Isenye
JF-Expert Member
- Dec 22, 2024
- 1,450
- 3,889
Wakuu mko salama?
Wakuu kiukweli mpaka nimeanza kujichukia kuhusu unywaji wa pombe. Mfano jana nimepiga maji hadi sijui nilirudije ghetto,sometimes kumbukumbu zinapotea sababu ya pombe, kiuchumi napo naathirika,yani naweza nikawa na ka laki moja kangu mfukoni,nikiingia bar tu hako kalaki kataisha na madeni juu.
Sasa asubuhi hii sijui ndo pombe jana nilizinywa nyingi au sijui ni nini nimeingia bafuni nimetapika sana.
Kwa kweli hii hali inanisononesha mno,natamani kuachana na huu unywaji lkn kila nikisema niache nitakaa siku mbili tu naanza tena.mfano leo nilipanga nisiguse pombe ila tayari kuna jamaa yangu ametoka kahama huko ana mpunga keshanambia jioni tukutane tupige vyombo.
Wakuu najinasuaje na unywaji huu wa tungi?
Wakuu kiukweli mpaka nimeanza kujichukia kuhusu unywaji wa pombe. Mfano jana nimepiga maji hadi sijui nilirudije ghetto,sometimes kumbukumbu zinapotea sababu ya pombe, kiuchumi napo naathirika,yani naweza nikawa na ka laki moja kangu mfukoni,nikiingia bar tu hako kalaki kataisha na madeni juu.
Sasa asubuhi hii sijui ndo pombe jana nilizinywa nyingi au sijui ni nini nimeingia bafuni nimetapika sana.
Kwa kweli hii hali inanisononesha mno,natamani kuachana na huu unywaji lkn kila nikisema niache nitakaa siku mbili tu naanza tena.mfano leo nilipanga nisiguse pombe ila tayari kuna jamaa yangu ametoka kahama huko ana mpunga keshanambia jioni tukutane tupige vyombo.
Wakuu najinasuaje na unywaji huu wa tungi?