako la awali pia ni kwamba, kuhusu ripoti ya kamati ya bunge, kuna sehemu nilisoma, lakini nadhani ni muhimu tukasubiri taarifa juu ya hilo, kutoka kwa mtu wa ndani - kwa nafasi yake ya uwakilishi - yani Mh. JJ Mnyika.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu tatizo siyo kupanda ghafla.
Tatizo wanalolisema wabunge (hakumtaja mdee lakini nyinyi mnaona kama CDM wanalengwa) ni kuwa wakazi wa kigamboni wanaonewa na serikali, kwamba shilingi 100 inatosha. Je, wewe unakubaliana nalo? Kama siyo, je huoni kuwa wabunge wameingiza siasa bila data?
Tupinge wanasiasa kujiingiza kwenye taaluma, haya mambo ndiyo yanayopingwa hapa...... wana access na data lakini hawazitumii.
Kinachosikitisha, ni ulimbukeni wa wanasiasa, ndiyo maana mnaulizwa, Mnyika hata wewe?

CDM kuna ushabiki wa majina na sio chama, kuna watu ukiwataja kwenye mitandao wamekosea basi utaambiwa wewe ni magamba, kunatofauti kubwa sana ya mdee na mnyika, navyomsoma mnyika kwa sasa anajichanganya sana
regea waziri wa ulinzi Barak alipoisema hovyo Tanzania, Mnyika badala ya kuona hiyo ndiyo hoja chadema wanalia nayo kila siku kwamba tunatatizo kwenye uongozi wa nchi mpaka tuna tunapingwa vijembe, akaenda upande mwingine as if we have a stable bold government
 
Toka Magufuli atoe kauli nimekuwa kimya kumjibu nikiendelea na majukumu mengine jimboni na ya kitaifa. Magufuli hakujibu hoja, na badala yake ametoa kauli zisizokuwa na ukweli wowote dhidi yangu, kauli potofu zikiachwa zitaonekana milele kuwa sahahi. Kwa hiyo nimeamua kesho nizungumze na wanahabari kuweka msimamo wangu wazi ili kuweka rekodi muafaka: Mosi, nitajibu hoja kwa hoja, kwa masuala yote aliyoyasema dhidi yangu. Pili, nitaweka bayana kwanini nimeunga mkono kwa GN ihairishwe kutekelezwa, hoja za msingi zijibiwe na mabadiliko muhimu yafanyike.

JJ

Mheshimiwa Mnyika, wakati tunasubiri ufafanuzi wako, naomba nikupe ushauri wa bure wakati unajiandaa kujibu hoja za Magufuli. Katika majibu yako kwa Magufuli, hoja zako zitapimwa katika mazingira yafuatayo:

Moja, kwamba, kwa Mh. Mnyika, ni haki kwa watanzania wanaoishi maeneo ya vivuko vingine huko mikoani (kama vile pangani), kuongezewa nauli mara kwa mara katika kipindi cha miaka 15 yani (1996 – 201l), lakini sio haki kwa wakazi wa Dar-es-salaam, ingawa wakazi wa mikoani, kiuchumi, wana hali mbaya zaidi ya wale wa DSM.

Mbili, msimamo wako kwamba nauli ibakie kuwa sh. 100, unatokana na hoja yako kwamba tatizo ni usimamizi wa mapato ya kivuko. Na huu ndio utakuwa ni uelewa wa mwananchi wa maeneo kama pangani ambae atakuwa anakusikiliza kama Katibu wa siasa na uenezi wa chama cha siasa anachokiunga mkono, ili kubaini kwanini vivuko vyao nauli zinapanda kila mwaka, wakati wenzao wa Dar-es-salaam, nauli zilibakia kuwa sh. 100 kwa miaka 15.

Tatu, kwa hali ilivyo sasa, nauli ya sh. 200 ni kubwa mno kwa mkazi wa kawaida DSM ukifananisha na nauli y ash. 100 ya awali, lakini kwa kule maeneo kama Pangani, ni sawa tu kwani wao wanaweza kumudu. Hapa wasikilizaji watatilia maanani kwamba Mh. Mnyika ni mtunga sheria na pia ni msimamizi wa utekelezaji wa sheria hizo, ambazo zinatakiwa kuzingatia fairness, equity and justice kwa watanzania wote.

Nne, katika kipindi cha miaka 15 (yani 1996 – 2011), wakati nauli ya Ferry Kigamboni imebakia kuwa shillingi mia, nauli ya daladala (katika kipindi hicho hicho) imeongezeka mara tatu. Lakini kwako binafsi, hili sio tatizo kubwa kama lile la ongezeko la sh. 100 ferry ya kigamboni.

Tano, wasikilizaji watakuwa wanakupima huku wakijaribu kubaini iwapo Magufuli yupo sahihi kwamba unapambana na vita visivyokuwa na maana zaidi ya vita nyingine kubwa zaidi iliyokuwa mbele yenu kama wawakilishi wa wananchi. Wasikilizaji watazingatia masuala yafuatayo kubaini nani yupo sahihi:

a) Katika kipindi hicho cha miaka 15 ambapo nauli ilibakia kuwa sha 100 kwa DSM, huku mikoani ikibadilika mara kadhaa, Bei ya mafuta ya diesel inayotumika kuendeshea ferry imeongozeka mara nne (kati ya mwaka 1996 – 2011). Mwaka 1996, lita moja ya diesel ilikuwa ni sh. 500, leo hii bei ya lita ni sh. 2,000.

b) Halafu haraka haraka watakumbuka takwimu za mfumuko wa bei (kutoka NBS) kama ifuatavyo:

Inflation Figures 2010 - 2011(%)
Item(s)12 month change (2010-2011)
1.Food and non – alcoholic22.5%
2.Housing, water, electricity and other fuel21.7%
3.Furnishing, housing equipment and routine maintenance of the house14.2%
4.Restaurant and Hotels11.5%
5.Transport10.8%
Source: NBS

Watazamaji watabaini kwamba, tatizo kubwa la wakazi wa DSM lipo katika bei ya chakula, kodi ya nyumba, mafuta ya taa, umeme na maji. Hapo watagundua kwamba, ingawa inawezekana Mh Mnyika ana hoja, lakini kumbe Magufuli yupo sahihi kwamba anapigana vita visivyo muhimu sana (yani ongezeko la nauli ferry kwa sh. 100), kwani mbali ya nauli ya ferry, hata nauli za mabasi ya kwenda mikoani na daladala za mijini, pamoja na ukweli kwamba zimekuwa zinaongezeka mara kwa mara, lakini hilo sio tatizo kubwa ukifananisha na kupanda kwa gharama za umeme, mafuta, chakula, chakula na kodi ya nyumba.

Watazamaji wengi wataanza kunyanyuka kutoka katika viti vyao baada ya kubaini kwamba kumbe kweli Mh. Mnyika anapigana the "wrong war", unless ni the "right war" kwa sababu za siasa;

Wakazi wengi wa DSM wenye umri wa kukumbuka maisha yalivyokuwa mwaka 1996, tofauti na sasahivi wataendelea kufikiria yafuatayo:

Mwaka 1996, bei ya kilo moja ya sembe ilikuwa ni sh.100. Leo hii (miaka 15 baadae), kilo hiyo hiyo moja ya Sembe ni Sh. 1,000, huku nauli ya ferry ikiongezeka kwa sh mia tu katika kipindi hicho hicho.

Mwaka 1996, kilo moja ya mchele ilikuwa sh. 300. Leo hii kilo hiyo hiyo ni sh. 2,000, huku nauli ya ferry ikiongezeka kwa sh. 100 tu katika kipindi hicho hicho.

Mwaka 1996, kilo moja ya Sukari ilikuwa ni sh. 200, Leo hii kilo hiyo hiyo moja ni zaidi ya Sh.2,000, huku nauli ya ferry ikiongezeka kwa sh. 100 tu katika kipindi hicho.

Wakazi wengi watabaini kwamba, kumbe sakata hili la nauli ya ferry ilitakiwa lichukue sura iliyo kinyume na hali ya sasa kwa maana ya kwamba – kumbe ilitakiwa Mheshimiwa Mnyika na wenzake kina Zungu, Ndugulile, Mtemvu na wengineo, kuwaongoza na kuwahimiza wapiga kura wao wampe pongezi nyingi sana Magufuli kwa sababu, pamoja na kupanda sana kwa gharama za maisha katika kipindi cha miaka 15 (yani 1996 – 2011), bado nauli ya ferry imebakia bei karibia na bure, tofauti na ongezeko la huko mikoani. Wakazi wengi zaidi watajipanga sasa kuwatumeni nyinyi wawakilishi wao kwenda bungeni mwezi Juni kupambana na Uchumi Uchwara wa Mkullo, na kumbana aje na mikakati itakayopelekea serikali kuja na bajeti itakayosaidia kuwapunguzia wapiga kura wenu, na wananchi kwa ujumla, ugumu ya maisha kwenye maeneo nje kabisa ya shilingi mia moja ya Feri.

Mwisho, wakazi hao wataomba sana kupitia imani zao mbali mbali kwamba, mjadala wa sasa uliojaa siasa kuliko mantiki, usipelekee hali ambayo kivuko cha ferry kitaacha kuwa chini ya usimamizi wa serikali, na badala yake soko huria, kwani wakazi hao kwa urahisi sana wataelewa kwamba iwapo hilo litatokea, basi ongezko la nauli ya kivuko cha ferry litaanza kukimbizana sambamba na bei ya kilo ya unga wa sembe, kama sio kilo ya sukari, mchele, au lita moja ya mafuta ya taa.
 
Mkuu tatizo siyo kupanda ghafla.
Tatizo wanalolisema wabunge (hakumtaja mdee lakini nyinyi mnaona kama CDM wanalengwa) ni kuwa wakazi wa kigamboni wanaonewa na serikali, kwamba shilingi 100 inatosha. Je, wewe unakubaliana nalo? Kama siyo, je huoni kuwa wabunge wameingiza siasa bila data?
Tupinge wanasiasa kujiingiza kwenye taaluma, haya mambo ndiyo yanayopingwa hapa...... wana access na data lakini hawazitumii.
Kinachosikitisha, ni ulimbukeni wa wanasiasa, ndiyo maana mnaulizwa, Mnyika hata wewe?

Mkuu ukiangalia baadhi ya sababu alizotoa Magufuli inawezekana wakazi wa Kigamboni wanaonewa. Kwa mfano, magufuli amesema kuwa kupandiswa kwa nauli, kutasaidia kununua kivuko kipya kwa ajili ya safari za Bagamoyo na feri. Kama ni hivyo kwa nini gharama za hicho kivuko cha Bagamoyo walipie wakazi wa kigamboni ambao hawatakitumia? Kama mdau mmoja alivyouliza kwenye thread nyingine, kwa nini "asiwapandishie bei za mabasi na daladala wanaosafiri kati ya dar na bagamoyo?"

Kama Magufuli angekuwa amewashirikisha watu wa Kigamboni kwenye maamuzi yake ya kupandisha nauli halafu wakamwuliza hilo swali angewajibuje? Kwa nini watu wa Kigamboni wagharimie usafiri wa watu wa Bagamoyo? Maana sasa tutaambiwa na gharama ya viwanja vya ndege itapanda kwa ili kusaidia kujenga uwanja wa ndege bagamoyo. Tutaambiwa gharama za bandari inabidi zipande ili kujenga bandari Bagamoyo.

Kuhusu suala la wabunge, of course, nao ni wa kulaumiwa. Magufuli anasema upandishaji wa nauli ulitangazwa kwenye gazeti la serikali toleo namba 367 Aprili mwaka jana. Ina maana wabunge wote wa Dar Es Salaam hawakuliona hilo tangazo? Kwa nini wamesubiri mpaka sasa ndio wanaanza kulalamika? Lakini pamoja na hayo mimi naangalia zaidi at the root of the problem which is serikali kulala for 14 years then kukurupuka ghafla na kufanya maamuzi bila kuwashirikisha waathirika.
 
Kwa nini tuna-avoid maswali magumu? Comparison yako ya kutopandisha nauli kwa miaka 14 na kutojenga daraja kwa miaka hamsimi naona kama ni absurd. Hapa serikali ilikuwa na uwezo wa kupandisha nauli kulingana na gharama za uendeshaji lakini haikufanya hivyo kwa muda wa miaka 14.

Kwa mtazamo wangu finyu, ni kwamba kivuko cha kigamboni kwa miaka mingi sana kimekuwa ni cha kusua sua, kwani kuna wakati huko nyuma kilikuwa hakitoa huduma kabisa, na tatizo hili lilikuwa miaka ile Mustafa Nyanganyi akiwa waziri wa uchukuzi, na pia miaka ya baadae chini ya mawaziri wengine; sasa katika hali kama hiyo, kuongeza nauli kwa huduma ambayo sio reliable ikawa tatizo kidogo 'kisiasa', hivyo serikali ikaamua kujitisha na mzigo huo kwa miaka mingi mpaka pale sustainability ya huduma ilipoanza kukaa sawa. i might be wrong.

Kuhusu ujenzi wa daraja, serikali haikuwa na pesa, na hata sasa, bado inatafuta hizo pesa. nadhani NSSF wao wameshapata kama 60% ya gharama za ujenzi, na wanategemea serikali isaidie pia; lakini tusisahau pia suala la economics za uwepo wa daraja pamoja na kivuko, hizi zimekuwa zinawasumbua sana decision makers;
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Back
Top Bottom